Tundu Lissu hebu tueleze vizuri tukio la kupigwa risasi lilivyotokea haya uliyotoa yanaacha maswali mengi sana

Maelezo ya Lissu alipohojiwa na CLOUDS
Nafasi za parking zimechukuliwa imebaki moja kwa sababu niko mbele nikaingia kwenye hiyo parking. Wakaingia upande wa kushoto wanatafuta eneo la kupaki kuna magari...
Baada ya Ibilisi Mwendakuzimu Jiwe Kufa Nchinimepata Ahueni

Hili ndio la Msingi
 
Kwa wanaoijua CHADEMA inawezekana kabisa ni inside job!
  1. CHADEMA mabingwa wa mapichapicha, walijitahidi kuhakikisha picha za tukio hilonhazisambai kinyume na utamaduni wao...
Mimi ni mwana CCM mwenzako naomba unisimulie ukweli wa tukio
 
Kwa wanaoijua CHADEMA inawezekana kabisa ni inside job!
  1. CHADEMA mabingwa wa mapichapicha, walijitahidi kuhakikisha picha za tukio hilonhazisambai kinyume na utamaduni wao...
Maswali yako yote jibu lake ni moja na rahisi sana;

Kwamba, whether it's inside or out of CHADEMA's job, jibu lake ni INTENSIVE INVESTIGATION by Tanzania police force!!

Na wewe kama ni muungwana na ni mtenda haki kweli, hebu majibu maswali haya matatu tu;

1. Unadhani ni kwanini polisi mpaka sasa hawajafanya uchunguzi wa tukio hili?

2. Je, kwa kuwa unadhani ni "CHADEMA's inside job", basi polisi wanagwaya kuichunguza CHADEMA?

3. Na hivi ni kweli kabisa Kwa akili yako ndogo hiyo unaamini CHADEMA wamemficha dereva na Kwa hiyo wanazuia uchunguzi!!??

Kama unaamini hivi, KAPIMWE AKILI ZAKO HIZO!!!
 
Watu wengine mna roho za ajabu sana. Yaani unaona sawa kuchagua muuaji Lakini sio victims wa hao wauaji?
Naona na wewe umechagua upande. na Ukome kunimezesha maneno.
Atleast we are squared on that.

Hata hivyo.... ukinisoma vizuri, sehemu nyingi, sisi wote, Jamii ya Mtanzania, Jamii ya Mwafrika. Jamii ya JF na hata Familia Zote, waliopotezwa, waliojipoteza, Wanaodaiwa kuua wanadai wameuliwa na.. n.k n.k wote ni Victims. Wanahujumiwa haki, wanabezwa na ku-kabehiwa if that is the word!...Victims of Circa-of-Stances.

Hawawezi kupata afueni kwa matusi na Udhalimu unaofanywa na upande wowote ule.
Hakuna,
Hakuna atayefufuka, Hakuna atakaye tokwa na risasi mwilini , basically hakuna miujiza itakayotokea. Ukweli ni kuwa, Ukweli Ujulikane.
Si waunde Tume yenye watalaam wa nje na ndani na kuchunguza hii issue?
Hayo uliyobandika juu ndio wanayodai wahusika. Nyuma au kwenye mabandiko yangu mengine nimegusia kuhusu hilo.
Tunajua tume kama hizo ni za Kufunika funika. Mfano mzuri ni tume ya Tutu. Yaani kuna jamii zilizoumizwa kisaikolojia, kifiziolojia kwa uhasama mkubwa, kuna waliopata ulemavu, kuna wengine waliokufa kwa magonjwa ya kipindupindu....Cha ajabu wahusika walikuwa wa Serikali, Cha ajabu wengi walipata maagizo kutoka juu, cha ajabu kuna mengi yaliongelewa chobisi kwa sababu za 'usalama wa taifa' cha ajabu wengi wao hawakupata hata nusu ya thamani ya udhalimu wao..yaani vifungo stahiki, yaani kuna wengi walitakiwa kunyongwa.

Nakubaliana na Tume lakini wale wote, yaani wote waliotengeneza mazingira, waliohusika n.k wafikishwe mahakamani....kusiwepo na yale ya kutofikishwa Mahakamani.
 
Kwa kifupi unadai. Case Closed!

Nafikiri utakuwa haumtendei haki T.L ambaye anawezekana ana taarifa nyingi zaidi.Temeke alisema huwa anatembea na kabrasha zenye Taarifa nyingi tu....
Wenye jukumu na wajibu kisheria wa kuchunguza ni POLISI.

..Ninachoshangaa ni watu kumsakama zaidi Lissu badala ya kuwashinikiza Polisi watimize wajibu wao.

..Labda sura au jina la Lissu ni tatizo kwa Polisi. Lakini aliyeshambuliwa ni CHIEF WHIP wa kambi ya upinzani bungeni. Sio mtu mdogo ktk masuala la KIBUNGE.

..Sasa kwanini Polisi wana-behave namna hii? Hivi kwenye nchi tunazotaka kufanana nazo Polisi wao wanaenenda kama wetu kwenye matukio makubwa kama la Lissu?

..Na kama mtu maarufu na mwenye wadhifa kama Lissu tukio lake linafanyiwa dharau na kebehi na Polisi, mtu wa kawaida akipatwa na mkasa itakuwaje?

..POLISI ndio wanaopaswa kuwa na maelezo mengi zaidi. Wao ndio wenye GARI lenye ushahidi wa matundu ya risasi. Ndio waliokusanya vidhibiti na vielelezo toka eneo la tukio.

..POLISI pia wana CCTV cameras zilozokuwa eneo la tukio. They should tell the public nani walionekana wakimshambulia Lissu. Tulitakiwa tuwe tunawajua kwa majina na picha wahusika wa tukio lile.

..POLISI wanapaswa kueleza kwanini WALINZI waliondolewa eneo la tukio. Nani aliwaondoa? Kwa nia gani? Alielekezwa na nani?

..Maswali ya Lissu kuumia mguu wa kushoto au kulia they dont change the fact kwamba kuna watu walijaribu kumuua. Swali muhimu la kujiuliza na kuwahoji Polisi ni watu hao ni kina nani? Nani aliwatima?
 
Maelezo ya Lissu alipohojiwa na CLOUDS
Nafasi za parking zimechukuliwa imebaki moja kwa sababu niko mbele nikaingia kwenye hiyo parking. Wakaingia upande....
Msema pweke ndio mshindi
 
I think mada bado ina miguu ya kusimama na Kudai yanayodaiwa....TL aseme ukweli
Eti unasemaje?

TL aseme kweli upi na kwa nani? Kwako wewe? Pls, try to be serious even for once, at least...

Tundu Lissu amesha - narrate his story ingalau kile ambacho umma ungetaka kusikia, mathalani;

✓ Yeye kutotoa ushirikiano kwa polisi. Kisingizio ilikuwa "atoke huko Ubelgiji aje nchini". Alikuja 2020 hakikufanyika chochote. Sasa huyo amekuja tena.. What are they going to do?

✓ Hoja nyingine ya kijinga eti ni ya kufichwa dereva tena husemwa na polisi wenyewe. Kama yupo Ubelgiji na wanadhani ni wa muhimu ktk uchunguzi wao, waende huko au wafuate utaratibu wa kumleta nchini wafanye kazi yao. It's just simple like that..!
======================================

MWISHO

Si TL wa kusema ukweli bali ni serikali na vyombo vyake vinavyohusika na jinai...!!

Statement yako inapaswa kuwa, SERIKALI ISEME UKWELI kuwa amri ya kuuwawa TL ilitolewa na Mwendazake Rais John P. Magufuli..!
Hii hata mtoto mdogo anaelewa!
 

Kama huyu SYLLOGIST! bado anakuwa hakuelewi, basi atakuwa na lake jambo..

Anauliza maswali ya eti;

✓ Where is the disconnect, au;

✓ Nani mkaidi nk nk..

Ndugu SYLLOGIST! you are trying people's intelligence, right..?

It's because you know the answers of all these questions..!
 
Hapo mwenyewe anajiona kauliza maswali ya akili kubwa sana!
 
Swala la 4 Ungeuliza wale walinzi pale getini walipotelea wapi siku huyo watu waovu wakaingia na kutoka bila ukaguzi au purukushani yoyote
Maelezo ya Lissu alipohojiwa na CLOUDS
Nafasi za parking zimechukuliwa imebaki moja kwa sababu niko mbele nikaingia kwenye hiyo parking. Wakaingia upande wa kushoto...
 
Unafikiri kujificha nyuma ya "Uzima tele" ndio sintoweza kukubutua na kukuambia unachutama vibaya. Unachutama kwa mihemeko.

Nionyeshe hiyo mistari inayoonyesha
It's because you know the answers of all these questions..!
Nionyeshe mstari ninapoonyesha najua kila kitu na mistari ninayouuliza maswali.?

Hata hivyo haijalishi, sintojificha na I.d nyingine nipige dongo.Yaani usifikirie ninayo id ya uchizi ya akili au hulka yeyote ile ambayo unataka watu wafikirie ninayo, sina.
Sipendi Unafiki.
Nakupiga hapa hapa ikifikia sehemu kuna ulazima wa kufanya hivyo. Nakucharaza tu.

Sasa kama wewe ni mfuatiliaji na una busara kana zile za kudai.. 'angalia usije onekana chizi kujibishana na chizi wewe endelea kunitafuta. Tutaelewana mie ni Kinyume chake Sijali. Sijali kwasababu mtu kama wewe nawategemea sehemu yoyote ile ambayo imejaa wenye akili, kwani wakishindwa wanaongeza akili na kuwa 'Wendawazimu' kwa kufikiri madongo ya kuchutama choo ndio yatanifanya niterereke.

Nimefurahi lakini ulipotumia huo mstari
"I think mada bado ina miguu ya kusimama na Kudai yanayodaiwa....TL aseme ukweli"
kuonyesha kuwa sitoki nje ya mada kuendeleza propaganda za kitoto. We endelea tu. Sasa subiri ninvyomjibu Joka Kuu. Wee utulie tu.
 
Ninakujibu bila ya mpangilio au mtiririko maalum.
 
..Maswali ya Lissu kuumia mguu wa kushoto au kulia they dont change the fact kwamba kuna watu walijaribu kumuua. Swali muhimu la kujiuliza na kuwahoji Polisi ni watu hao ni kina nani? Nani aliwatima

Naona unajaribu kudumaza mada, kwamba swali hili la moja kwa moja kwa Mh. T.L 'Kutueleza kuhusu tukio la kupigwa risasi' limewekwa kinafiki, limewekwa kwa sababu ambazo 'Zinakushangaza'

....

Kuhusu: Umuhimu.

Kuumia kwa Lissu mguu wa kushoto au wa kulia ni Muhimu!
Picha hazifanani na maelezo au Taarifa tunazosikia.... Sawa that dont change the fact alipigwa risasi, lakini it is not a fact au hatujui ilikuwa ni kwaajili ya kuuwawa au lah au ilikuwa ionekane kwamba ndi hivyo. Auwawe!

Nafikiri mada inajitosheleza kuuliza "" kwa sababu

Maelezo ya pande zote, Taarifa za Mitandaoni, Taarifa za polisi, Maelezeo na Taarifa za Mh. Lissu zinapishana pishana kwanini kusiwe na Umuhimu wa mguu wa upande gani?
 
Joka Kuu,
Hilo kuuliza Polisi nani alifanya na nani aliwatuma....na majibu ya Awali kwa wale ambao tunaamini kuwa ndio wenye taarifa....hazikuwaridhisha wengi tu, wa upande unaoamini alitandikwa risasi Afe....Taarifa ambazo zilidai uchunguzi wa awali unaelekea au zilikuwa zinaonyesha njama za kuchafua taswira ya Serikali ya Hayati Raisi.

Na Uchunguzi na Taarifa za Awali za upande unaodai Hayati Raisi na magenge yake ndio walikuwa wahusika wakuu. kwa sababu lukuki kama kuondolewa kwa CCTV cameras

Joka kuu, Umezusha Umaarufu na Wadhifa wa Mh.Lissu.

Tunajua kuna nadharia au taswira iliojengeka kuwa ni Hayati Raisi ndio "Maagizo ya Juu' na Aliyetandikwa Risasi ni Mh. Lissu. Kwa mantiki hiyo kuna watu wawili al Maaruf watu wawili al wadhif
Tofauti mmoja ni Raisi wa Nchi na Mwingine kama ulivyoeleza ni Chief Whip! Kati ya hawa watu, mmoja sio mtu mdogo katika masuala ya "Taifa" kama ilivyo kwa mwngine ambaye ni mkubwa kwa masuala ya " Kibunge" Nafikiri tunaweza afikiana kuwa al maaruf na al wadhif mmoja ana wadhifa mkubwa...ni wa Taifa. na Mwngine ni wa Kibunge Hawa hawalindwi na 'Polisi' wa kawaida

Hivyo basi, hata siku moja, katika taifa lelote lile haitoweza tokea mmoja asilindwe kwa nguvu zote nesesari andi avaelebo! hamna na ndio ukweli mchungu.

Polisi hao unaodai wewe hawana uwezo wa kujibu maswali yako, wenye majibu hayo unawajua tusipotoshane, haunipotoshi. Usipotoshe

Je unajua kuna polisi wa Kanda Maalum? na hizo ni kanda gani? Zina Umaalum gani? Kanda zinahama?
 
1. Kama parking ilikuwa imejaa wenye magari walikuwa wapi? Kikawaida kungekuwa na mayoress na watu wengi.
2. Alienda lunch, kwa nini wenzie hawakwenda lunch? Na hayo magari kujaa yangejaa vipi kama wenyewe hawakuenda lunch?
3. Walinzi wa parking walikuwa wapi? Walijuaje kama atakuja lunch siku hiyo? Walinzi wa hao wenye magsri yaliyojaa walikuwa wapi?
4. Kwa nini wauaji risasi 16 wakuvunje miguu, si wangepiga tumbo au kichwa?
5. Mlinzi hakukimbia alisema alilala kwenye kiti chake ambako ndiko risasi ziltokea. Aliponaje? Yuko wapi?
6. Uhusiano wa Tundu na majirani ulikuwaje wasimsaidie hadi leo, kikawaida husaidiana kwenye Iddi na Ubatizo na maziko. Tundu alikuwa adui wa kila mtu?
 

..Je, Polisi wa Tanzania wana nia ya kuchunguza mkasa uliomkuta Lissu?

..Je, Polisi wa Tanzania wana uwezo wa kuchunguza mkasa uliomkuta Lissu?

..Ni nani aliondoa walinzi wa Area D siku ambayo Lissu alishambuliwa?

..Kwanini Polisi hawatoi picha na majina ya walioonekana kwenye CCTV records walizochukua eneo la tukio?

NB:

..Magufuli alikuwa Raisi wa nchi na amiri jeshi mkuu. Mtu mwenye nyadhifa na mamlaka hayo hawezi kulinganishwa na mtu yeyote ndani ya nchi.

..Lissu yeye alikuwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani. Hivyo basi, alikuwa mmoja kati ya viongozi wakuu wa Bunge la Tanzania. Kuna Spika, Naibu Spika, Waziri Mkuu, Mnadhimu wa serikali, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani.

 

1. Parking anayoizungumzia Lissu ni ya magari mangapi?

2. Je, ni nani kwa mfano chombo cha habari au Polisi amekwenda na kuwahoji majirani wa Lissu?

3. Lissu anadai geti lilikuwa wazi na walinzi wa area D walikuwa wameondolewa. Nani aliwaondoa?

4. Lissu alikuwa ndani ya gari na waliomshambulia walikuwa nje ya gari. Katika hawakujua kama wanapiga tumbo, kichwa, au miguu.

5. Dereva aliruka nje ya gari. Kwa sasa hivi anaishi Ubelgiji. Polisi wanaweza kuwatumia Interpol kumkamata ikiwa wanaamini anahusika.

6. Majirani wa Lissu wa Area D ni Naibu Spika, na viongozi mbalimbali wa serikali ya CCM. Lissu alikimbizwa hospitali na msaidizi wa nyumbani kwa Dr.Tulia Ackson.
 
Unajua utaalamu wangu au unanichukulia juujuu siyo? Tuheshimiane sawa
Siipendi chadema ila wewe ni mtu wa ovyo kama vijana wa chadema una uccm sana akilini mwako kuliko uzalendo
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…