Tukio gani limewahi kukutokea mpaka ukajisemea kweli Mungu yupo?

Tukio gani limewahi kukutokea mpaka ukajisemea kweli Mungu yupo?

Utawezaje kuthibitisha kisichokuwepo?

Unaweza kuthibitisha uwepo wa Athuman ambaye ni mwanaume bishoo halafu hapo hapo ni mwanamke mrembo sana?

Hali iliyokamilifu zaidi ni kutokuwepo (nothingness)
Kadri unavyotoka kwenye kutokuwepo ndivyo hivyo hivyo unaanza kutoka kwenye hali ya ukamilifu.

Vitu vyote uvionavyo wewe vimekuwepo kwasababu vimekosa ukamilifu tu.

Hivyo bhasi kama kweli Mungu huyo ambae anasemwa kuwa ni kitovu cha ukamilifu angekuwepo, bhasi kusingekuwa na chochote, kusingekuwa na dunia, kusingekuwa na nafasi (space), kusingekuwa na hewa kusingekuwa na sayari, nyota hata ulimwengu kwaujumla usingewezekana kuwepo.

Hivyo bhasi kwakuwa ulimwengu upo, sayari, nyota, viumbe wapo na vinginevyo vinavyoonekana na visivyoonekana, huo ni uthibitisho kuwa Mungu huyo ambae ni mkamilifu hayupo, na hawezekani kuwepo.
Reference ?
 
Darasani maisha yote nilikuwa natokea wa 25 na kuendelea huko, siku ya mtihani mzee namuona anaongea na teacher. Hafla naona mzee kampa teacher kitu nae teacher kaweka mfukoni alicho pewa.

Mwanangu matokeo yamekuja naambiwa eti nimetokea wa 3 🤣🤣.

Hapo nikasema Mungu anatuona kiazi mimi leo nime kuwa wa 3, halafu teacher alikuwa ananipa majibu muhuni yule😂😂
Hahaaa baba ako aliamua kujiongeza baada ya kuona unamuaibisha sana 😆😆
 
Ni Mengi Mungu ametenda kwangu ila kwa hil tukio huw nawaza na kushkuru mpaka kesho. Kuna siku nilipigika yaani niliwamba na na kuchakaa sina pesa kabisa. Na wakati huo kodi ya kijiofisi changu na sehem ninayoishi zimebakiza siku moja ziishe, ukichek harakat zangu sina hata dalili ya kupata pesa nilipe kodi wenye nyumba tayari washaanza kunipigia simu, huyu wa Ofsi ambapo nilikuwa nalipa 210,000/= kwa miez mitatu anadai anaomba niwaishe kodi maana mtoto katimuliwa ada shuleni hvyo siku mbili zijazo anatakiwa kurud shule maana kule shule kuna zoez la ujazaji fomu flan zitafanyika siku hiyo maana alikuwa darasa la mitihani. Huyu ninapoishi yeye ni mfugani pia anadai vifaranga vya kuku tayari viko njiani vinakuja hvyo anategemea kodi yangu anunulie chakula cha kuku yeye nilikuwa nalipa 180,000/= kwa miez sita.

Ukweli nilikaa moyoni ile siku huk nikijisemeza Eeh Mungu kama upo kweli naomba uonekane sasa, niliendelea hvyo na ukweli sikuwa na tumain lolote la kibinadam maana nikiwaza kuipata hiyo pesa kwa pamoja bdo naona ni mtihani mkubwa sana nimeupata. Kama wasemavyo wengine kuwa matendo ya Mungu ni ya ajabu na hayaelezeki bas katika hili nilishindwa kueleza. Ikafika sik ya kulipa kodi na kuna kijimvua kilikuwa kinanyesha toka mida ya saa 11 alfajili na tayar saa tatu ila bado mvua inanyesha. Ikaingia namba mpya kwenye sim yangu ikawa inaita, naipokea alikuwa ni mdada akajitambulisha kuwa ni muasibu wa taasisi X na hii taasisi naifahamu maana nimewah fanya kazi kwao kwa mkataba na tayari mwaka ulikuwa umepita tangu niachane nao. Huyu mhasib aliniuliza kama mim ndiye anayenitafuta kwa kutaja majina yangu yote matatu, nikajibu kuwa mim ndimi haswaa, basi akanieleza kuwa anatambua kuw mkataba uliishia kipind flan lakin wao kuna makosa yalifanyika walikuwa wanaendelea kuniwekea mshahara wangu hivyo anaomba kama nina taarifa bas nimsaidie namna y kurudisha zile pesa, Nikil kuw sikuwa na faham chochote maana ile acount nilifungua kwa ajil ya kupokelea mshahara tu na sikuwa nimeunganisha kwa sim zangu kuw mshahara ukiingia bas niwe napata notifications flani hivyo baada ya kumaliza mkataba wangu na kupata mshahara wangu wa mwisho nilienda nikakomba wote na ATM CARD nikaitelekeza. Kwa maelezo ya yule dad nikamwambia kuw inawezekana ila naomba niende benk kuhakik maana sijui lolote, ilibid nitoke na mvua mpak bank na nikaomba statement, ni kweli nikakuta kuna tumilion kadhaa, nikampigia yule dada kumjuza kuwa ni kweli pesa ipo ila nina ombi kwake..

Ombi langu kwake lilikuw hvi. Huu ni ukwel mtupu wakati nafanya kazi kwenye taasisi ile kuna kipind ilitokea tatizo la kufanya malipo ya mishahara hivyo kuna watu wacheche mshahara haukuingia kabisaa kwa mwezi ule na mim nikiwa mmoja wa wahanga, nilifuatilia sana mpaka mwez ukapinduka ila sikuwa nimelipwa pesa yngu, mwez uliofuata ukaingia mshahara wa mwez husika na ikaendelea hvyo kwa miez mingine.. mpaka namaliza mkataba wangu niliendelea kufuatilia lakin sikupata majibu. Sasa ilipotokea hii nikaona ni sehem sahih ya kudai haki yangu. Nikamueleza kila siku kilivyotokea kule nyuma akaomba afuatilie atarud kwangu kunipa jibu. Ndugu msomaji pesa yangu wala sikuifikilia mara mbil nikaitoa na kwenda kulipa madeni yanyu ya kodi na nilifanya hvi kwa ujasili maana ile ilikuwa pesa yangu halali kabisaa na kuwa simzurum mtu, pesa yangu nilitoa na y kwao nikabakiza nikisubir maelekezo yke.

Toka siku amenipigia sim na kusema ngoja afuatilie zilipita siku mbil kimya, ikaj y tatu mara week ikabid nimpigie, nilimpigia sana na sim haikupokelewa nilipiga tena na tena takribani miez mitatu ila sim hazipokelewi, natuma text kuomba kupewa muongozo namna y kurejesha hzo pesa ila sikupata majibu yoyote chanya.. Hvyo baada ya takribani miez sita kupita bila majibu niliamua kuzitumia zile pesa na sasa ni miaka mitatu sijawah pokea sim yka. Hili tukio huw linakumbusha juu ya uwepo wa Mungu na naamin Mungu yupo.
Acha uongo kiongozi
 
View attachment 2732530
Kama kweli Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo, wala hata tusingalisikia hyo ajali.

Ajali hiyo isingaliwezekana kutokea.

Kutokea kwa ajali ile ya Prado ilipaswa kuwa uthibitisho wako wewe kutambua kuwa huyo Mungu hayupo?

Waza kidhahania hapa:

Imagine kwamba ungalikuwa mhanga wa ajali ile na ukafariki

halafu waza kwamba kuna mtu alikutana na scenario kama hii yako uliyoihadithia hapa JF, kwamba kuna mtu yeye alipona katika ajali ile ya Prado na anasema kuwa aliamini kuwa Mungu yupo na anaupendo wote kwasababu yeye kapona ilihali wewe umekufa vibaya na ukaacha watoto wanaokutegemea wewe kwenye kila kitu.

Umeona jinsi ulivyo mbinafsi?
Usichokielewa ni kwamba unatakiwa uamini Heri na Shari zote ni kutoka kwa mwenyezi Mungu.. na pia sote ni wa Mungu na kwake tutarejea.

So kama ilivyonikosa mimi siku ile basi ni kwa uwezo wa Mungu na waliofikwa pia na ajali ile ni kwauwezo wake sababu yeye ndo amepanga kuwachukua kwa staili ile.. Ukute nao katika wale waliofikwa wangekuwa hai sai na ukawauliza swali kama hili nao wangekupa ushahidi wa matukio yao endapo ukute wenyewe tu ndo walifanikiwa na wengine waliobaki walipatwa na shida.

Ni hata wewe ukiambiwa utoe sababu au matukio yaliyofanya uamini hakuna uwepo wa Mungu naamini utatoa hoja ambazo sio sawa 100% nawenzio ambao nao mna msimamo mmoja (kwamba hakuna uwepo wa Mungu)



Sio wote tutafaidika kwa pamoja katika kila jambo mzee.
 
Sitosahau 2006 kaka anauza majan(bangi) mimi dogo janja tu nina miaka 19 sasa geto kwangu ndio ilikuwa stoo ya mizigo ya kaka sasa bwana watu wakalengesha Mara difenda hii hapa polisi kama kumi na balozi halafu kaka hayupo nipo mwenyewe tu aisee asikwambie mtu hofu niliyokuwa nayo moyoni sasa pale hom tulikuwa na mbwa mkali sana nadhan kaka alikuwa anamvutisha nyasi bas akawadindia polis anabweka vibaya mno polisi wakanambia mfungie choon mbwa sijui akili ilitoka wap kwa vile gheto langu lilikuwa uwan wazee wanawakaa fungia choon choo hakina komeo nje kwa hiyo nikamfungia gheto kwangu basi polisi wakaanza upekuz nyumba nzima gheto kwa kaka wakakuta bangi kidogo bas wakaridhika hata vyumba vingine hawakusachi mda wote mm naomba mungu wasije sema mtoe mbwa huko tusachi maana wangenipiga vibaya sana kwa mzigo uliokuwepo nami nilikuwa nawaambia chumban kwangu nilikomfungia mbwa huku kwenye bangi ni kwa kaka Mimi sihusiki na biashara zake bas tukaondoka hadi kituoni mimi nawaza hivi ingekuwaje polis wangejua kama nilikomfungia mbwa ndio stoo ya mizigo hakika huwa nasema mungu yupo kaka nwenyewe alipagawa alivyoambiwa polis wamenichukua akajua na mizigo yote imekamatwa alishangaa sana kukuta gheto kwangu kuko poa mbwa tu anabweka jaman mungu yupo.
Kwaio Mungu alikulinda usiende jela ili uendelee kuuza bange ? Au alikusaidia usikamatwe na bange zisikamatwe ili uendelee kuangamiza vijana ???
 
Nilishushwa kwenye gari (Prado) kisa nlikataa kukaa siti ya nyuma nikaenda kupanda basi kufika chalinze napata taarifa ile gari (Prado) imepatwa na ajali na wote waliokuwa ndani ya ile gari wamefariki..




Daah asee tangu hapo niliona uwepo wa Mungu kabisa na hakuna wakukuepusha/kukuletea majanga isipokuwa Mungu pekeake.
Kwaio wale waliokufa kwa upande wao waseme Mungu hayupo kwakua wamekufa sindio ??
Au ww Mungu anakupenda lkn wao hawapendi siet ??
 
Kwaio wale waliokufa kwa upande wao waseme Mungu hayupo kwakua wamekufa sindio ??
Au ww Mungu anakupenda lkn wao hawapendi siet ??
Hujanielewa..

Yani hata wao ktk maisha yao ukute kuna siku walishawahi kukutana na matukio yaliyowafanya waamini Mungu yupo.
 
Usichokielewa ni kwamba unatakiwa uamini Heri na Shari zote ni kutoka kwa mwenyezi Mungu.. na pia sote ni wa Mungu na kwake tutarejea.

So kama ilivyonikosa mimi siku ile basi ni kwa uwezo wa Mungu na waliofikwa pia na ajali ile ni kwauwezo wake sababu yeye ndo amepanga kuwachukua kwa staili ile.. Ukute nao katika wale waliofikwa wangekuwa hai sai na ukawauliza swali kama hili nao wangekupa ushahidi wa matukio yao endapo ukute wenyewe tu ndo walifanikiwa na wengine waliobaki walipatwa na shida.

Ni hata wewe ukiambiwa utoe sababu au matukio yaliyofanya uamini hakuna uwepo wa Mungu naamini utatoa hoja ambazo sio sawa 100% nawenzio ambao nao mna msimamo mmoja (kwamba hakuna uwepo wa Mungu)



Sio wote tutafaidika kwa pamoja katika kila jambo mzee.
Wewe ni muislam et ??
 
Kwa sababu kuamini ni kukubali uwepo wa hicho unachokiamini lakini kutokuamini ni kukataa
Ikiwa unaamini uwepo wa Mungu ata ikitokea hayupo you have nothing to lose, Lakini kwa kukataa kwako ikatokea yupo you lose everything.
Kwa mantiki hiyo ni bora kuamini
Sio kweli,

Ukiamini uwepo wa Mungu na ikitokea hayupo unakuwa umeshapoteza vingi sana.
Utakuwa umeibiwa pesa zako nyingi sana, utakuwa umepoteza muda wako mwingi sana.

Na hii ndiyo namna dini/iman za miungu zinavyofanya kazi.
Zinafanya kazi kwa kujenga hofu na vitisho tu.
Hyo ni psychology tactics.

Kwahyo unaposema kwamba ni bora uamini hata kama usipomkuta hutopoteza kitu unakuwa unakosea kwa sababu unao uwezo wa kutambua ukweli wa jambo hilo kuhusu uwepo wa Mungu.

Ni sawa na mtu akuambie kuwa anaitwa John na ni mwanamke mrembo sana, halafu akutake umtumie nauli aje nyumbani kwako ulale nae.

Then wewe (wakiume) useme kwamba "ngoja nmtumie tu nauli Huyu mwanamke aitwaye John aje nilale nae,
akiwa wakike ntalala nae na nitaenjoy ila akiwa wa kiume i have nothing to loose"

Sasa hii logical imekaaje?

Je hauna uwezo wa kutambua kwa hakika kuwa hakuna mwanamke aitwaye John?

Hapo ni sawa na habari ya Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote ambae kaumba ulimwengu huu wenye mabaya kuwezekana halafu huyo huyo anakutaka wewe umuombe ndiyo atimize uyatakayo.
 
Mungu yupo......nilipoteza watu wote muhimu nikiwa Bado nawahitaji nililazimika kujitegemea kwa chakula, malazi, mavazi n.k nikiwa bado sijafikisha miaka 15..Lakini kwa uwezo wa Allah leo ni mtu mzima Nina familia na kimaisha najiweza hakika Mungu yupo
Logical non sequitur
 
Sio kweli,

Ukiamini uwepo wa Mungu na ikitokea hayupo unakuwa umeshapoteza vingi sana.
Utakuwa umeibiwa pesa zako nyingi sana, utakuwa umepoteza muda wako mwingi sana.

Na hii ndiyo namna dini/iman za miungu zinavyofanya kazi.
Zinafanya kazi kwa kujenga hofu na vitisho tu.
Hyo ni psychology tactics.

Kwahyo unaposema kwamba ni bora uamini hata kama usipomkuta hutopoteza kitu unakuwa unakosea kwa sababu unao uwezo wa kutambua ukweli wa jambo hilo kuhusu uwepo wa Mungu.

Ni sawa na mtu akuambie kuwa anaitwa John na ni mwanamke mrembo sana, halafu akutake umtumie nauli aje nyumbani kwako ulale nae.

Then wewe (wakiume) useme kwamba "ngoja nmtumie tu nauli Huyu mwanamke aitwaye John aje nilale nae,
akiwa wakike ntalala nae na nitaenjoy ila akiwa wa kiume i have nothing to loose"

Sasa hii logical imekaaje?

Je hauna uwezo wa kutambua kwa hakika kuwa hakuna mwanamke aitwaye John?

Hapo ni sawa na habari ya Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote ambae kaumba ulimwengu huu wenye mabaya kuwezekana halafu huyo huyo anakutaka wewe umuombe ndiyo atimize uyatakayo.
Vivyo hivyo kwa upande wa pili ukikuta yupo imekula kwako.
To the hell forever.
By the way your examples are illerelevant, Mungu anakupa ukimuomba na anaweza kukupa usipomuomba ndio maana akawa muweza wa yote yaani anaweza kukupa ukimuomba na ata usipo muomba anaweza kukupa.
Au wewe unaelewaje kauli ya 'Mungu ni muweza wa yote ?'
Mimi ninavyoelewa muweza wa yote ni kuwa anaweza mambo yote mabaya na mazuri kwa kuwa yeye ndiye anayoyamiliki, Sasa nashangaa kwenye mifano yenu mingi etii mnasema huyo Mungu mwenye upendo wote mbona anaua watoto wadogo kwenye ajali ..guys come on, No one will leave forever and thus why ata hao best Scientists Kama Newtown , Archimedes etc washakufa, Huyo ndio Mungu Muweza wa yote wakati ana kuchukua uhai wa watoto wadogo wasio na hatia wakati huohuo kwa uwezo wake wanazaliwa watoto wengine wasio na hatia..Huoni kaweza yote ?
 
Vivyo hivyo kwa upande wa pili ukikuta yupo imekula kwako.
To the hell forever.
By the way your examples are illerelevant, Mungu anakupa ukimuomba na anaweza kukupa usipomuomba ndio maana akawa muweza wa yote yaani anaweza kukupa ukimuomba na ata usipo muomba anaweza kukupa.
Au wewe unaelewaje kauli ya 'Mungu ni muweza wa yote ?'
Mimi ninavyoelewa muweza wa yote ni kuwa anaweza mambo yote mabaya na mazuri kwa kuwa yeye ndiye anayoyamiliki, Sasa nashangaa kwenye mifano yenu mingi etii mnasema huyo Mungu mwenye upendo wote mbona anaua watoto wadogo kwenye ajali ..guys come on, No one will leave forever and thus why ata hao best Scientists Kama Newtown , Archimedes etc washakufa, Huyo ndio Mungu Muweza wa yote wakati ana kuchukua uhai wa watoto wadogo wasio na hatia wakati huohuo kwa uwezo wake wanazaliwa watoto wengine wasio na hatia..Huoni kaweza yote ?
Wewe hauelewi kwamba kuna utata hapo.

Uwepo wa kifo tu hyo ni contradiction kwenye uwepo wa Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote.

Kama kweli angekuwepo asingekuwa mkatili kiasi hicho cha kuruhusu vifo, vifo ambavyo vinaleta majonzi na simanzi miongoni mwa ndugu na jamaa baada ya kutenganishwa na wapendwa wao kupitia kifo.

Halafu unaposema muweza wa yote, haimaanishi kwamba ndio aweze hadi aanze kutokwa na akili asababishe vifo, kitendo cha kuweza yote halafu ukasababisha kifo tayari unakuwa unacontradict sifa ya upendo wote kwa huyo Mungu.

Unaelewa hilo?

Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angeshindwa kuumba ulimwengu ambao hauwezekani mabaya kutokea?

Katika ulimwengu huu naamini hakuna muweza wa yote.

Kama utabisha naomba unijibu kama Mungu anauwezo wa kuumba jiwe zito kiasi kwamba hata yeye atashindwa kulibeba.
 
Nyie ni ajali na masomo tu ndo mmeona ukuu wa Mungu?

Kiukweli siku ya kwanza kumpiga demu mashine the way nilivoinjoy akat napiz nilisema Mungu fundi,
Ubaya wote wa muonekano wa papuch lakini flavour iliyopo ni ya kipepee mno🙌🏻Yehova yire atukuzwe Mungu
 
Wewe hauelewi kwamba kuna utata hapo.

Uwepo wa kifo tu hyo ni contradiction kwenye uwepo wa Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote.

Kama kweli angekuwepo asingekuwa mkatili kiasi hicho cha kuruhusu vifo, vifo ambavyo vinaleta majonzi na simanzi miongoni mwa ndugu na jamaa baada ya kutenganishwa na wapendwa wao kupitia kifo.

Halafu unaposema muweza wa yote, haimaanishi kwamba ndio aweze hadi aanze kutokwa na akili asababishe vifo, kitendo cha kuweza yote halafu ukasababisha kifo tayari unakuwa unacontradict sifa ya upendo wote kwa huyo Mungu.

Unaelewa hilo?

Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angeshindwa kuumba ulimwengu ambao hauwezekani mabaya kutokea?

Katika ulimwengu huu naamini hakuna muweza wa yote.

Kama utabisha naomba unijibu kama Mungu anauwezo wa kuumba jiwe zito kiasi kwamba hata yeye atashindwa kulibeba.
Sentensi ya " Mungu anaweza kuumba jiwe zito kiasi ashindwe kulibeba' haina logic kwa sababu ukishasema anaweza kuumba that means anao uwezo, Ukiendelea kusema kiasi ashindwe utakuwa umeondoa ule uwezo yaani ety Mungu awe na uwezo alafu uwezo wenyewe uwe wa kushindwa it doesn't make sense and no logic at all huwezi kusema mtu fulani anao uwezo wa kutokuweza
Mfano sentensi inayo sema" John Ni kipofu hivyo John anao uwezo wa kutokuona " sentensi hii sio sahii, Inatakiwa useme John Ni kipofi hivyo aoni.
Sijui umepata logic.
 
Hicho ni kitabu kimoja tu, unapaswa utambue hiyo ni dhana ya kifizikia
Sawa ni dhana ya fizikia swali langu ni hiyo dhana haiwezi kuwa uongo?
Kwanza umeshasema dhana.
Dhana ndio inaunda dhanio na dhanio sio lazima liwe kweli
 
Back
Top Bottom