Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

Kulingana na utafiti uliofanywa na Twaweza,MISA-TAN,Jamii Forum na TAMWA asilimia 50% ya waandishi wa habari hukumbana na vitisho,ukatili na unyanyasaji wa kijinsia nchini.

Ila hili la mwisho si walisema yameisha na JPM? siku hizi watu wote wanaimba kumbaiya ...
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.
Erythrocyte ama ChoiceVariable ni waandishi?

Nawaulizeni wajuvi.

Kunguru?
 
Mkuu si uje na wewe uanzishe chombo chako kitakachokuwa kinapishana na Serikali. Kwani unafeli wapi?

Yaani mtu ametoa mtaji wake kama Family ya Reginald Mengi kujenga empire ya vyombo vya habari. Anatengeneza ajira kwa maelfu na kulipa kodi, wewe unataka aandike habari za kufurahisha wanaharakati!!
Safari ya maendeleo Tanzania bado ni ndefu sana. Wewe unasema hivi, mwingine atasema "nilivyohangaika kusoma kwa tabu kwanini nianze kuikosoa serikali?, na mwingine atasema "nilivyohangaika kupata kazi hivi kwanini niikosoe serikali?, na wahadhiri wa vyuo vikuu wakisema "ya nini kuandaa bongo za wanafunzi kuwa critical thinkers waje wahoji utumbo wa serikali?...Tukienda hivi check and balance itatoka wapi? Bila check and balance hakuna kitakachofanyika nchi itabaki hivi hivi
 
Wandishi wa habari njaa tupu

Sakata la sukari bila Mpina lilitakiwa kuonwa na waandishi wa habari kabla ya mtu yeyote

Sakata hili linatisha vibaya sana, lakini huwezi kuona tarifa hiyo popote zaidi ya kumnukuu Mpina na ama Lissu

Wao wapo kupewa milungula!

Kwa TANZANIA bado saaana hii tasnia
Investigative journalism ni ngumu sana kwa mazingira yetu na ukizingatia kwamba sheria nazo sio rafiki kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari.
 
Investigative journalism ni ngumu sana kwa mazingira yetu na ukizingatia kwamba sheria nazo sio rafiki kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari.
Lakini hapa katikati kulifanyika investigave journalism ya hali ya juu sana. Enzi za MwanaHalisi nani anaweza kusahau; hata enzi za This Day....
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.

UsiDOWNLOAD hii attachment; na ukidownload usiseme kilichomo.
Vyombo vya habari vimetukana weee hamjaridhila tu bado. Mama ameruhusu endeleeni kutuka a yeye kimyaaa. Mnataka nini tena. Au uhuru ni upi kwenu. Mnataka mpaka muingie chumbani kwake ndo mjihisi mko huru
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.

UsiDOWNLOAD hii attachment; na ukidownload usiseme kilichomo.
Moja ya maandiko ya hovyo kabisa kuwahi kutokea ardhini na mbinguni. Sujui hii ni akili gani. Au ulikuwa umelewa
 
Kuna brother yangu aliwahi nidaka humu JF nikamkatalia sio mimi japo nilikuwa ni mimi alinidaka baada ya kunifanya profiling.Pia alimtambua mzee mwanakijiji ni Ndugu ...........
 
Ila hili la mwisho si walisema yameisha na JPM? siku hizi watu wote wanaimba kumbaiya ...
Kuna watu kwa makusudi kabisa,wanatumia namna utawala wa JPM ulivyo kuwa kuficha yale yanayo endelea sasa nchini.Na wakati huo waandishi wamekuwa katika hali tete katika awamu zote hapa nitataja matukio machache~

Mwaka 2012 mwezi Septemba tarehe 2,vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya Tanzania viliripoti juu ya kifo cha Mwandishi wa habari wa kituo Cha channel Ten,Daudi Mwangosi kilicho tokea katika kijiji cha Nyororo mkoani Iringa na Mwandishi aliye husika kupiga picha kipindi jeshi la police likifanya mauaji hayo Joseph Senga hakuachwa salama naye alitangulizwa mbele ya haki.Hiki ni kipindi cha JMK.

Bila kusahau kifo cha utata cha Mwandishi wa habari za kichunguzi bwana Stan Katabalo juu ya sakala la Loliondo,kipindi cha mzee Mwinyi.

Hata kipindi cha BWM,hakuwa na mahusiano mazuri na waandishi wa habari,sababu ya dharau zake za wazi wazi ,ndio maana aliwahi kunukuliwa akisema "Waandishi wa habari wa Tanzania hawajui kiingereza".Hili hata mara kadhaa Jenerali Twaha Ulimwengu amezungumza sana tu.

Ni juzi tu hapa,Mwandishi aliye andika habari kuhusu RC kumnajisi mwanafunzi chuo cha SAUT-MWANZA kasha kamatwa,hivyo basi kumpa lawama zote JPM si Sawa,licha kwamba katika kipindi chake kulitokea hali ya sito fahamu kwa baadhi ya waandishi,lakini kitendo cha wachache kumuona yeye ndo mkosaji mkubwa kuliko wengine ni kujivika kiremba cha unafiki na kilele za uzadiki mkubwa.
 
Kwanza hongera kwa kuliona hili ingawa liko obviously ktk jamij yetu. Ila nchi hii wazee waliokuwa katika system ndiyo walohusika kutufikisha hapa.

Vijana wamewaiga wazee. Kila mtu anafahamu hili. Itahitajika miaka 20 kutoka ktk jinamizi hili. Si vyombo vya habari tu hata vyuoni siku hizi hakuna kufikirisha fikra.

Ukiona wanafunzi wa vyuo wanaingia na kutoka miaka kadhaa na hakuna migongano ya demonstration au strikes unajua kuna shida. Elimu haijawahi kutengeneza misukule itakayokula kila unga wa ndele na kufuata mdundo wa ngoma. Hao waandishi ni muendelezo wa kinachotokea vyuoni.

Enzi fulani kama ya akina Zitto, Mtatiro, Mnyika na wachache wengine zinaisha. Lakini tunajua zilianzia universities.
Kwa hiyo, nionavyo, si waandishi tu peke yao. Ni suala la jamii mzima na mifumo yetu ya elimu, vyeo na uongozi. Leo, mtu anayesifu pasi na sababu "chawa" anaweza kupata cheo kikubwa serikalini kuliko mwenye sifa aliyejiandaa kitaaluma au kiutumishi.

Sasa basi hao waamdishi ni muendelezo tu wa kile mfumo wa kisiasa umetufiksha. Kesho utawala ukibadilika wote wanahamia timu iliyoshinda.
Magroup ya vyuo vingi yanaweka kabisa masharti kuwa ni marufuku ku-discuss siasa. Na hamna group maalum Kwa siasa,na uki-discuss wenzako wanakuona wa ajabu sana nawenye ujasiri wa kipekee Ilihali utakuta mtu kaongea kitu Cha kawaida kabisa na hapo hapo utasikia unamwanasheria kaka?,kaka Kunawatu wanaku-zoom tu humu.Siasa itakusaidia nini wewe?

Kwahiyo lazima uwe muoga tu kujihusisha kivyovyote vile na habari za kisiasa.(Huo ni kwaupande wa vyuoni)
 
Investigative journalism ni ngumu sana kwa mazingira yetu na ukizingatia kwamba sheria nazo sio rafiki kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari.
Wala sio ngumu, tuna outlet media za kutosha ndani ya nchi na nje ya nchi. Sema ni vile tu watuna waandishi wanaojitambua.

Kwa dunia ya sasa ya kidijitali huwezi kuwa na habari moto na ukawa unawalipua watu.

Kigogo na Mange waliweza vipi kuwa wanatoa habari za ndani.
 
Vyombo vya habari vimetukana weee hamjaridhila tu bado. Mama ameruhusu endeleeni kutuka a yeye kimyaaa. Mnataka nini tena. Au uhuru ni upi kwenu. Mnataka mpaka muingie chumbani kwake ndo mjihisi mko huru
No rahisi zaidi kumvumilia mtu akutukane kuliko mtu anayekusukuma kwa fimbo
 
Back
Top Bottom