Tuliopiga sana pesa za udalali kwenye biashara na bado life gumu tukutane hapa

Tuliopiga sana pesa za udalali kwenye biashara na bado life gumu tukutane hapa

😂😂😂😂😂😂 Alikuwa anakushona kinoma. Maana dose tatu ungenunua 36k angefunga faida yake ya 33K.
Angenishona haswa kama fala mmoja(sijui nimuite mjanja maana alinipiga parefu) aliwahi niotea akanibamiza kweli kweli na nilikuwa safarini. Nadhani kwenye dawa napo watu wanapigwa sana.
 
Bwana bwana miaka ya 2018-2020 kuna goli(duka) la magodoro nilikuwa nauza maeneo ya kinyerezi location ya duka haikuwa mbaya ilikuwa nzuri sana opo road kabisa na wanunuaji wengi walikuwa kipato cha kati.

Sasa bwana ilikuwa akija mteja ni lazima apigwe udalali kama bei ya kuuza ni tsh 200,000 basi godoro ningeliuza tsh 230,000.Ilikuwa godoro halitoki bila mimi kupata hata tsh 15,000 minimum

Nakumbuka kuna mzee mmoja mshabiki wa liverpool alikuja akanikuta nimelala akaniuliza "godoro 5 kwa 6 inchi 8 bei gani" mimi kwa wenge la usingizi nikaropoka tu "laki nne" wakati godoro bei yake ni tsh 210,000 yale ya kitambaa tunaita kashata.

Yule mzee bwana akaingia kwenye kiraumu chake akivuta kibunda cha milioni akanichomolea laki nne akaniuliza "na usafri vipi hakuna kirikuu??" nikamwambia "bodaboda mbona inabeba nalifunga freshi utanipa tsh 20,000 ya usafiri"...mzee akalipia usafiri akanielekeza kwake nikaita boda nikampa tsh 2000(hiyo sehemu gharama yake ni buku) kwahiyo nikawa nimepiga mshindo wa tsh 208,000.

Nilijifunza kitu kuna watu wana hela kiasi kwamba hata ukiwapiga ni sawa na unajiibia mwenyewe imagine hiko kilikuwa kipindi cha anko MAGU.

Jana nilikuwa maaneo ya BL park nachek game ya aseno nikamuona yule mzee niliyemdalalia tsh 200k bado anadunda tu wakati mimi bado najitafuta hahahaha.

Najua mpo wenzangu wengi ambao mmepiga sana mishindo ya udalali(Genji) na bado life ni vita karibuni.
Bila shaka hiyo laki mbili ulienda kula mbususu ya mrembo uliyekuwa wamfukuzia 🤣🤣🤣🤣
 
Huu ni wizi huyo muuzaji alikuwa anataka kukuibia wala sio udalali huo


Mkuu ulichokuwa unafanya ni wizi wala sio udalali.
Udalali ni hali inahusisha mtu wa kati kupata kitu .
So bei ya bidhaa inajulikana na bei ya udalali inajulikana .
So mteja anamlipa mwenye mali fedha yake na dalali anapewa commision yake.
Yaani unakabidhiwa duka uuze bidhaa wewe unapandisha bei unasema udalali? Wewe ulikuwa unafanya wizi wala sio udalali
Ni wizi ndio ila ndio cha juu chenyewe.
 
Wewe ni mwizi na kamwe hautafanikiwa kujikwamua kimaisha kwa kutumia mbinu hizo.Utabaki masikini tu kwakuwa kwenye kichwa chako hakuna mawazo mbadala ya namna ya kujipatia kipato zaidi ya kuiba.

Pia hiyo fedha unayodhulumu haiwezi kukaa wala huwezi kufanyia jambo la maana kwakuwa umeipata kirahisi,hivyo inaondoka kiraisi:EASY COME, EASY GO!
Fisadi naye ni mwizi, tena mwizi mkubwa.

Unazungumziaje maisha ya Seth wa IPTL, maisha ya late Lowasa, maisha ya ..., maisha ya madelu.
 
Piga kwa sababu hata wewe kuna mahali unapigwa hivyo hivyo.

Kuna dawa juzi nimeenda kuchukua inauzwa tsh 1,000 ila yule dada mfamasia akasema 12K, nikacheka nikamwambia dada mi mwenyewe mfamasia tena mfamasiala haswa nipe bei nilipie nichukue changu, kwa aibu sana akaniuliza unahitaji ngapi, nikatoa 10K nikamwambia kata 3 nipe chenchi. Akarudisha 7,000 yangu nikasepa. Ningekua sijui bei ningepigwa.
😅😅😅 pole yake.
 
Juzi nilikuwa kwenye mgahawa na rafiki zangu. Tumemaliza kula tukaletewa bili ambayo ina mashaka na mhudumu akaleta risiti ya TRA.
Tukamwambia ondoka tutakuita. Tukaenda kufuatilia bei, tukakuta kaongeza elfu 17.
 
Back
Top Bottom