Uchaguzi 2020 Tundu A.M. Lissu: Mgombea Urais wa upinzani machachari zaidi kuwahi kutokea katika chaguzi zote chini ya mfumo wa vyama vingi kurudi 1992

Lissu amewabananisha kwenye kona ya kitanda hadi imefika hatua wanaccm na mavitambi yenu mnavamia vyombo vichafu vya wapiga kura na kulazimisha kuviosha ili mpigiwe kura [emoji1787]
Baada ya oktoba utaelewwa
 
Huyu TAL ndiye presidential material katika uchaguzi huu kulioko mgombea yeyote. Namuombea kwa Mwenyezi Mungu amuondolee mazonge yote katika njia yake ya kuelekea Ikulu
 
Ogopa sana spana za huyu mtu anayeitwa Tundu Lissu zimewaingia CCM hadi imefikia hatua mgombea wa CCM na polepole na meza kuu wanawapigia wananchi magoti na kuwaomba kura 🤣

Dogo hiyo ni sanaa tuu, Maeneo ya Njombe unapoomba kitu kwa uaminifu na anaeombwa ni vigumu kukunyima ni kuomba kwa kupiga magoti. Uliza watu wa Njombe humu wakujuze. Wanasiasa Sanaa.
 

..uzuri wa TL ni kwamba anapozungumzia suala lolote lile anakuwa amelichimba mpaka historia yake.

..kwa mfano, jana alikuwa anazungumza na wananchi wa Serengeti, basi alianza na historia ya hifadhi hiyo, akaja mpaka kuzungumzia tafiti mbalimbali zilizofanyika kuhusu uhifadhi, na baadhi ya njia mbadala zinazopendekezwa kuhusu masuala ya uhifadhi.

..sasa uzuri ni kwamba alifanya yote hayo akitumia lugha rahisi inayoeleweka na wananchi wa kawaida. Na pia TL huwa na mazungumzo na wananchi, tofauti na wanasiasa wanaohutubia wananchi.

..Hiki ni kipaji ambacho nimegundua wanasiasa wengi hapa Tanzania hawanacho. Kingine kinachombeba Tundu Lissu ni REKODI yake ya miaka mingi kutetea wananchi wanyonge.
 

Kuna kitu ambacho lazima ukifahamu vizuri, Law is politics. kwa hiyo manasheria mzuri ni rahisi sana kuwa mwanasiasa mzuri.

Jee umewahi kujiuliza kwa nini asilimia karibu 90 ya politicians ni ama Lawyers ama waliochukua Humanities na wala sio Scientists ?

Lakini kwa kutatua tatizo Scientists ni wazuri sana kuliko Lawyers au waliochuku Humanities. Lakini pia wapo ambao wana vipaji vya kutatatua matatatizo. Lakini wengi wao wana lack ability to coherently organise people (leadership).

Kwa kuwa Political (election) campaigns zina endelea , tuta pata muda wa kutosha kuvumbua vipaji vingi sana katika siasa.
 
Ongezea na hii: ....mgombea urais aliyekuja na nuksi ya kuambulia wabunge 4 tu kwa chama chake na kupata kura kiduchu kuwahi kutokea single digit 7% ya kura za urais!
Kwa kutumia MAHERA inawezekana
 
Ukweli mtupu .
 
Ongezea na hii: ....mgombea urais aliyekuja na nuksi ya kuambulia wabunge 4 tu kwa chama chake na kupata kura kiduchu kuwahi kutokea single digit 7% ya kura za urais!
Nyomi lile mnang'oka...mkiiba kura Lissu anauwezo wa kuhamasisha watu waingie road..polisi watavua magwanda tutawachapa nyie Mataga na makalio yenu makubwa kama Bashite
 
Umeandika uchambuzi mzuri sana; binafsi nimejikuta napata hamu kumuona Lissu akiendelea kuwa mgombea Urais hata 2025 and beyond if possible, ni mwalimu, mshauri, mtetezi, na sifa nyingine nyingi tu.

Ni matumaini yangu atashinda this year, then ataendekea kuwa Rais mpaka 2030, muda wake wa vipindi viwili utakapokwisha.
 
Hana lolote, zaidi ya matusi na jazba. Baada ya slaa kuondoka, chama saccos kwisha kabisa. Mnapoteza muda kuzunguka nchi nzima, huku mkijua hamuwezi shinda.
 
Kwani kina Martin Luther walikuwepo wangapi?

Nyie magamba siku zote mna hoja za ajabu ajabu sana...

Unazungumzia kizazi kipya cha wabunge wa CCM bungeni kuja na hoja motomoto, chini ya bunge hili la Ndugai?! wewe kweli hujielewi.

Topic mbili au tatu kwa Lissu za nini? yule akili kubwa, anabeba topic nyingi na zote anazichambua wasikilizaji wake tunamuelewa vizuri kabisa na hamu ya kumsikiliza haiishi, wewe na kichwa chako cha lumumba beba hiyo moja uende nayo popote utakako.
 
Jipe muda kuelewa na kutofautisha utawala wa kimajimbo na wa kikabila. Utawala wa majimbo haina maana kuwarudisha watu katika maeneo asili ya makabila yao bali ni kuwapa wananchi katika maeneo yao wanayoishi fursa na nguvu zaidi ya kufanya maamuzi juu utawala,rasilimali na kodi katika maeneo wanayoishi bila kujali kabila la mtu.
 
Hakuna tatizo watu kuchagua watu kwa vigezo vya Mswahili,mnyika au mshamba.Hiyo ndio demokrasia na wakati mwingine ina gharama chungu sana ukiwa na taifa lenye wajinga wengi,jambo la muhimu ni uwanja sawa wa kisiasa wenye kutoa fursa ya uchaguzi huru na wa haki na ionekane hivyo.
 

1. Wewe unasema ishu ya kuchagua "topic" mbili ama tatu tu ili aende nazo kwa wananchi kuombea kura, au siyo?...

Mimi nakuambia hivi, "topic" hizo tatu ni nyingi mno na zinaingia katika agenda kuu ya UHURU, HAKI na MAENDELEO YA WATU...

Ndiyo sasa kusema kuwa, Tundu Lissu anasimamia na amebeba agenda (siyo topic) moja tu ambayo ni UHURU, HAKI na MAENDELEO YA WATU...

2. Ni kweli, mtu mmoja hata akiwa mzuri kiasi gani hataweza kuleta mabadiliko ya uzuri katika jamii yoyote bali mpaka wawepo kadhaa kama yeye...

Ndicho kinachofanyika sasa. Anafundisha, hamasisha, kutia morali na kuelekeza ili watu wajue na kutambua WAJIBU na HAKI zao za kiraia...

Hiki ndicho kunachopingwa na kujaribu kuzuiwa na watawala kwa hila na kwa nguvu zote....!!
 
Ongezea na hii: ....mgombea urais aliyekuja na nuksi ya kuambulia wabunge 4 tu kwa chama chake na kupata kura kiduchu kuwahi kutokea single digit 7% ya kura za urais!
Mahaba
 
Ongezea na hii: ....mgombea urais aliyekuja na nuksi ya kuambulia wabunge 4 tu kwa chama chake na kupata kura kiduchu kuwahi kutokea single digit 7% ya kura za urais!
Sasa huu ni ushabiki wa kisiasa unaokupelekea kuukataa ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…