Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

Tuna hatari zaidi kwa Vyombo vya Habari kuliko wakati mwingine...

SI wahadhiri, si wanafunzi, wote ni wafu wanaotembea.
Sikajiona chuo chenye elites wa kuongea ama kukosoa jambo lenye manufaa kwa nchi. Ni chawa na waganga njaa wakubwa!
Na hilo ni tatizo kubwa sana tulilonalo na ambalo wengi hawajalitambua.

Kwa kuwa neno uwajibikaji haupo katika serikali na vyombo vyake, ni vigumu sana kwa mwandishi wa IJ kufanya kazi yake maana atakapoanza kufanya uchunguzi wake atahitaji vifaa au "tools" au ufundi yaani "technical".

Kuna mambo kama kanzidata ambayo ina taarifa zote anozihitaji, awe na vyanzo vya siri au anonymous ambao waitwa "whistleblower" na si mtu tu kaiba taarifa. Hawa WBs waweza kuwa bado wako kazini au wameacha kazi lakini wana ile techinical knowledge ya mahali wanapozungumzia.

Na pia zipo mbinu zingine kadhaa ambazo siwezi kuziweka hapa zote lakini ni muhimu kwa mwandishi wa IJ.

Kwahiyo kusomea uandishi wa habari pekee hakukufanyi kuwa mwandishi wa habari za kiuchunguzi, ni lazima uingie kujifunza namna ya kufanya kazi za uandishi wa habari za kiuchunguzi kwa kukaa tena darasani.
 
Hakuna intellectuals wa kukosoa vitu; wamebakia legends kama kina Ulimwengu, Prof. Shivji, na wachache wao. Walioko vyuoni sasa hivi hawawezi kuthubutu.
Na si kukosoa tu kwa mfano katika IJ hiyohiyo kuna matawi kama "Preventive Journalism".

Hii PJ ni uandishi wa habari ambao umelenga kutoa taarifa ya kuvijulisha vyombo vya serikali au jamii juu ya tatizo linoanza kujitokeza au litalojitokeza endapo hatua hazitachukuliwa.

Kwa kuwa kuna mawasiliano mazuri kati ya serikali na waandishi wa IJ utakuta serikali yachukua hatua mara moja kwa kutambua mchango wa waandishi wa IJ.

Lakini juzi mwandishi kamamatwa polisi kwa kuandika taarifa juu ya RC alijigonga kwa mwanafunzi. Ila kwenye jamii lipo tatizo la watu kulawitiwa na wengine kuumizwa.

Kulawiti ni kosa la jinai kwani ni kumuingilia mtu kwa nguvu bila ridhaa yake khasa watoto wadogo kama yule wa Arusha.

Hili ni tatizo la kijamii na kwa kuwa jamii yatambua kuwepo kwa tatizo hili ni fursa nzuri kwa mwandishi wa IJ kuandika kwa kina akitumia vigezo vyote ili kuitaarifu serikali ambayo kazi yake ni kuchukua hatua.

Kwa kuwa mwandishi alieandika juu ya RC hana sifa za kutaarifu habari za IJ polisi kwa sheria zao wakaamua kumkamata.
 
Na hilo ni tatizo kubwa sana tulilonalo na ambalo wengi hawajalitambua.

Kwa kuwa neno uwajibikaji haupo katika serikali na vyombo vyake, ni vigumu sana kwa mwandishi wa IJ kufanya kazi yake maana atakapoanza kufanya uchunguzi wake atahitaji vifaa au "tools" au ufundi yaani "technical".

Kuna mambo kama kanzidata ambayo ina taarifa zote anozihitaji, awe na vyanzo vya siri au anonymous ambao waitwa "whistleblower" na si mtu tu kaiba taarifa. Hawa WBs waweza kuwa bado wako kazini au wameacha kazi lakini wana ile techinical knowledge ya mahali wanapozungumzia.

Na pia zipo mbinu zingine kadhaa ambazo siwezi kuziweka hapa zote lakini ni muhimu kwa mwandishi wa IJ.

Kwahiyo kusomea uandishi wa habari pekee hakukufanyi kuwa mwandishi wa habari za kiuchunguzi, ni lazima uingie kujifunza namna ya kufanya kazi za uandishi wa habari za kiuchunguzi kwa kukaa tena darasani.
Asante
 
Kulingana na utafiti uliofanywa na Twaweza,MISA-TAN,Jamii Forum na TAMWA asilimia 50% ya waandishi wa habari hukumbana na vitisho,ukatili na unyanyasaji wa kijinsia nchini.
Na wale 50% waliobaki ? Nadhani tukileta hizi excuses tutakuwa hatuendi hii kazi sio rahisi na mpaka ujitoe huko ni kwamba unaiweza.., sasa kama ikawa ngumu kuliko kugeuka kuwa cheerleader au kasuku bora uje huko kijijini tulime mihogo (hapo tutakuwa tunawatendea haki watanzania kwa kuwapatia chakula na sio kuwalisha matango pori)
 
Wenye vyombo vya habari ndio wanakiri wako salama sasa kuliko tuliiotoka(awamu ya 5),wewe chawa wa Mwendazake huna lolote unaloongea la msingi Kwa hiyo Tulia endelea kuomboleza.

Mumeambiwa awamu yenu ndio imeleta uandishi wa maigizo ya kusifia sifia hovyo ambao haukuweoo kabla.
Perception ni muhimu sana mnaweza kuangalia kitu kilekile lakini wewe ukadhani kwamba ni manyuzi nyuzi meusi wakati mwingine akaona kwamba ni nywele....

Kuna faida gani kwa mwananchi (mlaji) kama anaendelea kulishwa propaganda na hapati ukweli au uhalisia..., kama yule alitumia mabavu (very bad) lakini huyu anayetumia pesa zako (Kodi) kufanya kilekile ni kama kupe anayekunyonya ili uendelee kuambiwa kwamba nyekundu ni nyeusi....

 
Safari ya maendeleo Tanzania bado ni ndefu sana. Wewe unasema hivi, mwingine atasema "nilivyohangaika kusoma kwa tabu kwanini nianze kuikosoa serikali?, na mwingine atasema "nilivyohangaika kupata kazi hivi kwanini niikosoe serikali?, na wahadhiri wa vyuo vikuu wakisema "ya nini kuandaa bongo za wanafunzi kuwa critical thinkers waje wahoji utumbo wa serikali?...Tukienda hivi check and balance itatoka wapi? Bila check and balance hakuna kitakachofanyika nchi itabaki hivi hivi
Mkuu anzisha media yako kutekeleza malengo ya check and balance. Unafeli wapi?

Nyie mnawachochea wenzenu tu halafu mko pembeni mnakula kuku kwa mrija
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna kitu hakiko sawa. Inapotokea kuwa watawala wanashukuru, wanasifia, wanaunga mkono na wanaonekana kuwa wametulia na kuenjoy uhusiano wao na vyombo vya habari ni lazima tushtuke kidogo. Kwenye nchi zote zenye demokrasia ya kweli na zinazojaribu kujenga au zinazojenga utawala wa sheria mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala ni matokeo ya lazima.

Inapotokea vyombo vya habari (vile vya zamani na hivi vya mitandaoni) vinajaribu kuwasiliana na watawala na kupeleka habari zake ili zihakikiwe basi tuna tatizo. Kama habari ikiandikwa halafu mtu anasema "itoeni hiyo habari" na chombo cha habari kwa kuogopa kuudhi au kwa kuhofiwa kuudhiwa kinakubali basi tatizo linazidi kukua.

Kuna watu wanaamini kabisa kuwa si lazima kuwe na ugomvi kati ya vyombo vya habari na serikali. Nakumbuka wakati wa mtawala fulani vyombo vya habari vilisifika sana kwa kupokea "bahasha". Matokeo yake nakumbuka mchorani vikatuni wa Kenya Bw. Gado alichora picha ikionesha vyombo vya habari vikimlamba miguu mtawala wa wakati ule. Inawezekana tumerudi pale tena?

Lakini cha kutisha zaidi ni kuwa kama watu ambao hata hawako serikalini na si watawala labda wana utajiri wa kutupa tu nao wanaweza kuamua nini chombo cha habari kinafanya au kinasema basi kile kinachoitwa "uhuru wa vyombo vya habari" si kingine bali ni kugeuka kuwa "kunguru wa habari". Wanaruka ruka, kula, na kupiga kelele, za hapa na pale, huku wakidonyoa donyoa kile wanachopewa. Hawatakiwi kuudhi watu au kumuudhi mtu.

Tunajuaje kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari; watu wengine wanasema sasa hivi vyombo vya habari na waandishi hawafokewi, hawapigwa, hawatekwi, hawaumizwi, wamekaa kwa starehe wanafikiri kuwa hili ni jambo zuri. Ni zuri kwa nani? Ni lazima uwepo mgongano kati ya vyombo vya habari na watawala.

Jukumu la vyombo vya habari si kuunga mkono serikali au kuipa maneno mazuri. Kile ambacho watu walisema kinatokea wakati wa JPM ndiyo hicho hicho kinatokea tena wakati huu wa SSH. Ukiangalia utaona kuwa ni shilingi ile ile ila upande mwingine tu. Sikuwahi kuwa na tatizo hata kidogo na watu au waandishi waliokua wanaikosoa na kumkosoa Magufuli.

Kuna watu wanafikiri tulimuunga mkono Magufuli halafu tukaegesha akili zetu pembeni wenyewe tukaondoka. Niliandika mada hapa ya kumtaka Rais Magufuli Ajiuzulu kama aliona kazi ya Urais ni ngumu (nina uhakika kuna watu hawakumbuki wanafikiri tulikuwa tunaimba sifa tu!). MADA HII HAPA BONYEZA HAPA.

Na mada hiyo nakumbuka ilipigiwa chapo na mkongwe MAYALA kwenye mada yake hii NYINGINE BONYEZA HAPA.
Ni lazima tuwe na uhuru wa kusema kisichopendeza, kuonesha kisichotakiwa, na kukataa kinachopendwa na wengine. Inapofika vitendo vya kifisadi vinahaririwa kwanza basi kile kinachoitwa uhuru wa vyombo vya habari hakipo tena. Ngoja tuone ili tufanye maamuzi saa hii. Nimeweka tena mada ya mwelekeo mpya wa ufisadi Tanzania uliorudi kwa nguvu.

UsiDOWNLOAD hii attachment; na ukidownload usiseme kilichomo.

Anyway, lets not lose hope. Kusema kweli, haya uliyoandika yapo
 
Umesema sahihi, halafu Mwanakijiji amesahau alivyokuwa wakala wa JPM wa kuua ajenda za wananchi, wanachofanya wenzake yeye Mwanakijiji ndio muasisi
Huyu mzee Mzee Mwanakijiji ni TAFSIRI sahihi ya UNAFIKI ndiyo maana nimempa FRONT kuwa aanzishe chombo chake ndiyo kifanye hizo mavitu. Kukosoa vyombo vya watu ambavyo wame sacrifice kuanzisha kwa jasho na damu katika kutengeneza mtaji siyo sahihi.

Wakati wa Magufuli huyu mzee alikuwa CHEERLEADER wa sera za Dikteta za ukandamizaji demokrasia, kulitawqla bunge kwa remote control, kutishia mahakama na kukosekana kwa utawala wa sheria.

Hatukuwahi kumsikia Mzee Mwanakijiji akikemea tabia ya hovyo ya Magufuli ya kuvitishia vyombo vya habari na kubana uhuru wa maoni.

Kwenye JF Mwanakijiji anajidhirisha kabisa kama kinara wa Sukuma Gang
 
Huyu mzee Mzee Mwanakijiji ni TAFSIRI sahihi ya UNAFIKI ndiyo maana nimempa FRONT kuwa aanzishe chombo chake ndiyo kifanye hizo mavitu. Kukosoa vyombo vya watu ambavyo wame sacrifice kuanzisha kwa jasho na damu katika kutengeneza mtaji siyo sahihi.

Wakati wa Magufuli huyu mzee alikuwa CHEERLEADER wa sera za Dikteta za ukandamizaji demokrasia, kulitawqla bunge kwa remote control, kutishia mahakama na kukosekana kwa utawala wa sheria.

Hatukuwahi kumsikia Mzee Mwanakijiji akikemea tabia ya hovyo ya Magufuli ya kuvitishia vyombo vya habari na kubana uhuru wa maoni.

Kwenye JF Mwanakijiji anajidhirisha kabisa kama kinara wa Sukuma Gang
Kama wewe hukuwahi kusikia haina maana inawezakana masikio yako yanachagua cha kusikia. Kuna link ipo kwenye posting ya kwanza soma usiseme vilivyo kichwani tu.
 
Mwanzoni ulikuwa ukiunga mkono ukosoaji wa serikali na ulikuwa ukiwatia moyo Chadema. Hata ulikuwa ukichapisha makala kwenye Gazeti la Tanzania Daima, ulipoanza kuunga juhudi, ukaanza hata kuwa against Chadema. Nikipata nafasi nzuri ya kupata baadhi ya michango yako ya wakati huo katika context hii nitaileta.
Inawezekana umesahau kabisa kilichotufanya wengine tuigeuke Chadema. Nasubiri.
 
Kwani nchi hii wamiliki wake halali ni kina nani? Tusiache mbachao, kwa msala upitao
 
Kwanza hongera kwa kuliona hili ingawa liko obviously ktk jamij yetu. Ila nchi hii wazee waliokuwa katika system ndiyo walohusika kutufikisha hapa.

Vijana wamewaiga wazee. Kila mtu anafahamu hili. Itahitajika miaka 20 kutoka ktk jinamizi hili. Si vyombo vya habari tu hata vyuoni siku hizi hakuna kufikirisha fikra.

Ukiona wanafunzi wa vyuo wanaingia na kutoka miaka kadhaa na hakuna migongano ya demonstration au strikes unajua kuna shida. Elimu haijawahi kutengeneza misukule itakayokula kila unga wa ndele na kufuata mdundo wa ngoma. Hao waandishi ni muendelezo wa kinachotokea vyuoni.

Enzi fulani kama ya akina Zitto, Mtatiro, Mnyika na wachache wengine zinaisha. Lakini tunajua zilianzia universities.
Kwa hiyo, nionavyo, si waandishi tu peke yao. Ni suala la jamii mzima na mifumo yetu ya elimu, vyeo na uongozi. Leo, mtu anayesifu pasi na sababu "chawa" anaweza kupata cheo kikubwa serikalini kuliko mwenye sifa aliyejiandaa kitaaluma au kiutumishi.

Sasa basi hao waamdishi ni muendelezo tu wa kile mfumo wa kisiasa umetufiksha. Kesho utawala ukibadilika wote wanahamia timu iliyoshinda.

Inataka ujasiri kubadili yanayoendelea. Maana uozo uliopo umepitiliza kina na kiasi. Ila si busara kukata tamaa. Kwenye giza totoro, ni dalili kuwa kunakucha
 
Mkuu si uje na wewe uanzishe chombo chako kitakachokuwa kinapishana na Serikali. Kwani unafeli wapi?

Yaani mtu ametoa mtaji wake kama Family ya Reginald Mengi kujenga empire ya vyombo vya habari. Anatengeneza ajira kwa maelfu na kulipa kodi, wewe unataka aandike habari za kufurahisha wanaharakati!!
Aahaaaa
 
Back
Top Bottom