Tuliopitia Vita Na Chuki Makazini Tushirikishane Hapa

Utajuaje nani wa kumtreat vipi? Mzee kazini wabaya wabaya tu na wapo. Ili kujua yupi wa kuishi naye kwa style ipi lazima uwe na information. Kazini information ndo survival yako ili uchange karata zako vizuri. Kuna ofisi watu wa chini ndo wanaiformation zote maana wao huwai na kuchelewa kutoka kazini na hujua matukio mengi zaidi. Hata barua za application wao ndiyo mara nyingi wanaipokea. Tena akikupenda anaweza hata kukwambia kuwa badilisha hadi title ya ombi la kazi. Au akakwambia kuwa barua yako kampe nani.
 
Unatakiwa uwatreat wote vizuri tu,usimchukie mtu bila sababu au kwa maneno yakusikia "Hearsay" mtu mzuri na mbaya kwako utakuja kuona wewe mwenyewe.
 
Mzee tembea uone. Kuna wengine makazini hawakosolewi wala hawabishiwi yaani siyo bosi lakini usimkosoe mbele za watu au ktk kikao chochote yaani ni bora umuache amalize kuongea halafu wewe usifanye au kuamini alichosema lakini siyo kumkata moto mbele za zatu. Kwanini? Kwanza umri wake umeenda elimu yake ndogo ashamaliza mapambano. Wewe kijana bado una nguvu za kuoambana, ukimkosoa unatishia usalama wa kazi yake. Hiyo kazi imebeba wengi nyuma yake. So unaweza ukajifanya una mtreat mtu kama anavyokuja ukafanya formidable mistake kwa watu kama hao. Anaweza kuundia zengwe la hatari.

Ngoja nikupe mfano uliopo ktk familia. Kuna mwamba alikuwa ktk tawi la ofisi nyanda za juu kusini. Sasa kafanya kazi vizuri sana kwa miaka mingi. Kapata promotion. Kapelekwa dar, kala nyumba, usafiri, dereva na ofisi. Siku anatambulishwa ofisini na kukaa tu ktk kiti hapo hapo maluwe luwe yakaanza mpaka tunavyoongea saa hizi amerudi alipotoka. Ila angesanuliwa either angekataa au angejiandaa. Information ni nzuri makazini
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji119][emoji119]

Ni noma Mkuu
Nilifanya kazi na "WAPALE" kwenye ofisi Moja

Aiseee Hawa watu ni noma sana aisee

Sitakuja kusahau jamaa ni wanafki sana

Yaani ni hatari...Wana majungu sijwahi ona...
 
Ni hatari
 
Mtu asipokua na information zako hata kukuloga inakua ngumu,
Japo unaweza kulogwa ila lack of information inapunguza uwezekano
 
Kazi yangu ya kwanza natoka chuo nilipigwa spana mpaka nikasarenda.

Ilikua hivi nilipata kwa njia ya kujuana R.I.P mzee cosmas ndio alinifanyia mpango kwa kaburu.

Kwa sababu pande lilitoka kwa CEO mwenyewe kuanzia HR alinipa uzito.

Sina uzoefu wowote japokua ni kitu nimekisomea kwelii niliteseka balaaa ( Ili uelewe ofisi kuu zipo mjini ila kazini ni ngorongoro)nikawa naamishwa vitengo tuu kila wiki kitengo kipya na bdo naonekana sijui kitu ilhali nilikua napambana nisiwe mzigo.

Mwisho wa siku nikanyoosha mikono juu nikaandika barua kwa amani nikaondoka.
Sisahaugiiii😂😂😂😂😂nyie mnasema wahindi wanatesa hamjakutana na wabongo elimu ndogo cheo kikubwa kila saa anaona nafasi yake inaenda ilhali we huna habari nae kabisa.
 
Supervisor wangu nimemzidi elimu, nimemzidi/tunafanana salary. Kwa miaka mi4 sasa tunaishi na ww3.

Mm sina urafiki na workmates, nipo busy na kazi then narudi home lakini tabu iko pale pale. (chuki zipo tu hata ufanye nn, trust me hata Mungu anachukiwa na baadhi ya watu).

I will never Quit, I will never resign. (Siwezi kukata tamaa na kurudi nyuma kwa sababu ya mtu mmoja).

Kila sehemu kuna changamoto zake, changamoto haziishi. Safisha nafsi, kuwa mtu mzuri na mtegemee Mungu katika kila hatua.
 
Siku nyingine msanue kuwa huna inshu na kitengo chake na hata ukipewa hautakikubali. Mchane serious. Huwa Wana woga. Ila ukimchana kama mwelewa anakuelewa. Kuna mmoja alichanwa akawa mshkaji kinoma.
 
Jambo la Msingi nililojifunza ni PRIVACY& CONFIDENTIALITY Ni muhimu Sana wakati wa kujumuika na workmates. Lingine ni KUTOKUMUAMINI YEYOTE KWA WAKATI WOWOTE kwani sehemu kubwa ya Chuki na vita makazini husababishwa na mtu kuwa na DETAILS zako.
Sawa sawa! You are now mature!
Umekua!

Usiruhusu watu unaofanya nao kazi wajue maisha yako binafsi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…