Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
- Thread starter
-
- #21
Najua kazungumzia na mengine. Nimeyasikia.Amezungumzia historia ya utendaji wa Magufuli katika miaka yake mitano, hajazungumzia korona tu.
Kazungumzia:
1.kauli za Magufuli kipindi cha tetemeko Kagera
2. kauli za Magufuli kipindi cha ukame wa njaa
3. kauli za Magufuli kipindi cha Korona
4. Kauli za Magufuli wananchi wanapomdai nyongeza za mishahara
Yote haya ameyazungumza kuwaonyesha na kuwakumbusha Watanzania aina ya kiongozi tuliye naye na umuhimu wa kumbadilisha ili tuweke mwingine atakayewasaidia wananchi kipindi. cha majanga na atakayekuwa na kauli za staha na heshima kwa wananchi!
Maoni yako yatafanyiwa kazi.Katika kuzungumza huko naye anaonyesha ubovu wake kama mwanasiasa.
Yeye ni mwanaharakati tu.
Siasa haziwezi.
We jamaa una fiksi sana.Mimi uncle wangu juzi kafariki singida kwa Corona yaani anazikwa juma nne. Wajinga wachache wanasababisha ndugu zetu kufa kwa ushabiki wa Siasa. Ngoja upoteze mtu ndiyo utajua Corona ipo
Lissu yupo kwenye ziara ya kuona maendeleo kwa kipindi cha miaka mitatu ambayo alikuwa amelala, wenzie wanapiga kazi.Lissu yuko vizuri anazungumzia kuhusu utawala mbovu wa Magufuli na umuhimu wa kuung'oa madarakani ili kusimika utawala unaheshimu katiba, sheria za nchi wenye kufuata misingi ya utawala bora, usiotesa raia, kuwabambikia kesi na kubambikizia wafanyabiashara kodi!
Lissu anatetea maslahi ya watumishi wa umma, anataka wapate nyongeza za mishahara zilizoko kwa mujibu wa sheria na pia anapinga kauli za kinyanyasaji na zisizo na staha hasa kwa wanawake waliogeuzwa kuwa wanasesere wa mizaha kwenye utawala huu!.
Lissu katolea mfano wa kauli ya kukejeli barakoa baada ya Jiwe siku moja kuifananisha na sidiria, infact Jiwe aliifananisha na Titi moja la mwanamke lililokatwa!!. Maneno gani sasa yale kutoka kwa mtu mwenye hadhi ya ukuu wa kaya kuyatamka mbele ya hadhara?, Ni aibu!
Kiufupi Lissu anafaa kuwa raisi, na akipata atakuwa rais bora kuliko Magufuli
Unaweza kutumia dawa ya kuharisha wakati hujahalisha?Mkuu Nyani Ngabu, hapo alikuwa akirejea kipindi cha mtanziko wakati maeneo mbalimbali ya dunia yakihaha kukabiliana na janga la COVID-19. Kauli yake ilikuwa "retrospective" kwa mazingira ya tishio halisi lilivyoripotiwa kupitia takwimu zilizokuwepo kwa wakati huo, na kauli za serikali zilivyotolewa.
Nimepata kukitazama kipande cha video ambacho ameongea kuhusu hilo na ni dhahiri kuwa wewe haujapata kuielewa hoja iliyomo.
Corona si hoja hapo isitoshe corona ni suala la juzi tu hapa katika yale yaliyomo katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya tano.
Hoja iliyoko hapo ni kauli za Rais katika masuala mbalimbali ya kitaifa. Ndio maana amezungumzia pia suala la majanga ya kiasili kama tetemeko la ardhi n.k.
Hoja si corona wala natural disasters alizozisema bali hoja ni kauli za kiongozi kwa wananchi pale ambapo majanga hayo yanatokea.
Kama hukumsikia bora ukae kimya! Tafuta clips alipokuwa anafungua majengo kule Dodoma mwezi uliopita.Kamkosoa Magufuli kwa kuwaambia watu wasivae barakoa, ‘kwanza zinafanana na sidiria za wanawake’.
Sijui ni lini na wapi Rais alisema hivyo. Mnaojua mtanifahamisha.
JiweUnadhani Magufuli na Lissu nani ana kauli zisizo za staha zaidi?
Lissu hajadai kama hivyo unavyosema wewe.Kitendo cha jiwe kuifananisha Barakoa na titi la mtu lililokatwa ni sexism, si kauli ya staha na haimfai kiongozi wa nchi!.
Pole sana mkuu ila kama unatudanganya hapa kwa manufaa ya kushinda mjadala basi ulaaniweMimi uncle wangu juzi kafariki singida kwa Corona yaani anazikwa juma nne. Wajinga wachache wanasababisha ndugu zetu kufa kwa ushabiki wa Siasa. Ngoja upoteze mtu ndiyo utajua Corona ipo
Mimi nailaumu NEC walitakiwa kupima akili wachukua fomu kabla ya kuwapa Nina uhakika ngukekuweko upimaji akili Kama ziko timamu au la Lisu asingepewa fomuYeye mwenyewe hajielewi!
Anapozungumzia barakoa, yeye anakuwa kaivaa?
Kampeni hazijaanza hivyo siyo wakati wa kumwaga Sera huu!Tundu Lisu akiwa kwenye jukwaa la Sera za CHADEMA apambanue na kupambana na sera za CCM, akipambana na Magufuli, hatamkwepesha ikulu, kwa kuwa CHADEMA isipoiweza CCM, ndio hivo Tena!
Lissu hajadai kama hivyo unavyosema wewe.
Rudia tena kusikiliza.
Leo akiwa huko Muheza ‘kwenye kampeni zake za urais’, Tundu Lissu kazungumzia tena suala la Corona.
Japo kalizungumzia kidogo tu, lakini kaligusia kwa kumkosoa tena Rais Magufuli na jinsi alivyoamua kukabiliana nayo.
Kamkosoa Magufuli kwa kuwaambia watu wasivae barakoa, ‘kwanza zinafanana na sidiria za wanawake’.
Sijui ni lini na wapi Rais alisema hivyo. Mnaojua mtanifahamisha.
Ila kwa Tundu Lissu kusimama mbele ya watu ambao hawana ‘time’ na Corona, ambao wamesimama kwa kurundikana bila kuacha nafasi, na ambao wala hawajavaa barakoa, akiwemo yeye mwenyewe, ni unafiki wa daraja la kwanza.
Kila siasa huwa ni za mahali pake. Kwa Tanzania hii, suala la Corona si hoja yenye mashiko, na kwa mtaji huo, si hoja ya ushindi.
Mbaya zaidi ni kutokitenda kile ambacho unakihubiri.
Huyo Tundu Lissu yeye anachukua tahadhari gani dhidi ya Corona tokea aje?
Ile barakoa yake aliyoivaa kwa dakika chache ile siku aliporudi, iko wapi?
Huyu jamaa ni kama vile yuko nje ya mguso na mambo ambayo Watanzania wanayajali.
Hebu mtazame hapa kuanzia dakika ya 6:30.....
Huna hoja wewe! Umeng'ang'ania ya Lissu utadhani ni mtalaka wako?
Kwamba kakuacha huku unampenda!
Lissu hajadai kuwa Magufuli aliilinganisha barakoa na titi, kama ulivyodai wewe.Hiyo clip nimeisikiliza sana na kuielewa sana na mimi actually ndo wa kwanza kuileta na kuianzishia mada hapa JF.
(Mada inayohusu ziara ya Lissu Muheza Tanga ipo hapa kwenye jukwaa la siasa)
Lisu,Unadhani Magufuli na Lissu nani ana kauli zisizo za staha zaidi?