Tujikumbushe Walimu wa sekondari waliokuwa wakali sana kiasi cha kuwa maarufu hadi shule zingine

Tujikumbushe Walimu wa sekondari waliokuwa wakali sana kiasi cha kuwa maarufu hadi shule zingine

Ningeshangaa sana kama usingemtaja Mwalimu Mpande wa Moshi Technical, daah umenikumbusha mbali sana japokuwa umri umeenda sasa ila sitakaa nimsahau huyu mtu. Alikuwa noma sana na usemi wake eenhe bwaana..😄😄, mara ya mwisho nilikutana naye pale Moshi mjini Fresh coach 2018 nikamtupia wekundu kadhaa, alinishape sana kitabia namshukuru kwa kweli may be leo nisingekuwa hivi nilivyo. Live longer Mr. Mpande
Dah mwl mpande alikuwa noma Sana...asubuhi mchakamchaka ole wako akukute umelala bwenini
 
Muttakyamirwa aka SUPER COMMANDO
Mwamfupe aka UNYAMAUNYAMA

Hawa wehu walipatikana MAZENGO TECH SEC SCHOOL.
Wiki ya zamu zao tulikuwa tunaiona shule ya moto kama jehanamu vile.

Bila kumsahau mwl Mshumbuzi huyu alikuwa boya sana kwenye kipindi chake cha kingereza, ilikuwa akikukuta umezubaa tu anakuvuta shavu unanaswa bonge la bao mpaka unaona nyotanyota!

Nakumbuka alikuwa anakuja na novel flan yenye story ya mabala the farmer na ... The bus driver!
Yule fara alikuwa anatugawa kwenye magroup halafu anatuchanganya na watoto wa kike day scholer. Sasa sisi watu wa boarding tulikuwa wakaksi tunajiita wagumu hatushobokei mademu.

Mara paaap mshumbuzi huyu hapa akukute huoneshi ushirikiano kwa mademu anakuvuta shavu mkono wa kulia then upande mwingne anakushushia wepa la shoto matata sana tena mbele ya mademu maneeena zake mshumbuz...!
 
Hahahaha asbh tulikuwa tunaita kombolela kutukimbiza wachelewaji. Mgimwa hakuwa mnoko kivile.
Mkuu kumbe nawe ulisoma Mkwawa? Mkwawa ilikuwa balaa, hiyo kombolela isikie tu, mimi niliwahi jikuta nimekubwa na kombolela walimu wanne waliingia bwenini na viboko vya kutosha saa 1 asubuhi sisi tukiwa bado tunaoga tulikuwa washkaji kama 5 hivi , basi jamaa walitembeza bakora ivo ivo bila kujali mpo uchi, ilibidi tukimbie na kupanda juu ya dari la bweni hapo tukiwa na mataulo tu. jamaa walitusihi tushuke tuyamalize lakini tuligoma , tuliwapa sharti moja zito waondoke au tujirushe chini nje ya bweni tupasuke au tufe kabisa maana palikuwa parefu. Basi dogo mmoja alijirusha kweli ile kumchungulia dogo alitapakaa tamu kama kapigwa ngumi Sugunyo ya bmandoga, taya na meno vilikuwa vinadam, including pua, ilibidi walimu waache hiyo tabia ya kufanya kombolela baads ya hapo. tulikuwa tukiishi maisha mazuri tu, hata ukichelewa pared hakuna kombolela.
 
Masatu alinifundisha English one,Mgimwa Geography 2.Mgimwa alikua best sana.Kipindi hicho ni kijana wa miaka 17 hata sijaanza kuchakata mbususu.Umenikumbusha mbali enzi hizo Mkuu ni Mr Mbao
Mbao alikuwa na pigo kama za kiongozi flani mkubwa wa kiserikali.
 
Nimeandika huu uzi baada ya kuwakumbuka waalimu wangu hasa wale wakuu wa miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni waliokuwa wakali sana wasiotaka masikhara kiasi cha kuweza kujulikana hadi mkoa mzima na kanda. Wafuatao walivuma sana kanda ya kaskazini;

1. Mwalimu Kibatala - Shule ya sekondari Karatu, Arusha.
2. Mwalimu Shayo - Shule ya Sekondari Arusha.
3. Mwalimu wa malezi Ilboru sec, jina limenitoka ila ana jina la kimasai. Waliosoma 1998 - 2001 wanaweza kumkumbuka.
4. Mwalimu Teti - Tanga technical Secondary school. Huyu mkuu wa shule ilikuwa sio poa...
5. Mwalimu Mpande - Moshi Technical Secondary School. Huyu mwalimu kwenye umisetta alikuwa tishio. Ukileta zako ni kibano unakula.
6. Munga - Kaloleni sec, Arusha.
7. Kipingu -
8. Mwalimu Masatu na Mgimwa - Mkwawa High School (complex)
Ongezeeni majina mengine tujikumbushe enzi za u-teenage.
Da! umetaja mwl Mpande umenikumbusha mbali saaana kwa kwa dada Asha!!!
 
Huyu alikuwaga ana historia ya kuto wahi msamehe mtu.halafu hajawahi cheka pia
Mwamba huyu hapa…
13C27482-79F6-41CC-A83F-621CEB04AD92.jpeg
 
Galanos Galaxy Msocha na mchaka mchaka yule Mzee alikuwa akinifatilia Sana kidogo nimpe za uso,
 
Back
Top Bottom