DOKEZO Tunaomba Msaada: Tumedhulumiwa na LE MARAHEB RESTAURANT & more mishahara yetu na kubambikiwa kesi ya jinai na mwajiri wetu mwarabu

DOKEZO Tunaomba Msaada: Tumedhulumiwa na LE MARAHEB RESTAURANT & more mishahara yetu na kubambikiwa kesi ya jinai na mwajiri wetu mwarabu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Nitashukuru sana Mkuu. Tunaumia sana na huu Unyanyasi dhidi yetu, cha ajabu hata pale Mahakamani Kinondoni wanatuhurumia ila hawana Namna ya Kutusaidia Kumzuia Unyanyasaji wake
Nyie mnaenda kimwili mnafikiri mtasaidiwa?
Mnafikiri na wenzenu wanaenda kimwili km nyie? Ukiona anajiamini na Yuko nchi ya watu ujue kipo anachojivunia nyuma yake
 
Kosa ni kutorekodi matukio hayo.

Mngerekodi kila tukio na matusi yake hayo dhidi ya ninyi.

Pili mlikosea kwenda Mamlaka Moja tu.

Mngekwenda Immigration na ushahidi wenu huo kwamba kwamba huyu mwamba kadha wa kadha.

Huku pia mkiwahi kuripoti polisi.

Mngeona kama hatua zisingechukuliwa

Ila kwa Sasa ni kupoteza muda tu na zitabakia tuhuma

Angekuwa deported within 72 hours na kuwa prohibited immigrant

Na pesa zenu mngelipwa
Kweli kabisa
Eti ndo tabia Yake halafu hamrekodi kwann?
 
Wana Uraia wa Tanzania ila asili yao ni Yemen, wanazungumza Kiarabu na Kiswahili, Walikua na Mgahawa Mwanza Rock City Mall, Wametapeli Mishahara watu kibao mpaka Suppliers huko Mwanza wakakimbilia Dar. Pia Huyo Bosi wakike Familia yake ndio wamiliki wa Star Light Hotel Iliopo Kisutu, ila wengine wanasema Waliuza hio Star Light Hotel ndio wakafungua huo Mgahawa Wa Masaki.

Bosi wa kike anaitwa: ARIFA AL-BEITY
Bosi wa Kiume anaitwa: MAHMOUD OMAR AL-SHATRY
Edit Uzi wako juu pale weka haya majina
 
Hiyo kesi yenu ya CMA madai yenu kwenye ile fomu ya kufungulia nadai ya migogoro ya kazi mliyaweka vizuri?

Mliachishwa kazi tarehe ngapi na nyinyi mlifungua mgogoro CMA tarehe ngapi? maana unfair termination mgogoro unatakiwa kufunguliwa ndani ya siku 30 toka mgogoro ulipojitokeza.

Kwenye Fomu ya maombi mliomba stahiki zipi? Kazini mmekaa kwa muda gani? malipo mlikuwa mnalipwaje, cash au benki? Mna vitambulisho vya kazi?

Hapo CMA kama mambo yenu kwenye fomu yamekaa vizuri stahiki zenu mnaweza kuzipata. Haki Inaweza kuchelewa kwa vile mahakamani mambo huchukua muda, but kama ni haki yenu mtaipata tu.

USHAURI:
Kwa kesi zote mbili,Hiyo rufaa ya jinai na Labour case tafuteni wakili awasimamie, Laymen mnaweza msijue namna ya kupangilia kesi yenu vyema na mkaiharibu kwa kushindwa kusema mambo ya msingi.

Hasa hiyo kesi yenu ya CMA kama hamuwezi kuweka wakili basi mtafuteni wakili awe anawashauri kila mkienda mahakamani mkaseme nini na kila hatua mfanye nini..!

Ningejua cha kushauri zaidi endapo kama nongeona namna mlivyoweka madai yenu kwenye fomu ya CMA.
 
Katika masuala ambayo serikali inabidi iyatambue na iyatatue haraka ni ya unyanyasaji kwenye ajira hasa kutoka kwa watu wageni na hawa weupe.

Wengi wananyanyaswa kwa kulipwa mshahara mdogo, matusi, udhalilishaji lakini serikali yetu ni kama haijui haya yanatendeka hapa nchini. Intelijensia ilitakiwa itatue changamoto hizi zinazowakuta wananchi kila siku.

Hawa wangekuwa zambia au kenya sasa hivi na mgahawa wamefunga wamekimbia wenyewe nchi.
Au SA, Nigeria....
Thubutu yake
 
Wewe n mjinga Sana

Umenyanyaswa

Umenyimwa stahiki zako

Lakin unatetea upuuzi wa kutoitaja hyo ofisi uliyokuwa unafanyia kazi

Endelea kunyanyaswa hvyo hvyo sababu ya ujinga wako

TAJA HUO MGAHAWA TUCHUKUE HATUA



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Umenena vyema , humu jf kuna network ya hatari hata ukitaka appointment wa mawaziri tunakusaidia sasa unasema kwa mafumbo ulitarajia tukuone serious ????
 
Inaendelea👇🏽

Tulisomewa Shitaka la Kufanya Fujo na Kufukuza Wateja eneo la Biashara Majira ya asubuhi

Wote 12 Tulikana Kosa kwamba sio kweli!! Wavulana (6) na Waschana (6),
Kesi ikasogezwa mbele wiki 2/3

Hakimu: Washtakiwa wote 12 wamekana Kosa, Je una Mashahidi?

Bosi: Ndio

Hakimu: utakua na Mashahidi wangapi?

Bosi: Mashahidi wapo wengi sana

Hakimu: Utakua na Mashahidi wangapi??

Bosi: watatu, wanne, Tano hivi,

Hakimu: Utakua ba Mashahidi wangapi??

Bosi: watano (5)

Baada ya Hapo sisi Tukarudishwa Lockup ya Mahakama tukisubiri Ndugu zetu watudhamini, Bosi wa Kike akaja Lockup akatucheka sana na Kuapa Watahakikisha Tunafungwa Japo mwezi mmoja mmoja, hatuwezi kushindana na Hela. Wote 12 ilikua ndio kesi ya Kwanza maishani mwetu tena ya Kusingiziwa! Hatuna Uzoefu wowote Woga ulitushika, Hakika tulikumbuka ule msemo “Wanaokwenda Jela sio wote wana Hatia” wengine wana Watoto wadogo Majumbani wengine Wanauguza Wazee wao Majumbani tunafkiria itakuaje Hatma yetu na Familia zetu.

Baada ya Hapo yule Bosi hakutokea Mahakamani Mara mbili (2). Tulivoitwa kwa mara ya Tatu (3) tukiamini Kesi inafutwa Alitokea Mahakamani siku hio na Mashahidi wawili (Mmoja Mlinzi, mwengine Hatumtambui)
Magufuli hapa ndipo tu atakumbukwa hakukuwa na watu wa aina hii yaani wa kuvimbishiana misuli hasa kitaani.
 
Si haoni mwigulu jana kaja kutetea kiwa hana magari 60 na kaalika mawaziri wake kumtetea na kutetea tozo. Kimsingi JF ni kubwa sana na hata mama anapitia humu.
""UTANIJUA MIMI NI NANI NA NITAKUNYOOSHA"AMEFUFUKA KATIKA AWAMU YA SITA MH.SAMIA TUNAKUOMBA ZUIA KIRUSI HIKI NA KIONDOSHE KIMWAGIE SUMU KIFE NI HATARI KWA HAKI ZA WALIO WENGI.
Nina hakika huyo kubaaz anatumia fedha nyingi Sana kuhonga,wasio waaminifu badala ya kujazia ili alipe fedha za watanzania hawa wanyonge!#wayemen hovyo Sana na dhulmat.
 
Ikabidi Wafanyakazi Tufunguke kwa Askari namna Tulivotukanwa na Kutishiwa hatulipwi Mishahara yetu, yule Askari akaamuru Bosi apigiwe simu, hivo akapigiwa simu(Bosi wa Kiume ambae ni Mume wa yule Mama) na Kwa Bahati nzuri Supervisor alifanya akili akarekodi Voice ya Mazungumzo baina ya Askari na Mwajiri Wetu.m hivo ushahidi wa Voice Tunao ambapo Yule Askari aliamuru Siku inayofata (29-January-2022) saa 2 asubuhi Bosi akutane na Wafanyakazi wote kusolve hili tatizo na Atulipe Mishahara Yetu lasivo tukishindwa Kuelewana Turipoti kituo cha Polisi ili Tuelekezwe wapi tutapata Msaada.

Ikabidi Tuwajulishe na Wenzetu ambao waliingia shift ya Mchana yaliojiri usiku huo ili wote Tukutane asubuhi.

Siku ya Pili tulifika Kazini asubuhi tukimsubiria Bosi kabla ya Muda wa kazi Kufika (Mgahawa unafunguliwa saa 6 Mchana),

Yeye na Mkewe waliwasili saa 5, Wakatuita Tuongee na sisi tukatii, Tulikua 15, Bosi wa Kiume akaomba Supervisor ajitokeze na alivojitokeza tu Gafla yule Bosi akamtukana Matusi na Kumsukuma. Sisi wote tukainuka na Kuondoka kwani tuliona Hamna Usalama.

Baada ya dakika Chache Likaja Defender likataka kumchukua Supervisor Pekee ila akajitetea ana madai yake ya Mshahara pamoja na Sisi wengine hivo Wote tukapanda kwenye Gari kasoro watu 3 walibaki waliona Sio Dalili nzuri.

Hilo ndo kosa Tuliofanya, baada kufika Polisi Tukaeleza Madai yetu ya Mishahara, yule Mama akadai sisi tuna wiki mojamoja Kazini hivo hawez kutulipa kitu ambacho ni Uongo!

Pia Ilivofika Saa 12 Jioni Mkuu wa Kituo akasema Tupo chini ya Ulinzi tusubiri Kupelekwa Lockup, na yy pamoja na Askari wake waliondoka Na Bosi zetu Wakidai wanaenda Kufanya Uchunguzi, ila ukweli ni kwamba walialikwa Mgahawani na Kupewa Dinner ya Nguvu (Wenzetu waliobaki Kazini walitutonya)

Polisi waliporejea Kituoni saa 3 Usiku tuliruhusiwa Kurudi nyumbani kwa Sharti kwamba iwe Siri kwamba Hatukulazwa Lockup hata Wenzetu waliobaki Kazini tusiwaambie Siri hii.

Hatimae wakaamriwa Watulipe Mishahara Yetu na wao wakasema Watatulipa siku ya Jumanne hapo Kituoni.

Sasa jinai ipo wapi? Hamjielewi! Elimu elimu elimu
 
NAWASHAURI JIACHAGUENI VIONGOZ 3 NENDENI MKAFUNGUE KESI KITUO CHA POLISI, WAKUBALI AU WAKATAE KUFUNGUA KESI, NENDENI PIA KWA RPC MKAMPE TAARIFA YA SHIDA YENU...
Yakishindikana yote haya kama police wataamua kukaa upande wa hao ngurue wa kigeni... Chomeni moto huo mgahawa au wekeni hata sumu wateja waharishe tu bila kufa...
USIKUBALI kuonewa ktk ardhi ya nyumban kwako...

Hivi Amza bado upo hai? Si ulikufa pale sarenda?
 
Back
Top Bottom