Tukiacha ushabiki wa kivyama na Unafiki, Hoja ya Spika haijajibiwa

Tukiacha ushabiki wa kivyama na Unafiki, Hoja ya Spika haijajibiwa

Tukiacha ushabiki wa kivyama na kujipendekeza (unafiki), Licha ya kila mtu kujitokeza kujaribu kujibu hoja ya Spika Ndugai ama kuizungumzia hoja hiyo, na hata Serikali (Rais) ameitisha mkutano wa kidola nikidhani anajibu hoja, badala yake wamejikuta wanamjadili Ndugai ama kumdhihaki ama kumdhalilisha tu, hoja ya Spika Job Ndugai haijajibiwa hata chembe, na ina nguvu kubwa. Hoja ya Ndugai si kwamba ina nguvu za kitaasisi tu, bali ni hoja inayohatarisha madaraka ya Rais, kwasababu kuu mbili,

Mosi: Liko kundi kubwa la Watanzania waliopewa jina la masikini na utawala wa John Magufuli, wakaaminishwa kuwa Rais Magufuli alikataa kukopa popote duniani tangu aingie madarakani hadi anafariki, na kwamba aliwagomea wazungu kwakuwa ni mabeberu waliotaka kupora raslimali zetu. Hawa waliaminishwa ujinga kuwa miradi yote nchini inajengwa kwa pesa yetu wenyewe.

Hili kundi utaliambia nini leo ukianza kukopa kwa uwazi na kutangaza hivi kila mkopo, bila kwanza kulipa elimu kuwa Magufuli katika utawala wake alikopa kimyakimya mikopo mikubwa ya kibiashara iliyovunja rekodi ya mikopo nchini? Kosa kubwa ambalo Rais Samia alifahya ni pale alipoingia madarakani akataka kuwawin makundi yote masikini na wenye akili, akasema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Ni wazi hili kundi la masikini litamuunga mkono mtu yoyote atakayekosoa mikopo yenu.

Pili: Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 ibara ya 63(2) nanukuu; Ibara ya 63 (2) "Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwaniaba ya wananchi, kuisimamia na KUISHAURI Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wamajukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Kwa ibara hii ya 63 (2), Spika Ndugai ametimiza wajibu wa kikatiba wa Bunge katika kuishauri serikali, Kwamaoni yangu Spika hajakosea chochote katika kauli yake kuhusu serikali kuacha kukopa. Ametimiza matakwa ya kikatiba kama mkuu wa muhimili,

Ukiacha wajibu wa kibunge kama Spika, Job Ndugai kama rais wa Tanzania ametumia ibara ya 18 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa maoni yake. Ni sheria ipi Tanzania inayomzuia mtu kutoa maoni yake, ama kukosoa serikali?

Na Yericko Nyerere

View attachment 2069920
View attachment 2069921
Ni kweli, watu wanafanya personal attacks kuliko kujibu hoja
 
Hapana, Bunge likipitisha Bajeti kinachofuata ni UTEKELEZAJI tu. Serikali ndiyo ina wataalamu wanaojua watakopa wapi? Kiasi gani? Na watalipaje principal na interests?

Kazi ya Bunge inakuja wanapopitia kama UTEKELEZAJI ulikwenda kadri ya Bajeti iliyopitishwa mwaka uliotanguliwa
Kama serikali huwa inakopa bila mikopo kupitiwa na kupewa kibali bungeni Ndugai na Nape wako sahihi kuhoji mikopo na afya yake kwa uchumi wa taifa.
 
Aikane hoja yake, kisha sisi tuseme ni hoja yake? Kama kweli anaiamini hoja yake ajitokeze hadharani tumuunge mkono.
Halafu baada ya kumuunga mkono na uspika utampa?
Hofu yake kubwa ni uspika na si vinginevyo.
 
Mimi binafsi nipo na Ndugai.
Wapinzani tutakosea sana tukiwa upande wa Samia kisa Ndugai ni mtu tusiyempenda, Hoja ya Ndugai ni moja kati ya sera zetu "kupunguza mikopo na kutumia rasilimali zetu na uwekezaj"
Ndugai hatumpendi lakini upepo wa wananchi wajinga wa Tanzania upo na Ndugai maana wanaamini Magufuli alikuwa jembe hakopi nje.

Mkuu Tua Ngoma ,upo sahihi kwa asilimia 100.
JPM aliwaaminisha "wanyonge" kuwa yeye hakopi, anafanya miradi kwa hela zetu za ndani. Na hilo ndilo lililo ndani ya vichwa vya Watanzania wengi masikini,kwamba JPM hakuwa akikopa wala kusaidiwa na mabeberu.
Leo anapotokea kiongozi mmoja na kuwa "alert" kwamba mikopo imezidi,wao lazima washituke.
Wanajiuliza,kwa nini tukope!? Mbona JPM aliweza bila kukopa!?
Washauri wa Samia ama hawajui athari za hii approach ya kupigia debe mikopo wazi wazi kwa Samia,au wanamwingiza chaka makusudi kwa sababu zao.
Hii "vita",nimeona wananchi wengi wa kawaida, hasa wa CCM wapo upande wa Ndugai wakiamini kuwa JPM hakuwa akikopa.
 
Mimi binafsi nipo na Ndugai.
Wapinzani tutakosea sana tukiwa upande wa Samia kisa Ndugai ni mtu tusiyempenda, Hoja ya Ndugai ni moja kati ya sera zetu "kupunguza mikopo na kutumia rasilimali zetu na uwekezaj"
Ndugai hatumpendi lakini upepo wa wananchi wajinga wa Tanzania upo na Ndugai maana wanaamini Magufuli alikuwa jembe hakopi nje.
Mimi sipo na yeyote wapambane na hali zao.
 
Mwendawazimu tu ndio atamuunga mkono Ndugai, kwanza anasema hiyo hoja ni ya kutunga. Pili ameomba msamaha kwa hoja hiyo. Kama yeye binafsi anakataa hoja yake, kwanini sisi tujipe jukumu la kuitetea hoja yake? Akitaka hoja yake ibaki na nguvu ashikilie msimamo wako.
Kaomba msamaha baada ya kutema nyongo.

Kwa sasa anajisikia mwepesii.
 
Tukiacha ushabiki wa kivyama na kujipendekeza (unafiki), Licha ya kila mtu kujitokeza kujaribu kujibu hoja ya Spika Ndugai ama kuizungumzia hoja hiyo, na hata Serikali (Rais) ameitisha mkutano wa kidola nikidhani anajibu hoja, badala yake wamejikuta wanamjadili Ndugai ama kumdhihaki ama kumdhalilisha tu, hoja ya Spika Job Ndugai haijajibiwa hata chembe, na ina nguvu kubwa. Hoja ya Ndugai si kwamba ina nguvu za kitaasisi tu, bali ni hoja inayohatarisha madaraka ya Rais, kwasababu kuu mbili,

Mosi: Liko kundi kubwa la Watanzania waliopewa jina la masikini na utawala wa John Magufuli, wakaaminishwa kuwa Rais Magufuli alikataa kukopa popote duniani tangu aingie madarakani hadi anafariki, na kwamba aliwagomea wazungu kwakuwa ni mabeberu waliotaka kupora raslimali zetu. Hawa waliaminishwa ujinga kuwa miradi yote nchini inajengwa kwa pesa yetu wenyewe.

Hili kundi utaliambia nini leo ukianza kukopa kwa uwazi na kutangaza hivi kila mkopo, bila kwanza kulipa elimu kuwa Magufuli katika utawala wake alikopa kimyakimya mikopo mikubwa ya kibiashara iliyovunja rekodi ya mikopo nchini? Kosa kubwa ambalo Rais Samia alifahya ni pale alipoingia madarakani akataka kuwawin makundi yote masikini na wenye akili, akasema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Ni wazi hili kundi la masikini litamuunga mkono mtu yoyote atakayekosoa mikopo yenu.

Pili: Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 ibara ya 63(2) nanukuu; Ibara ya 63 (2) "Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka, kwaniaba ya wananchi, kuisimamia na KUISHAURI Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wamajukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Kwa ibara hii ya 63 (2), Spika Ndugai ametimiza wajibu wa kikatiba wa Bunge katika kuishauri serikali, Kwamaoni yangu Spika hajakosea chochote katika kauli yake kuhusu serikali kuacha kukopa. Ametimiza matakwa ya kikatiba kama mkuu wa muhimili,

Ukiacha wajibu wa kibunge kama Spika, Job Ndugai kama rais wa Tanzania ametumia ibara ya 18 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa maoni yake. Ni sheria ipi Tanzania inayomzuia mtu kutoa maoni yake, ama kukosoa serikali?

Na Yericko Nyerere

View attachment 2069920
View attachment 2069921
Samia asemae hela za tozoamepeleka wap.
 
Mimi naona ndugai ana hoja kwa kuwa tunakopa lakini bado huyu mtanzania anatwushwa mzigo wa Kodi kufanya kitu kilekile, huyo mama yao kapuyanga sana maana kama angetaka kumjibu ndungai angemwita huko kwenye vikao vya chama. mwanzo wa Babel kuanguka ni kupishana lugha kwaiyo chama kinatakiwa kujitazama.
 
Kama serikali huwa inakopa bila mikopo kupitiwa na kupewa kibali bungeni Ndugai na Nape wako sahihi kuhoji mikopo na afya yake kwa uchumi wa taifa.
Kama yuko sahihi, kwanini aliomba msamaha kwa kusema kitu anachoamini kiko sawa?
 
Jambo gani lilipitishwa bungeni na kulikosoa nnje ndugu The Monk !!??

Kwa mujib wa huu mjadala, spika alihoji kuhusu mikopo, kitu ambacho kinaweza kujadiliwa bungeni wakati wa budget. Sasa kama huko wanapitisha na hasemi chochote, iweje huku nje aseme kwamva anashangazwa na mikopo inavyoongezeka?
 
Vyovyote iwavyo, kukopa Trillioni 10 ndani ya miezi 9 kwa miradi isiyo ya kimkakati ni jambo lisilovumilika, hili ni lazima liondoke na mtu!
 
Ndugai hana hoja.Ndugai hana hoja. Siyo kweli unachosema. Bunge ndiyo hupitisha bajeti ya recurrent and development. Wanaposema makusanyo yatakuwa Tsh 24 T rillion huku Bajeti ya mwaka ni Tsh 32 Trillion unadhani hiyo nakisi inatoka wapi? Nakisi hujazwa kwa grants, donations and loans. Ndugai hajitambui, he is lunatic and unfit to the position
Bajeti ya 32T au 34T au 36 T ni ya serikali yote including taasisi zake ambazo hazitegemei makusanyo ya TRA kujiendesha.
 
Back
Top Bottom