Pre GE2025 Tundu Lissu: Abdul (mtoto wa Rais Samia) alitaka tukutane kwenye hoteli moja Masaki anihonge, nikamwambia njoo kwangu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
hongo huwa inasababu, daktari akjtibu, hakimu ushinde kesi, polisi uachiwe sasa yeye wamhonge kwa lipi? kama aliona ni hongo nayeye ni wakili kwanini hakutoa taarifa takukuru?
Dogo ndo umekuja mjin Jana? Takukuru which?
 
Huyu kijana Lissu si wa kumwamini kabisaa. Ni mropokaji tu
 
Shida Mbowe kakaa kibiashara biashara. Na ukiona Lissu hajataja atakuwa yeye au Mrema. Ndio maana Kuna kamvutano fulani. Siasa hii nchi ujinga kabisa wananchi tusipoamua wenyewe tukategemea Hawa tumepotea
 
Angeenda aone maana alimsimanga wakati huyo kijana alienda Uganda kuiwakilisha nchi.
 
Je ni kweli ushahidi haupo
 
Bhc atakua mnafiki kwann asimtaje na wa chama chake tujue ni kweli?
Alaf kama alikua hazitaki kwann amuambie amletee kwake?
Siasa mchezo mchafu
Salum Mwalim
 
Anakataa pesa ila za kuchangiwa ndio anataka si ndio? 😂😂😂😂
 
hongo huwa inasababu, daktari akjtibu, hakimu ushinde kesi, polisi uachiwe sasa yeye wamhonge kwa lipi? kama aliona ni hongo nayeye ni wakili kwanini hakutoa taarifa takukuru?
😂😂😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣😁😁😁😆😆
 
Cha msingi alipelekewa hongo asigombee......mwaka huu kitawaka.

Nguvu ya Lissu iko Wazi 2025 Patachimbika.

Kwanini wanahangaika kumhonga? Ina maana wanaamini Lissu anaweza kushinda kwa Kura?

Time will tell
Nguvu yake iwe kubwa au ndogo hawezi kushinda na hakuna kitu mtafanya
 
Your browser is not able to display this video.


Kwa muhitasari:

Tundu Lissu: "aliwatumia watu wema wa chama changu. Na kwanza aliniomba tukutane katika hotel moja sijui inaitwaje huko maeneo ya Masaki, DSM...."

Tundu Lissu: "Nikawaambia mwambieni kama ana shida na mimi wamlete nyumbani kwangu. Walimleta na tulikaa hivi hivi face to face kama tulivyokaa mimi na wewe hapa mwandishi"

Tundu Lissu: "Alisema anataka kunisaidia. Nikamwambia kama kweli unataka kunisaidia, mwambie mama yako ambaye ni Rais alipe pesa zangu za matibabu zenye risisti. Hizi za kwako ni hongo, hazina risiti"

Tundu Lissu: "Akasema, ooh, mama (Rais Samia) analalamika hujawahi kumwandikia kuomba hizo pesa. Nikamwambia nilishaandika mara mbili. Pamoja na hayo nilimpa nakala ya madai yangu, nikamwambia si anasema sijamwandikia? Mpelekee barua yangu ya madai nakala hii hapa. Mpaka leo kimya, hajawahi kuwasiliana nami tena......!"

Tundu Lissu: "Kwangu hakuna CCTV cameras. Lakini sikiliza, nafahamu mimi ni mwanasheria. Na katika sheria ya ushahidi, ushahidi ulio bora kabisa kisheria ni ule wa mtu kuona, kusikia, kushika na kunusa mwenyewe. Mimi niliona mwenyewe. Zaidi pia ni kuwa katika mazungumzo yale, tulikuwa na watu wanne jumla ndani/au mahali tulipokuwa na huyo mgeni na huko nje kulikuwa na walinzi wa kutosha"

Kwa uelewa zaidi, tumia bundle lako kumsikiliza na kumtazama mwenyewe hatua kwa hatua hadi mwisho...
 
Haya CCM tunaomba majibu, hii ndiyo sera yenu?
 
Kwa njaa ya Msigwa angezichukua fastaa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…