Tundu Lissu: Tunataka Rais afute mashtaka dhidi ya Mwenyekiti Mbowe bila masharti yoyote

Tundu Lissu: Tunataka Rais afute mashtaka dhidi ya Mwenyekiti Mbowe bila masharti yoyote

Elimu ya kuunga-unga ndiyo inaimaliza Tanzania. Unajua au umewahi kusoma historia yoyote ya ukombozi? Unadhani kina Nyerere wangekuwa wana mawazo mgando na ya kioga namna hii uhuru ungepatikana?
Kipindi hicho WaTanzania hawakua waoga na waliungana na Nyerere, leo hii unaona wa Tanzania kama hao?

Tundu Lissu hakuwa mwoga, alipingana na Magufuli kwa hoja, kilichonkuta unakifahamu, Watanzania walionyesha reaction gani?
Uchaguzi wa S/Mitaa ulifanywa kihuni kabisa hadharani hadi CCM wengi wanakiri, Wa Tanzania walifanya nini? Uchaguzi Mkuu hivyo hivyo, je kulikuwa na reaction gani?
Kama yote hayo yalitokea hakukua na reaction yoyote, Mbowe akiendelea kukaa gerezani kutakuwa na reaction gani ya maana?
 
Sijasema aombe msamaha,
Mkuu una nia nzuri. Lakini fahamu kuwa, kwanza, Mbowe amejitoa mhanga mkubwa sana kuifikisha CHADEMA hapo ilipo. Nafikiri sihitaji kukueleza madhila aliyopitia katika harakati hizo. Hata kifo kimemkosakosa toka kwa haohao wanaotaka kumfunga. Pili, lengo kuu la serikali/CCM ni kummaliza Mbowe na CHADEMA kisiasa. Hiyo kesi ni sehemu ya mkakati huo ingawa imewaendea vibaya. Sasa Janja inafanyika kumpigisha Mbowe na CHADEMA magoti kuomba msamaha (kwa kosa ambalo hakutenda) Ili anyenyekee utawala wa awamu ya sita.

Sasa jiulize, Mbowe akishasamehewa kihivyo na kukiri "maovu" aliyotaka kulifanyia taifa kisha kushukuru fadhila za Rais, credibility yake na ya CHADEMA zitakuwa wapi? Nani atawasikiliza tena?

Angalia mfano wa James Rugemalira aliyekaa miaka minne jela kusimamia haki yake ya kuwa innocent na kuonewa na serikali chini ya Rais JPM. Kwa kifupi, kuna masuala na wakati mwanaume analazimika kusimamia "principle" zaidi ya chochote. Mbowe ametoka mbali sana na CHADEMA yake. Hawezi kupoteza yote KWA MSAMAHA UCHWARA hivi hivi tu. Alivyokomaa kuhusu harakati za katiba mpya alijua hatari na gharama yake. Alikuwa tayari kuilipa na mchakato unaendelea. Lissu is right.
 
Haya maneno yangekuwa na meaning kama yangetoka kwa Mbowe mwenyewe na sio walio nje,Na hakika wanafamilia yake watataka mzee wao atoke kwa vyovyote vile.
Ni kweli Mkuu, kuna mambo mengine inabidi kupiga kimya sometimes
 
"Rights never pleaded but demanded strongly regardless who you are facing."
 
TUNAONGEA SANA KWA KUWA TUKO NJE YA MAHABUSU
Yaani issue iwe ya haki sio huruma ya Mama. Kama Mbowe ana makosa ya kweli, basi mahakama iyaone bila shaka yoyote nasi tuone hukumu ya haki. Sio ati asamehewe kisa mashahidi wa kuchonga, mawakili wa kuchonga na jaji wa kuchonga. Kama Mama kweli ni muumini na mcha Mungu na hataki akahukumiwe kwa uonevu alio mfanyia Mbowe aachane na hii kesi na aombe radhi. Kinyume na hilo, sala zinazo wekwa mbele ya Mungu juu ya huu uonevu hazita muacha mtu salama.
Ona sasa amesahau alisha iambia dunia Mbowe ni gaidi. Leo anasema Mbowe ana dharau sheria. Mungu huwaweka wanafiki hadharani kweupe.
 
Lisu angerudi tu nchini ili awasaidie kazi ya utetezi kina Kibatala.
Waliomshambulia Kwa risasi waliwahi kukamatwa??? Au unamaaisha nn??? Au unataka aje amaliziwe kama sio kumuunganisha kwenye kesi ya kubumba???
 
Nchi yetu ni kama ina laana. Watu ni wavivu mpaka kufikiri. Hivi wanadhani waafrika wa enzi hizo wangekuwa waoga uhuru ungepatikana? Mandela aliambiwa mara ngapi aachiwe kwa masharti akakataa?
Mkuu tuna tatizo kubwa sana la Elimu hapa nchini mwetu. Wengi wamekwenda darajani kuhitimu na siyo kuelimika.
 
Lisu anapenda kuamrisha kama yeye anavyoamlishwa na mme wake Amsterdam
Na wewe mbona unapenda kutukana tatizo huwezi ona kundu lako kwani aliyosema Lissu kakosea wapi??jua sheria itakuweka huru.
 
Waliomshambulia Kwa risasi waliwahi kukamatwa??? Au unamaaisha nn??? Au unataka aje amaliziwe kama sio kumuunganisha kwenye kesi ya kubumba???
Labda yalikuwa ni maagizo toka kwa mtu ambae ameshafariki. Hivyo ugomvi umeshaisha.
 
Sasa unasema hivyo upo nyumbani, ila Mbowe yupo magereza, Dunia inajua, imefanyaje Dunia?
Kuna viongozi huko Belaraus, sijui Myanmar, Venezuela n.k wamefungwa kibabe kwa sababu za kiasiasa Dunia inasonga tu, unataka Mbowe yamtokee hivyo?
Siasa ina gharama zake na wanasiasa wanajua hilo,na sio lazima mfungwe wote,ukisema eti wanaongea humu wako nyumbani lakini Mbowe yuko magereza unamaanisha nini?wala haina mantiki.Kama Mbowe angetangaza kuacha kile alichokuwa anakipigania yaani katiba mpya ana namna nyingi za kuwasiliana na SSH na angemwomba amsamehe.Lakini kutumika kwa Zitto kumwombea ni ukakasi mkubwa akikanwa na Mbowe kuwa hakumtuma huoni itakuwa fedheha kwake Zitto??
 
Mtanisameh Bure ila Sina uhakika Kama kumwaachia mbowe kunaweza kuleta kile kinachoitwa maridhio ya kisiasa, mbowe akiachiwa Basi hata sambaya anapaswa kuachiwa, kwa nn nasema hivyo!![emoji15][emoji15]??

Wote wanamakosa ya kisiasa, wote walikuwa wanabifu, wote walikuwa eneo 1, wote wanatuhuma zinazofana kwa asilimia 80, wote wanauhanga wa kisiasa,

Tofauti yao Ni kuwa wanauhasama wakisiasa, 1akiona kanyang,anywa Jimbo,(na kwel sambaya) alifanya kazi yake vzr, mwingine akiona anaonewa kwa sabb mtu aliempa kazi hayupo, kwa hyo kila mmoja analia kwa namna yake,

Kwa namna kesi ilivyo na ipo mahakamani, haiwezekani uRais kuingilia, hii kesi inanikumbusha ile kesi ya wale wanamamziki, mvua iliwahusu, japo huenda haikuwa stail yao, Sasa kwa mbowe na sambaya wao kwa kwel wapambane tu na hali zao, mpka mwisho mahakama itende haki, ili kila mtu apate anacho stail kukipata..

Nini athari ya kuingilia maamzi ya mahakama?

Itakuja kwenye tafsr ya imbalance of law, kwamba kunawatu nchi hii wakifanya makosa hawezi kushitakiwa au kupatikana na makosa, Ikiwa tutafikia huko Ni hatari kubwa

Jambo jingine Ni hli itaathiri mahakama zote na maamzi yote ya kimahaka, tuache mahakama zifanye kazi,
 
Sasa unasema hivyo upo nyumbani, ila Mbowe yupo magereza, Dunia inajua, imefanyaje Dunia?
Kuna viongozi huko Belaraus, sijui Myanmar, Venezuela n.k wamefungwa kibabe kwa sababu za kiasiasa Dunia inasonga tu, unataka Mbowe yamtokee hivyo?
Huyo Samia ajaribu kumfunga Mbowe, aone. Anajua alivyoanza na alivyotengeneza hao watu wa mchongo, ila sijui kama anajua jambo hili litakavyoisha!! Laiti angejaliwa hekima kidogo tu asingefanya huu ujinga.

Ajue yeye siyo Magufuli.
 
Utetezi wa Mbowe
1. jaza wazungu wengi mahakamani na uwape sifa na hadhi ya ubalozi,
2. weka mawakili wengi ambao kazi yao ni kudharirisha watu kwa kufanya hivyo kuchekesha wahudhuriaji
3. Alika wanachama wengi ikiweme na maaskofu na wapikiwe mihogo kama wale waliohudhuria mkutano wa Yesu na kupewa vipande vya mkate na samaki
4. fungua kesi ndogo nyingi ndani ya kesi kuu
5. weka mapingamizi mengi iwezekanavyo
6. jaza mitandao yote ya kijamii kwa #mbowesiyogaidi
Umeisahau kuweka matokeo = baadae inakuwa Nini?
 
Lissu angekaa kimya kwanza, Mbowe atoke, then ndio aanze.
Kulumbana kuanze baada ya Mbowe kutoka
Maana sidhani kama CDM wana leverage yoyote ya kumtoa Mbowe hata kama ni kesi ya mchongo kama inavyoonekana
Ni muda wakawa pragmatic
Nadhani uko sahihi. Lakini vile vile hatuwezi kuusemea Moyo wa Mbowe, làbda Mbowe yuko tayari kufia jela
 
Back
Top Bottom