Uchaguzi 2020 Tunaojiandaa kumpa tena kura Rais Magufuli tukutane hapa


Naona umeamua kuuleta huu uzi tena leo baada ya ule wa jana kutokupata mapambio uliyoyataka. Hatuko tayari kuendelea kuongozwa na chama cha kizee na kiongozi asiyeheshimu watu wenye mitazamo tofauti, huku usalama wetu wenye mtazamo tofauti ukigeuzwa uhaini. Sana sana jiandaeni kukaa madarakani bila ridhaa ya walio wengi. Muwe kama serikali ya kijeshi.
 
Mtakuja nipa matokeo, maana mwaka huu nitajichimbia porini, nimegundua mchango wa siasa kwenye maendeleo binafsi ya kiuchumi ni 0%, labda uwe kwenye payroll ambayo haina check number.
 
Ubarikiwe.
cc. , Rosemary John nyerere, Peter Mavunde and the rest. RIP mdogo wangu Salome Kiwaya you can read what is going on now.
Ni ujinga kuandika majina ya watu huku lako ukilificha china ya jina bandia


USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jpm ni kama ronardo hachuji

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ameishiaa kuwa teua marafik zake vyeo na kila kukucha ni kuteuu tu so far teuzi zake zawezakufika 1000 ,...kaz kdg sana afu uteuzii. naa kufukuzaa fukuzaa pangapanguwaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda kakutane na mmeo chumbani kumpongeza dikteta!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwako Mh. Rais John Pombe Magufuli

Najua siwezi kukufikia ili nikupe kura yako ambayo kimsingi nimeitunza toka 2016 mara tu baada ya wewe kuanza kufanya mabadiliko makubwa hapa nchini.

Kwa hakika umefanya 'exactly' nilichokutuma ukafanye mara tu baada ya uchaguzi 2015.

Zaidi, umevuka mipaka ya maendeleo kwa uwezo wetu kama Watanzania na kwa Africa kwa ujumla.

Walikula reli ya Dar - Arusha ukafufua.
Walikula madini yetu wakawa wanahamisha hadi mchango kwenda kujenga miji yao, umewastopisha.

Walikula ndege za mwalimu zote na shirika likafilisika, umewajaza mindege hiyo (kwa sauti ya Rais Mwinyi).

Baada ya miaka 120 ya reli ya kati ya
Mjerumani, umevunja rekodi hiyo kwa kujenga Standard Gauge.

Walijaza watu ambao hawajasoma wakawa wanatutibu kwenye hospitali hadi pale Muhimbili, umewasafisha.

Shule ya msingi hadi secondary watoto wa wakulima wanasoma bure, nimelipia tu 2500 ya picha kwa mwanangu alieanza kidato cha kwanza.

Wakazi wa Dar hawakuwahi kuona Fly Over kama nilizoona Marekani, Korea, Dubai, umewaletea Ma-Ubungo exchange ya hatari.

Umetunyoosha haswa lakini wapinzani wasaka tonge umewanyoosha zaidi. Walizoea kupiga dili na mashirika ya Umma kama Tanapa. Nasikia miaka hiyo Tanapa walimchangia Mh. wa upinzani mmoja Mil. 500, Barrick Gold wakamjengea shule kwake, akazuga kwenda Uswisi kufuatilia walioficha hela kule kumbe alipiga fungo kubwa.

Binafsi umenifungua macho, nilikuwa kwenye dimbwi la giza niliposikia kuna watu hawachukui posho za kibunge kumbe walivimbewa na mabilioni za rushwa. Siku hizi sisikii tena "siasa za posho za kibunge".

Nimechoka kutaja, naomba uje kwangu, kama utaweza, uchukue kura yako, ikiwa ni ya kwangu, na ya mama Z.

Nitarudi kuendelea!

Ahsanteni!!
 
Kuendelea na nini?Si umeshamwambia aje achukue kura?Sasa unataka utujazie server kwa lipi?

Nways nauona mwendelezo wa kuabudu,weka namba ya simu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…