Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu. Magufuli na Lipumba ni wagombea halali

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu. Magufuli na Lipumba ni wagombea halali

Kwani Tume wajibuje? Hahahaha chadema bhana hahaha hata Membe alihakikiwa kule kule majimboni wadhamini wake kwanini Lissu hakunuwekea pingamizi? Lissu amesoma sheria bila kusoma kanuni hahaha

Na picha je? HahahaView attachment 1549300
Unajichekesha nini mtoto Wa kiume mbele za kadamnasi? Tukueleweje? Halafu ungejibu hoja yako politely tu.
 
Hizo sheria hazifanyi kazi wanaccm wanapopita bila kupingwa?
Sijui kwa sababu hakuna ushahidi wa kuwa kuna wagombea wa CCM wamepita bila kupingwa. Jana tume ya uchaguzi ilitahadharisha kuwa hakuna mgombea yeyote aliyekwisha pita bila kupingwa. Hata hivyo ikionekana wana CHADEMA wamazikosea sheria na kanuni hizo, basi sheria itachukua mkondo wake

Swala moja linaloonekana kujirudia sana ni kuhusu picha za wagomea. Ila elewa kuwa kuambatanisha picha hakuna maana ya kubandika picha kwenye fomu. Unaweza kupelea form kwenye bahasha moja na picha kwenye bahasha nyingine mradi umekabidhi bahasha zote kwa pamoja. Watui wengine wanalalamika tu kuwa hakuambatanisha picha kwa sababu tu ya kutokubandika picha kwenye form.
 
Kwakweli naanza kuamini kuwa Upinzani hautakaa ushike dola bila katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. "Nikuteuwe Mimi, nikupe gari, nikupe nyumpa, nikupe mshaara na pisho, harafu eti umtangaze mpinzani kuwa mshindi!!" Hayo siyo maneno yangu Bali nimemnukuu "Kichaa fulani" akijiongelesha.
 
Mbona Magufuli hajaenda kuyajibu? Hakutakiwa kuwasilisha utetezi, bali afike ofisini.
Hizi sheria na kanuni haya majamaa huwa yanatunga kwa ajili yetu sie kina kajamba nani tu,zikiwarudia wanarukaruka kama mahindi ya bisi.

Fambafu kabisa.
 
Upinzani una dalili zote za kushindwa vibaya sana. Tuache utani lissu ni mwepesi sana kwa Magufuli. Alishindwa jabali la siasa mzee lowassa.
 
Lissu katetemesha viumbe
Ikibidi tume ya uchaguzi ilipize kisasi kwa kumpingamiza mr lisu ilu liwe fundisho kwa wagombea wengine siku za mbele wasijaribu kutingisha kiberiti,maana kiberiti kiko full.
 
Sheria na kanuni za uchaguzi zinazosimamia uteuzi wa wagombea na mapingamizi dhidi yao ni hizi hapa: Uchaguzi 2020 - Tume ya Uchaguzi yatupilia mbali mapingamizi ya Tundu Lissu. Magufuli na Lipumba ni wagombea halali. Ni kifungu gani kilichokiukwa kama Lissu hakutaka kufurahisha wafuasi wake tu ambao anajua hawasomi sheria zenyewe bali kukubali kila anachowaambia?
Kifungu cha 32(1)(b)(c) cha cap 343
Kifungu Cha 38(4)(B), kanuni ya 37(4)(a) inataka picha nne za passport za rangi.
Kifungu 38(5) cap 343
 
Ikibidi tume ya uchaguzi ilipize kisasi kwa kumpingamiza mr lisu ilu liwe fundisho kwa wagombea wengine siku za mbele wasijaribu kutingisha kiberiti,maana kiberiti kiko full.
Muda ushapita
Time barred
 
Hatuwezi kutumia akili za kichaa kuongoza nchi, huyo huyo kasema tume inaweza kuwapa mamlaka wasimamizi, bado tena anasema sio harali,
Pili kuhusu picha
Naomba unipe tafasiri ya
pasport size?
full size na?
half size?
Medium size?
Big size
Je maana yake ni lazima uangalie mbele au ni kipimo cha ukubwa wa picha?

Kuhusu kuangalia mbele ni masharti ya taasisi au hitaji husika na sio kiwango cha ukubwa wa picha. Na ndo maana tunasema tundu ni kichaa ila bado mnamshangilia tu. Alisema magufuli katoa rushwa ya laki moja bado mkashangilia. Nyie ni mazuzu tu.

Ukitaka kujua tundu anamuogopa magufuri, toka jana usiku anatafuta makosa ya magufuli tu siku nzima na nadhani hajalala.

Kaka hapa kichaa ni wewe, haujui hata unachoandika kama Magufuli unaandika Magufuri, halali unaandika harali uko sawa kweli, na kwa akili yako unadhani Lissu alitarajia Magufuli ataenguliwa?Mnafundishwa sheria kwa vitendo, next time watarekebisha sheria, na ndio lengo.

Mnakuwa wajinga wa kutafsiri hata sheria, ajabu wengine ni Judges pale tume, na Lissu ana Bachelor moja tu, lakini anawafanya wanaonekana wapuuzi mbele ya "wazamivu wa sheria".

Shukuru kupata mtu kama huyu.CCM pia wapo lakini wameamua kuwa waduanzi.

Kama wewe ulivyoamua,yani hata vitendo vya 'kibabe' kama vya kuengua wapinzani hakuna siku utasema kuna kosa.

Bakia hivyo hivyo halafu nenda msikitini au kanisani ukaseme Mungu kawateua, na wewe ni mja wake mpenda haki....

Hauwezi hata ku feel guilty kuwa kwa sababu za kijinga za tume na mipango yenu wameshakufa watu watatu ukerewe 1,Tunduma 2.
Hauoni kabisa kila jimbo wanasumbuliwa watu wa CDM kupokelewa form.

Jaribu kidogo kupenda haki, au labda hiyo siku ya uchaguzi mama yako auwawe bahati mbaya akiwa katika shughuli zake akikutana na vurumai la wizi wa masanduku ndio utarudia sense yako.

Ujinga wa wengi kama wewe kwa maslahi ya wang'ang'ania madaraka ndio umetufikisha hapa.

Tunataka free and fair election ashinde anaeshinda basi.
 
Pigo jengine kwa Wana Sacco's,kila wanachofanya wanashindwa, Chadema ni losers [emoji23][emoji1787]
Ongeza ongeza maarifa kichwani, ushindi umepatikana na unapatikana kwa awamu, mfano form tumepeleka NEC wamekagua mpaka usiku, na hazikupelekwa majimboni, mpaka hapo sheria imeonekana kutokuwa sawa, Magufuli kajifunza wapi anatakiwa kukabidhi form zikaguliwe na wewe pia umejifunza. Ushindi ni pamoja na kuelimisha wapuuzi kama wewe.
Kwa mfano hapa nachukua ushindi, kiswahili fasaha ni "jingine" sio "jengine".
Sasa kiswahili umesoma tangu darasa la kwanza mpaka ulipofikia na bado msamiati unakusumbua,kweli unaweza kuelewa vitu complicated kama sheria na " ushindi"?
Una cheti kipi kwanza la saba, form IV,formVI au elimu ya juu?
 
Mapingamizi uchwara ya mwanasheria muongo muongo wa Chadema.
 
Mkuu Lisu hapa kaonesha umbumbumbu!

Unaposema form zimehakikiwa na wasimamizi wa uchaguzi majimboni hao ndio NEC yenyewe ndio maana hata matokeo ya uchguzi yanaanza kutolewa huko.

Alipocheleweshwa pale kwenye tume ile juzi tume walitoa maelezo kwamba waliopitisha form zao huko majimboni hajakaa sababu tume haikupata shida ya kuanza kukagua maelfu ya hao wadhamini.

Kwahiyo wote tangu kina Membe ni wajinga ila yeye Lisu tu ndio alikuwa na akili?
Fomu za Rais hazipaswi kuhakikiwa na wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo
Maelekezo ya tume yanakinzana na sheria ya uchaguzi cap343 kifungu cha 126 hivyo hayapaswi kukinzana na sheria, na kikawaida subsidiary legislation haitakiwi kukinzana na Act na ikitokea mkanganyiko Sheria ya bunge ina prevail hivyo maelekezo ya tume hayana nguvu tena
Sheria ya uchaguzi Sura 343 kifungu cha 32(1)(b)(c) kinamtaka mgombea Urais kupeleka fomu za uteuzi tume (NEC).
Hivyo maelekezo yaliyo kwenye sheria ndiyo yakufuata.
 
Kifungu cha 32(1)(b)(c) cha cap 343
Kifungu Cha 38(4)(B), kanuni ya 37(4)(a) inataka picha nne za passport za rangi.
Kifungu 38(5) cap 343


Hiyo 32(1)vifungu vidogo (b) and (c) vinataka majina ya wadhamini na namba za kadi za kupigia kura za wadhamini hao. Lisu hakuwa na proof yoyote kuonyesha kuwa hyo hsyskutekelezwa. kazi ya kutafuta wadhamini ndiyo kupata majina na namba zao. Mtu mwenye akili timamu hawezi kuja na sababu hizo
1598508296377.png

Kifungu cha 38(4) kifungu kidogo (b) k pamoja na kifungu cha 38(b) vinahusu uteuzi wa wagombea wa Ubunge, siyo wagombea wa urais.

1598509309737.png

Picha za pasport za rangi zinaambatanishwa pamoja na form siyo kuwa zinabandikwa kwenye form.


Unaona jinsi watu wanavyotafsiri shera vibaya halafu wanaishia kulalamika kwenye internet muda wote
 
Fomu za Rais hazipaswi kuhakikiwa na wasimamizi wa uchaguzi wa majimbo
Maelekezo ya tume yanakinzana na sheria ya uchaguzi cap343 kifungu cha 126 hivyo hayapaswi kukinzana na sheria, na kikawaida subsidiary legislation haitakiwi kukinzana na Act na ikitokea mkanganyiko Sheria ya bunge ina prevail hivyo maelekezo ya tume hayana nguvu tena
Sheria ya uchaguzi Sura 343 kifungu cha 32(1)(b)(c) kinamtaka mgombea Urais kupeleka fomu za uteuzi tume (NEC).
Hivyo maelekezo yaliyo kwenye sheria ndiyo yakufuata.
Ama unazisoma sheria hizo vibaya, au untaka ziwe na maana unayotaka wewe. Kama wewe ni mwanasheria, basi inawezekana taaluma ya sheria Tanzania nayo inaanza kwende ICU. Ndiyo maana mwanasheria msomi Lissu anaongea mambo kama haya.
 
Back
Top Bottom