Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Nikiibiwa kura nitawaingiza Wananchi barabarani

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Nikiibiwa kura nitawaingiza Wananchi barabarani

aseme akishindwa, na watapigwa kweli
Wananchi gani?
Hawa hawa wadanganyika wanaokupa moyo mitandaoni ikifika siku yenyewe kila mtu amejifungia kwake?

Sisi ambao tumefuatilia siasa za Tanzania tokea awamu ya kwanza tumewahi shuhudia watanzania wakiasi nchi na kutaka hadi kumuua Baba wa Taifa zaidi ya mara moja. Kaa ukikumbuka kwamba huyu Baba wa Taifa ndiye Raisi ambaye aliwahi kupendwa kuliko maraisi wote Tanzania na alilindwa sana na vyombo vya usalama. Lakini miaka yake ya mwisho ilikuwa imejaa vimbwanga vingi kutoka kwa watanzania hadi ikampelekea ang'atuke kwa amani.

Sasa sembuse utawala wa awamu ya tano kweli ??? Hivi nyie wandungu mmepeleka akili zenu likizo hadi kuzisahau siasa za Tanzania kipindi cha funga mkanda. Nadhani wewe ni shabiki na una utoto mwingi sana, lakini kama ungekuwa ni mtu mzima nadhani ungefahamu kwamba Tanzania inapita katika kipindi kigumu kuliko wakati wowote ule. Kama hatutakuwa makini basi tutakuja kuikumbuka hii miaka kwa masikitiko sana huko mbeleni.
 
Naamini tukipata watanzania 10 tu aina ya Lissu tunaweza kufanya yale ambaye The Jacobins waliyafanya Ufaransa mwaka 1789 au yale Bolsheviks waliyafanya Urusi mwaka 1917. Unajua Tanzania ya 2015-2020 ni kama Petroli(Very Ripe for a revolution), inahitaji watu wachache sana tu kupitisha kiberiti kwa juu moto ulipuke halafu mchezo uanze.

Unasema Tanzania ipi kulinganisha na hayo mataifa (Ufaransa au Urusi)? Mlinganisho gani huo usiofanana? Vigezo gani unatumia?
 
Unasema Tanzania ipi kulinganisha na hayo mataifa (Ufaransa au Urusi)? Mlinganisho gani huo usiofanana? Vigezo gani unatumia?
Nawazungumzia watanzania hawahawa ambao walilazimisha Mwalimu Nyerere ang'atuke mwaka 1985. Au unadhani alikuwa anataka kuachia madaraka ??? Soma historia ufahamu matukio ambayo yule Mzee alifanyiwa na watanzania kuanzia mwaka 1980-1985: Halafu ukiwa na ufahamu utatambua kwamba kama busara haitatumika basi tunaweza kuona ule ukurasa mwekundu unajirudi hapa nchini. Be vigilant my friend, Raisi Magufuli analivuruga Taifa.

Ubaya wa Afrika ni huu, tofauti kabisa na Ulaya ambako mapinduzi yalifanywa na wananchi huku kwetu huwa yanaanzishwa na maafisa wa vyombo vya usalama wakishirikiana na wanasiasa. Nimesoma vizuri siasa za mapinduzi duniani kama sehemu yangu ya masomo ya Chuo Kikuu,na nikafanya Case Study yangu Afrika.

Hivyo navyokwambia kwamba Tanzania iko pabaya sana namaanisha ninachokwambia maana dalili zote zinaonekana, na sifahamu kwanini wenzangu ambao ni wasomi na mko Serikalini au kwenye chama hamyaoni haya na hamna hata chembe ya woga. Tunaweza tukakaa hapa JF tukiandika Propaganda kuwatishia wananchi vifo lakini ukweli ni kwamba watu ambao wanaweza kulivuruga hili taifa na serikali wako huko huko serikalini (TISS, JWTZ na CCM).

Soma vizuri historia na uchambue mambo kwa hekima utafahamu kwamba Lissu is not a threat entirely but an agent of chaos or in other words A man who opens Pandora's box.
 
Toka 1995 upinzani unadai kuibiwa kura kwahiyo nawashauri tu wananchi mnaotegemea kuingizwa barabarani na Lisu muanze kupiga "tizi".
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Mwizi wa kura alihama akaenda chadema anaitwa chizii. Sasa Nani atamuibia kura? Muandamanaji wao mange Kesha bwaga manyanga labda ahamasishe walevi wa Mbowe.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Hayo maneno, kwamba amekuwa hivyo kwa sababu ya risasi, unampamba tu. Kwa wale tunaomjua Lissu hajabadilika. Maisha yake yote haheshimu mamlaka. Kwake yeye ndiye mamlaka ya mwisho. Ushahidi ni maneno aliyoyatamka wakati wa kuomba kura kwenye Mkutano wa Baraza Kuu la CHADEMA. Hayo maneno yanawakilisha kwa 100% tabia yake.

Lissu, anajua fika kuwa kesi zinazomkabili zinamweka katika mazingira magumu. Kwenye huo mkutano, akijibu swali kuhusu hizo kesi alijigamba kuwa hatishiki. Kwa hivyo anatafuta njia ya kutokea, ambayo ni ya yeye kuchaguliwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais. Kichwani mwake, kwa jeuri aliyo nayo, anamini kuwa, kama mgombea Urais, kutampa kinga dhidi ya hukumu na kitendo chake cha kufutiwa dhamana, baada ya wadhamini kujitoa.

Na isitoshe ana "kiporo" cha kueleza kuhusu tukio la kushambuliwa, wakati dereva, shahidi wake muhimu, kafichwa.
Kama kuna chochote hapo kwenye post yako basi unahalalisha point yangu ya kuwa Lissu ni narcissist, yeye anajiona yupo juu sio ya mamlaka tu bali he is special in every aspect. He is only short of calling himself a prophet hilo swala naona kawaachia wafuasi wa CDM ndio watamke.

Unajuwa nchi za wenzetu matatizo ya mtu yanaweza onekana baada ya ‘negative significant life event’. Mfano Lissu tangia ametua hakuna mtu yeyote alieshughulika nae mpaka leo lakini sikiliza anavyoongea utadhani amekuwa akikabiliana na vyombo vya ulinzi kila siku tangia amefika.

Kwa ivyo unaweza ona psychological impact ya tukio lake bado lipo kichwani it’s OK yeye ni binadamu lakini kumsaidia inahitajika psychological intervention ni jambo la kawaida nchi za wenzetu kuna mamia ya watu wanapoteza wenza kwa vifo vya ajali na kubaki na shock, kufukuzwa kazi bila ya kutarajia, watu wanapata ajali mbaya na kubaki na vilema, askari wanatoka vitani wameona mengi na kuuwa watu kadhaa, watu wanaporwa at gun point; etc with negative events. Kinachotokea sio kila mmoja wetu anaweza sahau kirahisi tukio lililomkuta, wengine coping mechanism inakuwa tested and we need help to make adjustments into the new reality.

Kwa kauli za Lissu anaonekana hayupo sawa anahitaji psychology/therapeutic intervention anaongea vitu ambavyo havipo kiuhalisia walau ajakumbana navyo tangia amerudi everything else is only on his head.
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Amesema AKISHINDWA, au AKIIBIWA?
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Labda ataingiza nyumbu ila sio watu
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Very hopeless argument. Yeye amesema akiibiwa kura, wewe unasema hata kama akiwa ameshindwa - unafahamu vizuri Kiswahili?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
LISU HAKUBALI KUIBIWA KAMA ILIVYO KWANGU
Sasa kaibiwa na nani wakati uchaguzi bado au amewahi kuibiwa lini wakati miaka yote amekuwa akishinda ubunge.

It’s in his head only inabidi aanze kuangalia mazingira kama yalivyo sio kuongelea vitu vya kufikiria kichwani kwake.
 
Wakuingiza watu barabarani alikuwa MH. MBOWE sio huyu mtoa povu.
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.
Kuna mqmbo mengine ni kuyawaza na kuweka mzani. Kama anahisi anakubalika hivyo. Asingepata na kugeuka omba omba kule alikokuwa.

Kiukweli kwa sasa, Hana mtaji mkubwa wa kura za wananchi.
 
Hiyo ndio Kauli ya Mh Tundu Lissu iwapo ikitokea ameshindwa kwenye uchaguzi mkuu mwezi October 2020. Ataingiza watanzania barabarani ikiwa ataibiwa kura zake.

View attachment 1526711

My take: Ni mapema Sana kwa mgombea urais kutoa kauli Kama hii si kiashiria kizuri. Anataka kutuaminisha kuwa hata ikitokea ameshindwa kihalali tuamini kuwa kaibiwa kura ili atimize azima yake.

Uongozi wa CHADEMA umshauri huyu mgombea kauli hizi hazifai kwa usalama wa nchi yetu.

Amesema akiibiwa sio akishindwa
 
Back
Top Bottom