Ni ajabu sana kuona watu mnakimbilia uchaguzi tu bila kujali sheria zinazosimamia uchaguzi wenyewe. Hata kwenye michezo tu sheria zinabadilishwa kila mara kuhakikisha kila anayeshiriki anapa haki. Uchaguzi mkuu wa wabunge na rais huamua hatima ya maisha ya jamii husika (wananchi). Kusipokuwepo na sheria isiyopendelea upande wowote ni rahisi sana kupata viongozi (wawakilishi) wasiojali maslahi ya wananchi na kujiamlia mambo kulingana na utashi na kwa faida yao. Mfano aje hapa mzalendo sana aseme kwa nini rais halipi kodi, kwa nini hawezi kushitakiwa kwa makosa ya kiongozi, nk. Kuleta uwajibikaji lazima tujiwekee sheria na taratibu zinazombana kila mtu bila kujali cheo chake.Neno, kipuuzi tu ndipo ulipoharibu sio misimamo ya kipuuzi. Ila uko sawa kwenye misimamo. Alegeze masharti achague watu makini sana wa kuingia kukohoa bungeni mpaka huku nje panatetemeka hata kama hawatapata Urais nchi itachangamka.