Tundu Lissu akamatwa na Polisi akiwa Ngorongoro hotel Wilayani Karatu
Activists and politicians serve different roles in society.

Activists are individuals or groups who advocate for specific social, political, or environmental changes. They often use protests, advocacy, and public awareness campaigns to raise issues and pressure those in power to make changes.

Politicians are individuals elected or appointed to public office who work within established political systems to create and enforce laws and policies. They often engage in negotiations, compromise, and legislative processes to achieve their goals.

Kwa hilo Tudu Lisu amesha kua activist sio mwana siasa tena, kuna haja ya Chadema kurevist kazi zao.
Mnashida sana nyie, nimeshasema achaneni na tabia za kukariri kila kitu bila kutumia akili zenu, hiyo itawasaidieni kuwa salama.
Hebu rudia kusoma ulichokiandika.
 
Kuna tetesi kuwa Tundu Lissu amekamatwa na Polisi asubuhi hii akiwa hotelini huko Karatu.

Taarifa zaidi kukujia hapahapa jukwaani.

UPDATE:
Waliokamatwa Karatu hadi sasa ni

  1. Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Lissu
  2. Walinzi wote wa Tundu Lissu
  3. Katibu wa BAWACHA Catherine Ruge
  4. Mzee Hashim, Mwenyekiti Wa Baraza La Wazee CHADEMA Taifa
  5. Suzan Kiwanga na
  6. Mwandishi wa Jambo TV (Oscar).

Polisi wanaendelea kuwatafuta wengine walio ambatana na Tundu Lissu Wilayani Karatu

View attachment 2744826

====

Leo Septemba 10, 2023 Majira ya saa nne asubuhi Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu lilifika Hotel ya Ngorongoro iliyopo Karatu na kuizingira, Polisi hao wakiwa na mitutu ya bunduki pamoja na mabomu. Jeshi hilo liliwaeleza wahudumu wa hotel hiyo kuwa wanataka kujua chumba alicholala Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara Mhe. Tundu Lissu wakaelezwa na kwenda kwenye chumba hicho.

Baada ya purukushani ya Jeshi la Polisi na walinzi wa Mhe. Lissu, Jeshi hilo lilingia kwa nguvu katika chumba alichofikia Mhe. Lissu na kuondoka nae bila kueleza wanaenda nae wapi.

Baadae wengine waliokamatwa na Jeshi hilo ni Mhe. Susan Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Catherine Ruge Katibu Bawacha Taifa, Mhe. Twaha Mwaipaya, walinzi wa Mhe. Lissu pamoja na watu wengine.

Tunaendelea kufuatilia kinachoendelea Karatu.
View attachment 2744848
Samwel Welwel
Jeiwii mbona mnatazama tu huu uonevu kwa raia wema wa nchi hii,wanaotetea wenzao dhidi ya ukandamizwaji wanaofanyiwa. Tena hawavunji Sheria za nchi ila polisi ndio wanaokiuka katiba na Sheria. Tunawaomba JWTZ mtusaidie raia wa nchi hii. Tumechoka kunyanyaswa ndani ya nchi yetu. Maadui sio lazima watoke nje ya mipaka ya nchi yetu! Tumegundua maadui wabaya zaidi wapo ndani ya mipaka. Kweli Bora wakoloni wazungu warudi kututawala kuliko kutawaliwa na hawa viongozi wanaotunyanyasa na kuharibu nchi kiasi hiki. Ee Mwenyezi Mungu tusaidie.
 
Hii nchi ina watu waajabu sana Jana niliwasikia wakiomba wakamatwe,wapigwe risasi na wakajinadi kwamba hawaogopi mtu na hawataondoka Barabarani.
Kwa ufupi waligoma kuondoka barabarani.

Leo tunaambiwa wamekamatwa kosa halijulikani na wameonewa sana wale mabingwa waliosema hawezi kufanywa lolote kwakuwa wana nguvu!

Siasa za namna hii sizipendi kabisa pamoja na kwamba siwapendi CHADEMA hasa baadhi ya viongozi wao lakini pia sioni CHAMA kinachoweza kutoa suluhisho la matatizo ya wanachi ingawa hakuna ubishi kwamba huwezi kuwaridhisha wanadamu wote.

Suluhu kije CHAMA kipya chenye watu wapya wenye maono na Sera pendwa angalau asilimia 90.
 
Kama ni kweli, basi hakutakuwa na jipya. Tutakuwa tunaendelea kushuhudia uhayawani wa watawala.

Hayo huwa yanatokea wakati waovu na wavunjaji wa sheria na katiba wanapopewa kazi ya kusimamia utiifu wa sheria na katiba.
Tatizo mmegoma kuacha kuwaza Bandari, Sasa Lissu lazima asaidie muisahau bandari kama inachukuliwa kwa utaratibu unaokubalika na wengi ama hapana!

Kalagha bao!
 
Sawa, hawa wakimkamata, hiyo haijibu hoja....

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Nimekusikia Muhifadhi uchwara.

Ongezeko la watu ni Ngoro ngoro pekee?

Use common sense.

Just incase... Unataka kuzungumzia uhufadhi njoo ukiwa umekamilika... Yellowstone conservation doesn't work with NCAs.
We can't do things the way Americans does. Hivi Yellow kuna endangered species kama tembo,chui na faru?
 
Mnashida sana nyie, nimeshasema achaneni na tabia za kukariri kila kitu bila kutumia akili zenu, hiyo itawasaidieni kuwa salama.
Hebu rudia kusoma ulichokiandika.
Nilijua tu majibu yako utatukana tu kwasbb you are parochial huna hoja zaidi ya matusi
 
We can't do things the way Americans does. Hivi Yellow kuna endangered species kama tembo,chui na faru?
Yes. na kama hatufanyi kama Americans solution sio kuwahamisha wamasai kwa excuse ya uhufadhi.

Wamasai kwa namna ya pekee wana Co exist na ecology ya NCA, hakuna endangered spp ambae anawindwa kwa namna yeyote na wamasai, tena wao ndio wenye interests na indigenous knowledge ya conservation ya hizo endangered big mammals.

Kuwaondoa Wamasai haisaidii kabisa ku preserve NCA.. ni hisia za wahifadhi uchwara kuliko sayansi.
 
Jeshi letu hakika halina hekima ya kazi. Hivi inakuwaje unamkamata mtu ambaye anajitafutia riziki?? Hivi sisi CCM hatuwezi kupita huko kuondoa sumu??? Hivi tangu lini polisi watumike kisiasa???? Hakika Dkt Samia anayokazi kwa utendaji huu wa polisi. Na inawezekana polisi wanamhujumu Mama kwa makusudi kabisa kuharibu rekodi yake nzuri ya haki za binaadamu. Lisu mwenyewe huyo ikitokea kafa kwa sababu ya magonjwq si atakujilikana kauawa. Yaani leo polisi wametukera sana sisi wana CCM. Na kibaya zaidi Dkt Samia alishatoa onyo kuwa siasa za wazi ruksa na uhuru wa kujieleza usibinywe.
..
IMG-20200121-WA0012.jpg
 
Nilijua tu majibu yako utatukana tu kwasbb you are parochial huna hoja zaidi ya matusi
So, ukionacho hapo ni matusi? Nimeshaandika, acha tabia ya kujariri utaishia kujipotosha kwenye kila kitu.
Grow up it, zitumie akili usikubali kichwa chako kiwe store ya tafsiri na misemo ya wengine.
 
Kuna tetesi kuwa Tundu Lissu amekamatwa na Polisi asubuhi hii akiwa hotelini huko Karatu.

Taarifa zaidi kukujia hapahapa jukwaani.

UPDATE:
Waliokamatwa Karatu hadi sasa ni
  1. Makamu Mwenyekiti CHADEMA Tundu Lissu
  2. Walinzi wote wa Tundu Lissu
  3. Katibu wa BAWACHA Catherine Ruge
  4. Mzee Hashim, Mwenyekiti Wa Baraza La Wazee CHADEMA Taifa
  5. Suzan Kiwanga na
  6. Mwandishi wa Jambo TV (Oscar).

Polisi wanaendelea kuwatafuta wengine walio ambatana na Tundu Lissu Wilayani Karatu

View attachment 2744826

====

Leo Septemba 10, 2023 Majira ya saa nne asubuhi Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu lilifika Hotel ya Ngorongoro iliyopo Karatu na kuizingira, Polisi hao wakiwa na mitutu ya bunduki pamoja na mabomu. Jeshi hilo liliwaeleza wahudumu wa hotel hiyo kuwa wanataka kujua chumba alicholala Makamu Mwenyekiti wa Chama Bara Mhe. Tundu Lissu wakaelezwa na kwenda kwenye chumba hicho.

Baada ya purukushani ya Jeshi la Polisi na walinzi wa Mhe. Lissu, Jeshi hilo lilingia kwa nguvu katika chumba alichofikia Mhe. Lissu na kuondoka nae bila kueleza wanaenda nae wapi.

Baadae wengine waliokamatwa na Jeshi hilo ni Mhe. Susan Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. Catherine Ruge Katibu Bawacha Taifa, Mhe. Twaha Mwaipaya, walinzi wa Mhe. Lissu pamoja na watu wengine.

Tunaendelea kufuatilia kinachoendelea Karatu.
View attachment 2744848
Samwel Welwel

===

Jeshi la Polisi wilaya ya Karatu wameamuru kufungwa kwa ofisi ya Chadema wilaya ya Karatu na kuwakamata watu wengine wakiwemo viongozi wa Chadema wa wilaya hiyo.

1. Joseph Mtui
2. John Malle
3. Fabiola Niima
4. Daniel Mnyampanda
5. Eliya Kibola, Katibu wa Chadema wilaya ya Karatu
6. Valerian Qurama
7. Samwel Welwel, Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Karatu
Utii bila shuruti ni kitu kidogo sana. Hata nyinyi CHADEMA kama mtabahatika kuchukua uongozi wa nchi mtataka maagizo yenu yatekelezwe.

Maasai deserve a better life outside the Ngorongoro area where they are mixed with wild animals. Let us support the Government initiative to re-settle then in Handeni where they will live a decent life like other Tanzanians. Say #NoToPrimitiveSocieties
 
Back
Top Bottom