“Tunaamua tuseme ukweli.” Hii kauli ya Ummy Mwalimu inafikirisha sana

“Tunaamua tuseme ukweli.” Hii kauli ya Ummy Mwalimu inafikirisha sana

Point yako ni ipi hasa? Hata nimeshindwa kutambua unahitaji nn?

Sent using Jamii Forums mobile app
sihitaji kitu.
Point ni kukufahamisha kuwa hauna exposure na dunia hii ndio maana unadhani Us wanaichukulia Tz kama nchi moja kubwa sana duniani. They barely know tz, they know Maymar zaidi kulio Tz.
Umenifurahisha ma pointless yako eti china wameweka data sawa sababu us kasema anachunguza basi na tz wameamua waweke data sawa sababu us atakuja chunguza.
Hopeless!
 
Bado hatujachelewa kupiga lockdown Dar es salam na Zanzibar, siku 21 zitatosha kutokomeza Corona.

Serikali ifanye maamuzi haya haraka kabla hospitali zetu hazijazidiwa ili kuwwka urahisi kwa wagonjwa waliopo vinginevyo hospitali zitafurika na watu wengi watapoteza maisha.

Let's do it very fast hatujachelewa.
Amana Hospital tayari ishakuwa loaded

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Intelijensia ya marekani ni kubwa,Trump alisema China inapika takwimu wakabisha,akasema tena WHO inashirikiana na China kuficha wakabisha,akasema Marekani haitachaingia misaada kwenda WHO ndo wakasema ukweli
Ni bora weseme ukweli
China inaingia gharama kubwa ya kuaminika duniani kutokana na tabia zao za uongo uongo

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Wale wabunge wa CCM ni mazuzu kila hoja wanagonga meza
Nchemba aliposema takwimu zisitajwe, mlimpigia makofi na kumuunga mkono!
Ummy amesema ukweli usemwe, napo mmo!
Hivi nyie makada wa chama joka a.k.a mataga mna matatizo gani lakini...!?!
Vigeugeu sana nyie...


Sent from my iPhone using JamiiForums

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Ajabu sana kwamba humu Jf hakuna hata member mmoja ambaye ana ndugu katika hao wagonjwa wengi wa corona tunaofichwa na serikali wala hakuna member aliyefiwa na ndugu wala rafiki kwa kifo chenye kuhusishwa na corona. Yani humu wote tunasikia tu wagonjwa wa corona ni wengi na vifo ni vingi.
 
“Mnaweza kuona nimetoa takwimu kubwa lakini tunaamua tuseme ukweli kwa sababu Watanzania lazima waelewe kwamba changamoto hii ipo na kila mtu sasa kwa nafasi yake, kama kulikuwa na mtu anadhani tunatania ni wakati wa kuchukua hatua”- Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

Kwahiyo sasa ndio mmeamua kusema ukweli..?!
Na kuwa na hofu na kutapatapa juu ya sala za maonyesho!
 
Ajabu sana kwamba humu Jf hakuna hata member mmoja ambaye ana ndugu katika hao wagonjwa wengi wa corona tunaofichwa na serikali wala hakuna member aliyefiwa na ndugu wala rafiki kwa kifo chenye kuhusishwa na corona. Yani humu wote tunasikia tu wagonjwa wa corona ni wengi na vifo ni vingi.
Kwa maandishi haya unaweza ukadhani umejibu hoja ya kuwepo au kutokuwepo wagonjwa wengi na vifo vingi zaidi ya hao/hivyo vinavyotangazwa na serikali, lakini ukweli ni kwamba hujibu chochote.

Sio kazi ya members wa JF kutafuta wagonjwa au vifo; hii ni kazi ya serikali.
Kwa mtu mmoja mmoja, vifo viwili au vitatu kijijini kwa siku haviwezi kuweka tofauti kubwa na vile vya siku zote. Lakini hivi vikijumuishwa na vifo vya mkoa au nchi nzima kwa siku, hapo ndipo unapoweza kujua tofauti iliyopo.
Hii haiwezi ikafanywa na mtu aliyepo JF.

Kwa hiyo usifanye kupoteza lengo la takwimu. Ukweli ni kwamba wapo wagonjwa wengi zaidi ya hao waliopimwa na kuonekana ugonjwa wao ni COVID-19, hiyo ndio maana ya kupima.
Pangekuwepo na uwezo mkubwa wa kupima watu wengi, namba hiyo inayotangazwa kila siku ingekuwa ni tofauti.
Hali kadhalika, vifo pia vinavyotokana na corona vitakuwa ni tofauti na hivyo vinavyojulikana serikalini.

Kutokuwa na uwezo wa kutambua, hakuwezi kuwa halali kujumuisha kwamba vifo au wagonjwa ni wachache.
 
“Mnaweza kuona nimetoa takwimu kubwa lakini tunaamua tuseme ukweli kwa sababu Watanzania lazima waelewe kwamba changamoto hii ipo na kila mtu sasa kwa nafasi yake, kama kulikuwa na mtu anadhani tunatania ni wakati wa kuchukua hatua”- Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

Kwahiyo sasa ndio mmeamua kusema ukweli..?!

Kama kwa Xi kule Wuhani, vifo vilivyokuwa vimefunikiwa ni 50% zaidi....eti wamemua "kusema ukweli sasa"....CCP kule huku ni CC(!) khaaa......
 
Hata kwenye vifo tunawasubiri,
Utasubiri sana!
Bahati yako iwe kwamba watoe za kujiondolea aibu na zisiwe kamilifu zinazowasuta kwa maamzi yao ya ajabu sana.

Wao ni watafuta sifa, wasipopata sifa kwa kuzidiwa na ushahidi uliopo, ushahidi huo utafanyiwa kazi usiwe lawama kwao.

Utawala huu ndivyo ulivyo, huwezi kutegemea zaidi ya hivyo.

Kwa maana halisi, sio utawala wa uwazi.
 
Back
Top Bottom