Pre GE2025 Tundu Lissu: Kuna Rushwa inatuvuruga ndani ya CHADEMA

Pre GE2025 Tundu Lissu: Kuna Rushwa inatuvuruga ndani ya CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
View attachment 3064424
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bara Tundu Lissu akizungumza katika mtandao wa kijamii wa Clubhouse amenukuliwa akisema

"Kuna tatizo la rushwa ya uchaguzi, yeyote anayesema hakuna tatizo anatudanganya, kuna tatizo la rushwa ya uchaguzi na rushwa ya uchaguzi ya mtu yeyote yule ni adui wa demokrasia na ni adui wa haki, kiongozi yeyote anayepatikana kwa kununua wapiga kura huwauza siku ikifika, kwa hiyo nilichokisema Iringa ninakisimamia kama nilivyokisema, kuna tatizo la rushwa linatuvuruga CHADEMA.

Tuangalie sisi wapika kura tuwe macho na wagombea wanaokuja kwa sababu wamenununua kugombea kwao, kwa sababu wamehonga ili wateuliwe wagombea, kwa sababu wamechafua ili waje wapate nafasi za kugombea na kuchaguliwa, Ninasimamia katika kile nilichokisema Iringa na tuwe macho"-

JAMBO TV
kiongozi muandamizi wa chama unalalamikia rushwa badala ya kuchukua hatua ?🤣

sasa unamlalamikia nani na wew ni mwanasheria?

kwahivyo ukieleza hayo kwa wananchi ndio itasaidia nini sasa? 🐒

eti huyu ni kiongozi muandamiz wa chama kitaifa, dah...


viongozi wengine bana,
ndio maana Hayati E.G.Lowasa aliwahi kusema ni lazma awepo kiongozi anaeweza kuchukua maamuzi magumu, tena maamuzi yanayotekelezeka...
haiwezekani kiongozi analalamika na mwanachi analalamika.....🐒
 
Unaongea utadhani hatufahamu alichokuwa anakifanya bwana Mrema kule Iringa.

Haya kina Emmanuel Chengula nao waliiba kura au walienguliwa kwasababu tu ya siasa za makundi ndani ya chama, ambapo hawakuwa upande wa mwenyekiti ?​
Unamaana msigwa aliibiwa kura
 
kiongozi muandamizi wa chama unalalamikia rushwa badala ya kuchukua hatua ?[emoji1787]

sasa unamlalamikia na na wew ni mwanasheria?

kwahivyo ukieleza hayo kwa wananchi ndio itasaidia nini sasa? [emoji205]


viongozi wengine bana,
ndio maana Hayati E.G.Lowasa aliwahi kusema ni lazma awepo kiongozi anaeweza kuchukua maamuzi magumu, tena maamuzi yanayotekelezeka...
haiwezekani kiongozi analalamika na mwanachi analalamika.....[emoji205]

Gaidi ndiyo stering wa rushwa ndani ya chama , mlelewa Ubelgiji hana ubavu wa kupambana nae
 
Hii nchi bila rushwa madaraka utabidi uyasahau...

It's a rotten system and you can't get out of it by mere words...

Kupambana na rushwa sio jambo LA mchezo.
I wish him well, but he is fighting the battle he can't win....

Tupo Africa not Copenhagen
Rushwa Tanzania imeasisiwa na Chama Cha Mapinduzi. Ndiyo maana wapiga Kura Huwa tuna tunauliza wakishahotubia wanapoondoka "UNATUACHAJE?"
 
Rushwa Tanzania imeasisiwa na Chama Cha Mapinduzi. Ndiyo maana wapiga Kura Huwa tuna tunauliza wakishahotubia wanapoondoka "UNATUACHAJE?"
Bila rushwa nchi zetu hizi unadhan utapata madaraka?
Harakati ni mbali sana na uhalisia.
 
Lisu kapanick baada ya Kuona Kuna mgombea anataka kugombea nafasi yake ya makamu mwenyekiti
Mwendelezo wa kukimaliza cdm, siioni chadema bila LISSU walio baki wote hawana hoja wala mvuto na kibali mbele ya wananchi huu ndio ukweli mchungu maskioni mwa chawa wa mbowe.
 
Rushwa ipo kwenye majengo ya ibada,si jambo la kushangaza kuwepo kwenye vyama vya siasa,lakini ni jambo la kushangaza kwa anayetaka kuwa mbadala wa mtengeneza na mkumbatiaji rushwa naye kuwa na rushwa.

Taifa linahitaji mtu ambaye unaona anavyoichukia rushwa kuanzia kwenye sauti yake, muonekano wake wa mwili na hata sura yake anapoizungumzia rushwa.

Tunahitaji kiongozi ambaye hataogopa kukemea rushwa na kuchukua hatua madhubuti za kumaliza huu mfumo rushwa uliotamalaki nchini ambao unaumiza sana wananchi kuanziq kwenye kupata huduma za msingi za kijamii mpaka haki za kidemokrasia kama kuchagua na kuchaguliwa uongozini.

Mungu ambariki sana Tundu Lissu na wale wote tunaopambana katika kuikemea, kuipinga na kuimaliza rushwa na mfumo rushwa.
 
Gaidi ndiyo stering wa rushwa ndani ya chama , mlelewa Ubelgiji hana ubavu wa kupambana nae
mwanasheria mbobevu kiongozi mwandamizi eti anabweka bweka tu kuhusu rushwa huku kaufyata mkia mguu sawa akili yake ni kwa mabwenyenye magharibi ✈️✈️✈️🛫🛬
 
Hii nchi bila rushwa madaraka utabidi uyasahau...

It's a rotten system and you can't get out of it by mere words...

Kupambana na rushwa sio jambo LA mchezo.
I wish him well, but he is fighting the battle he can't win....

Tupo Africa not Copenhagen
Kweli, mzizi wa rushwa upo Serikalini, yaani CCM ndiyo mzizi wenyewe.
Kipindi cha uchaguzi ndiyo kipindi cha mavuno.
Mbaya zaidi hela zinatembea hadi vyama vya Upinzani yaani CCM kichomeka mamluki wao.
 
Kweli, mzizi wa rushwa upo Serikalini, yaani CCM ndiyo mzizi wenyewe.
Kipindi cha uchaguzi ndiyo kipindi cha mavuno.
Mbaya zaidi hela zinatembea hadi vyama vya Upinzani yaani CCM kichomeka mamluki wao.

Tuliwaonya kuwa laana ya kushangilia kifo cha Magufuli ni kubwa.

Baada ya miaka 3 mnayo hiyo amani mliyosema mtapata? Hamtekwi tena? Hamshindwi tena kwenye chaguzi? Watu hawakimbii chama chenu tena?

Na laana iwatafune milele nyie
 
Lissu anakosea sana kwenye hili. Kwa kufanya anachofanya anaaminisha jamii kuwa Chadema ina tatizo la kipekee la rushwa. Kitu ambacho sio kweli. Hatakiwi kustaajabu watu kutumia kila mbinu kupata uongozi ndani ya Chadema kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa Chadema kuwa na wabunge, madiwani na wenyeviti wengi baada ya chaguzi za mwaka huu na ujao.

Aidha, mshindani wao mkubwa kujaribu kupenyeza watu wake au kuwarubuni waliopo nao ni ishara kuwa chama chake kinakubalika sana na kimekuwa tishio. Yeye na viongozi wake wawekeze kwenye ku vet wagombea wote na watendaji wa chama kuhakikisha kuwa wamo kwa sababu wanakubaliana na sera zake,na sio opportunists. Kama nia yao ni kukivuruga chama basi matamshi yake yatawarahisishia kazi hiyo.

Kitu kingine ambacho hakipendezi ni yeye kurudia shutma hizi baada ya kiongozi mwenzake kuonyesha nia ya kuitaka nafasi aliyokuwa nayo. He is better than this.

Amandla...
 
Lissu anakosea sana kwenye hili. Kwa kufanya anachofanya anaaminisha jamii kuwa Chadema ina tatizo la kipekee la rushwa. Kitu ambacho sio kweli. Hatakiwi kustaajabu watu kutumia kila mbinu kupata uongozi ndani ya Chadema kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa Chadema kuwa na wabunge, madiwani na wenyeviti wengi baada ya chaguzi za mwaka huu na ujao.

Aidha, mshindani wao mkubwa kujaribu kupenyeza watu wake au kuwarubuni waliopo nao ni ishara kuwa chama chake kinakubalika sana na kimekuwa tishio. Yeye na viongozi wake wawekeze kwenye ku vet wagombea wote na watendaji wa chama kuhakikisha kuwa wamo kwa sababu wanakubaliana na sera zake,na sio opportunists. Kama nia yao ni kukivuruga chama basi matamshi yake yatawarahisishia kazi hiyo.

Kitu kingine ambacho hakipendezi ni yeye kurudia shutma hizi baada ya kiongozi mwenzake kuonyesha nia ya kuitaka nafasi aliyokuwa nayo. He is better than this.

Amandla...
Ila huyu jamaa mara nyingi huwa anaongea mambo yenye ushahidi huwa hakurupuki chadema hapo Kuna dalili ya mambo kuharibika sababu ya watu fulani kuonekana wamekuwa ni tishio pale juu
 
Ila huyu jamaa mara nyingi huwa anaongea mambo yenye ushahidi huwa hakurupuki chadema hapo Kuna dalili ya mambo kuharibika sababu ya watu fulani kuonekana wamekuwa ni tishio pale juu
Ushahidi angewapelekea wenzake ili watoa rushwa wachukuliwe hatua. Kama ana ushahidi kuwa kuna watu wanashughulikiwa kwa sababu wanaonekana ni tishio kwa Mbowe awakingie kifua katika kamati zao. Kama ana tatizo na Mbowe aseme wazi kuliko haya anayoyafanya. Mimi kinachonishangaza ni kuwa karibu wote waliosema Mbowe anawafanyia figisu figisu wamekimbilia CCM. Wangekuwa kweli ni upinzani kwa nini wasianzishe chama chao Kama alivyofanya Zitto au wabakie wapinzani huru.

Amandla...
 
Lissu anakosea sana kwenye hili. Kwa kufanya anachofanya anaaminisha jamii kuwa Chadema ina tatizo la kipekee la rushwa. Kitu ambacho sio kweli. Hatakiwi kustaajabu watu kutumia kila mbinu kupata uongozi ndani ya Chadema kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa Chadema kuwa na wabunge, madiwani na wenyeviti wengi baada ya chaguzi za mwaka huu na ujao.

Aidha, mshindani wao mkubwa kujaribu kupenyeza watu wake au kuwarubuni waliopo nao ni ishara kuwa chama chake kinakubalika sana na kimekuwa tishio. Yeye na viongozi wake wawekeze kwenye ku vet wagombea wote na watendaji wa chama kuhakikisha kuwa wamo kwa sababu wanakubaliana na sera zake,na sio opportunists. Kama nia yao ni kukivuruga chama basi matamshi yake yatawarahisishia kazi hiyo.

Kitu kingine ambacho hakipendezi ni yeye kurudia shutma hizi baada ya kiongozi mwenzake kuonyesha nia ya kuitaka nafasi aliyokuwa nayo. He is better than this.

Amandla...
mbowe kauwa saccos-CDM ambayo ni familia business sasa inaisababishia famila hasara kubwa mno royal family 😀
 
Back
Top Bottom