Tunaomlaumu Tundu Lissu hebu basi tuvae viatu vyake

Tunaomlaumu Tundu Lissu hebu basi tuvae viatu vyake

Tundu Lissu hafai kuwa Rais wa JMT. Mimi siyo CCM wala CHADEMA, yaani sina chama. Lakini sina trust na Lisu kabisa kwa usalama wa Taifa letu.
Huo usalama wa taifa letu sasa

IMG-20210324-WA0053.jpg
 
Hakuna bora kati ya Magufuli wala Lisu, isipokuwa, msaliti wa Taifa hukumu yake ni kifo tu, hayo hufanyika USA kwa mababa wa demokrasia, hufanyika Russia, Ufanyika China na kwingineko. Sisi bado tupo nyuma sana kwenye execution za namna hii, na zinatakiwa kufanyika hadharani kabisa watu wajifunze.

Mpango wa aliyetuumba lazima utimie hata mkikesha kwa maombi, ulitimia kwa Lisu kujeruhiwa, umetimia kwa prezoo kupita hivi, mwishowe, kila nafsi itaonja mauti, hata wale ambao hawajawahi kuchinja hata kuku tu.

Maombi ya hadharani hayana maana yeyote, maana unachokiomba hata hakionekani pia. Kwa muktadha huo, Basi kila nafsi ijililie yenyewe na uzao wake, period.
 
Hiki kitendawili nmewahi kujiuliza kwamba Sirikali inafanya sirikali juu ya Uhai wa watu makini..Kama TAL.!!Sikuwahi waza sirikali kushindwa kutafakari Unyama ule kuwa Kundi lililohusika ingeweza kulifanya ni Sirikali!! SIRIKALI TUONANE PARIDISO!! PARADISO BHAKWETU!! AMENI
 
Ukisikia ule msemo unaosems "Mkuki kws Nguruwe" ndiyo unaingia hapa sasa. Lissu ni mwanafamu. Hivyo na yeye ana hisia. Sidhani kama anafurahia kuishi uhamishoni. Ila kwa sababu za kisiasa na pia usalama wake, ilimlazimu kufanya hivyo.

Mwacheni ateme nyongo yote, ili arudi kuwa binadamu wa kawaida kama sisi.
 
Tundu Lissu hafai kuwa Rais wa JMT. Mimi siyo CCM wala CHADEMA, yaani sina chama. Lakini sina trust na Lisu kabisa kwa usalama wa Taifa letu.

Wazo lako zuri ila ni op hatari na uzi huu
 
Mimi ni mwanaccm lakini kuondoa nafsi ya mtu duniani kwa kisingizio cha usaliti ni dhambi isiyosameheka hata utubu vipi bila kumuomba radhi mtrndewa. Mungu apambane nao waliomshambulia Lissu bila hatia.
 
Wasalaam wapendwa!

(Mods mniwie radhi msiunganishe uzi huu na ziingine tupeane ukweli pengine tutapunguza chuki baina yetu na kusahau yaliyopita tugange yajayo)

Kila mara humu mtu ukisoma vizuri comments za kila mada huwezi kupita bila kukutana na neno UNAFKI. Hili neno linasemwa kulingana na sisi wenyewe tulivyo na vitabia vyetu.

Hivi Tundu Lissu kabla haijapigwa risasi akachungulia kaburi na kurudi tuwahi kusikia akiitwa msaliti na nani?

Hebu vaa viatu vyake chukulia kua wewe ni tundu Lissu,
1.Upigwe risasi 16 saa 7 mchana kweupe na mpaka leo hii wasijulikane waliotenda tukio hilo
2.Chukulia wewe ndio Tundu Lissu unyimwe gharama za matibabu yako kama mbunge bila sababu yeyote ya msingi
3.Chukulia wewe ndio Tundu Lissu mpaka leo unyimwe nafsi yako ya ubunge na stahiki ziingine
4.Chukulia hii wewe ni Tundu Lissu unaporwa ubunge wako hadharani bila sababu ya msingi
6.Chukulia wewe ndio yeye unapata matatizo watu wanazuiwa hata kukusanyika kukuombea kwa Mola upone.
6.Chukulia wewe ni Tundu Lissu unaarifiwa na vyanzo vya ndani ya mfumo kama asemavyo yeye kua ilitolewa amri kua shughuli ilitakiwa imalizike mapema kisha apumzishwe haraka kijijini kwao mapema bila kuagwa, hivi kwa maneno haya upendo utoke wapi?


Tunaomwita Lissu mtumwa wa Mabeberu hebu mfikirieni na yeye kwa vyote aliyofikia nayo. Mbona hatukumwita msaliti kabla? Hivi yeye si binadamu na asinune wala kuchukua ana moyo wa chuma?
Hivi chuki zako kwa JPM hadi lini? Unachosha
 
Tundu Lissu hafai kuwa Rais wa JMT. Mimi siyo CCM wala CHADEMA, yaani sina chama. Lakini sina trust na Lisu kabisa kwa usalama wa Taifa letu.
Mbona hukusema hayo kabla haijapigwa risasi?
 
Mbona Billicanas ilivunjwa lakini Mbowe haongei ujinga ujinga kama huyo Tundu Lisu?
Wewe chok&o husifananishe mali na haki ya kuishi. Mali zinatafutwa,uhai hautafutwi. Magu kafa kama alivyokufa baba yangu tu, kulia na kuudhunika ni matakwa ya binadamu mwenyewe. Kama binadamu aliishi kwa upanga haoa dunia, munataka tusema aliishi kama malaika?
 
Hivyo viatu sijui safari buti au mokasini tutavivaa baadae, sasa hivi wengine tunaomboleza kwanza.
 
Mkuki ni mtamu kwa Nguruwe, Kwa Binadamu mchungu.

Binafsi sijaona huo ubaya wa Lisu. Yote anayosema ni ya kweli. Namshukuru alinijuza kuwa Rais wetu ni mgonjwa, na nikaja kuujuwa uhalisia wa ukweli.
 
N
Wewe chok&o husifananishe mali na haki ya kuishi. Mali zinatafutwa,uhai hautafutwi. Magu kafa kama alivyokufa baba yangu tu, kulia na kuudhunika ni matakwa ya binadamu mwenyewe. Kama binadamu aliishi kwa upanga haoa dunia,munataka tusema aliishi kama malaika??
Mbwiga yule boss wenu Lisu analilia mafao ya ubunge!
 
Back
Top Bottom