Nawaambia Kama ilivyoandikwa kwenye Vitabu vitakatifu Biblia na Quran Kuna siku yaja Tundu Lissu atakuja kuwa Rais wa nchi hii.
Mkuu
technically, kwanza hongera sana kwa bandiko hili very powerful la kitu kinachoitwa mind suggestibility, naunga mkono hoja, kwa hoja kuwa mtu yoyote aliyetimiza sifa na vigezo vya kuwa rais wa JMT kwa mujibu wa katiba, anaweza kuwa rais wa Tanzania, na sifa hizo na vigezo vyote Tundu Lissu anavyo hivyo ni kweli anaweza kuja kuwa rais wa nchi hii yetu ya Tanzania na ule uchaguzi wa 2015 ni mimi ndie nilimshauri Lissu
Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!
Sikujua kwamba ushauri ule ungekuja kumponza, hadi kupata zile pyu pyu
Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana
Ila kwa nchi yetu Tanzania na kwa siasa zetu za kiTanzania, ili mtu kuweza kuwa rais wa nchi hii ni lazima awe CCM, kwa Tanzania, urais una haki miliki, haki miliki ya urais wa JMT ni kwa chama cha Mapinduzi CCM pekee. Haki miliki hiyo ilitolewa kwa CCM na muasisi wa taifa hili, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pale aliposema "Mtu yoyote anaweza kuwa rais wa Tanzania, ila rais bora ni kutoka CCM".
Balozi Karume: ‘CCM pekee iwe inasimamisha mgombea urais Zanzibar’
Wewe katika bandiko hili umetumia definitive statement kuwa Tundu Lissu atakuwa rais wa nchi hii as if you are very sure!. Kwa vile Tundu Lissu yuko opposition, na its very unfortunately Tanzania hatuna any serious opposition wa kuiondoa CCM madarakani hivyo Lissu kupitia opposition kamwe hawezi kuja kuwa rais wa nchi hii unless ahamie CCM, ateuliwe na CCM kugombea urais, mgombea urais wa CCM ndiye rais wa Tanzania!.
Kama ambavyo Mkapa, Kikwete na Magufuli walipambana na Tundu Lissu wakashindwa.
Walipambana vipi?, wakashindwa vipi?, inamaana Tundu Lissu aliwashinda Mkapa, Kikwete na Magufuli, please share with us alishindana na hao wote watatu kwenye nini na Tundu Lissu ndio akawashinda?.
Ila Rais Samia yeye ataanguka kabisa iwepo Katiba mpya au isiwepo Tundu Lissu will become the next president after Samia.
Duu!..., hii kali!, ila naomba nisikubeze maana kuna kauli nyingine ambazo mimi naziita "kauli umba", zina nguvu ya kuumba kwa...
Tunza hii kwenye kumbukumbu ya memory ya kichwa chako kwamba Tundu Lissu atakuja kuwa Rais wa nchi hii.
Hili kwa kweli naitunza, ila hujasema how?. Ila kwa uzoefu wangu wa kura za urais, sisi sio kama Kenya ambapo matokeo yanaweza kuhojiwa, sisi matokeo yakitangwa ni final and conclusive, hivyo kama determinant ya ushindi kwa chaguzi zetu ni matokeo ya kura za ndio zilizopigwa na wapiga kura, yaani vote cast then its posible mgombea yeyote mwenye kura nyingi ndie mshindi, hivyo uchaguzi wa 2025 Lissu akigombea na Samia, na Lissu akapata kura nyingi, anatangazwa mshindi na kweli Tundu Lissu anakuwa rais wa nchi hii ya JMT.
But ivery unfortunately the determinant of victory in our elections is not the vote cast but the vote count!, nikimaanisha the determinant ya nani anashinda uchaguzi, sio kura zilizopigwa bali ni kura zilizohesabiwa, hivyo mwamuzi wa nani ni mshindi ako mpiga kura bali mwesabu kura!.
Maadam 2025 haiko mbali, lets wait and see to it hili likotokea!.
Wish you all the best kwenye kauli umba yako hii!.
P