Tukio gani limewahi kukutokea mpaka ukajisemea kweli Mungu yupo?

Tukio gani limewahi kukutokea mpaka ukajisemea kweli Mungu yupo?

Katika dunia tunapitia mambo mengi ya huzuni na furaha, ya amani na magomvi vipi katika maisha yako jambo gani limewahi kutokea na ukajisemea kweli Mungu yupo.

Binafsi ni jinsi nilivyo faulu kidato cha sita yaani daah!

Nikikumbuka naishia kusema kweli Mungu yupo na anatenda maana nilijua nikijitahidi sana ntakuwa na division 3 ila asilimia kubwa nilijua hii ni division 4 lakini matokeo yalivyokuja daah! Sikuamini niliishia kusema kweli Mungu yupo kwani nilifaulu vizuri.

Vipi wewe kwa upande wako please share experience.

ANGALIZO: Wale wazee wa Mungu hayupo tafadhali hii sio thread ya ubishani juu ya uwepo wa Mungu so pita kimya kimya tu.
 
Ni Mengi Mungu ametenda kwangu ila kwa hil tukio huw nawaza na kushkuru mpaka kesho. Kuna siku nilipigika yaani niliwamba na na kuchakaa sina pesa kabisa. Na wakati huo kodi ya kijiofisi changu na sehem ninayoishi zimebakiza siku moja ziishe, ukichek harakat zangu sina hata dalili ya kupata pesa nilipe kodi wenye nyumba tayari washaanza kunipigia simu, huyu wa Ofsi ambapo nilikuwa nalipa 210,000/= kwa miez mitatu anadai anaomba niwaishe kodi maana mtoto katimuliwa ada shuleni hvyo siku mbili zijazo anatakiwa kurud shule maana kule shule kuna zoez la ujazaji fomu flan zitafanyika siku hiyo maana alikuwa darasa la mitihani. Huyu ninapoishi yeye ni mfugani pia anadai vifaranga vya kuku tayari viko njiani vinakuja hvyo anategemea kodi yangu anunulie chakula cha kuku yeye nilikuwa nalipa 180,000/= kwa miez sita.

Ukweli nilikaa moyoni ile siku huk nikijisemeza Eeh Mungu kama upo kweli naomba uonekane sasa, niliendelea hvyo na ukweli sikuwa na tumain lolote la kibinadam maana nikiwaza kuipata hiyo pesa kwa pamoja bdo naona ni mtihani mkubwa sana nimeupata. Kama wasemavyo wengine kuwa matendo ya Mungu ni ya ajabu na hayaelezeki bas katika hili nilishindwa kueleza. Ikafika sik ya kulipa kodi na kuna kijimvua kilikuwa kinanyesha toka mida ya saa 11 alfajili na tayar saa tatu ila bado mvua inanyesha. Ikaingia namba mpya kwenye sim yangu ikawa inaita, naipokea alikuwa ni mdada akajitambulisha kuwa ni muasibu wa taasisi X na hii taasisi naifahamu maana nimewah fanya kazi kwao kwa mkataba na tayari mwaka ulikuwa umepita tangu niachane nao. Huyu mhasib aliniuliza kama mim ndiye anayenitafuta kwa kutaja majina yangu yote matatu, nikajibu kuwa mim ndimi haswaa, basi akanieleza kuwa anatambua kuw mkataba uliishia kipind flan lakin wao kuna makosa yalifanyika walikuwa wanaendelea kuniwekea mshahara wangu hivyo anaomba kama nina taarifa bas nimsaidie namna y kurudisha zile pesa, Nikil kuw sikuwa na faham chochote maana ile acount nilifungua kwa ajil ya kupokelea mshahara tu na sikuwa nimeunganisha kwa sim zangu kuw mshahara ukiingia bas niwe napata notifications flani hivyo baada ya kumaliza mkataba wangu na kupata mshahara wangu wa mwisho nilienda nikakomba wote na ATM CARD nikaitelekeza. Kwa maelezo ya yule dad nikamwambia kuw inawezekana ila naomba niende benk kuhakik maana sijui lolote, ilibid nitoke na mvua mpak bank na nikaomba statement, ni kweli nikakuta kuna tumilion kadhaa, nikampigia yule dada kumjuza kuwa ni kweli pesa ipo ila nina ombi kwake..

Ombi langu kwake lilikuw hvi. Huu ni ukwel mtupu wakati nafanya kazi kwenye taasisi ile kuna kipind ilitokea tatizo la kufanya malipo ya mishahara hivyo kuna watu wacheche mshahara haukuingia kabisaa kwa mwezi ule na mim nikiwa mmoja wa wahanga, nilifuatilia sana mpaka mwez ukapinduka ila sikuwa nimelipwa pesa yngu, mwez uliofuata ukaingia mshahara wa mwez husika na ikaendelea hvyo kwa miez mingine.. mpaka namaliza mkataba wangu niliendelea kufuatilia lakin sikupata majibu. Sasa ilipotokea hii nikaona ni sehem sahih ya kudai haki yangu. Nikamueleza kila siku kilivyotokea kule nyuma akaomba afuatilie atarud kwangu kunipa jibu. Ndugu msomaji pesa yangu wala sikuifikilia mara mbil nikaitoa na kwenda kulipa madeni yanyu ya kodi na nilifanya hvi kwa ujasili maana ile ilikuwa pesa yangu halali kabisaa na kuwa simzurum mtu, pesa yangu nilitoa na y kwao nikabakiza nikisubir maelekezo yke.

Toka siku amenipigia sim na kusema ngoja afuatilie zilipita siku mbil kimya, ikaj y tatu mara week ikabid nimpigie, nilimpigia sana na sim haikupokelewa nilipiga tena na tena takribani miez mitatu ila sim hazipokelewi, natuma text kuomba kupewa muongozo namna y kurejesha hzo pesa ila sikupata majibu yoyote chanya.. Hvyo baada ya takribani miez sita kupita bila majibu niliamua kuzitumia zile pesa na sasa ni miaka mitatu sijawah pokea sim yka. Hili tukio huw linakumbusha juu ya uwepo wa Mungu na naamin Mungu yupo.
Daah aisee kweli Mungu yupo mkuu...!!
 
Kama tulivyokuwa tofauti kimtazamo, maumbile, Rangi n.k basi na akili, itikadi na uelewa wa mambo tunatofautiana pia.
Umechagua upande wako wa kutokuamini katika Mungu That's up to you.
But my advice try to research more and more usiishie kujifungia kwenye cage ya science tu, In this world there is thousand of knowledge and good enough all of them zinaishia ku prove Uwepo wa mungu na kutukuza matendo yake makuu.
Have a good jorney when you're ready to find the truth of God existence.
 
Kuna kipindi nilikuwa napitia madeni na pia majukumu kibao aisee kuna sehemu nilikuwa naombaga Kazi bila kuchokaaa na nilishasahau kama walitoa tangazo nikaomba.. Aisee Mungu yupo na Anaishiii ile Kazi sikuipata kwa akili zanguu kabisaa He is the Lord of Miracle tukumbuke kutoa sadaka na kushukuru kila tunapofanikisha ndugu zangu maana Tukiwa tunapitia Magumu huwa tunaweza sana nadhirii ila tukishapata tunasahau viapo na nadhiri hasa za kumtolea Mungu...!! Jumapili njema wakuu.
 
Kuna kipindi nilikuwa napitia madeni na pia majukumu kibao aisee kuna sehemu nilikuwa naombaga Kazi bila kuchokaaa na nilishasahau kama walitoa tangazo nikaomba.. Aisee Mungu yupo na Anaishiii ile Kazi sikuipata kwa akili zanguu kabisaa He is the Lord of Miracle tukumbuke kutoa sadaka na kushukuru kila tunapofanikisha ndugu zangu maana Tukiwa tunapitia Magumu huwa tunaweza sana nadhirii ila tukishapata tunasahau viapo na nadhiri hasa za kumtolea Mungu...!! Jumapili njema wakuu.

Kwa hiyo ulipata kazi ki masiala
 
Nilikutwa na mke wa jamaa kwenye nyumba ya jamaa, yule Yezebeli alinijaza kuwa anakaa mwenyeww kumbe jamaa alikua peace keeping Sudani


Jinsi nilivyopona kuanzie ile siku ukiniambia Jehovah Nisi hayupo nakuona bonge la zuzu
 
Mungu yupo kwa vile anakupangia kile unachostahili , mpaka leo naamini ulichopoteza haukustahili.

Nilipomaliza form 4 nilifaulu sana masomo yote mwishoe selection za advance nikapelekwa combination siitaki Dah! niliumia sana na kuchekwa ila walimu wakanipa ushauri nihame .

Nikamchek mdingi akasema hivi "Mimi binafsi siwez kupingana na Mungu ndo amekupangia na suala la kubadili kwangu hapana" nikaripot huku sina mzuka .Nikapambana huko huko .

From there ,niko mbali sana nilipata ajira fasta baada ya chuo tena taasisi hizi nyeti ,wanangu wote waolienda huko kwingine hawana cha maan walipata mpaka kesho yaani wazee wa vizinga na part time jobs.
Aisee M
ngu yupo bhanaaaaaa
Daah aisee kweli Mungu yupo mkuu...!!
 
Nilidondoka toka kwenye meli(man overboard) bahar ikiwa imechafuka balaa alaf wale wapuuz walikua wanajua fika kuwa uogeleaj wangu ni wa mchongo lkn wakaishia kunitupia lifering tu


Ingawaje nilitoka nikiwa hai lkn mtanange wake ulikua si wa kitoto mbiringe iliyotokea hapo viumbe hai vilivyopo pale vyote vilikimbia


Baada ya zahma ile nikawa muumin mtiifu na kila uchwao lazima nitoe sadaka na silal bila kusal na ktk begi langu la safar lazima nibebe kitabu changu cha dini
 
Nilikuta msg za mapenz anachat na rafiki yangu akaninyakua cm akafuta ushahidi akakataa hana mahusiano nae, Mungu alivyomkuu baada ya wiki 1, wakajirecord wanaongea mambo ya mapenz na jinsi mechi ilivyokua na hawakujua kama cm inarecord....nikaja sikiliza kilakitu
Hapa hakuna ulichooneshwa na Mungu sista, wanaume wote tupo hivyo hatuna mwanamke mmoja. Hata ulienae Sasa hivi anafanya kimya kimya ni vile hujajua tu.
 
Katika dunia tunapitia mambo mengi ya huzuni na furaha, ya amani na magomvi vipi katika maisha yako jambo gani limewahi kutokea na ukajisemea kweli Mungu yupo.

Binafsi ni jinsi nilivyo faulu kidato cha sita yaani daah!

Nikikumbuka naishia kusema kweli Mungu yupo na anatenda maana nilijua nikijitahidi sana ntakuwa na division 3 ila asilimia kubwa nilijua hii ni division 4 lakini matokeo yalivyokuja daah! Sikuamini niliishia kusema kweli Mungu yupo kwani nilifaulu vizuri.

Vipi wewe kwa upande wako please share experience.

ANGALIZO: Wale wazee wa Mungu hayupo tafadhali hii sio thread ya ubishani juu ya uwepo wa Mungu so pita kimya kimya tu.
Acha tu. Nakosa cha kukiongelea.
Kwa kifupi maisha yangu yote, kwa kila hatua, kwa kila pumzi, yanadhihirisha uwepo wa Mungu.
 
Kama tulivyokuwa tofauti kimtazamo, maumbile, Rangi n.k basi na akili, itikadi na uelewa wa mambo tunatofautiana pia.
Umechagua upande wako wa kutokuamini katika Mungu That's up to you.
But my advice try to research more and more usiishie kujifungia kwenye cage ya science tu, In this world there is thousand of knowledge and good enough all of them zinaishia ku prove Uwepo wa mungu na kutukuza matendo yake makuu.
Have a good jorney when you're ready to find the truth of God existence.
Hebu leta hizo source zako za knowledge zinazo prove uwepo wa Mungu.

Hukatazwi kuwa na imani yako, Lakini ukianza kusema kuna source za kuthibitisha uwepo wa Mungu uzilete hapa tuzione.
 
Katika dunia tunapitia mambo mengi ya huzuni na furaha, ya amani na magomvi vipi katika maisha yako jambo gani limewahi kutokea na ukajisemea kweli Mungu yupo.

Binafsi ni jinsi nilivyo faulu kidato cha sita yaani daah!

Nikikumbuka naishia kusema kweli Mungu yupo na anatenda maana nilijua nikijitahidi sana ntakuwa na division 3 ila asilimia kubwa nilijua hii ni division 4 lakini matokeo yalivyokuja daah! Sikuamini niliishia kusema kweli Mungu yupo kwani nilifaulu vizuri.

Vipi wewe kwa upande wako please share experience.

ANGALIZO: Wale wazee wa Mungu hayupo tafadhali hii sio thread ya ubishani juu ya uwepo wa Mungu so pita kimya kimya tu.
Siku nilipanda bodaboda mshikaji nikiwa na my young brother kutoka kariakoo kwenda mbagala mida saa Moja jion kagiza kanaingia ilikua katika early stage wa ujenzi wa mwendokasi....

Boda boda aka overtake daladala akamulikwa na gari za upande wa pili hakawa haoni vizuri mm nikiwa katikati nikawa wa kwanza kuona Yale matofari makubwa yanayo block njia likiwa limelala nikataka noruke Ile boda kushangaa lahaula uso Kwa uso...

Miujiza pikipiki ikapanda mpaka upande wa pili ikiwa na mwendokasi bila kuanguka Wala kupotezaa uelekeo ilikua ni maeneo kati ya mission na Saba Saba kwa mpili watu wote hawakuamini kilicho tokea...................

Mdogo angu Kwa kukasirika na hasira alikataa kuendelea na yule bodaboda nikamwambia MUNGU NI MWEMA KATULINDA NA HII AJARI

JESUS IS LORD
 
Katika dunia tunapitia mambo mengi ya huzuni na furaha, ya amani na magomvi vipi katika maisha yako jambo gani limewahi kutokea na ukajisemea kweli Mungu yupo.

Binafsi ni jinsi nilivyo faulu kidato cha sita yaani daah!

Nikikumbuka naishia kusema kweli Mungu yupo na anatenda maana nilijua nikijitahidi sana ntakuwa na division 3 ila asilimia kubwa nilijua hii ni division 4 lakini matokeo yalivyokuja daah! Sikuamini niliishia kusema kweli Mungu yupo kwani nilifaulu vizuri.

Vipi wewe kwa upande wako please share experience.

ANGALIZO: Wale wazee wa Mungu hayupo tafadhali hii sio thread ya ubishani juu ya uwepo wa Mungu so pita kimya kimya tu.
Je tukio hili la kufaulu kidato cha Sita lina Thibitisha vipi uwepo wa Mungu na si mawazo yako tu ya kufikirika na imani?

Je vipi kama wasahishaji wa mitihani na wapangaji wa matokeo walifanya "Standardization" ya matokeo?
 
Siku nilipanda bodaboda mshikaji nikiwa na my young brother kutoka kariakoo kwenda mbagala mida saa Moja jion kagiza kanaingia ilikua katika early stage wa ujenzi wa mwendokasi....

Boda boda aka overtake daladala akamulikwa na gari za upande wa pili hakawa haoni vizuri mm nikiwa katikati nikawa wa kwanza kuona Yale matofari makubwa yanayo block njia likiwa limelala nikataka noruke Ile boda kushangaa lahaula uso Kwa uso...

Miujiza pikipiki ikapanda mpaka upande wa pili ikiwa na mwendokasi bila kuanguka Wala kupotezaa uelekeo ilikua ni maeneo kati ya mission na Saba Saba kwa mpili watu wote hawakuamini kilicho tokea...................

Mdogo angu Kwa kukasirika na hasira alikataa kuendelea na yule bodaboda nikamwambia MUNGU NI MWEMA KATULINDA NA HII AJARI

JESUS IS LORD
Ajali zingine zinazo tokea na kuua Watu wengi licha ya kwamba Abiria Husali na kuomba sana Mungu awa kinge na kuwa epusha na Ajali hiyo,

Je Huyo Mungu huwa ana walinda kweli?

Ndege ya precision Air iliyozama ziwa Victoria, Abiria walio pona ni kwamba Mungu aliwalinda?

Je Abiria walio kufa, Hawakuwa wana muomba Mungu na wenyewe wapone kama wenzao?

Huyo Mungu ana walinda kweli watu?
 
FB_IMG_16924287275775231.jpg
 
Back
Top Bottom