Tundu Lissu hebu tueleze vizuri tukio la kupigwa risasi lilivyotokea haya uliyotoa yanaacha maswali mengi sana

Nadhani huna kumbukumbu. Kumlinda mhalifu ni kazi sana.

Maelezo ya dereva ni kwamba alipoona mshambuliaji anatoka na bunduki, alimvuti Lisu na kumpeleka upande wa dereva na kumshusha chini eneo ambalo kuna accelerator na brake pedals. Yeye dereva alitambaa kushuka chini na kwenda kulala kwenye uvungu wa gari lililokuwa hapo karibu. Dereva anasema alishuhufia na kumwona mshambuliaji aliyekywa amevaa cap na mask. Wakati shambulizi linaendelea alimsikia Lisu anapiga kelele, akajua atakuwa amefikiwa na risasi. Gari lilipoondoka tu, ndiyo alienda kumwona akiwa amejeruhiwa vibaya. Dereva alishuhufia tukio lote, na hiyo ndiyo sababu ya wauaji kumtaka sana dereva kwa sababu wanajua alishuhufia shambulizi lote.

Ifahamike kuwa kwa kuwa nafasi ile aliyowekwa Lisu ni ndogo, huwezi kuwa na uhakika kwa kujibana kwenye nafasi ile, alilala kwa namna gani. Huenda kiwiliwili na kichwa vilikuwa chini, na miguu ilikuwa juu.
 
Hiyo namba 6 umetisha sana bwashee!
 
Kwahiyo Dereva alitenda kama Marando pale Tanga kumuokoa Lyatonga?

Nchi ngumu sana hii
 
Kipindi kile kuvaa tshirt za pray for Lissu haikutakiwa. Tukio la ajabu lile. Jambo gani baya lingeipata nchi kwa watu kumuombea TL?
Muuji alikuwa na hofu kuwa labda sala kwaajili ya Lisu zingemaanisha hukumu dhidi yake.

Marehemu alitapatapa sana baada ya lile tukio. Mwiglu aliamua kuzima simu yake. Akaamua kumpigia Mahga RIP, akaongea na Mwiglu kupitia simu ya Mahga. Akamwambia Mwiglu aitishe vyombo vya habari, aseme kuwa Sirikali haihusiki na hilo shambulio. Mwiglu akashauriana na Mahga, wakaamua wakae kimya. Na hiyo ndiyo ikawa sababu ya Mwiglu, baada ya muda mfupi Mwiglu kufutwa kazi.

Marehemu pamoja na ubabe na ukatili wake, baada ya tukio lile, na reaction ya wananchi na jamii ya kimatifa, alibakia amechanganyikiwa. Na hiyo ndiyo sababu ya yeye wakati wote kukaa kimya kabisa, na kutoongelea tukio hilo wala kulitaja jina la Lisu. Adhabu aliyoipata, ya kisaikolojia, hakuna anayeijua isipokuwa yeye binafsi na watu wake wa karibu.

Watu wa karibu wanadai kuwa marehemu, baadaye alifikia kuwachukia waliotekeleza shambulio kwa madai kwamba kushindwa kwao kumwua kumekuwa chanzo cha matatizo mengi hasa kwenye siasa za kimataifa.

Marehemu hayupo. Hakuna kinaweza kufanyika dhidi yake. Lakini akina Bashite, Ksanduku, Kalemni, bado wapo. Lazima hatua zichukuliwe.
 
vijana mmefundishwa kujadili hoja au kumjadili mtoa hoja?
mbona alichouliza ni cha kawaida kabisa? si ujibu tu kwamba risasi zilipigwa kwa nyuma zikakata kona
Muuliza swali ni mjinga aliyeuliza swali la kijinga.

Maelezo yote yalikwishatolewa, mpigaji alitoka, alishambulia akiwa nje ya gari. Kama una analytical thinking huwezi kuuliza swali la kipuuzi kama hilo.
 
Na Wewe unaamini walioshindwa kumuua?
 
Ukweli ana ujua yeye mwenyewe ila hawezi kusema na watu waliomshamulia ana wajua kwa sababu kawaona, huu mchezo ni wao kwa wao wanajuana ndio maana ni ngumu sana kutoa usirikiano, bila kutumia akili nyingi mtu aliekushambulia huwezi kumtambua hata kwa maumbile wakati unamuona kabisa ana kushambulia?
 
Aisee
 
Sasa kwanini huyo dereva amejificha?

Au yeye ndiye asiyejulikana?
Wauaji walikuwa wanataka kumwangamiza na yeye. Watu wema ndani ya vyombo vya usalama walishauri aondoke haraka sana.

Ikithibitika Serikali ina will ya kushugulikia jambo hili, dereva atakuja haraka sana. Mpaka sasa dhamira hiyo haipo.
 
Yeye ameshasema mbaya wake ni nani.
 
Utuambie wewe je ?yakuwa maigizo kama unawasiwasi na alicho ongea ipigie kelele serikali iweke uchunguzi huru ili maswali yako yapate ufumbuzi.
Katika suala la lissu inatakiwa ukweli uwekwe huru ili tuyafichue maovu
 
Wauaji walikuwa wanataja kumwangamiza na yeye. Watu wema ndani ya vyombo vya usalama walishauri aondoke haraka sana.

Ikithibitika Serikali ina will ya kushugulikia jambo hili, dereva atakuja haraka sana. Mpaka sasa dhamira hiyo haipo.
Huyo dereva ananikumbusha Mabere vs Tamimu pale Kinondoni Mkwajuni, Ilikuwa kama senema vile
 
Sasa kwanini huyo dereva amejificha?

Au yeye ndiye asiyejulikana?
Wewe ungefanyaje? Bosi wako kashambuliwa na risasi, bosi wako anasema ni serikali kupitia mkuu wa nchi, ww ni shuhuda wa tukio lote, ndani ya nchi yako obtion iliyopo ni vyombo vya ulinzi na usalama, vyombo vya ulinzi na usalama mkuu wake ni mtuhumiwa mkuu wa shambulizi.
 
Katika mazingira kama yale dereva aliwezaje kutoroka na asipatikane hadi leo?
 
Katika mazingira kama yale dereva aliwezaje kutoroka na asipatikane hadi leo?
Huenda ni udhaifu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa serikali ya JPM. Hata tukio zima(with assumption kuwa sio serikali) ni udhaifu mkubwa maana halikutokea ghafla, kuna warning zilikuwa zinatolewa na mhusika.
 
Tena amerudi bila dereva huku anabwabwaja Uongo Mitandaoni na kwenye Press Media!
 
Huenda ni udhaifu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa serikali ya JPM. Hata tukio zima(with assumption kuwa sio serikali) ni udhaifu mkubwa maana halikutokea ghafla, kuna warning zilikuwa zinatolewa na mhusika.
Sasa Lisu kwa kujua anawindwa alishindwa kujiwekea Ulinzi binafsi kama wa akina Diamond, Shabby, GeoDavie nk?

Sasa akiwa Rais huyu anaweza kuchokoza nchi jirani na akashindwa kutulinda
 
Utu ni jambo la msingi sana kwa mwanadamu
 
Sasa Lisu kwa kujua anawindwa alishindwa kujiwekea Ulinzi binafsi kama wa akina Diamond, Shabby, GeoDavie nk?

Sasa akiwa Rais huyu anaweza kuchokoza nchi jirani na akashindwa kutulinda
Kama serikali haihusiki basi Jeshi lilikuwa dhaifu sana sababu wahalifu wameingia eneo la makazi ya bunge, wametoa cctv camera, wamemshambulia mbunge, wametoroka, key witness ambaye ni dereva katoroka, aliyeshambuliwa kaenda nje ya nchi. Yote haya yanafanyika ndani ya nchi yenye jeshi la polisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…