Tumalize Ubishi: Tundu Lissu nitajie IGA au BIT inayoeleza kutakuwa na HGA alafu bado inayoenesha kiwango cha uwekezaji na mgawanyo wa mapato?

Asante!!
 

Attachments

  • F05C7993-9B73-4179-AC36-B0489A9D35FC.jpeg
    60 KB · Views: 3
Huna habari tumewapa bandari DP World kwa sababu sisi ni wajinga wasio na akili wala uadilifu wa kusimamia kilicho chetu?

Sawa, lakini mbona hatutumii akili zetu wenyewe kuzisimamia taasisi zetu kama bandari hadi tuwakabidhi Waarabu?
Sina habari hiyo. Jibu mada iliyopo, usihamishe magoli.
 
Kuna muda sio mrefu unakuja mbeleni hawa wanasiasa watashindwa kupata wajinga wa kuwadanganya huko kwenye mikutano ya kisiasa.

Mtaji mkubwa sana wa wanasiasa ni wale wanaowadanganya huko mikutanoni, na hao wanakwenda wakipungua kila siku kwani jamii inazidi kuelimika na google inatumika vizuri katika kupunguza idadi ya wajinga wanaodanganywa.

Lissu anajichora kuzunguka kote anapopita na kuongea pumba za kisheria.
 
Sio masuala mepesi kama sentensi zako zinavyoyaongelea. Bungeni unapita ufupisho wa mkataba mzima kumbuka biashara ni pana sana ya bandari na huko kwenye mikataba ya ukodishaji na upangishaji ndio kila kitu kinawekwa.

IGA inaweza kuwa na kurasa 30 tu lakini Consession na Lease zinakuwa na kurasa mpaka 200, kila kitu kinawekwa humo kwa kirefu.
 
Na wewe ungetuletea IGA nyingine zaidi ya hii yetu kama zinapatikana kirahisi hivyo.
 
Hayo mapato ya 27 trillion yapo wapi ktk IGA
 
Kwa kumbukumbu zangu, hili swali ungemwuuliza aliyesema Tanzania itaingiza mapato trillioni kazaa. Hili sio swali la kumuuliza Lissu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…