Tumefanywa Misukule muda mrefu. Lema tukomboe

Tumefanywa Misukule muda mrefu. Lema tukomboe

Ukute hauna hata uhakika wa kupata milo miwili iliyo kamilika kwa siku.

Nyumbani kwako kisamvu na ndondo kila kukicha alafu unacho thamini ni kununua mashati ya kijani na njano.View attachment 2557745

Sasa hii imekua personal, sitaegemei member wa miaka mingi kama wewe unaishiwa arguments na kuanza kumshambulia mtu binafsi.

Kwahiyo kama mimi ni kapuku sina mbele wala nyuma, huoni wewe ni mpumbavu kulazimisha nitete mtu anaepata laki 8 kwa mwezi? 😂

I am surrounded by idiots, with no logic or reasoning capability. 😥
 
Acha uchumi uchwara, kwenye uchumi hakuna lazima kuna kitu kinaitwa ceteris paribus.

Sasa kama huwezi kuwa na rasilimali watu wa kutosha katika utumishi wa umma, huo ufanisi utatoka wapi!? Bado hata waliopo bado hawafanyi kazi inavyotakiwa, ndio hao manesi wasioheshimu wagonjwa, walimu wanaojua kupiga tu, na ujinga mwingine mwingi. Ebu angalia, serikali inatumia bilioni 500 kwa mwaka kununua magari ya walafi (viongozi wasio na tija). Badala yake, ingeongeza walimu na manesi. Yaani, hatuna vipaumbele.
 
Utakataa kwa sababu za kisiasa, lakini hizo ndio principal za kiuchumi,, unapopandisha mishahara ya watumishi,, cost lazima zipande, serikali haiwezi kuajiri watu zaidi ya milioni,
Katika watanzania milioni 30,, it means milioni 29 itabidi waingie private sector, au kujiajiri kwa sector zisizo rasmi ikiwemo bodaboda, mamantilie, etc.
Lema yeye anadhani serikali inawezs kuwapa kazi watu milioni 30,na iwalipe kima cha chini milioni 5,, 🤷
in short hata waliopo sasa ni wengi na pato kubwa linaishia kwenye mishahara, tunahitaji redundance.
 
Ona aibu wadogo zangu nimewatftia mwenyewe kazi anayenza kazi na certificate ya ualimu analipwa tsh 540,000/ kabla hajakatwa akikatwa anabaki na 476000 Kama sijakosea kdg,,,huo ndo mshahara wa kumpa mtu?

Yaani kwa mwaka havuki 4,900,000/ huo si umaskini wa Hali ya juu, hata majeshini nmeingiza wadogo zangu mishahara yao naijua kinachowabeba ni posho zao tu angalau vinginevyo mishahara yao ni vichekesho, viinua mgongo vyao unaweza ukalia ukiona au kuambiwa.

Mzee unasema uongo kwa manufaa ya Nani!!! Hizo 800,000 unazoona nyingi ni kwa mtu aliye na ka degree au amakaa kazini muda mrefu Sana pengine anakaribia kustaafu enyi walafi tuachieni nchi yetu tuitengeneze
unafikiri alipaswa alipwe kiasi gani ?
Wa Digrii alipwe kiasi gani?
Masters alipwe kiasi gani ?
PhD alipwe kiasi gani?

Na hiyo iwe hivyo kwenye kada zote au ualimu pekee Maana wengi wao wameingia baada ya kupata dsivision four?
 
in short hata waliopo sasa ni wengi na pato kubwa linaishia kwenye mishahara, tunahitaji redundance.
Watumishi 600,000 kwa nchi kubwa kama Tanzania , sio wengi,, tatizo la nchi hii, watu hawataki kulipa kodi, watu wanakwepa kodi, na wizi,
Watanzania wanaiba sana makazini, tunahitaji dikteta,
Mtu akiiba, anakula shaba, no discussion
 
Watumishi 600,000 kwa nchi kubwa kama Tanzania , sio wengi,, tatizo la nchi hii, watu hawataki kulipa kodi, watu wanakwepa kodi, na wizi,
Watanzania wanaiba sana makazini, tunahitaji dikteta,
Mtu akiiba, anakula shaba, no discussion
Ewaaa, umesema vyema ila unafikir Watu hawataki kulipa kodi ama wakusanyaji ndio hawataki kukusanya kodi?
 
Jamaa anadhani walimu kwa mfano wakilipwa milioni 5 ndo maisha yatakaa sawa,, uchumi una mambo yake,, ukilipa kima cha chini milioni 5,, elewa sokoni watu wataenda na matoroli ya hela kufanya shopping,,
Fungu la nyanya tatu utanunua 20,000,
Kwenye uchumi lazima pawepo na balancing act,, huwezi kupandisha mishahara for the sake of kupandisha mishahara, kwani gharama automatically zitapanda, kwani cost of production ita skyrocket, na hivyo quality ya maisha itazidi kudidimia,
Kwasababu, unapoongeza mishahara, cost za uzalishaji zinakua juu kwa waajiri, so wao hawafanyi biashara ya huduma, wanataka faida, so watapandisha bei vitu, mfano mbolea, sukari, kiufupi kila kitu kitapanda bei, hivyo hela bado haitatosha na sasa watu watataka kima cha chini kiwe bilioni moja,, bado mzunguko utarudi palepale, HAZITATOSHA[emoji23][emoji23][emoji134]
Uko sahihi kwa kiasi fulani, hii ndo sababu kwa nini serikali ndio yenye mamlaka ya kuprint fedha, lakini hawatumii pesa walizoprint kufanya mambo yao, wanazileta kwene mzunguko then wanadai kodi kwa sisi maskini ili wafanye mambo yao.
Hii ina maana shughuli za uzalishaji ndo zinazocontrol uchumi na maisha.. hivyo basi kuacha mishahara midogo bado sio suluhisho la kukuza uchumi na maisha ya watu, ila kurahisisha mazingira ya shughuli za uzalishaji ambazo ndio uti wa mgongo wa uchumi, mfano kilimo, uvuvi, ujenzi, teknolojia na mengine ya aina hiyo...
Bila ivo bado tutakuwa na safari ndefu na tutakuja tutawaliwe tena

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Ewaaa, umesema vyema ila unafikir Watu hawataki kulipa kodi ama wakusanyaji ndio hawataki kukusanya kodi?
Mwamko haupo kuanzia walipa kodi na wakusanya kodi,, mfano binafsi mimi nakwepa sana kodi,
Watanzania karibu wote hatupendi kodi, mizigo inaandikiwa risit za thamani ndogo, makampuni yanadeclare mapato kidogo kuliko uhalisia,
Mamilioni ya watu wanakwepa kodi, hakuna maadili,
 
Lema ana hoja za msingi Sana shinda kubwa ni kuwa tumefanya baadhi ya vitu kuwa katika sehemu ya maisha yetu hivyo mageuzi yoyote huwa kama kero kwa walio wengi.

"Maisha bora hayako mbali tatizo hatujui kulenga tumemfanya dhiki rafiki hatujui kumtenga" one ft Songa
 
Kaka Lema hii ngoma unayopiga imefika mpaka Ndani walipofugia misukule( wtz) endelea kuipiga hiyo ngoma kwa ustadi zaidi ili wafuga misukule ( viongozi waovu) waamke na kutubu.

Haiwezekani tufikirishwe vitu vidogo vidogo.

Haiwezekani eti bodaboda ni ajira wakati hainihakikishii maisha marefu na mazuri baada ya kuacha kuifanya.

Haiwezekani Vikoba ikawa njia ya kumkwamua mtu,,akina mama wananuka madeni,,unampaje mtu kamkopo ka kununulia chupi alafu akienda kukafanyia biashara nayo anakutana na soko lisilotabirika anaishia kukonda kwa madeni na umaskini.

Haiwezekani mwl, Askari na wengine wengi walipwe Tsh 400,000

Haiwezekani akina mama wajifungulie chini halafu tuchekelee.

Haiwezekani wagonjwa watukanwe kama mbwa halafu tumuone Lema mbaya.

Haiwezekani mafisadi yajilipe mamilion ya fedha kwenye tenda alafu tukae kimya.

Haiwezekani Rais atembeee na msafara wa magari 200 halafu hakuna kinachobadilika.

Haiwezekani kivuli cha rais kifunike kila mahali nchi hii, tunahitaji mamlaka yetu wananchi, hatutaki Ma DC, RC, RAS na Ma DAS ni ujinga mtupu tunahitaji viongozi watoke baina yetu.

Wafuga misukule endelea kufukiza dawa misukule isitoke nje, ikitoka mmekwisha.

Lema Kaka umekuja na upako mzito ebu endelea kuuelewesha umma hata kwa gharama ya kukosa kura.
Uzi huu ni chukizo kwa walinda legacy!!!
 
Lema ana hoja za msingi Sana shinda kubwa ni kuwa tumefanya baadhi ya vitu kuwa katika sehemu ya maisha yetu hivyo mageuzi yoyote huwa kama kero kwa walio wengi.

"Maisha bora hayako mbali tatizo hatujui kulenga tumemfanya dhiki rafiki hatujui kumtenga" one ft Songa
Watanzania wengi hasa wanachama wa ccm wamesharidhika na dhiki.

Wamepumbazwa kipindi kirefu sana hivyo kuwatoa kwenye huo usingizi mzito inahitajika nguvu kubwa sana.

Mfano tazama kuku ukimfungia sana kwenye banda lenye giza siku ukimtoa nje ya banda lazima ataanza kuogopa mwanga na kuzubaa.
 
Mwamko haupo kuanzia walipa kodi na wakusanya kodi,, mfano binafsi mimi nakwepa sana kodi,
Watanzania karibu wote hatupendi kodi, mizigo inaandikiwa risit za thamani ndogo, makampuni yanadeclare mapato kidogo kuliko uhalisia,
Mamilioni ya watu wanakwepa kodi, hakuna maadili,
Ccm ni janga la watanzania
 
hii elimu unampa ataweza kuelewa?

Kuna walimu wa Halmashauri na kuna wa TAMISEMI.

Kama mpaka leo ana -amini mshahara wa mwalimu ni 400,000 huyo si POYOYO tu.

Walimu wote wanao anza kazi hakuna chini ya 800,000/- bado wana posho za mazingira magumu kwa wale wa mikoani na vijijini, bado kuna semina na mambo kibao, hii nchi bado sana kama mtu ana bando anashindwahata kutafuta uzi huku kuna mishahara ya walimu:
Hivi ww uko nchi hii au unaota!!!? Eti posho ya mazingira magumu!! Eti hakuna mwl analipwa chini ya 800,000!! Utakuwa mgonjwa wewe,nakubaliana na wewe kwamba wapo wenye 800,000 lkn ni wale wenye elimu ya juu au waliokaa kazini muda mrefu karbu kustaafu,,,wengine mfano diploma wanapata 650,000 kabla ya Makati,,certificate hazidi 540,000 kabla ya makato sasa huo ndo unaotaka kusema mshahara kweli!?? Au una tatizo la kufikiri!? Mimi najua mishahara yao vizuri nimewaingiza ualimu na uaskari nk
 
Lema ana hoja za msingi Sana shinda kubwa ni kuwa tumefanya baadhi ya vitu kuwa katika sehemu ya maisha yetu hivyo mageuzi yoyote huwa kama kero kwa walio wengi.

"Maisha bora hayako mbali tatizo hatujui kulenga tumemfanya dhiki rafiki hatujui kumtenga" one ft Songa
Maisha bora hapa duniani hayapo,,, maisha bora ni mindset yako tu ,kutoka bronze age kuja iron age, watu wakaacha kuishi mapangoni na kuanza kujenga vibanda, waliona ni maisha bora, lakini ukweli ni, maisha bora yako kichwani mwako zaidi,
 
unafikiri alipaswa alipwe kiasi gani ?
Wa Digrii alipwe kiasi gani?
Masters alipwe kiasi gani ?
PhD alipwe kiasi gani?

Na hiyo iwe hivyo kwenye kada zote au ualimu pekee Maana wengi wao wameingia baada ya kupata dsivision four?
Wewe tukikupa hiyo basic 800,000 utaweza kupay bills zako zote na usevu kahela kidogo kwa ajili ya ujenzi,ada,misaada na kufanya utalii wa Ndani kipindi Cha likizo ili ku refresh akili!???
 
Maisha bora hapa duniani hayapo,,, maisha bora ni mindset yako tu ,kutoka bronze age kuja iron age, watu wakaacha kuishi mapangoni na kuanza kujenga vibanda, waliona ni maisha bora, lakini ukweli ni, maisha bora yako kichwani mwako zaidi,
I Nyie ndo wajumbe wa kamati kuu ya ccm,,,kumbe ndo maana nchi imefeli na sioni ajabu kwanini mnasema bodaboda ni ajira!!! Hivi ndo mko hivi enyi walafi!!
 
Uko sahihi kwa kiasi fulani, hii ndo sababu kwa nini serikali ndio yenye mamlaka ya kuprint fedha, lakini hawatumii pesa walizoprint kufanya mambo yao, wanazileta kwene mzunguko then wanadai kodi kwa sisi maskini ili wafanye mambo yao.
Hii ina maana shughuli za uzalishaji ndo zinazocontrol uchumi na maisha.. hivyo basi kuacha mishahara midogo bado sio suluhisho la kukuza uchumi na maisha ya watu, ila kurahisisha mazingira ya shughuli za uzalishaji ambazo ndio uti wa mgongo wa uchumi, mfano kilimo, uvuvi, ujenzi, teknolojia na mengine ya aina hiyo...
Bila ivo bado tutakuwa na safari ndefu na tutakuja tutawaliwe tena

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Uko vizuri japo Kuna mahala umeanza kwa kuungana nae mkono lkn angalau nimekuelewa,,,katika shughuli zakiuchumi ulizotaja sijaona ukitaka bodaboda ikimaanisha kwamba tunakubaliana kwamba badaboda haiwezi kuwa ajira na haiwezi kuinua uchumi wa nchi bali ni kuharibu future ya vijana
 
I Nyie ndo wajumbe wa kamati kuu ya ccm,,,kumbe ndo maana nchi imefeli na sioni ajabu kwanini mnasema bodaboda ni ajira!!! Hivi ndo mko hivi enyi walafi!!
Nchi ilifel tangu lini jomba?, 😥
USA👇
 

Attachments

  • Screenshot_20230319-131644~2.png
    Screenshot_20230319-131644~2.png
    109 KB · Views: 1
  • FrBajjqaMAIgIgU..jpg
    FrBajjqaMAIgIgU..jpg
    516.8 KB · Views: 1
  • Screenshot_20230319-132655~2.png
    Screenshot_20230319-132655~2.png
    66.1 KB · Views: 1
Back
Top Bottom