Tundu Lissu: Tunasikia taarifa watu wanakufa kwa Corona lakini haisemwi wazi. Serikali imerekebisha Sheria inayozuia kupeana taarifa

Tundu Lissu: Tunasikia taarifa watu wanakufa kwa Corona lakini haisemwi wazi. Serikali imerekebisha Sheria inayozuia kupeana taarifa

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kuukimbia ukweli hakutatusaidia:

Watanzania, Kuukimbia ukweli hakutatusaidia

Heko Lissu hauko peke yako kwenye hili.

Mchana ni mchana haijalishi ni wapumbavu wangapi wangependa kwa kiasi gani kujidanganya kuwa ni usiku.

Koleo na liitwe kwa jina lake kwani koleo siyo kijiko!
Mpumbavu ni yule anaesema ndani kuna simba alafu anaingia hivyohivyo bila tahadhali!

Lisu anasema tz kuna corona lakini yeye anapuyanga bila thadhali
 
Kimzaha mzaha chadema wanaweza wasipate mbunge hata mmoja. Magufuli leo kaenda kuchukua fomu nec, kaongea vizuri sana kama mgombea urais.
Lisu ana hasira, visasi na chuki kwa watanzania. Yeye amekwenda kenya leo, amepimwa lini corona huko kenya? Amewekwa karantini?.
Kweli akili za kuambiwa changanya na zako. Naishauri serikali lissu akitua Tanzania apimwe corona lakini pia awekwe karantini maana huko alipotoka hali si shwari.
 
Yaani sisi watanzania tuliofunga siku tatu tukalia na kuomba Mungu akasikia kilio chetu akatuondolea hili balaa la corona leo hii anakuja mtu mmoja tena anayetegemea kugombea nafasi ya raia number moja hapa nchini anatunanga na kubeza juhudi zetu na huruma ya Mungu! Kwa kweli inauma sana.
 
Hata mm nimeshangaa mm binafisi napenda wapinzani wawepo ili kuleta maendeleo, maana kama hakuna upinzani serikali iliyopo madarakani italala usingizi. Lakini nashauri upinzani linapokuja swala la utaifa wetu tuwe kitu kimoja, kama tundu lisu anaamini bado korona ipo kwanini anaendelea na mikusanyiko? Sio poa inatakiwa aseme ataifnyia nini inchi iwapo atachaguliwa,sio kuendekeza porojo za kitoto eti tz kuna korona na watu wanakufa mbona anaendelea na mikutano yake bila kuchukua tahadhari yoyote.
 
Kimzaha mzaha chadema wanaweza wasipate mbunge hata mmoja. Magufuli leo kaenda kuchukua fomu nec, kaongea vizuri sana kama mgombea urais.
Lisu ana hasira, visasi na chuki kwa watanzania. Yeye amekwenda kenya leo, amepimwa lini corona huko kenya? Amewekwa karantini?.
Kweli akili za kuambiwa changanya na zako. Naishauri serikali lissu akitua Tanzania apimwe corona lakini pia awekwe karantini maana huko alipotoka hali si shwari.
Sema makonda katolewa bila ivyo tundulisu angefikia karantin
 
Ama kweli ni aibu sana kwa vyombo vyetu vya habari hapa nchini.

Mtu aliyekuwa mbunge na aliyeshambuliwa kwa risasi zaidi ya 16 kama tembo mharibifu wa mazao na tishio la maisha ya binadamu.

Anarudi nyumbani mnashindwa hata kufanya naye interview kuhabarisha wananchi!
Muda mfupi mh Tundu Lissu atakuwa mbashara kuanzia saa 8: 00 mchana,Vituo vitakavyokuwa live Ni @standardKenya na @KTNNews, hii Ni kwamjibu wa Tumaini Makene

======
Mwandishi: Ulikuwaje mchakato wa kupona ulikuwaje?

Lissu: Asante kwa kushiriki kwenye kipindi chenu na kuongea na wananchi wa Kenya kuhusu mambo ya Tanzania, Nimekaa miezi minne Nairobi, nilipata huduma nzuri sana za kiafya kutoka kwa madaktari wa Kenya, nina damu nyingi ya wakenya inatembea kwenye mishapa yangu ya damu, nawashukuru watu wa Kenya kwa kuniangalia kwa miezi minne na baadae nikaenda Ubelgiji kutibiwa kwa miezi 11.

Mwandishi: Ulipoteza kiti chako bungeni wakati uko kwenye matibabu, ilikuwa halali kisiasa au kisheria?

Lissu: Wanasema sikuwepo bungeni lakini kila mtu anajua sikuwepo bungeni kwa sababu ya jaribio la mauaji September 2017. Wale waliojaribu kuniua kwa bunduki waliposhindwa ndio wakaamua kunipokonya siti yangu bungeni. Haikubaliki kibinadamu na kisheria labda kisiasa kwenye hesabu zao za siasa.

Mwandishi: Upinzani bado haujaungana kukikabili chama tawala cha CCM, kuna uwezekano wowote upinzani kuongea kwenye sauti moja?

Lissu: Nafikiri kwa upinzani umemaanisha chama changu cha CHADEMA na ACT- WAzalendo(Lissu amekatika). Tunafanyia kazi hilo, kuna baadhi ya mambo ya kisheria yanatakiwa kufanyiwa kazi na mitego ya kisheria.(Lissu amekatika).

Mwandishi: Tanzania imekuwa haitoi namba rasmi za Corona toka April 19, wapiga kura wakienda kupiga kura, tunawezaje kuwalinda wakati wa mchakato wa upigaji kura, kitu gani kitakuwa tofauti kwenye mchakato ambacho kitawalinda?

Lissu: Hili ni suala ambalo linatufikirisha, tuko katikati ya gonjwa la mlipuko lakini serikali yetu imesema wazi kwa dunia kwamba hakuna corona hivyo Rais aliposema hakuna shida wananchi wamefata, watu hawaachi nafasi baina ya mtu na mtu, litakuwa tatizo kubwa kutoka sasa mpaka uchaguzi mkuu. Napenda kuwaomba wananchi wa Tanzania kuamika silika zao na wafanye maamuzi yao hasa kutokana na Rais kutolikubali hili gonjwa.

Nawaomba wananchi wapeane nafasi, wavae barakoa, wanawe mikono na kufanya vyote ambavyo wataalam wamewaelekeza kuepuka maambukizi ya korona.

Mwandishi: Tukiongelea Covid19, unaweza kutupa picha gani kutoka nchini kwako?

Ni picha inayohuzunisha, tunasikia taarifa watu wanakufa kwa corona lakini haviongelewi wazi, serikali imerekebisha sheria ya mitandao inayozuia kupeana taarifa kuhusu huu ugonjwa, ukisema unavunja sheria na unaweza kufungwa. Wananchi wafanye maamuzi yao na wasisikilize ushauri mbaya wa watu kutoka serikali kwamba hamna tatizo, corona inaua na ipo Tanzania.

Mwandishi: Unaongeleaje haki za binadamu?

Lissu: Rekodi ya haki za binadabu Tanzania ni janga, hii miaka mitano tumeona historia mbaya zaidi katika historia yetu yote.(Lissu amekatika)

 
kwa sababu ni mda wa kampeni wacha tu waongee, sisi tunataka aongezewe mda atake asitake
 
Hoja za Lissu ni kuhakikisha Wapiga dili wanakwamisha Mipango yetu ambayo mpaka saizi wamekwama.

Mfano Mtu unajikweza kwa Wakenya waliorubuni ndege za EAC ambazo ni za Watz na wana EAC si lazima unatambulika kwamba upapeti wako ni wa namna vipi [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Wakenya hao hao walikubali kumchangia damu mh Lissu wakati yupo mahututi wakati nyie mliwakataza watu kumchangia damu, hata watu kumuombea mliwakataza!

Kabla ya kuchangia lazima uwasiliane na ubongo wako kukumbuka yaliyo pita.
 
Wapinzani wa Tanzania bwana.

Sasa kama hali ni mbaya Kwanini alikusanya watu kipindi anatoka ulaya?

Kwanini bado wanaendelea kuwakusanya watu kwenye mikutano yao?

Kuna tatizo kubwa kwenye upinzani hasa Lissu na chama chake.
 
Back
Top Bottom