Tulienda shule kufanyaje kama hata hizi kazi za muda wanapewa watumishi wa serikali

Uchaguzi inabidi usimamiwe na watu wanaoaminika. Kama hawa wengine wanapotosha mambo ya kawaida, ndio uwakabidhi uchaguzi, wanaweza kuanza kujirekodi na kutangaza matokeo feki yakazua taharuki mitandaoni na kwenye jamii

Tanzania hatu-beti kwenye mambo ya msingi kama wanavyofanya kenya
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Mkuu samahani, ulishawahi kutumia BVR machine,
Kitu ambacho MTU anaweza iba pale ni min laptop TU,
Hakuna kijana jobless anayeweza kuhatarisha kazi yake kwa laptop yenye uwezo mdomo.

Kikwete, kazi kama hizi aliwapatia vijana ,Tena kama una degree ndio first priority. Ndio maana unaona jk anapendwa sana na vijana.

Lakini lengo linajulikana ni kwa ajili ya wizi wa kura , ndio maana Wana watumia walimu wanajua wataficha siri ya wizi wa kura,. Yale Yale ya JPM

Lakini kijana degree holder jobless, hawezi kufumbia macho wizi wa kura coz , haimunufaishi chochote.

Jobless ni waaminifu ,na wachapakazi damu Bado changa,
 
Mtumishi tayari ana vitu vingi vya kupoteza,ana familia inamtegemea na wengi umri umisha kwenda na tayari wana viapo hivyo ni vigumu kqenda against maelekezo yoyote.Sasa wewe ambaye huna cha kupoteza ukipewa hiyo ni risk,it is simple maths.
Suluhisho la ajira ni kuhakikisha tunazalisha vya kutosha na tunafungua viwanda vikibwa na vidogo dogo vingi.Mdio maana nchi kama China idadi ya watu ni mara 150 ya Tanzania but unemployment ni ndogo kuliko Tz.
 
Kwani siyo watanzania kwamba hawatapatikana Tena? Sema mifumo ya upigaji tu inatutesa watanzania.
Kwenye sensa madogo walizingua sana!
Kuna ambao baada ya kupewa ile 700k wakakimbia nchi na kitendea kazi - tablet; wengine walivurunda kazi walivyoitwa kurekebisha makosa wakatokomea mikoa ya mbali; kuna wengine makasiriko yalikuwa makubwa kwa kuwa hawajazoea kufokewa na kukaripiwa; ...
 
FYI watumishi wengi wa serikali ni wafuasi wa upinzani kimya kimya
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Kwan hvy vifaa watu wanapewa kukaa navyo makwao?
 
Mbona usemacho mkuu kimefanyika Kuna kesi inanguruma huko mahakamani kuhusu kupinga huu mchakato wa uchaguzi huo.
Fatilia vizuri.
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Wewe jamaa muongo uandikishaji wa daftari la uchaguzi wa serikali za mitaa ni manual unaandikwa jina na pen kwenye dodoso.
akuna picha Wala aupewi kadi ni jina TU linaandikwa kwenye limu ya sh 100 kazi imeisha Sasa hapo serikali inaogopa kuibiwa limu na jobless?.
Pili hivo vifaa uvitajavyo sijui vitaibiwa bvr, vishikwambi sio kweli mbona sensa sisi jobless tulifanya Nini kilipotea ? Na vishikwambi tulipewa.
Na uchaguzi mkuu wa 2015 mbona pia sisi jobless tulifanya kuanzia mchakato wa uandikishaji hadi wa kusimamia upigaji kura tulizingua wapi?.
Tena kipindi kile bvr kit ilikuwa ya thamani sana ukilinganisha na hizi za Sasa zile zilikuwa Zina PC sio hizi nyingi za vishikwambi vya pluton vya kichina vinavyouzwa kikuu kwa mafungu.
Kifupi jobless atuna Cha kukiiba hapo sema ni roho mbaya ya serikali tu .
Wanapenda kuwaona graduate wakikosa hata pesa ya kula ikiwezekana wafe njaa kabisa wasiwaone kwenye nchi hii.
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Sio kweli mkuu! Hamna kitu kigeni kwenye hizo mashine hata wewe unawez kuzioperate kabisa! Ni sheria za uchaguzi zinawataka wafanye hivyo! Ndo maana mnaambiwa tupate katiba mpya
 
Eti walisema sisi ambayo hatuna ajira tunaweza kuharib na hawana pa kutukamatia tukiaribu
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Siyo kweli ulichoandika yaani hadi wanaona una sifa za kusimamia uchaguzi/uandikishaji halafu wasijue wapi watakupata seriously?

Kwa namna hiyo Sasa watekaji watakuwa Wana kamatwa vipi?
Itakuwa ni serikali ama ni kijiwe tu Cha kahawa.
 
Inasikitisha sana vijana ni wengi mtaani ila wanapewa kazi watumishi afu vijana wanahaha mtaani,hili taifa la ajabu sana
 
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
Sasa Kwa nn walituambia tufanye application?
 
Kwa nn walituambia tufanye application ya iyo kazi tukapoteza muda wetu???
Mfumo wa uandikishaji uatumia BVR na Vishikwambi ambavyo ni vya bei ya juu Kwahyo wanaogopa kuwapa watu ambao sio watumishi wasije kuondoka na vifaa vya serikali ndio maana wanatumia watumishi ili wakialibu wanapakuwataftia.
nn
 
Sasa uandikishaji na wizi wa kura wapi na wapi, kinachoendelea sasa hivi ni mchakato wa kuandikisha wapiga kura na siyo kupiga kura, by the way mashine zinazotumika sasa ni mpya siyo zile za zamani zenye laptop kwa sasa ni tablet na zinaambatana na vifaa tofauti tofauti kama power bank, external hard drive, power adapter, type c charger, nk ambavyo vinaibika kirahisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…