Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Rais anasema hatutashitakiwa, kwa mwaka 2020 pekee makampuni matatu yametushitaki kwenye mahakama za kimataifa

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Rais anasema hatutashitakiwa, kwa mwaka 2020 pekee makampuni matatu yametushitaki kwenye mahakama za kimataifa

Akiwa mjini Kahama, mgombea urais wa Jamhuriya muungano ndugu Tundu Antipas Lissu amesema kuwa makampuni makubwa matatu kwa mwaka huu pekee yameishtaki Tanzania kwenye mahakama za kimataifa.

"Si walisema hatutashtakiwa? Oooh Lissu alisema tutashtakiwa...mbona sasa hatujashtakiwa? Niwaambieni, kwa mwaka huu pekee makampuni matatu yametushtaki kwenye mahakama za kimataifa" Amesema Lissu bila kubainisha haya makampuni.

My take: Kutokana na Rais kubana uhuru wa upatikanaji habari na kutokana na mambo ya ajabu tunayoelezwa na serikali huku mengine yakiwa waziwazi ya uongo, naamini alichosema Lissu.
Ni makampuni ya madini yaliyonyang'anywa Retention Licenses huku yakiwa yametumia mamilioni ya fedha.

Mabadiliko yale ya Sheria ya madini yaliyofanywa na Kabudi yana upuuzi mwingi sana.

Hebu fikiria Serikali yenyewe ndiyo iliyowapa retention licenses wawekezaji. Wawekezaji hawajakiuka sheria yoyote ile wala masharti ya leseni. Unalala unaamka unasema nimefuta retention licenses zote. Na waliokuwa wanamiliki retention licenses hawana maeneo! Lazima uwe mwendawazimu hasa kufanya kitu kama hicho halafu uamini kuwa huyo aliyeonewa hatakushtaki.

Tumeshtakiwa, hatuwezi kushinda hata tungepeleka wanasheria wa kutoka sayari ya Jupiter. Tutalipa. Tusipolipa, mnajua kitachotupata. Aheri anayetembea umbali wa km 20 kwa siku, kuna siku atamaliza km 200, kuliko anayeenda kilometer 40 kwa siku halafu anarudi nyuma km 50.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hatuogopi kushitakiwa unajua ni kwanini matokeo ya urais Tanzania hayapingwi mahakamani?
Lakini hapa mada ni serikali kushitakiwa.

BTW:Ungetuambia kwanza ni kwa nini MwanaCHADEMA akipinga maamuzi yoyote ya chama mahakamani anakuwa amejifukuzisha uanachama.
 
Lakini hapa mada ni serikali kushitakiwa.

BTW:Ungetuambia kwanza ni kwa nini MwanaCHADEMA akipinga maamuzi yoyote ya chama mahakamani anakuwa amejifukuzisha uanachama.
Mkuu tafuta kujua kwanza kwenye kupinga matokeo ya urais nani anashitakiwa kabla ya kulinganisha nchi na chama cha siasa.
Chadema ilinganishe na CCM na Tanzania ilinganishe na kenya,Malawi and other countries.hope umenielewa
 
Sasa kataja hizo kampuni?

Lisu ataaibika san kwenye uchaguI huu
 
Ha
Akiwa mjini Kahama, mgombea urais wa Jamhuriya muungano ndugu Tundu Antipas Lissu amesema kuwa makampuni makubwa matatu kwa mwaka huu pekee yameishtaki Tanzania kwenye mahakama za kimataifa.

"Si walisema hatutashtakiwa? Oooh Lissu alisema tutashtakiwa...mbona sasa hatujashtakiwa? Niwaambieni, kwa mwaka huu pekee makampuni matatu yametushtaki kwenye mahakama za kimataifa" Amesema Lissu bila kubainisha haya makampuni.

My take: Kutokana na Rais kubana uhuru wa upatikanaji habari na kutokana na mambo ya ajabu tunayoelezwa na serikali huku mengine yakiwa waziwazi ya uongo, naamini alichosema Lissu.
Hana sera huyo hajui anaongea nini, kama anajua hakuna uhuru aliwezaje kusema tuna kesi?
Yeyebkila siku anaongea ujinga kuhusu kesi, sasa akichukua nchi atazuia hizo nchi kutushitaki?
Au hizo kesi zilizofunguliwa zitafutwabkwa kuwa zinamlenga magufuri na sio nchi?
Huyu jamaa ni poyoyo sana.
 
Mkono Nimrod ameitetea tanesco sana mkuu

..siyo yeye aliyewakilisha Tanesco huko nje.

..unaweza kwenda kwenye website ya mahakama tunayoizungumzia na utakutana na listi ya mawakili wote wenye leseni za kusimamia kesi ktk mahakama hiyo.
 
Nchi nyingi zilizo/zinazo (kuwa/tumia) mfumo wa Ujama ni ngumu sana kuachia Dola walioitafuta kwa jasho la kutokomeza ukoloni.

Ili kuipata Dola ni lazima muungane nao ili kueneza itikadi zenu za kizalendo (mjifanye nanyi ni wajamaa), ingawa ni vigumu kupitia huko na kuja kuwa bepari.

Ni kweli hali ya maisha ni ngumu, kinachofanya maisha yanakuwa na nafuu kidogo ni kwasababu ya kuishi kijamaa.

Nchi hii ili iendelee ni lazima kung'oa mizizi ya ukoloni mamboleo na kuwa kitu kimoja katika ujenzi na keki ya Taifa.

Sipingi mfumo wa vyama vingi lakini napinga mtindo wanaoutumia kushika Dola.
Gambia walikuwa wajamaa na yahya jammeh alitoka
 
Mwambieni tunajua..hata mkulima katushtaki zaidi ya mara moja.. ila vipi kuhusu miga?
 
Muulizeni Lissu ile kesi aliwaomba wale wamakanikia wampe kazi ya kuishitaki Tanzania imefikia wapi? Mbona haiongelei tena? Kulikoni?

Huyu analotatizo kubwa, si kidogo, ndani ya Ubongo wake, si kidogo na rudia, tatizo kubwa abalo huyu!!! Alitaka tenda ya uwakili kwa wale wezi wa raslimali za Watanzania kwa jina la makanikia. Leo hii kisha sahau anafikiri Watanzania ni mandondocha wake. Anataka wamchague awe rais wao. Anapoteza muda na raslinali zake na za cdm bure kabisaa, hapati kitu.

Huyu huko Ubeligiji atakuwa kafundishwa mambo ya utapeli wa kisiasa. Kawa political coneman. Na ni mjanjamjanja sana tu. Kaiga staili ya JPM ya kusimama njiani akiwa safarini kuongea na wafuasi wake. Sasa Lissu kaona kila anaposimama idadi kama haisomeki kivile,sicho alicho kitarajia. Cheki zuga zake, ooh sijui kampeni hazijaanza nitarudi wakati wa kampeni. Unajua anachota ni umma udanganyike kuwa idadi ile ya watu wachache ni kwasababu kampeni bado hazijaanza Muambieni blabla za kisiasa hazitamsaidia kumfikisha popote.

Lakini mbaya zaidi sijui kama wengine mmeliona hili ambalo ndilo hatari zaidi. Huyu mpuuzi anataka kuingiza vyombo nyeti vya Usalama wataifa hili katika michezo yake hii ni hatari kwelikweli. Huyu mtu tusipochukua tahadhari kama taifa. Viko vyombo vya ulinzi na usslama ambavyo bila ya umamahiri wake amani na taifa hili la Tanzania pengine tusingekuwa navyo leo. Jamani keep a very close watch kwa huyu mtu ni hatari kwa usalama wa taifa hili, na sema janaa huyu ni hatari kuliko corona.
wew ni bure kabisa
 
TL binafsi nilisikitika sana alipojeruhiwa. Ila sikubaliani Naye kabisa kwa jinsi anavyopenda kuona Tanzania inanyanyasika na kupata shida na mataifa ya nje. Yeye ananufaika na nini?
 
Upande mmoja wenye haki yao walisha anza tangu 2015
Hawajawahi kukoma kupiga kampeni, wanahubiri barabara na madaraja kila siku kama vile ndicho chakula kwetu.
Huo ni ushamba, hawaoni hata haya kuhubiri vitu ambavyo tulipaswa kuwa navyo tangu miaka ya 90 sawa na wakenya
 
Back
Top Bottom