Tujikumbushe Walimu wa sekondari waliokuwa wakali sana kiasi cha kuwa maarufu hadi shule zingine

Tujikumbushe Walimu wa sekondari waliokuwa wakali sana kiasi cha kuwa maarufu hadi shule zingine

Nimeingia tu form one, wakati huo tunavaa kaptula za khaki! Kaptula ilikuwa inafika kwenye ugoko, shati sijachomekea lilikuwa puto (oversize) chini Nina Buti nimenunua kwa mwanangu kituo Cha zimamoto pale fire nadunda kinoma, daftari nilikuwa naweka mfuko wa nyuma wa kaptula....
kutimba skuli... mwamba huyuhapa! alikuwa Mwalimu wa nidhamu.... nilianza nae bifu siku hiyo ya kwanza naingia shule mpaka namaliza.

Yule jamaa hata tukikutana after life atanikumbuka tu kwa matukio niliyompiga.

RIP Mchwa

Anayejua kaburi lake lipo anitaarifu nikamwage mahindi na pombe kwani nimekuwa mkulima mlevi badala ya engineer kwa aniliyake.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mr. PATEL and Mr. Dogo,,, hawa ma Mafia wawili wali run Forest Hill Secondary. Waliowahi kupita pale wanawajua since 1990's
Kuna siku nilitoroka airport Dogo alinitafuta siku nzima shenzi type. Umemsahau mtu m-bad makusi hakuna kucheka.
 
Nimeandika huu uzi baada ya kuwakumbuka waalimu wangu hasa wale wakuu wa miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni waliokuwa wakali sana wasiotaka masikhara kiasi cha kuweza kujulikana hadi mkoa mzima na kanda. Wafuatao walivuma sana kanda ya kaskazini;

1. Mwalimu Kibatala - Shule ya sekondari Karatu, Arusha.
2. Mwalimu Shayo - Shule ya Sekondari Arusha.
3. Mwalimu wa malezi Ilboru sec, jina limenitoka ila ana jina la kimasai. Waliosoma 1998 - 2001 wanaweza kumkumbuka.
4. Mwalimu Teti - Tanga technical Secondary school. Huyu mkuu wa shule ilikuwa sio poa...
5. Mwalimu Mpande - Moshi Technical Secondary School. Huyu mwalimu kwenye umisetta alikuwa tishio. Ukileta zako ni kibano unakula.
6. Munga - Kaloleni sec, Arusha.
7. Kipingu -
8. Mwalimu Masatu na Mgimwa - Mkwawa High School (complex)
Ongezeeni majina mengine tujikumbushe enzi za u-teenage.
Sa umesoma shule zooote hizo🤔🤔
 
Alikuwa anafundisha Literature 2 basi mashairi magumu ndio anataka tuyashike mazima kama development, building the nation, the Vulture.

Alikuwa anatuambia mashairi ya eat more sio level zetu. Novel alikuwa anaichambua na kututafsiria kama unaangalia movie vile. Ila alitusaidia sana kutushape kitabia na kielimu pia.
Kakufundisha pandahill au swilla sec
 
Nalimi a.k.a kocha wa Ifunda Tech Sec School
Mwakalindile a.k.a Brigedia Ifunda Tech Sec School

Hawa jamaa, inapokuja wakati wa wao kuwa walimu wa zamu, ni kwamba assembly hakuna kuchelewa..!! Ole wako
Nalimi a.k.a kocha wa Ifunda Tech Sec School

Nikajua ni mwanajf mwenzetu Don Kisando
 
Shelimo alitukuta Pugu 2007 jamaa alikuwa mpole na msataarabu. Baadae alikuwa Afisa Elimu Temeke
RIP mkuu aliiwezea sana Pugu hata ukiwa unadrop anakupa lift hadi town suala la simu shule zote wanakataza ila kwa Mwamba alikua anataka kila mwanafunzi awe na number yake ili akipata shida ampigie.
Screenshot_20230118-220829_Instagram.jpg
 
Kitu nilicho kigundua ma teacher wakali kupitiliza walikuwa na matatizo haya.
1. Uelewa wao wa masomo wanayofundisha ulikuwa mdogo hivyo ku apply intimidation method kufunika kaujinga kake.

2. Walitokea familia katili walitembezewa mboko utotoni kiasi hawakuweza kujitetea sasa wamekuwa hawana namna ya kulipiza kisasi kwa watesi wao na wana substute kwa kuwatandika na kuwa wakali kwa watoto wa shule.
3. Umalaya wa walimu wana wachalaza mboko hovyox2 ili siku akitaka kupita na kitoto cha kike kiwe kioga na kukubali kwa hofu ya mboko.
4. Ugumu wa maisha au tuseme kuwa na msongo wa mawazo.
 
Nimeandika huu uzi baada ya kuwakumbuka waalimu wangu hasa wale wakuu wa miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni waliokuwa wakali sana wasiotaka masikhara kiasi cha kuweza kujulikana hadi mkoa mzima na kanda. Wafuatao walivuma sana kanda ya kaskazini;

1. Mwalimu Kibatala - Shule ya sekondari Karatu, Arusha.
2. Mwalimu Shayo - Shule ya Sekondari Arusha.
3. Mwalimu wa malezi Ilboru sec, jina limenitoka ila ana jina la kimasai. Waliosoma 1998 - 2001 wanaweza kumkumbuka.
4. Mwalimu Teti - Tanga technical Secondary school. Huyu mkuu wa shule ilikuwa sio poa...
5. Mwalimu Mpande - Moshi Technical Secondary School. Huyu mwalimu kwenye umisetta alikuwa tishio. Ukileta zako ni kibano unakula.
6. Munga - Kaloleni sec, Arusha.
7. Kipingu -
8. Mwalimu Masatu na Mgimwa - Mkwawa High School (complex)
Ongezeeni majina mengine tujikumbushe enzi za u-teenage.
Waliomaliza shule juzi juzi utawajua tu
 
S/master mbugani sec nimemsahau jina alikua na roho mbaya sana yule mtu, ijumaa tulikua tunatorokaga mapema sana sasa siku hiyo tukakutana nae pale mesi yeye akiwa kwenye boda boda.

Sasa akili zetu tukawa na mawazo hajatuona, kumbe alituona akamkariri mmoja akapotezea.

J3 akaingia darasan akamuinua jamaa na kofi zito sana, "simama taja wenzako nimewakuta msituni majambazi hamtaki shule" kwanza tulimwagiwa maji tukachezea kipigo kizito kwa kuchangiwa na walimu alafu tukapewa barua mje na wazazi.

Kidogo tufukuzwe shule, tuliishia kufyatua matofari ya kutosha kama adhabu.
 
Back
Top Bottom