Mh Lissu amefanya misa ya kutoa shukrani kwa mungu kwa kumponya na mauti akiwa nyumbani kwao Ikungi, Singida.
Azungumza mengi na kuwaliza mamia ya watu waliokuwepo hapo juu ya mateso aliyoyapitia kama binadamu.
"Naahidi sitampitisha mtu yeyote kwenye maumivu yale niliyoyapata hata kama atakuwa amenikosea kwa kiwango gani."
Ni kauli ya Tundu Lissu leo 10.08.2020 baada ya kushiriki Misa ya shukrani, Kanisani Ikungi, Singida.
Kweli Watanzania tumshukuru sana mwenyezi Mungu kwa kutuletea huyu kiumbe maana atatuvusha na kutupeleka nchi ya asali na maziwa.