Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tena ya kienyeji ndo wanapasuka hatari mno.Hii kitu wengi hawajui ila kwenye madawa yawe ya kienyeji na hizi za kisasa watu wanapigwa sana.
Mjini akili tu unapata helaTena ya kienyeji ndo wanapasuka hatari mno.
Niliwakaz kaza kimtindo enzi za ubora wangu.Bila shaka hiyo laki mbili ulienda kula mbususu ya mrembo uliyekuwa wamfukuzia 🤣🤣🤣🤣
Basi ulifanya vizuri maana kwa wakati huo ndio kitu roho ilipenda. Bora utumie pesa kwako mwenyewe kuliko kukopesha ndugu alafu mkagombanaNiliwakaz kaza kimtindo enzi za ubora wangu.
Wabongo tunaacha mapapa wezi wa taifa halafu wanaleta unafiki kwa sie wazee wa genjiFisadi naye ni mwizi, tena mwizi mkubwa.
Unazungumziaje maisha ya Seth wa IPTL, maisha ya late Lowasa, maisha ya ..., maisha ya madelu.
Sio powa kaka....watu wanaropoka tu.😅😅😅😅
Kumbe udalali nayo ni taaluma.Wewe ni tapeli kishoka na sio dalalali, unachafua taaluma za watu
akili ya mtu, wengine hujiwekeza pesa hizo kwa uwoga wa maisha ya kesho wengine huzitumbua kwa kuamini kesho watapata tenaMara nyingi pesa zisizo za jasho Huwa haziwezi kukuimarisha kiuchumi.
Utaishia kulewa, kuvaa Nguo, kula kwa anasa na kushughulikia wanawake.
Hii inatokana na fikra kuwa hata kesho utapata pesa Tena, kumbe sivyo!
Duh 😁😁😁Hebu angalia yaani wanampangia maisha mtu mwenye mali yake
Kuna siku cousin yangu aliita usaili wa madereva garage
Madereva wakajitokeza, wakiwa wanasubiri kuitwa wakawa wanaongea zao
Hapo alikuwa amekaa mtoto wa boss akiwasikiliza na kucheka kwa story zao
Basi akaja dereva mtarajiwa akakaa nae basi kwa ukiherehere akawauliza waliomtangulia akasema jamani kuna upigaji lakini hapa au ni ka mshahara tu?
Yule dogo mtoto wa boss akaenda kumtonya anaefanya interview
Kuna majeneZa napo ukiujua ukwl utalia sanaAngenishona haswa kama fala mmoja(sijui nimuite mjanja maana alinipiga parefu) aliwahi niotea akanibamiza kweli kweli na nilikuwa safarini. Nadhani kwenye dawa napo watu wanapigwa sana.
Nipe mbinu mliyojua mkuu maana tunapigwa sana hukuJuzi nilikuwa kwenye mgahawa na rafiki zangu. Tumemaliza kula tukaletewa bili ambayo ina mashaka na mhudumu akaleta risiti ya TRA.
Tukamwambia ondoka tutakuita. Tukaenda kufuatilia bei, tukakuta kaongeza elfu 17.
YamefanyajeKuna majeneZa napo ukiujua ukwl utalia sana
Kuna upigaji kama idara nyingineYamefanyaje
Upigaji upo kila nyanja mkuu, madalali ndio chamboKuna upigaji kama idara nyingine
Niliuliza wahudumu wengine bila yeye kujuaNipe mbinu mliyojua mkuu maana tunapigwa sana huku
Ndio maana Kuna mpaka kampuni za udalaliKumbe udalali nayo ni taaluma.
Ukifata maandiko unalaza familia njaa kabisa lazima ule kwa haki, lakini ukiona unaminywa sana lazima upigane ugawane kidogo na mwenzako.....japo wanasema faida iwe robo tatu ya mtaji.Sio powa kaka....watu wanaropoka tu.
Hauwezi kuendelea kwa fedha za dhuluma ,udalali ni udhulumati tu.Bwana bwana miaka ya 2018-2020 kuna goli(duka) la magodoro nilikuwa nauza maeneo ya kinyerezi location ya duka haikuwa mbaya ilikuwa nzuri sana opo road kabisa na wanunuaji wengi walikuwa kipato cha kati.
Sasa bwana ilikuwa akija mteja ni lazima apigwe udalali kama bei ya kuuza ni tsh 200,000 basi godoro ningeliuza tsh 230,000.Ilikuwa godoro halitoki bila mimi kupata hata tsh 15,000 minimum
Nakumbuka kuna mzee mmoja mshabiki wa liverpool alikuja akanikuta nimelala akaniuliza "godoro 5 kwa 6 inchi 8 bei gani" mimi kwa wenge la usingizi nikaropoka tu "laki nne" wakati godoro bei yake ni tsh 210,000 yale ya kitambaa tunaita kashata.
Yule mzee bwana akaingia kwenye kiraumu chake akivuta kibunda cha milioni akanichomolea laki nne akaniuliza "na usafri vipi hakuna kirikuu??" nikamwambia "bodaboda mbona inabeba nalifunga freshi utanipa tsh 20,000 ya usafiri"...mzee akalipia usafiri akanielekeza kwake nikaita boda nikampa tsh 2000(hiyo sehemu gharama yake ni buku) kwahiyo nikawa nimepiga mshindo wa tsh 208,000.
Nilijifunza kitu kuna watu wana hela kiasi kwamba hata ukiwapiga ni sawa na unajiibia mwenyewe imagine hiko kilikuwa kipindi cha anko MAGU.
Jana nilikuwa maaneo ya BL park nachek game ya aseno nikamuona yule mzee niliyemdalalia tsh 200k bado anadunda tu wakati mimi bado najitafuta hahahaha.
Najua mpo wenzangu wengi ambao mmepiga sana mishindo ya udalali(Genji) na bado life ni vita karibuni.