Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anaanza kutumia lugha chafu

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anaanza kutumia lugha chafu

Broo tujadili mambo ya kitaifa hayo ya kisiasa hayatuhusu sana.

Hata jiwe alikuwa anaita Lowasa na Sumaye kuwa ni majizi na mafisadi yamenikimbia CCM leo yupo nao CCM na alishindwa kuthibitisha wizi wao.
 
Hoja gani? Tangia kampeni zimeanza uneshasikia kuna hoja yoyote kutoja kwa lisu?
Kwani hoja ni nini jamani? Na magufuli huwa anajibu maana tumeshamsikia akijitetea juu ya uwanja wa chato na vitambulisho vya wamachinga
 
Broo tujadili mambo ya kitaifa hayo ya kisiasa hayatuhusu sana.
Hata jiwe alikuwa anaita Lowasa na Sumaye kuwa ni majizi na mafisadi yamenikimbia CCM leo yupo nao CCM na alishindwa kuthibitisha wizi wao.
Hawa ndugu hawana kumbukumbu,lakini pia uccm unawatoa ufahamu hadi wanasahau nchi yao
 
Tunajua mnatamani sana kuingia ikulu na ni haki yenu, ni bahati mbaya kwamba tayari mmesha feli kukamata dola, sababu zitazowafelisha ni ilani yenu. Kinachowafelisha ni hiki hapa;..
CCM imeharibu pengi na ina matatizo mengi, lakini hawa wengine ndio hovyo kabisa kuliko CCM. Kwa kuwa sumu haionjwi, wacha tuendelee na CCM.
 
Alie itwa mwizi akanushe mwenyewe kampuni ya mayanga na mengineyo kaa kwa kutulia mkuu mnyolewe make Lissu anatufumbua macho tulikua hatujui wengi.
Na zile elfu ishirini za vitambulisho, ule ni wizi maana matumizi yake hayajulikani na hazikaguliwi na CAG
 
jiwe ni mwizi tu aliyejivika ngozi ya uzalendo kwa watanzania wanyonge, kama hawajaridhika wakafungue kesi wamushitaki Lisu
 
Kwenye harakati zangu za kufuatilia majukwaa mbalimbali ya kampeni ya wagombea Urais mbalimbali, kwa hali isiyotegemewa ghafla nimemsikia mgombea Urais wa Chadema Ndugu Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano wake wa kampeni kule Karagwe, Bukoba kuhusu viongozi wetu wa dini.

Kwenye mkutano huo, Lissu licha ya mambo mengine aliyoyazungumza lakini zaidi alitamka hadharani kwamba katika nchi hii yote ya Tanzania viongozi wa dini wenye akili na waliobaki ni watatu tu. Lissu aliwataja kwa kile alichokiita viongozi hao ndio national conscious yaani ndio viongozi wenye akili na wanaojitambua kuwa ni Askofu Bagonza, Askofu Mwamakula na Sheikh Katimba nje ya mamia ya viongozi wetu wa dini.

Lissu anasema hao watumishi wa umma watatu ndio viongozi pekee wanajitambua nje ya mamia kwa mamia ya viongozi wetu wa dini. Wakati nikitafakari kauli hii, ghafla nakumbuka namna sasa ilivyokuwa ni kama tabia iliyoota mizizi kwenye chama hicho na mwendelezo wa Lissu na chama chake kushambulia, kutweza utu, heshima na kutukana makundi mbalimbali kwenye jamii yetu na mara hii kwa viongozi wetu wa dini.

Baada ya kutweza na kuwavunjia utu waandishi wa habari kwa kuwafukuza kwenye mikutano yao, kukashfu wasanii kwa kuwaita watu wanaojipendekeza na wanaoburuzwa, kuwaita watumishi wa umma watu wa majalalani na makundi mengine mengi kwenye jamii sasa Lissu amevuka mipaka mpaka kuwavunjia adabu viongozi wetu wa dini. Hivi kwenye nchi hii viongozi wenye akili ni watatu tu? Hao wengine wote kwa mujibu wa Lissu ni hovyo na wala hawana akili yoyote ile. Lissu anakashfu watu hawa muhimu kwa ustawi wa nchi yetu mbele ya mkutano unaorushwa mpaka na vyombo vya habari. Dharau gani hii?

Viongozi wa dini ni kama Baba, Walezi wa amani na wapatanishi kwenye nchi, leo mtu mmoja tu tena anayetaka ridhaa ya cheo kikubwa kama cha Urais anakaa hadharani mchana kweupe kukashfu na kutukana waziwazi viongozi wetu wa dini. Watu wanaofanya kazi kubwa namna hii kwenye nchi.

Hii, moja ni dharau kwa watumishi wenyewe wa dini, familia zao na kundi kubwa la waumini walioko nyuma yao. Mtu kama Askofu Kakobe au Mufti Zubeir unamvunjia heshima maana yake umekashfu kundi kubwa la watu lililoko nyuma ya watu hawa. Pili ni hatari kwa mtu anayetaka Urais wa nchi kufanya kejeli kiasi hiki ambapo hana hata huo Urais, kushambulia na kutukana makundi mbalimbali kwa jamii.

Hili ni la kukemewa na kupigwa vita na watu wote. Na viongozi wa dini kama walezi wanalo jukumu la kutoa tamko kukemea vitendo hivi. Tunafahamu nyakati za kampeni ni za kuomba kura na kujinyenyekea kwa watu ili wakuchague. Sasa hawa ambao hata kabla hawajapata huo Urais wanakuwa viburi na kejeli namna hii kesho wakiupata huo Urais itakuwaje? Mtu mwenye shida anakuwa jeuri namna hii mkimpa hicho cheo hali itakuwaje? Watanzani twende tukawanyime kura watu hawa Oktoba 28.

Bwanku M Bwanku
 
Kwenye harakati zangu za kufuatilia majukwaa mbalimbali ya kampeni ya wagombea Urais mbalimbali, kwa hali isiyotegemewa ghafla nimemsikia mgombea Urais wa Chadema Ndugu Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano wake wa kampeni kule Karagwe, Bukoba kuhusu viongozi wetu wa dini...
Wewe umemuona lisuu tu huyo mwenyekiti wa vijana heri ukumuona
 
Kwenye harakati zangu za kufuatilia majukwaa mbalimbali ya kampeni ya wagombea Urais mbalimbali, kwa hali isiyotegemewa ghafla nimemsikia mgombea Urais wa Chadema Ndugu Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano wake wa kampeni kule Karagwe, Bukoba kuhusu viongozi wetu wa dini...

Hata me Nashangaa ww kwa kuwaheshimu viongozi wa dini

Hawa ni viongozi wa dini au wanasiasa vivuli?
 
Kwenye harakati zangu za kufuatilia majukwaa mbalimbali ya kampeni ya wagombea Urais mbalimbali, kwa hali isiyotegemewa ghafla nimemsikia mgombea Urais wa Chadema Ndugu Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano wake wa kampeni kule Karagwe, Bukoba kuhusu viongozi wetu wa dini...
Mungu huwapinga wenye kiburi, bali huwapa wanyenyekevu neema. Watanzania karibia wote, wanajua huyu mjumbe wa beberu hawezi shinda maana hawata mpa kitu.
 
Mungu huwapinga wenye kiburi, bali huwapa wanyenyekevu neema. Watanzania karibia wote, wanajua huyu mjumbe wa beberu hawezi shinda maana hawata mpa kitu.

Nani mjumbe wa beberu kati ya Lisu na nyie ambao mnawapa Mpaka makazi?
 
Kwn akina Gwaj boy na TBC wanautofauti gn ?? Licha ya kwamba umeongea uongo
 
Kwenye harakati zangu za kufuatilia majukwaa mbalimbali ya kampeni ya wagombea Urais mbalimbali, kwa hali isiyotegemewa ghafla nimemsikia mgombea Urais wa Chadema Ndugu Tundu Lissu akiongea kwenye mkutano wake wa kampeni kule Karagwe, Bukoba kuhusu viongozi wetu wa dini...
Hivi kama hawana akili awaambie wanazo?

Viongozi wa dini walikubali kumfrahisha jiwe na kuikataa kweli hivyo ni wapumbavu kama wewe mtoa mada uliesahau kuacha namba yako ya cm sijui hiyo buku saba utalipwaje
 
Kama unafika wakati hotuba ya kiongozi wa dini inahaririwa na Polepole ili tu impendeze jiwe sasa watu kama hao unataka waongelewe kwa lugha gani?
 
Nani asiyejua kuwa marais wote, ispokuwa Nyerere, walijitajirisha wao na ndugu zao isivyo kihalali. Huyu naye ameishapiga za kutosha mpaka kumfukuza CAG na kuweka ndugu zake wa karibu katika taasisi mhimu za kifedha na kiusalama. lissu yataje majizi yote yaaibishwe
CCM hakuna msafi hakuna malaika wanaccm wote ni wapiga dili
 
Back
Top Bottom