Tundu Lissu ni mwanasiasa bora wa upinzani kwa sasa

Tundu Lissu ni mwanasiasa bora wa upinzani kwa sasa

Lisu yupo sehemu sahihi kwasababu nguvu waliyoitumia kukifikisha chama kilipo itamchukua miaka mingi iwapo atahama. Labda chair wa chama anatakiwa ku step down harakati ziendelee. Kwasiasa za DJ hawajitofautishi na CCM maana ni masifu na mapambio.
Acha kubeza Mwenyekiti wetu. Ndiye aliyewalea hao akina Lissu, akima Zitto na wengine woote unaoona ni bora.
 
Wana hitajika wanasiasa wengi wenye kaliba ya Lissu kupambana na huyo aliye madarakani kwa msaada wa nguvu za dola.
Nguvu ya Lissu ya ujasiri na hoja ilichangia sana afya ya yule bwana kuwa sio dhaifu. Ingawa kufariki tumeandikiwa na Mungu lakini Lissu alimtia stress sana
 
Hatupaswi kuzikatia tamaa mkuu, ndizo zinazo amua hatima ya maisha yetu yaweje. tunapaswa kuzi rekebisha mahali zinapo enda ndivyo sivyo.
Watu waliofanikiwa ktk jambo lolote hawakati tamaa no matter what.
 
Ni kweli kabisa, Mbowe hastahili kabisa kuendelea tena kuwa mwenyekiti wa CDM, maana anaanza kugeuka kwa kasi kuwa kama akina Mrema, Shibuda, Cheyo nk. CDM wakiendelea kumuacha Mbowe kuwa mwenyekiti atakipasua chama. Mbowe ashauriwe kukaa pembeni, au atolewe kwa lazima kwenye uenyekiti.
Hatutaki siasa za visasi. Mbowe kwa sasa anapigania nchi ipate tume huru ya uchaguzi na katiba mpya kabla ya uchaguzi na haya ni makubaliano kwenye maridhiano. Huko mnakotaka tuanzishe ugomvi na serikali hatutakwenda huwezi kushindana na dola. Siasa hasa ya upinzani inahitaji busara na akili ya hali ya juu kutimiza malengo mbona kama mmeshasahu kwa muda mfupi tulipotoka?
 
Hatutaki siasa za visasi. Mbowe kwa sasa anapigania nchi ipate tume huru ya uchaguzi na katiba mpya kabla ya uchaguzi na haya ni makubaliano kwenye maridhiano. Huko mnakotaka tuanzishe ugomvi na serikali hatutakwenda huwezi kushindana na dola. Siasa hasa ya upinzani inahitaji busara na akili ya hali ya juu kutimiza malengo mbona kama mmeshasahu kwa muda mfupi tulipotoka?

Bora tusifanye siasa kuliko kufanya siasa za kuendeshwa kwa utashi wa CCM. Kwa taarifa yako siasa za kuongozwa na CCM ni bora wote mjiunge CCM.
 
Nime kuwa mfuatiliaji wa siasa za kitaifa na kimataifa kwa muda mrefu sasa.

Taifa letu la Tanzania limekuwa na siasa za uonevu mkubwa wa haki za msingi kutoka kwa watawala kwenda kwa watawaliwa.

Aina hii ya uonevu unao tendeka hapa nchini unao sababishwa kwa asilimia kubwa na watawala ambao ni CCM una hitaji aina ya siasa na wanasiasa watakao weza kukabiliana nao.

Tundu Lissu kutokana nami kumfahamu kwa muda mrefu kutokana na msimamo wake ni mtu sahihi kwa sasa kupambana na huu mfumo, kikwazo kikubwa kwa lissu kwa sasa ni chama alichopo na aina ya siasa ifanyazo kwa sasa haziendani na kaliba ya mwanasiasa kama Lissu.

USHAURI: Kwa sasa taifa lina hitaji aina ya wanasiasa kaliba ya Lissu waki ungana naye na kuweza kuanzisha chama kipya kitakacho endana na aina ya misimamo waliyo nayo ambayo ni sahihi kwa sasa katika kupambana na watawala [ CCM ] tofauti na misimamo ya kisiasa ya vyama vya upinzani vilivyopo nchi kwa sasa.

Tundu Antiphas Lissu hayupo mahali sahihi[ CHADEMA ]

: Haya ni maoni na ushauri wangu, vipi kuhusu wewe ndugu mwanachama mwenzangu wa jamiiforums katika jukwaa hili la siasa maoni na ushauri wako kwa lissu ni upi ? Karibu
Huyu si mwanasiasa bali ni mwana harakati. Alianza kama mwana harakati, anaendelea kama mwanaharakati na ataishia kama mwanaharakati.

Hana jipya, hasa katika zama hizi za siasa za kistaarabu. CHADEMA MSIFANYE KOSA 2025 KUMPITISHA MWANAHARAKATI KUGOMBEA URAIS AU UENYEKITI/chadema.
 
Hatutaki siasa za visasi. Mbowe kwa sasa anapigania nchi ipate tume huru ya uchaguzi na katiba mpya kabla ya uchaguzi na haya ni makubaliano kwenye maridhiano. Huko mnakotaka tuanzishe ugomvi na serikali hatutakwenda huwezi kushindana na dola. Siasa hasa ya upinzani inahitaji busara na akili ya hali ya juu kutimiza malengo mbona kama mmeshasahu kwa muda mfupi tulipotoka?
Busara na akili ipi ya kunyenyekea watawala wanao wamumiza watawaliwa pamoja na wao vyama vya upinzani ?
 
Huyu si mwanasiasa bali ni mwana harakati. Alianza kama mwana harakati, anaendelea kama mwanaharakati na ataishia kama mwanaharakati.
Mwana harakati ni mtu wa namna gani na mwanasiasa ni mtu wa namna gani ?
Hana jipya, hasa katika zama hizi za siasa za kistaarabu.
Siasa za kistaarabu zipi ? Za wizi wa kura ? , Za kupiga, kujeruhi, kuua na kupoteza watu kutoka kundi la watawaliwa ?, Kuminya na kukanyaga haki za kikatiba kwa kundi la watawaliwa ? Za kutumia vyombo vya dola? Za kuiba na kufilisi mali za watu kutoka kundi la watawaliwa walio kinyume na watawala ?
CHADEMA MSIFANYE KOSA 2025 KUMPITISHA MWANAHARAKATI KUGOMBEA URAIS AU UENYEKITI/chadema.
Mimi sio mwanachama wa Chadema.
 
Bora tusifanye siasa kuliko kufanya siasa za kuendeshwa kwa utashi wa CCM. Kwa taarifa yako siasa za kuongozwa na CCM ni bora wote mjiunge CCM.
Hakika.
 
Back
Top Bottom