Tujikumbushe vitu na bidhaa mbalimbali za zamani ambazo kwasasa hazipo tena

Umenikumbusha baiskeli ya Phoenix, mzee alikuwa nayo nakumbuka alikuwa hadi anailipia ushuru sh 200 kama sikosei.

Aliinunulia hadi kufuli lile anafunga funguo anakaa nayo. Akukute umechezea au umeharibu [emoji3]
Ilikuwa noma sana mkuu
 
Tuwakumbushe watoto wa kizazi hiki kuhusu bidhaa na vitu mbalimbali vilivyokuwepo zamani lakini kwasasa havipo.

Naanza na Sabuni ya Mbuni…
Sabuni ya KOMOA, MSHINDI, GEISHA

Ndala za umoja
Magari ya shule za sekondari za serkali
Nidhamu kwa watumishi wa umma
Malezi bora
 
-Mtungi wa maji ya kunywa
-Kibuyu cha kuhifadhi maziwa
-Chungu cha kupikia chakula,msosi
wake mtamu sana
Kwa bibi alikuwa na mtungi huo maji ni baridi na safi balaa. Ule mtungi ulikuwa balaa sana
 
peni za bic

mashati ya bushoke

Juisi ya sobo ya kuchanganya na maji

viatu vya fokona (four corner)
Kuna christmas moja nilipiga jeans na shati ya Bushoke niliwakimbiza sana mtaani madogo wenzangu
 
We jamaa umenikumbusha vitu vingi sana aisee. Noma sana
 
Mimi huku kwetu watoto wangu hawajui chawa ni wadudu gani. Enzi zetu wadudu hawa walitutesa Sana. Tulikuwa pia na wimbo wa kuwaambia chawa waache kutusumbua usiku tukiwa tumelala na kutulazimisha kunyolewa nywele hadi vipara.
Chawa/kunguni siwajui.
 
Chemli, last born nilimuuliza unaijua hii??

Akaniambia na mwenyewa hauijui hiyo sema inaitwaje?[emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…