Tunahitaji mjadala mpana wa kitaifa juu ya timu ya watu inayounda 'Mamlaka za Uteuzi' nchini

Tunahitaji mjadala mpana wa kitaifa juu ya timu ya watu inayounda 'Mamlaka za Uteuzi' nchini

Sasa umeona ndugu yangu kuwa unaona busara ya kubalance nafasi za juu tena umesema unapenda hilo—Kwa nini usione busara hiyohiyo katika utumishi wote wa serikali?

Maana haiwezekani hilo unalolipenda liwe zuri kwa ngazi za juu ila liwe baya kwenye ngazi za chini
Mkuu wadau humu wamechangia na kukujibu vizuri sana na kuna hoja nzito zimeiburiwa kutokana na uzi wako lakini umeshindw kuzijibu..naomba upitie vzuri michango ya wakuu humu.ina hoja na maswali mazito sema wameondika katika hali fikirishi.....kama bado hutaelewa,itabidi watu waanze kuandika magazeti ili kukuelewesha
 
Tatizo ni uiano mfano Dini B wapo kumi na Dini A wapo wawili, hapo uwezekano wa kuteuliwa itakuwa ni A au B.
Kuwa mkweli wa Moyo wako.
au unataka kusema wapi 5:5.
Na mara Nyingi wajuvi wana penda kufanya haya pilot study ili usipoteze resource, nenda pale uni uone ratio ya waalimu ipoje kwa kuanzia, isipotosha nenda hata kwenye ualimu au ma daktari, halafu nenda kwenye vitivo
Nafasi zote za teuzi za rais huwa hazifiki watu 3000.
Sasa waislamu Graduates, wenye sifa na vigezo wanazidi nafasi zote hizo nilizozitaja.

Sasa ukiniambia eti hakuna waislamu wa kutosha kuteuliwa mpaka ipelekee teuzi zifanyikazo zilalie kwa sana kwa watu wa dini moja kila wakati ni hoja ambayo haina ukweli wowote.

Sasa ukiteua makatibu wakuu 20, unataka kuniabia nchi hii hakuna waislamu 8, 9, 10, 12 wenye vigezo vya kuwa makatibu wakuu?
 
hii mada ingekuwa na hoja endapo mtoa mada angetuambia Wakristo ni asilimia ngapi ya wananchi wote na Waislam ni asilimia ngapi
maana huwezi kutaka uwe na 50% ya teuzi zote huku kwenye population upo kwa 25%
 
MADA HII IMEJIKITA KATIKA TEUZI ZA MAKATIBU WAKUU ULIOFANYIKA TAREHE 4/4/2021

Mimi kama raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anaishi katika nchi inayoongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninayo haki ya kutoa maoni juu ya mustakbali wa nchi hii.

Katiba yetu inatambua kuwa, palipo na binadamu hapawezi kukosekana mapungufu ya kibinadamu ikiwemo ubaguzi, uonevu upendeleo n. k, ndiyo maana Katiba ikapiga marufuku vitu hivyo.

Sasa kwa muda mrefu, nimekuwa hapa JF nakemea teuzi ambazo haziakisi demografia ya nchi yetu, nilikemea teuzi zilizokaa kidini, kijinsia na kikanda. Kuna watu humu JF wako comfortable kukemea teuzi zilizokaa kikanda, au kikabila lakini wanafumba macho teuzi zilizokaa kidini, na wanakuwa wakali kwelikweli pindi ukilisemea. Kuna wengine wanakua comfortable kukemea teuzi zilizojaa ujinsia lakini wanaogopa kukemea teuzi zinazonuka udini. Na Tupo wengine tuko tayari kukemea kila viashiria vya teuzi zenye sura ya udini, Ukanda, Ujinsia, Ukabila n. k

Sasa kuna Pattern ninayoiona katika Teuzi hizi kuanzia serikali ya Magufuli na ninaona zimeanza kujitokeza katika utawala wa Samia

Kwanini overall teuzi nyingi zinakuwa na Ratio zaidi ya (75-80%) Wakiristo na only( 20%-25%) Waislamu, Hii ratio inakuwaje fixed, Hii imetokea tu kwa nasibu au imewekwa by design?

Kwanini pattern hii inajirudiarudia kila mara, pindi uteuzi unaoinvolve watu wengi unapofanyika?

Mimi kama Mwananchi, mpenda mshikamano wa Kitaifa, ninaona kuna harufu ya ubaguzi wa makusudi katika kugawa keki hii ya Taifa, na kwangu mimi binafsi naamini na naamini pia maelfu ya Watanzania wenzangu wengi wapenda haki bila kujali dini zao hawalipendi hili, kwa hiyo ninasema wazi kuwa hili halikubaliki hata kidogo.

Nimeangalia leo teuzi za makatibu wakuu, naona kuna ratio kama ya waislamu Watatu au Wanne katika timu nzima ya makatibu wakuu Ishirini walioteuliwa hii ikiwa ni ratio ile ile ya 20% Waislamu na 80% Christians. Ningependa kujua, hii ni by design au kuna mchezo mchafu?

Kuna watu wanajenga hoja kuwa, hii ishu haina maana bali uchapakazi wa mtu —Hii hoja yangu bado ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hizi teuzi ni chanzo cha kipato, ni keki ya Taifa, Unapokuwa na watu janii moja wanaenjoy keki hii kuliko wengine maana yake unawaandalia hata vizazi vyao elimu bora zaidi, huduma bora zaidi za afya, nyumba bora zaidi kwa hiyo maana yake vizazi vya hawa wanaoenjoy sehemu kubwa ya keki ya Taifa leo, wana nafasi ya vizazi vyao kuendelea kuwa tabaka la juu katika nchi wakati hawa wengine wakiendelea kuwa kama raia wa daraja la pili!. Hili hakikubaliki.

2. Lakini teuzi za hivi zinazolalia upande mmoja ni hatari kwa umoja, amani na mshikamano wa Kitaifa—Haiwezekani teuzi za hivi zilalie upande mmoja halafu udhani kuwa wale wengine ambao wako marginalized wafurahi, hilo haliwezi kutokea

Kwa hiyo natoa wito sasa Kwa mamlaka za juu za serikali.

1. Lazima uchunguzi ufanyike kwa timu nzima inayohusika na kupeleka majina ya teuzi mbalimbali kwa Rais, Je hakuna udini katika kuchuja kwao majina?, na kama hakuna udini kwa nini hii pattern ya 20% by 80% inajirudiarudia, Kwa nini kwa mfano hatujawahi kuona teuzi zenye wauslamu 80% na Wakiristo 20%?

2. Tunataka kujua, je ni kweli hakuna waislamu wa kutosha kushika nafasi za juu kwa ratio nzuri? —Kama hawapo kwa nini? Na kama wapo kwa nini ratio inaendelea kuwa katika mtindo huo wa ALWAYS WAISLAMU NAMBA ZAO ZIWE Chini?

Suala la pili ni suala la Jinsia
Nimeona pia idadi ya wanawake walioteuliwa katika nafasi za makatibu wakuu ni almost negligible. Je, kwa utaratibu tuliokuwa tumeanza kukubaliana wa kufanya women empowerment, teuzi za namna hii zinasaidiaje katika ajenda hii?

Mada hii nataka iwafikie wafuatao

1. Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
3. Mkurugenzi Mku

MADA HII IMEJIKITA KATIKA TEUZI ZA MAKATIBU WAKUU ULIOFANYIKA TAREHE 4/4/2021

Mimi kama raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anaishi katika nchi inayoongozwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninayo haki ya kutoa maoni juu ya mustakbali wa nchi hii.

Katiba yetu inatambua kuwa, palipo na binadamu hapawezi kukosekana mapungufu ya kibinadamu ikiwemo ubaguzi, uonevu upendeleo n. k, ndiyo maana Katiba ikapiga marufuku vitu hivyo.

Sasa kwa muda mrefu, nimekuwa hapa JF nakemea teuzi ambazo haziakisi demografia ya nchi yetu, nilikemea teuzi zilizokaa kidini, kijinsia na kikanda. Kuna watu humu JF wako comfortable kukemea teuzi zilizokaa kikanda, au kikabila lakini wanafumba macho teuzi zilizokaa kidini, na wanakuwa wakali kwelikweli pindi ukilisemea. Kuna wengine wanakua comfortable kukemea teuzi zilizojaa ujinsia lakini wanaogopa kukemea teuzi zinazonuka udini. Na Tupo wengine tuko tayari kukemea kila viashiria vya teuzi zenye sura ya udini, Ukanda, Ujinsia, Ukabila n. k

Sasa kuna Pattern ninayoiona katika Teuzi hizi kuanzia serikali ya Magufuli na ninaona zimeanza kujitokeza katika utawala wa Samia

Kwanini overall teuzi nyingi zinakuwa na Ratio zaidi ya (75-80%) Wakiristo na only( 20%-25%) Waislamu, Hii ratio inakuwaje fixed, Hii imetokea tu kwa nasibu au imewekwa by design?

Kwanini pattern hii inajirudiarudia kila mara, pindi uteuzi unaoinvolve watu wengi unapofanyika?

Mimi kama Mwananchi, mpenda mshikamano wa Kitaifa, ninaona kuna harufu ya ubaguzi wa makusudi katika kugawa keki hii ya Taifa, na kwangu mimi binafsi naamini na naamini pia maelfu ya Watanzania wenzangu wengi wapenda haki bila kujali dini zao hawalipendi hili, kwa hiyo ninasema wazi kuwa hili halikubaliki hata kidogo.

Nimeangalia leo teuzi za makatibu wakuu, naona kuna ratio kama ya waislamu Watatu au Wanne katika timu nzima ya makatibu wakuu Ishirini walioteuliwa hii ikiwa ni ratio ile ile ya 20% Waislamu na 80% Christians. Ningependa kujua, hii ni by design au kuna mchezo mchafu?

Kuna watu wanajenga hoja kuwa, hii ishu haina maana bali uchapakazi wa mtu —Hii hoja yangu bado ni muhimu kwa sababu zifuatazo

1. Hizi teuzi ni chanzo cha kipato, ni keki ya Taifa, Unapokuwa na watu janii moja wanaenjoy keki hii kuliko wengine maana yake unawaandalia hata vizazi vyao elimu bora zaidi, huduma bora zaidi za afya, nyumba bora zaidi kwa hiyo maana yake vizazi vya hawa wanaoenjoy sehemu kubwa ya keki ya Taifa leo, wana nafasi ya vizazi vyao kuendelea kuwa tabaka la juu katika nchi wakati hawa wengine wakiendelea kuwa kama raia wa daraja la pili!. Hili hakikubaliki.

2. Lakini teuzi za hivi zinazolalia upande mmoja ni hatari kwa umoja, amani na mshikamano wa Kitaifa—Haiwezekani teuzi za hivi zilalie upande mmoja halafu udhani kuwa wale wengine ambao wako marginalized wafurahi, hilo haliwezi kutokea

Kwa hiyo natoa wito sasa Kwa mamlaka za juu za serikali.

1. Lazima uchunguzi ufanyike kwa timu nzima inayohusika na kupeleka majina ya teuzi mbalimbali kwa Rais, Je hakuna udini katika kuchuja kwao majina?, na kama hakuna udini kwa nini hii pattern ya 20% by 80% inajirudiarudia, Kwa nini kwa mfano hatujawahi kuona teuzi zenye wauslamu 80% na Wakiristo 20%?

2. Tunataka kujua, je ni kweli hakuna waislamu wa kutosha kushika nafasi za juu kwa ratio nzuri? —Kama hawapo kwa nini? Na kama wapo kwa nini ratio inaendelea kuwa katika mtindo huo wa ALWAYS WAISLAMU NAMBA ZAO ZIWE Chini?

Suala la pili ni suala la Jinsia
Nimeona pia idadi ya wanawake walioteuliwa katika nafasi za makatibu wakuu ni almost negligible. Je, kwa utaratibu tuliokuwa tumeanza kukubaliana wa kufanya women empowerment, teuzi za namna hii zinasaidiaje katika ajenda hii?

Mada hii nataka iwafikie wafuatao

1. Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
3. Mkurugenzi Mkuu wa TISS
Hizi teuzi zimefanyika kwenye kipindi cha Easter ndiyo maana zimewa-favor ndugu zetu wakristo ngoja afanye teuzi katika kipindi cha Ramadhani utaona nao waislamu watakavyopewa shavu.
 
hii mada ingekuwa na hoja endapo mtoa mada angetuambia Wakristo ni asilimia ngapi ya wananchi wote na Waislam ni asilimia ngapi
maana huwezi kutaka uwe na 50% ya teuzi zote huku kwenye population upo kwa 25%
Waislamu waliomba sensa ya mwaka 2012 iwe na kipengele cha dini ya mtu, Kanisa na Serikali vikapinga.

Kimsingi Waislamu walitaka mfano wa mambo hayahaya ninayokemea ya viashiria vya ubaguzi kwenye teuzi vikome, maana data zinaonyesha representation yao kwenye nafasi za teuzi ni kiduchu sana kitu ambacho kinahitaji utafiti wa kitawala, kwa nini Myslims siku zote ni wachache kwenye teuzi, Je kuna udini behind?, Je hawapo wa kutosha wenye vigezo?, ni kwa namna gani vetting inafanyika?—Vyote hivyo lazima vifanyike ili tuzidi kupata nchi iliyofair zaidi!
 
Hii hoja kwamba waislamu hawajasoma ni hoja iliyopitwa na wakati, wapo mamia ya waislamu wenye PhDs na maelfu ya wenye digrii za kawaida
Naungana na wewe.Binafsi sipendi kukosoa dini za wengine as long as humanity unazingatiwa..sipendi kutawala na kuwa juu ya imani za wengine...kuwa dini fulani kusitujengee uadui.umeona katika ngazi mbalimbali kuna wawakilishi wa dini mbalimbali..inatosha KWA namna na sula hiyo ndg yangu.narudia tena kuna hoja zimeiburiwa humu je ujaziona mkuu?
 
hii mada ingekuwa na hoja endapo mtoa mada angetuambia Wakristo ni asilimia ngapi ya wananchi wote na Waislam ni asilimia ngapi
maana huwezi kutaka uwe na 50% ya teuzi zote huku kwenye population upo kwa 25%
Mambo ya udini kwenye teuzi yamepitwa na wakati, tujenge nchi yetu kwa maslahi ya watanzania wote.
 
Waislamu waliomba sensa ya mwaka 2012 iwe na kipengele cha dini ya mtu, Kanisa na Serikali vikapinga.

Kimsingi Waislamu walitaka mfano wa mambo hayahaya ninayokemea ya viashiria vya ubaguzi kwenye teuzi vikome, maana data zinaonyesha representation yao kwenye nafasi za teuzi ni kiduchu sana kitu ambacho kinahitaji utafiti wa kitawala, kwa nini Myslims siku zote ni wachache kwenye teuzi, Je kuna udini behind?, Je hawapo wa kutosha wenye vigezo?, ni kwa namna gani vetting inafanyika?—Vyote hivyo lazima vifanyike ili tuzidi kupata nchi iliyofair zaidi!
Missile of the Nation Dini ikichanganyika na siasa katika nchi isiyokuwa ya kidini ni sawa uchanganye maji na mafuta. Wanadini wote ni sawa katika Tanzania hii, kuna leo na kesho labda leo unavyo ona wakristo wengi katika teuzi huenda kesho waislamu wakawa wengi kwenye teuzi, kwani kuna hata wakristo hawasapoti wakristo wenzi wao na kuna waislamu hawasapoti waislamu wenzi wao, hivyo haya ni mambo ya mpito tu.
 
Tatizo ni uiano mfano Dini B wapo kumi na Dini A wapo wawili, hapo uwezekano wa kuteuliwa itakuwa ni A au B.
Kuwa mkweli wa Moyo wako.
au unataka kusema wapi 5:5.
Na mara Nyingi wajuvi wana penda kufanya haya pilot study ili usipoteze resource, nenda pale uni uone ratio ya waalimu ipoje kwa kuanzia, isipotosha nenda hata kwenye ualimu au ma daktari, halafu nenda kwenye vitivo
Naunga mkono hoja....mfumo wa dunia uliopo sasa hauleti uwiano wa kijamii kisiasa na hata kiuchumi hivyo ni vigumu sana kuweka uwiano hata linapokuja kwenye swala la kidini....nyerere alijitahidi sana kubalansi haya mambo na aliibua hoja nzito sana kutetea uamuzi wake
 
Missile of the Nation Dini ikichanganyika na siasa katika nchi isiyokuwa ya kidini ni sawa uchanganye maji na mafuta. Wanadini wote ni sawa katika Tanzania hii, kuna leo na kesho labda leo unavyo ona wakristo wengi katika teuzi huenda kesho waislamu wakawa wengi kwenye teuzi, kwani kuna hata wakristo hawasapoti wakristo wenzi wao na kuna waislamu hawasapoti waislamu wenzi wao, hivyo haya ni mambo ya mpito tu.
Si vizuri ubaguzi kuupoza kwa lugha za kidiplomasia au kuufumbia macho kwa jicho la mshikamano.

Dawa ya ubaguzi ni kuuondoa, ili tuwe na taifa lenye fairness na haki kwa wote.

Ngoja nikuulize swali, leo hii rais akateua Wazanzibar watupu kwenye ukatibu mkuu, utaona tatizo au utaona ni sawa tu!?
 
Waislamu waliomba sensa ya mwaka 2012 iwe na kipengele cha dini ya mtu, Kanisa na Serikali vikapinga.

Kimsingi Waislamu walitaka mfano wa mambo hayahaya ninayokemea ya viashiria vya ubaguzi kwenye teuzi vikome, maana data zinaonyesha representation yao kwenye nafasi za teuzi ni kiduchu sana kitu ambacho kinahitaji utafiti wa kitawala, kwa nini Myslims siku zote ni wachache kwenye teuzi, Je kuna udini behind?, Je hawapo wa kutosha wenye vigezo?, ni kwa namna gani vetting inafanyika?—Vyote hivyo lazima vifanyike ili tuzidi kupata nchi iliyofair zaidi!
Kaka naona tunashindwa kuelewana..na mda wa kujibu umeisha kumbuka ni mida ya kazi hii....ila natamani sana kubadilisha mawazo yako kwa kuwa ni hatari KWA ustawi wa nchi yetu hivyo itabidi niandike gazeti
 
Nafasi zote za teuzi za rais huwa hazifiki watu 3000.
Sasa waislamu Graduates, wenye sifa na vigezo wanazidi nafasi zote hizo nilizozitaja.

Sasa ukiniambia eti hakuna waislamu wa kutosha kuteuliwa mpaka ipelekee teuzi zifanyikazo zilalie kwa sana kwa watu wa dini moja kila wakati ni hoja ambayo haina ukweli wowote.

Sasa ukiteua makatibu wakuu 20, unataka kuniabia nchi hii hakuna waislamu 8, 9, 10, 12 wenye vigezo vya kuwa makatibu wakuu?
Naona wewe ndugu yangu una shida, Dunia yote ktk nchi zote zinatumia system kama ya Tanzania na sio ya 1:1
Nenda hata ZnZ, Kenya, Uganda, Nigeria, Chad, CAR n.kn.k
Na ukienda USA au UK weupe watakuwa wengi kuliko Rangi yangu au yako na sio 1:1:1:1
 
Mimi kwangu awe Muislamu,Mkristo, Hindu e.t.c ninachopenda kuona ni
1.Katiba kuheshimiwa
2.HAKI isiwe jambo la hisani ya Kiongozi
3. Taasisi imara zisizoingiliwa na mhimili wowote kimaamuzi.

Kubwa zaidi watu waishe kwa furaha.
 
Naona wewe ndugu yangu una shida, Dunia yote ktk nchi zote zinatumia system kama ya Tanzania na sio ya 1:1
Nenda hata ZnZ, Kenya, Uganda, Nigeria, Chad, CAR n.kn.k
Na ukienda USA au UK weupe watakuwa wengi kuliko Rangi yangu au yako na sio 1:1:1:1
Hiyo ratio ni based on assumption katika nini?
 
Si vizuri ubaguzi kuupoza kwa lugha za kidiplomasia au kuufumbia macho kwa jicho la mshikamano.

Dawa ya ubaguzi ni kuuondoa, ili tuwe na taifa lenye fairness na haki kwa wote.

Ngoja nikuulize swali, leo hii rais akateua Wazanzibar watupu kwenye ukatibu mkuu, utaona tatizo au utaona ni sawa tu!?
Akifuata vigezo hakuna shida kwani watakuwa wanachukua maendeleo ya bara au resource zaidi ya hiyo ratio ya 96:4
 
Nafasi zote za teuzi za rais huwa hazifiki watu 3000.
Sasa waislamu Graduates, wenye sifa na vigezo wanazidi nafasi zote hizo nilizozitaja.

Sasa ukiniambia eti hakuna waislamu wa kutosha kuteuliwa mpaka ipelekee teuzi zifanyikazo zilalie kwa sana kwa watu wa dini moja kila wakati ni hoja ambayo haina ukweli wowote.

Sasa ukiteua makatibu wakuu 20, unataka kuniabia nchi hii hakuna waislamu 8, 9, 10, 12 wenye vigezo vya kuwa makatibu wakuu?
Hoja ni kwamba, waislam wapo wachache.
 
Back
Top Bottom