Tumshauri kijana huyu cha kufanya, muda bado upo

Cha kumuokoa hapo si ajira tena aachane na masuala ya kutafuta ajira maana haitomuokoa kabisa, kesho kukikucha aanze mishe mishe za biashara aanze alichonacho ila aplan road map ya kufika sehemu kubwa within a certain time,
Mwambie hana cha kupoteza tena wala wa kumwonea aibu maan type yake wapo wengi hata uko waliojiriwa
 
Kwanza kijana ajue muda sio mchache Kama utakua unautumia,, alafu ukishakua msomi jifunze kua mtu jamii wasomi awana hii awako tayari kuungana na ambao awajasoma bila kujua yeye alijifunza kukalili mwenzake alielewa jambo moja niwashauri,, kwasasa nikukubali kuungana na waanze na Mimi nipo tayari kuungana na kijana anaitaji mafanikio,, tutengeneze umoja wetu Kama team we are not poor but we are poor on menagement
 
Binafsi nilihitimu Shahada 2016 nikakosa ramani mtaani ikanibidi niingie VETA kusoma fani ya Umeme wa majumbani Kwa miaka miwili(kozi ndefu). Namshukuru Mungu Kwa Sasa nimejiajiri na nimeajiri vijana. Kwa Sasa nimerudi VETA kusoma umeme wa viwandani mwaka wa 3.

Jiongeze kutafuta ujuzi, hujachelewa.
 
Kutokana na ugumu wa ajira na msemo usemao "doesn't matter what you know but whom you know" NINGEPENDA KUWASHAURI VIJANA KUWEKEZA KATIKA DIGITAL MARKETS KAMA VILE
1.CRYPTO CURRENCY
2.FOREX
3.COMMODITIES
4.STOCKS

Kwa sasa crypto currency ni chaguo zuri kwa vijana. Especially kwa wanaofanya automated trading au artificial intelligence kama vile ROYAL Q
 
Mama kafungua nchi ameleta ajira za hausiboi na hausigeli uarabuni, achangamkie huko hakuna watoto wa viongozi wa CCM.
 
Kama ni kurudi kijijini vijiji viko vingi sana Tanzania ukisogea vijiji vya mbalali kuanzia mwezi wa kwanza mpaka wa tatu hukosi laki tatu kwa mwezi na zaidi cha msingi usiwe mvivu.piga kazi huko mashambani watu wanaweka CPA zao mfukoni elimu kichwani
 

Redio zinaajiri comedians na tik tokers. Hao ndio wanapendwa na wasililizaji.

Zimeachana na kuajiri wasomi wasomi.

Udsm pale school of journalism and mass communication. Wanatema graduates kila mwaka lakini ajira hawapati
 
Kuna wakati unatakiwa uwe mult tasking,usichague kazi wala kuwa mzito wakuganya kazi ambayo haiendani na taaluma yako,jifunze kila ambacho unaweza kujifunza nakukifanyia kazi ,mfano mim nina taaluma ya Afya,HR ,na project management,ninaweza kusuka umeme wa majumbani,naweza kujenga kidogo natengeneza sofa kwa ufasaha kabisa,ninauwezo wakufuga gympsum bodies katika paa ama kufanya partition ,yote niliamua kujifunza ili nijipate,elimu yangu taaluma zangu hazikuwahi kunifanya nione aibu kufanya kazi nyingine na nikiwa katika kazi hiyo ninaganya kwa kujituma sana tu
 
Binafsi nilihitimu Shahada ya sanaa 2016 (Mwl. Wa Kisw&Hist)nikakosa ramani mtaani ikanibidi niingie VETA kusoma umeme wa majumbani Kwa miaka miwili (kozi ndefu) namshukuru Mungu sikosi ya vocha, nimejiajiri na nimeajiri vijana. Kwa Sasa nimerudi tena VETA mwaka wa 3 kusoma umeme wa viwandani na mwakani nahitimu.

Fanya maamuzi magumu Kwa kuona ni lipi linafaa kwako kujiingizia kipato, kama ni kilimo, ufugaji, fani, n.k maisha ni Yako.
 
Akili sana mwaisa
 
Nikipita maeneo ya vyuo vikuu i.e UDSM,TIA,SAUT etc nikaona wanafunzi wanaenda madarasi kusoma hua nasikitika Sana.

Yajayo hayatawafurahisha.
Nchi hii kubwa bado inahitaji nguvu kazi ya wasomi. Hata hivyo ajira inahitaji mtu mwenye ufahulu wa juu mwenye maharifa kiasi hata ukimfanyia interview utajua kuwa hiki ni kichwa. Sasa wengi wanaenda chuo wakishapata boom wanasahau kilichowapeleka na kuishia kupata GPA ya PASS Gentlemen! Sahau kuajiliwa! Komaa kitaa kamanda
 
W
Wangapi wana GPA nzuri ila bado wapo kitaa na msoto tu,na wangapi wana GPA fyongo ila wana ajira,mimi aliyekuwa best student katika kozi yangu pale MUHAS , mpaka leo hana ajira ,,
 
Kuna videmu nakutanaga navyo vinaniambia vinasoma udsm halaf kwa kuniringia kabisa visijue udsm nshasomaga hapo... Naishia tu kucheka
Juzi nikikuwa DIT pale jengo flani hivi refu sana nilienda kuwatafuta wanafunzi wenzangu kule juu,sasa siwafahamu,na mimi ndio nimeanza mwaka wa kwanza,nikwmuuliza dada flani,samahani unasoma kozi gani,akanijibu Mechanical,mwaka wa ngapi wa mwisho,anajibu kwa madaa kabisa yule kahapa nikasema kanajiona ,fresh street is waiting for you with joy
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…