Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

Moja ya maandiko ya hovyo kabisa kuwahi kutokea ardhini na mbinguni. Sujui hii ni akili gani. Au ulikuwa umelewa
Mimi naweza kulikosoa andiko lake, lakini si kwasababu ni andiko la hovyo, nikilikosoa andiko lake ni sababu hajawahi kuona madhara ambayo wanahabari na vyombo vya habari vilikutana nayo chini ya JPM. Hata ukimuonyesha sasa bado atakataa, ila kwamba andiko lake hili la hovyo nitakukatalia na nitamtetea yeye,
 
Kigogo na Mange wana vyanzo au "source" za habari zao ila hawa hawawezi kujiita ni waandishi wa IJ.

Wanokifanya wao chaitwa kuvujisha habari au "information leakage" ambapo vyanzo hutoa taarifa za siri kutoka ndani ya taasisi kwa kufahamu (with knowledge) au kwa kutokufahamu (unintentional) kwenda kwa umma kupitia vyombo vya habari.

Na kwa kuwa vyombo hivi vyabanwa na sheria za TCRA nakadhalika, ndo maana huruka maili kadhaa na kutua kwenye mitandao ya kijamii kwa Kigogo au Mange.

Hii ni moja ya silaha za kwanza na muhimu sana kwa mwandishi wa habari yoyote yule wa IJ ni vyanzo vya kuaminika.

Tofauti kubwa iliopo kati ya waandishi wa kwetu na wale walioko huko duniani ni kwamba wale wana vyanzo, wana mtandao yaani "network", watambulika kwa uwezo wao wa kitaaluma na kiuandishi na pia wanaheshimika.

Tukija kwenye IJ ni kwamba hawa wa huko duniani kabla hawajatoa habari yoyote ambayo yahusu IJ hutoa angalizo kwa wahusika kwamba kuna spana yaja na yatoka siku fulani, hivyo wajiandae kisaikolojia. Wakati mwingine kutokana na umuhimu wa IJ huitwa majina kama "watchdog reporting" au "accountability reporting" ikiwa na maana kwamba kinoripotiwa ni kitu muhimu na kinohitaji "attention" ya wahusika au vyombo vya serikali.

IJ ni ghali sana na huchukua muda kuandaa taarifa moja tu kabla ya kuiweka hewani hivyo hatuwezi kusema fulani na fulani ni waandishi wa IJ kumbe ni wapasha habari tu. Hata vyombo vingi vya habari hukwepa sana IJ kwani huitaji masuala kama matangazo na gharama za utayarishaji.

Hivyo bado kabisa Tanzania haijapata waandishi wa IJ ambao wameiva kwa kazi hiyo na siku wakipatikana utaona tofauti ya habari zao na zile za kuvuja.

Hapa nilipo nimewahi kutembelea chuo kikuu cha Missouri ambacho kina kitovu cha IJ mahsusi kwa wale wanotaka kujifunza IJ.

Chuo hiki naweza sema ni chuo bora kabisa duniani kwa ufundishaji IJ na wana taasisi kabisa inohusu waandishi wa habari za uchunguzi na wahariri inoitwa IRE-Investigative reporters and editors.
Umeelezea vizuri sana; kuvujisha habari siyo sawasawa na uandishi wa uchunguzi. Mfano upo kwenye mada hii hii; mtu anaweza kuvujisha habari bila kwenda ndani zaidi ya hilo. Kudos!
 
Umesema sahihi, halafu Mwanakijiji amesahau alivyokuwa wakala wa JPM wa kuua ajenda za wananchi, wanachofanya wenzake yeye Mwanakijiji ndio muasisi
Acha kulaghai watu; angalia rekodi yangu uone. Yaani, kweli kabisa na akili zangu timamu ulitarajia niunge mkono mabadiliko ya kuvingirisha mikono? Nilimuandika JPM kabla hajawa Rais, nilijua akiwa Rais atakuwaje (na hakuna alichonishangaza); na nilimuandika akiwa Rais - pamoja na kuwa nilimuunga mkono. Nilipotakiwa kukosoa nilikosoa na nilipamua kuunga mkono niliunga mkono. Ukiweka kwenye mizani miaka yake mitano kimaendeleo ilikuwa ni bora zaidi kuliko miaka 25 kabla yake. Hutaki?
 
Wenye vyombo vya habari ndio wanakiri wako salama sasa kuliko tuliiotoka(awamu ya 5),wewe chawa wa Mwendazake huna lolote unaloongea la msingi Kwa hiyo Tulia endelea kuomboleza.

Mumeambiwa awamu yenu ndio imeleta uandishi wa maigizo ya kusifia sifia hovyo ambao haukuweoo kabla.
Huyo aliyesema hivyo labda hakuishi wakati wa JK... acheni masihara bana. Au labda wengine ni vijana wadogo kabisa mmesahau kabisa yaliyotokea wakati wa Mkapa na JK nyinyi...
 
Ulitaka kusema wakati wa JPM?

Ila naona hadi sasa msimamo wako ni uleule wa kutomkosoa JPM, kwako hadi leo JPM hakuwahi kukosea popote .
Kipindi hiki naona unajaribu kujitokeza kuipinga serikali, wakati wa JPM hukuona shida ulimtetea zaidi na mwisho ukaamua kukaa kimya kuliko kumkosoa Homeboy.
Naam, I stand corrected.
 
Ulitaka kusema wakati wa JPM?

Ila naona hadi sasa msimamo wako ni uleule wa kutomkosoa JPM, kwako hadi leo JPM hakuwahi kukosea popote .
Kipindi hiki naona unajaribu kujitokeza kuipinga serikali, wakati wa JPM hukuona shida ulimtetea zaidi na mwisho ukaamua kukaa kimya kuliko kumkosoa Homeboy.
Jamani, mbona kwenye hii hii mada hapo juu nimewawekea ni link ya kuwa sikuwa muunga mkono juhudi bila kukosoa. Au ni vigumu sana hata kubonyeza link hapo juu. Nilimkosoa Magufuli na sikutumiwa watu kunitafuta; wakati wa JK walitumwa watu hadi Marekani.. Hawa watu waache utani. Sina tatizo lolote la kumkosoa Magufuli alipokuwa hai au alipokufa. Jaribu ku "search" hapa JF mada nilizoanzisha zinamhusu Magufuli uone. Nimeweka link ya moja tu hapo juu.
 
Jamani, mbona kwenye hii hii mada hapo juu nimewawekea ni link ya kuwa sikuwa muunga mkono juhudi bila kukosoa. Au ni vigumu sana hata kubonyeza link hapo juu. Nilimkosoa Magufuli na sikutumiwa watu kunitafuta; wakati wa JK walitumwa watu hadi Marekani.. Hawa watu waache utani. Sina tatizo lolote la kumkosoa Magufuli alipokuwa hai au alipokufa. Jaribu ku "search" hapa JF mada nilizoanzisha zinamhusu Magufuli uone. Nimeweka link ya moja tu hapo juu.
Ulikuwa ukiwakosoa pia waliomkosoa (yaani mkiwa vitani halafu askari mwenzio anaelekeza silaha upande wako unaogopa), labda hapo ndipo wadau walipoona kwamba na wewe ulikuwa sehemu ya au mshirika wa "mhimili uliojichimbia chini zaidi."
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA HAPA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA HAPA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.

UsiDOWNLOAD hii attachment; na ukidownload usiseme kilichomo.
Ndio maana sisi wengine tuliacha kabisa kusoma magazeti na kusiklize habari za media zaTanzania. Ni dhahiri waziri wa habari ni mtu hatari sana kwa uhuru wa vyombo vya habari, medio zote zimegeuka uchawa, habari za upinzani hautangazwi kabisa. Mbaya zaidi hata taarifa za ufisadi mkubwa unaofanywa na watawala zinazuiwa zisitoke. SSH ni janga jipya
 
Ndiyo linaloshtua...nimesoma ushahidi wa Mpina..ile ingekuwa habari kwenye gazette au hata hapa JF..na ushahidi wote u gewekwa. Sidhani kama mtu anaweza kuleta ushahidi hapa bila kupitiwa na kamati maalum ya JF na kuwauliza wahusika kwanza.
Nakumbuka JF ya zamani iliyokuwa home of great thikers and where we dared to talk/speak openly
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA HAPA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA HAPA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.

UsiDOWNLOAD hii attachment; na ukidownload usiseme kilichomo.
ITV/Radio One viroboto wa CCM tangu Mengi alipofariki, WAPO Radio wao siku nyingi walijitambulisha na kujiunga na Polepole uchaguzi uliopita, ni pacha wa gazeti la Uhuru. JF imejifunika hijab gubigubi isitambulike kuwa imo!
 
Ukiona serikali inaungana na vyombo vya habari ujue hata sisi wachangiaji hatupo safe.

Jambo la msingi ni kuendelea na mazungumzo kuhusu umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari na kuchukua hatua za kulinda na kuimarisha.

Kwa kufanya kazi pamoja, tunaweza kuhakikisha kuwa vyombo vya habari vinaweza kutekeleza jukumu lao muhimu katika jamii yenye demokrasia.
 
Huyo aliyesema hivyo labda hakuishi wakati wa JK... acheni masihara bana. Au labda wengine ni vijana wadogo kabisa mmesahau kabisa yaliyotokea wakati wa Mkapa na JK nyinyi...
Tuko awamu ya 6,mambo Iko hivi 👇👇
Screenshot_20240531-211908.jpg
 
Back
Top Bottom