Tukiacha ushabiki wa kivyama na Unafiki, Hoja ya Spika haijajibiwa

Tukiacha ushabiki wa kivyama na Unafiki, Hoja ya Spika haijajibiwa

Tukiacha ushabiki wa kivyama na kujipendekeza (unafiki), Licha ya kila mtu kujitokeza kujaribu kujibu hoja ya Spika Ndugai ama kuizungumzia hoja hiyo, na hata Serikali (Rais) ameitisha mkutano wa kidola nikidhani anajibu hoja, badala yake wamejikuta wanamjadili Ndugai ama kumdhihaki ama kumdhalilisha tu, hoja ya Spika Job Ndugai haijajibiwa hata chembe, na ina nguvu kubwa. Hoja ya Ndugai si kwamba ina nguvu za kitaasisi tu, bali ni hoja inayohatarisha madaraka ya Rais, kwasababu kuu mbili,

Mosi: Liko kundi kubwa la Watanzania waliopewa jina la masikini na utawala wa John Magufuli, wakaaminishwa kuwa Rais Magufuli alikataa kukopa popote duniani tangu aingie madarakani hadi anafariki, na kwamba aliwagomea wazungu kwakuwa ni mabeberu waliotaka kupora raslimali zetu. Hawa waliaminishwa ujinga kuwa miradi yote nchini inajengwa kwa pesa yetu wenyewe.

Hili kundi utaliambia nini leo ukianza kukopa kwa uwazi na kutangaza hivi kila mkopo, bila kwanza kulipa elimu kuwa Magufuli katika utawala wake alikopa kimyakimya mikopo mikubwa ya kibiashara iliyovunja rekodi ya mikopo nchini? Kosa kubwa ambalo Rais Samia alifahya ni pale alipoingia madarakani akataka kuwawin makundi yote masikini na wenye akili, akasema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Ni wazi hili kundi la masikini litamuunga mkono mtu yoyote atakayekosoa mikopo yenu.

Pili: Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 ibara ya 63(2) nanukuu; Ibara ya 63 (2) "Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwaniaba ya wananchi, kuisimamia na KUISHAURI Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wamajukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Kwa ibara hii ya 63 (2), Spika Ndugai ametimiza wajibu wa kikatiba wa Bunge katika kuishauri serikali, Kwamaoni yangu Spika hajakosea chochote katika kauli yake kuhusu serikali kuacha kukopa. Ametimiza matakwa ya kikatiba kama mkuu wa muhimili,

Ukiacha wajibu wa kibunge kama Spika, Job Ndugai kama rais wa Tanzania ametumia ibara ya 18 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa maoni yake. Ni sheria ipi Tanzania inayomzuia mtu kutoa maoni yake, ama kukosoa serikali?

Na Yericko Nyerere

View attachment 2069920
View attachment 2069921
CCM wanaongoza kwa kuwakumbatia maskini ambao maisha yao yanategemea kwa sehemu kubwa, kujipendekeza kwa viongozi wa chama hasa Mwenyekiti na Katibu.
Wanaiona CCM kama bahari na wao ni samaki. Kwamba hawawezi kupumua licha ya kuishi nje ya CCM.
Kwanini wanaishia kumdhalilisha Speaker Ndugai badala ya kuweka hoja zote mbili mezani?
 
Tukiacha ushabiki wa kivyama na kujipendekeza (unafiki), Licha ya kila mtu kujitokeza kujaribu kujibu hoja ya Spika Ndugai ama kuizungumzia hoja hiyo, na hata Serikali (Rais) ameitisha mkutano wa kidola nikidhani anajibu hoja, badala yake wamejikuta wanamjadili Ndugai ama kumdhihaki ama kumdhalilisha tu, hoja ya Spika Job Ndugai haijajibiwa hata chembe, na ina nguvu kubwa. Hoja ya Ndugai si kwamba ina nguvu za kitaasisi tu, bali ni hoja inayohatarisha madaraka ya Rais, kwasababu kuu mbili,

Mosi: Liko kundi kubwa la Watanzania waliopewa jina la masikini na utawala wa John Magufuli, wakaaminishwa kuwa Rais Magufuli alikataa kukopa popote duniani tangu aingie madarakani hadi anafariki, na kwamba aliwagomea wazungu kwakuwa ni mabeberu waliotaka kupora raslimali zetu. Hawa waliaminishwa ujinga kuwa miradi yote nchini inajengwa kwa pesa yetu wenyewe.

Hili kundi utaliambia nini leo ukianza kukopa kwa uwazi na kutangaza hivi kila mkopo, bila kwanza kulipa elimu kuwa Magufuli katika utawala wake alikopa kimyakimya mikopo mikubwa ya kibiashara iliyovunja rekodi ya mikopo nchini? Kosa kubwa ambalo Rais Samia alifahya ni pale alipoingia madarakani akataka kuwawin makundi yote masikini na wenye akili, akasema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Ni wazi hili kundi la masikini litamuunga mkono mtu yoyote atakayekosoa mikopo yenu.

Pili: Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 ibara ya 63(2) nanukuu; Ibara ya 63 (2) "Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwaniaba ya wananchi, kuisimamia na KUISHAURI Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wamajukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Kwa ibara hii ya 63 (2), Spika Ndugai ametimiza wajibu wa kikatiba wa Bunge katika kuishauri serikali, Kwamaoni yangu Spika hajakosea chochote katika kauli yake kuhusu serikali kuacha kukopa. Ametimiza matakwa ya kikatiba kama mkuu wa muhimili,

Ukiacha wajibu wa kibunge kama Spika, Job Ndugai kama rais wa Tanzania ametumia ibara ya 18 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa maoni yake. Ni sheria ipi Tanzania inayomzuia mtu kutoa maoni yake, ama kukosoa serikali?

Na Yericko Nyerere

View attachment 2069920
View attachment 2069921
Na hoja ya Ndugai ni ya msingi kwa sababu:
1. Sio uongo kwamba kuna nchi zimezidiwa na mikopo.
Mfano, jirani yetu Zambia tayari ni International defaulter. Na tayari kwenye management na bodi za mashirika yake matatu, kuna raia wa kigeni ili kurejesha mkopo wao kwa kusimamia mapato na matumizi ya hayo mashirika.
Sri Lanka pia waliachia bandari kwa mchina baada ya kuzidiwa na mkopo.
Mkopo wa Ujenzi wa Reli unawatesa jirani zetu wa Kaskazini.
2. Kutoa tahadhari juu ya mikopo, sio jambo baya hata kidogo. Ni kujibizana na kueleweshana.
Kudhalilishana, kuona kwamba watu wanataka kiti 2025; ni hofu tu ya madaraka na hofu ya kupoteza kitumbua. Kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake hasa kwa swala la kitaifa kama hilo.
3. Wananchi wana haki ya kusikilizwa. Ni jambo la ajabu kuwasikiliza wale waliokuzunguka tu. Waliokuzunguka hawawezi kumwambia SSH ukweli. Ni kama ambavyo hawakumwambia JK ukweli juu ya Richmond Dowans na Escrow.
Hawakumwambia Mkapa ukweli juu ya EPA, Radar, Meremeta, Kagoda na Alex Stewarts.
 
Ndugai hana hoja.Ndugai hana hoja. Siyo kweli unachosema. Bunge ndiyo hupitisha bajeti ya recurrent and development. Wanaposema makusanyo yatakuwa Tsh 24 T rillion huku Bajeti ya mwaka ni Tsh 32 Trillion unadhani hiyo nakisi inatoka wapi? Nakisi hujazwa kwa grants, donations and loans. Ndugai hajitambui, he is lunatic and unfit to the position
Mkuu Stuxnet , thanks for this.
Huko nyuma niliwahi kuuliza
P
 
BAVICHA nao ni kama wamekua wajinga, sijui uelewa mdogo sijui ujinga, sijui ni stress
 
Mwendawazimu tu ndio atamuunga mkono Ndugai, kwanza anasema hiyo hoja ni ya kutunga. Pili ameomba msamaha kwa hoja hiyo. Kama yeye binafsi anakataa hoja yake, kwanini sisi tujipe jukumu la kuitetea hoja yake? Akitaka hoja yake ibaki na nguvu ashikilie msimamo wako.
Acha matusi, nami nasema Kichaa uchwara pekee ndiye atampinga Ndugai maana ibara ya 18 ya Katiba inampa Uhuru wa kutoa maoni yake.
 
Mimi binafsi nipo na Ndugai.
Wapinzani tutakosea sana tukiwa upande wa Samia kisa Ndugai ni mtu tusiyempenda, Hoja ya Ndugai ni moja kati ya sera zetu "kupunguza mikopo na kutumia rasilimali zetu na uwekezaj"
Ndugai hatumpendi lakini upepo wa wananchi wajinga wa Tanzania upo na Ndugai maana wanaamini Magufuli alikuwa jembe hakopi nje.

Kwahiyo nyie mpo kufuata upepo wa wajinga? Kama mlivyofanya kipindi cha Lowasa? Mwenye akili atafurahia kuona tuna Rais anayeweka wazi mikopo na matumizi yake.
 
Ndugai hana hoja.Ndugai hana hoja. Siyo kweli unachosema. Bunge ndiyo hupitisha bajeti ya recurrent and development. Wanaposema makusanyo yatakuwa Tsh 24 T rillion huku Bajeti ya mwaka ni Tsh 32 Trillion unadhani hiyo nakisi inatoka wapi? Nakisi hujazwa kwa grants, donations and loans. Ndugai hajitambui, he is lunatic and unfit to the position
Kwa akili yako ndogo na pumba ulizozoea kupost unadhani Ndugai hajui nakisi ya bajeti inapatikana vipi? Hoja ilukuwa kama kuna tozo zinazojenga madarasa kwa nini tukope? Tumia akili acha kujibu ishu kwa chuki.
 
What goes around comes around. Lisu naye Alisema wakitumaliza sisi itafuata zamu yao. Wahenga nao Ukila nyama ya binadamu huwezi wacha. Hata kama jobo anahoja kwenye hili ndio muda wa kulipia aliyotenda bungeni. Mungu hajawahi kulala ataendelea kutulipia hapa hapa mpk wasiojulikana pia.
 
Kwa akili yako ndogo na pumba ulizozoea kupost unadhani Ndugai hajui nakisi ya bajeti inapatikana vipi? Hoja ilukuwa kama kuna tozo zinazojenga madarasa kwa nini tukope? Tumia akili acha kujibu ishu kwa chuki.

Ni kweli kabisa usemayo, lakini Ndugai kakanusha kuwa hiyo sio hoja yake bali ni clip ya kutengeneza, kibaya zaidi kaomba msamaha kuhusu hoja hiyo. Hapo unatetea nini?
 
Kuomba msamaha kwake hakuondoi hoja aliyoiweka mezani

Ni hoja gani mahdusi aliyoiweka mezani? Ni mkopo huu wa Covid 19 stimulus package au mikopo yote? Kama yote, alikua wapi siku zote?
Inaleta ukakasi kidogo kuwa mkopo wa Covid19 uwe ni chanzo cha Nchi kuuzwa, wakati kuna mikopo kibao haikuhojiwa, ukakasi uko hapo
 
Shida ni approach yake. Hauwezi kupitisha jambo na kulibariki bungeni ukatoka nje kulikosoa, haiendi namna hiyo.
Bungeni unaweza kuwa na msimano tofauti na wenzako lakini hoja ikapitishwa kwa sababu wabunge wengi wanaiunga mkono. Hivyo kupitishwa hona sio sababu ya wasioitaka hoja hiyo kutoipinga nje ya bunge. Inawezekana Ndugai binafsi hakukubaliana na hoja hiyo ya mikopo kama kweli ilupita bungeni.
 
Shida ni approach yake. Hauwezi kupitisha jambo na kulibariki bungeni ukatoka nje kulikosoa, haiendi namna hiyo.
Msikilize vizuri ndugai jinsi vitu vya ajabu vinavyopitishwa bungeni, ndio utaelewa
 
Ndugai hana hoja.Ndugai hana hoja. Siyo kweli unachosema. Bunge ndiyo hupitisha bajeti ya recurrent and development. Wanaposema makusanyo yatakuwa Tsh 24 T rillion huku Bajeti ya mwaka ni Tsh 32 Trillion unadhani hiyo nakisi inatoka wapi? Nakisi hujazwa kwa grants, donations and loans. Ndugai hajitambui, he is lunatic and unfit to the position
Anajua huwa ni budget ya uongo yaan ni ilimradi liende tu, kwan ni mwaka gani hiyo bajeti iliwahi kutekelezwa?
 
Bungeni unaweza kuwa na msimano tofauti na wenzako lakini hoja ikapitishwa kwa sababu wabunge wengi wanaiunga mkono. Hivyo kupitishwa hona sio sababu ya wasioitaka hoja hiyo kutoipinga nje ya bunge. Inawezekana Ndugai binafsi hakukubaliana na hoja hiyo ya mikopo kama kweli ilupita bungeni.

Kama ni kweli kutokubaliana na mikopo ilikua ndio hoja yake, kwanini aombe radhi kwamba alieleweka vibaya?
 
Back
Top Bottom