Pre GE2025 Tundu Lissu: Tuhuma za Msigwa kwa CHADEMA zichunguzwe, sisi si Malaika

Pre GE2025 Tundu Lissu: Tuhuma za Msigwa kwa CHADEMA zichunguzwe, sisi si Malaika

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapana.
Tundu Lissu kuwa muwazi ni sahihi kabisa. Ndiyo, mtuhumiwa mkuu, sasa ni wazi ni Mbowe mwenyewe. Acha maji yafuate mkondo wake.
Mbowe anaonekana tu kuwa si mpinzani wala mwanasiasa wa kweli na hayuko serious kwenye siasa zaidi ya kuichukulia siasa kama mradi wa biashara. Anakwamisha sana harakati za upinzani.
 
hawezi kupokelewa ccm, na hata akienda huko hawez kupata platfom.
lisu ni kigeugeu hata akienda ccm kuna siku atamgeuka mwenyekiti
Sema "Lissu siyo MNAFIKI"..., huo "ukigeugeu ni kuhusu nini? Ni lini ulimsikia akiwa kigeugeu?"
 
Kumekucha yeye ni makamu mwenyekiti taifa hivyo anapotaka MTU atoe majibu ni direct anamlenga Mwenyekiti WA Taifa WA Chadema Mbowe kuwa yeye kama Makamu hawezi jibu

Mbowe upoooo? Jibu tuhuma za Msigwa ukinyamaza kimywa maana Yake kweli

Lisu anakutaka ujibu usikae kimywa

Lisu yuko pamoja na Msigwa kwenye hoja zake na anaamini Msigwa ana hoja jibu Mbowe
of course yeye kama makamu mwenyekiti, aliyepo juu yake ni mmoja tu, Mwenyekiti. ukiona anachelea kusema hivi jua anawaambia watz kuwa mwenyekiti hachukui hatua, azichukue haraka au anawaambia pccb kuwa mwenyekiti na wenzake wanalamba asali waende wawachunguze. maana yake yeye angekuwa mwenyekiti angeshachukua hatua.
 
Mimi sina chama au itikadi lakini Nimekuwa nikifuatilia kwa umakini hojaji zao kuhusu masuala ya chadema au kupitia Lissu au Dr Slaa au mwingine yeyote. Inaonekana kuwa wanaibua issues zenye mwelekeo wa kuibomoa chadema. Mara kadhaa Dr Slaa amekuwa akiwakwepa sana katika kuwajibu. Na pia Tundu Lissu mpaka kufikia kuwaambia" wanataka aseme yajayo wanavyotaka wao" kwa kujaribu kumwekea maneno mdomoni ili hali ya kisiasa ichafuke.Chukueni tahadhari na mijadala yao.
 
Mbona ukikaribia uchaguzi tuhuma kama hizi hutolewa ndiyo kauli ya Lissu.He is not principled in mind. leo tena anataka haya yajibiwe wakati alisema kipindi cha kuelekea uchaguzi haya hujitokeza yapuuzwe.
 
Kwa kauli hii Lisu anatoa ujumbe kwamba umakamu mwenyekiti wake ni ceremonial (hauna meno), hivyo chama kinaongozwa na Mbowe tu.

Lisu kama kiongozi wa juu kabisa wa chama, kwanini hayo anataka yafanyike hajayafanya?
Nafikiri lissu ajiuzulu umakamu mwenyekiti awe mwachama wa kawaida kama anaona collective responsibility Ina muinflunce naye hapendi. Hii hali vinginevyo aendelee kuwa mnafikifi
 
Sema Yuko straight kuwa chama kinatakiwa kujibu yeye ndie kiongozi Namba mbili kitaifa kuwa yeye hawezi jibu ni direct message Kwa Mwenyekiti taifa kuwa ajibu Tuhuma Ake zinazohusu ufisadi wake wa Mali za chama kama Tuhuma za Msigwa zisemavyo
Kweli si vizuri myenyekiti kuacha kukujibu tuhuma inabidi aji u hiyo ni mojawapo ya damage control dhid ya tuhuma za msigwa
 
View attachment 3064512
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bara Tundu Lissu akizungumza katika mtandao wa kijamii wa Clubhouse amesema tuhuma zilizotolewa na Mchungaji Peter Msigwa dhidi ya CHADEMA zinapaswa kuchunguzwa kwasababu CHADEMA si malaika kwamba wasikosee.

"Inategemea hayo maneno mabaya (dhidi ya CHADEMA) yanahusu kitu gani na anayoyatoa ni nani, kama ni tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka, za ubadhirifu na ufujaji wa mali za chama hata kama yametolewa na mtu aliyeondoka katika mazingira hayo ya ndoa kuvunjika yanahitaji yapimwe ili kama ni ya kweli hatua zichukuliwe, na sisi sio malaika, sisi sio mitume sisi ni chama cha siasa kinachoongozwa na binadamu, inawezekana kuna makosa mahali,.

Sasa huyu anayetoa tuhuma pamoja na kwamba anatoa tuhuma baada ya kutoka nje hizo tuhuma ama zinahusu mambo mazito kama hayo niliyoyataja zinahitaji ziangaliwe na kutolewa maelezo kwa sababu kuzinyamanzia hivihivi siyo sawa, kama ni za kweli usipozitolea maelezo maana yake ni kwamba unaficha uovu, unaficha uchafu, na kama sio za kweli vilevile zioneshwe kwamba sio za kweli na katika hayo ambayo ameyasema Peter Msigwa nilisema yanahitaji kujibiwa kwa sababu ni masuala ambayo uthibitisho wake upo kwenye nyaraka, akaunti za chama zinasemaje, orodha ya mali za chama zisizohamishika ni ipi?

Kwa hiyo licha ya tuhuma hizi kutolewa na mtu aliyetukimbia katika mazingira tatanishi kama hayo hizi tuhuma zinahitaji kujibiwa na kutolewa maelezo ili wanachama na umma waondokane na taharuki ya haya yanayosemwa"- Lissu.
Kwa ufupi kwa Sasa ndani ya CHADEMA kuna ufa mkubwa. Na kwa yule asielewa maana utaona ni kwa nini juzi Ezekiah Wenje (Mmwenyekiti wa CHADEMA, kanda ya Ziwa) ametangaza rasmi kuwania nafasi ya Tundu Lissu (U-Makamu Mwenyeki Taifa).

Haya na tuendelee kuisoma picha🙂
 
Kumekucha yeye ni makamu mwenyekiti taifa hivyo anapotaka MTU atoe majibu ni direct anamlenga Mwenyekiti WA Taifa WA Chadema Mbowe kuwa yeye kama Makamu hawezi jibu

Mbowe upoooo? Jibu tuhuma za Msigwa ukinyamaza kimywa maana Yake kweli

Lisu anakutaka ujibu usikae kimywa

Lisu yuko pamoja na Msigwa kwenye hoja zake na anaamini Msigwa ana hoja jibu Mbowe
Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa nje wana kazi gani wajibu kwa niaba ya Mwenyekiti kama wanavyofanya wenzao CCM. kumbukeni kelele zote hizi ni kwa vile chadema kinaisumbua Chama Tawala, jipangeni uchaguzi ni keshokutwa.
 
Back
Top Bottom