Uchaguzi 2020 Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Pascal Mayalla,

Pascal naunga mkono hoja yako.

Kuhusiana na swali lako kama Tundu Lissu akishinda atapewa ushindi au la, ni wazi kuwa kwa mazingira yaliyopo hatapewa.

Kwanza ni vizuri ieleweke kuwa CCM bado ni chama dola na Tanzania bado iko katika mfumo wa utawala wa udikteta wa chama (dola). Huu uchama dola na udikteta wa chama kimazingira vimesimikwa kikatiba na kisheria. Mapendekezo ya Jaji Nyalali yaliyokuwa na lengo la kuiondolea CCM hii hadhi ili vyama vyote vya siasa viwe na uwanja sawa wa mapambano ya kisiasa nchini yalitupiliwa mbali.

Sifa moja kubwa ya mfumo wa udikteta wa chama dola ni kukosekana kwa demokrasia ndani na nje ya chama. Hii maana yake ni kwamba, kwa mfano, wananchama hawana sauti katika maamuzi makubwa yanayohusu chama kama nani apeperushe bendera ya chama katika uchaguzi wa urais.

Nafasi ya kutoa maamuzi ambayo yangetolewa na wananchama kidemokrasia kuhusiana na nani awe mgombea urais kwa tiketi ya chama huporwa na kutekwa na kikundi kidogo cha vigogo (kinaitwa deep state) ambacho sio rasmi lakini ndicho chenye maamuzi ya mwisho. Na deep state ikiishamua ni nani awe mpeperusha bendera wa chama dola basi biashara imekwisha; huyo ndiye de facto rais wa nchi. Huu ndio utaratibu unaotumika kwenye mifumo ya kiutawala ya Kikomunisti/Kijamaa na ambao CCM imeurithi.

Kiufafanuzi, itakumbuka mwaka juzi wakati wa kinyang'anyiro cha kumpata mgombea urais wa CCM wajumbe wa kamati kuu (CC) ya CCM Sophia Simba na Emmanuel Mchimbi walishangaa na kuhamaki ni vigezo gani vilitumika "kuwakata" watia nia zaidi ya 30 akiwemo mtu wao. Hii maana yake ni kwamba hata CC kwenye hili suala ilikuwa ni rubber stamp tu!

Ni deep state pia ndio imeweka utaratibu unaofuatwa siku zote (ambao pia sio rasmi kikatiba) wa kupokezana urais kati ya waumini wa dini mbili kubwa nchini. Na haitoshi tu rais kuwa muumini ya moja kati ya hizo dini mbili kubwa nchini, pia ni lazima atoke katika kikundi/dhehebu fulani.

Pamoja na haya maelezo, ni muhimu sana kwa upinzani na hasa Cdm kuwa na mgombea urais mwenye nguvu za kisiasa zinazotokana na uthubutu wake, uwezo wa kujenga hoja, ushawishi na weledi. Kama ulivyosema katika kambi ya upinzani mwenye hizi sifa kwa sasa ni Tundu Lissu pekee.

Lakini ni muhimu zaidi kwa upinzani kuweka mikakati makhsusi ya kuhakikisha wanaongeza idadi ya wabunge na madiwani. Lengo kimkakati liwe ni kufikia uwiano wa idadi ya wabunge katika bunge na madiwani katika mabaraza utakaowezesha kuwepo kwa checks and balances; kitu ambacho ni muhimu kwa demokrasia kushamiri pamoja na kuwepo kwa uwajibikaji.

Nitarudi ili kujaribu kutegua hiki kitendawili: "Sijasema Lissu ni zaidi ya Magufuli kwenye nini, na nawaomba sana msiniulize!"
 
Hahahahaha,asimame tu,yaani CCM inashinda bila jasho.Huyo Lissu hana personality ya kumfanya awe Rais.
TZ kwani tunaangalia hizo personality au mtu anawekwa tu hapo na aliyepo anasema alibeep tu ikajipa teh,teh,teh,teh.....
 
Usikute ni maoni kama haya yakawa yameponza watu bure!. You can never know with politics za kuelekea 2020 usikute ni kweli Lissu ameonekana a real threat!.
N.B, this is not conspiracy theory, it's just thinking aloud.

P
 
Paskali,
Naona mmeshaanza kumchulia na sijui mnamtakia nini....

Nataka nikutaarifu ya kuwa yule mzee ni hatari kuliko unavyodhania.............

Watu wa yule mzee ni wana machungu kuliko unavyodhania...............

Gharama iliyotumika kumtengeneza yule mzee ni kubwa ajabu kuliko unavyodhania..................

Sasa kumbe kuwa domokaya ni kigezo???



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali,

Unapenda sana kurusha jiwe gizani ila hata Wewe ipo siku utapiga mwanao au mkeo nakusihi uwe makini, nilikuonya ukajirekebisha naona bado kaugonjwa kanakurudia dozi labda haikukolea.

Lisu kwa Lipi?
1. Magufuli alifanya nini Jimboni akiwa Mbunge na Lissu kafanya nini Jimboni?
Uzuri wa Lisu unaupata wapi?

2. Unashangaa kudhubutu??????
Paskali- Kwani umesahau ni nani mbunifu na mwandishi orodha ya mafisadi papa??? Okay
Bila kashfa suala la kujivua Magamba lingekuja????

Je ENl angefukuzwa uwazir?? Imekuwaje Leo hii Tena huyo huyo waliyemharibia hadi kuonekana TakTak ktk Jamii waanze tena kusafisha Jamii hadi Leo haimwelewi huyo mlopokaji




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali,

Rejea barua ya Katibu Mkuu wa CDM wiki zisizozidi mbili ambayo ilifuta uchaguzi uliofanyika kupata viongozi wa kanda, na kupiga marufuku chaguzi zingine za kanda kwa madai kuwa kuna magenge ya Urais ndani ya chama yanavuruga demokrasia, ni Makundi gani hayo????

Naona mnampampu, ngoja aingie mazima,..............

Ila mie Nina wasiwasi kile chama sio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
spencer, Mkuu Spencer, soma bandiko langu kwa makini, nimesema Tundu Lisu ni zaidi ya Magufuli, hivyo he stands better prospects kumkabili Magufuli 2020, the motive behind the shooting could be a friendly fire to make believe ili idhaniwe ni kufuatia Lisu kuwa mwiba mkali.

P.
 
spencer,
Mm nimekuelewa vizuri mkuu gharama zao walizotumia ni kubwa sana nadhani hadi sasa wanalaani kitendo cha Tundu kunusurika ila hakuna namna itabidi waukubali ukweli kijana huyo kama akisimamishwa jukwaani na Jpm sijui kitatokea nn ila watu wamisha ona mbali Lissu ana uwezo wa kushinda kwa 70% Shida ni kwamba je atapita hata ktk mchakato wa awali wale watu watakubali billion zao kadhaa ziende Bure.

Sent using Iphone 7+
 
Usikute ni maoni kama haya yakawa yameponza watu bure!. You can never know with politics za kuelekea 2020 usikute ni kweli Lissu ameonekana a real threat!.
N.B, this is not conspiracy theory, it's just thinking aloud.

P
Uko sahihi mkuu watu wanaangalia upande mmoja tu
 
Back
Top Bottom