Tundu Lissu na wenzake waachiwa kwa dhamana

Tundu Lissu na wenzake waachiwa kwa dhamana

Unafanyeje mikutano ya HADHARA bila ya kibali cha polisi ?!![emoji15][emoji15][emoji1787]

TL ni wakili wa aina gani ?!!!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Wewe ni mjinga.

Kuna sheria inayoelekeza ukitaka kufanya mkutano upate kibali cha polisi?

Sheria inasema kuwa ukitaka kufanya mkutano umpe taarifa OCD kwa barua angalao masaa 48 kabla, kwaajili ya kupata ulinzi. Takwa hilo la kisheria lilitimizwa.

Huo ujinga uliofanywa na polisi wala hawataenda kuutetea mahakamani. Lengo la hao polisi wajinga ilikuwa tu kuvuruga mkutano uluokuwa umepangwa, wala hawatamshtaki Lisu.
 
Unafanyeje mikutano ya HADHARA bila ya kibali cha polisi ?!![emoji15][emoji15][emoji1787]

TL ni wakili wa aina gani ?!!!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Sheria haisemi polisi watoe kibali ,bali sheria inasema unatoa taarifa polisi ili watoe ulinzi sasa ukitoa taarifa na wasije hilo si jukumu lako wewe endelea na ratiba zako
 

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limempatia dhamama Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na viongozi wengine wa chama hicho waliokamatwa muda huu saa 2 usiku jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure amesema viongozi hao wametakiwa kesho saa tatu asubuhi kuripoti polisi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo iliyotolewa leo Jumapili Septemba 10, 2023 ilisema kuwa Lissu na wenzake watatu walishikiliwa kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia polisi kufanya kazi zao.

Mwandishi wa Habari kutoka Jambo TV, Oscar Kasubi aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo naye ameachiwa usiku huu.
View attachment 2745589

===[/B]

Pia soma:

Tundu Lissu akamatwa na Polisi akiwa Ngorongoro hotel Wilayani Karatu

Jeshi la Polisi: Tunamshikilia Tundu Lissu kwa kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia Polisi kufanya kazi yake
CCM inazidi kufa.
 
Habari ndiyo hiyo, wajeshi nao yasemekana wanataka ukweli kuhusu bandari kwani ni jukumu lao kulinda mipaka.
Jeshi gani? Hili la kujenga Taifa au la Iraq? Wanajeshi wanajitambua bana sio wajinga wajinga kama nyie Chadema
 
Mtu yupo hotelini chumbani kwake huo mkusanyiko ulikuaje!?mbona kama atawashinda mapema sana mahakamani,kwann hamkusubiria atoke nje!?

Kuna muda jeshi letu huwa silielewi
Kabisa!
Wanampotezea muda tu.
 
Someni Bibilia vizuri kitabu Cha wafalume ni somo sana kwa viongozi wa Ccm soma Wafisome yote jinsi ambavyo mkono wa Mungu hauzuiliki. Kuna mahali viongozi wanakuwa vipofu Ili jina la Mungu liinuliwe unawezaje kuwaza kuwalazimisha wananchi wahame kwenye asilia yao?
 
Habari hii ni kwa mujibu wa Martin Maranja Masese kupitia mtandao wa X.

-

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limempatia dhamama Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na viongozi wengine wa chama hicho waliokamatwa muda huu saa 2 usiku jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure amesema viongozi hao wametakiwa kesho saa tatu asubuhi kuripoti polisi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo iliyotolewa leo Jumapili Septemba 10, 2023 ilisema kuwa Lissu na wenzake watatu walishikiliwa kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia polisi kufanya kazi zao.

Mwandishi wa Habari kutoka Jambo TV, Oscar Kasubi aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo naye ameachiwa usiku huu.

policccm waliufanyia ushauriwangu kwamba ucku wa jana wasilale wajifungie ndani kupitia PGO sasa inaonekana wamegundua imekula kwao bora wawaache tu
 
Back
Top Bottom