Chief Kabikula
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 7,567
- 9,037
Hapa tunaongelea makosa ya mgombea, jiwe limerushwa na mshabiki au mpenzi wa chama flani tume haiusikinaye. TUME INADEAL NA MAKOSA YA MGOMBEA TU.Soma vizuri ulichoandikaMleta mada kwa hiyo mgombea akipigwa jiwe hiyo kesi inatakiwa ipekwe tume sio polisi?
Na mgombea akimkata panga polisi hiyo kesi inatakiwa ipelekwe tume ?
Una akili finyu ugombea hauondoi jinai
Siro nenda kesho ukamkamate Lissu mbele ya mabalozi , uonekane bonge la IGP au vipi kijani kibichi mataga wa Lumumba mshaurini Siro afanye hivyo apandishe CV , awe wa kwanza kutangulizwa ICC bosi wake anayemtuma atamfuatia baadaye .
hivi kwanza nataka kujua, kosa la lisu ni lipi?
Mbona hili ni kosa dogo sana! why linakuzwa namna hiyo?Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amemtaka mgombea urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu, kuripoti kituo cha Polisi Moshi Kilimanjaro, kutokana na kitendo anachodaiwa kufanya cha kukaripia, kuwagombeza na kugombana na viongozi wa polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amemtaka mgombea urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu, kuripoti kituo cha Polisi Moshi Kilimanjaro, kutokana na kitendo anachodaiwa kufanya cha kukaripia, kuwagombeza na kugombana na viongozi wa polisi.
lissu anatafuta sqbabu ya kushindwa
kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu,maelezo utayakuta polisi,na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote
Amefanya kosa gani?Basi utakamatwa kwa kukataa kutii sheria bila shuruti!
Elfu saba huyo, anatapatapa kupigania ujira wake.Tulia wewe mtu mdogo huelewi kitu
Ongezea Komredi kinana hapo.Uhamiaji watamtaka Lissu athibitishe uraia wake. Hoja ni kwamba haiwezekani Lissu awe mtanzania. Uliona wapi mtanzania jasiri hivi? Watanzania halisi ni kama akina Komredi Membe, Lyatonga Mrema, akina Askofu Gwajima, Komredi Makonda, na watu wa aina hiyo
BamTundu Lissu katika Ukurasa wake wa Twitter, ameweka Barua ya Polisi na kuandika Maneno haya "Wito wa polisi sio barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria. Wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa. Barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama. Huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria. Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho."
View attachment 1587622
View attachment 1587514
Sie mbona huwa tunapigwa tanganyika jeck tu, ukifika selo unaambiwa tumekuweka ndani kea usalama wako au DPP kaghairi kukushitakiHeheheee.... Ukweli ni kwamba, hiyo ni sawa sawa na barua ya harusi tu!
Wito au barua ya polisi LAZIMA ieleze KOSA ANALOITIWA KWALO ikiambatana na "statement of probable cause" kuhusu kosa hilo!
Huwezi tu kuita mtu kienyeji enyeji! Angalau sio kwenye nchi tunayoiita "Jamuhuri" (sijui hata kama unaelewa maana ya Jamuhuri wewe mataga?)
Vinginevyo hiyo itakuwa ni Jamuhuri ya kihuni tu kama mapolisi watakuwa wanajiendesha kama genge la walevi.
Polisi hawako juu ya sheria. Wafuate hizo procedures waache kujidekeza!
Polis wanafanya makosa makubwa sana kisheria, sio kila kosa ni LA kushughulikiwa na polis hata kama linawagusa polis wenyewe.Kwa mfano tukio analodaiwa kutenda lissu limetokea katika mazingira ya kampeni za uchaguzi, polis walipaswa kupeleka malalamiko kamati ya maadili ya tume ya uchaguzi, tukisema kila kinachofanywa na mgombea kipelekwe polis muda huu sio sawa..Mkumbusheni Lisu kuwa kuna mstari baina ya kuwa mgombea na kuwa Rais,
Sasa yeye anafikiri kuwa mgombea wa Urais ndio tayari ushakuwa Rais hivyo unakuwa juu ya vyombo vya dola.
Aende tu huko anakoitwa kwani jamaa wanauwezo wa kumfuata na kumchukua muda wowote wakitaka.
Barua haijatoa muda anaweza enda hata mwakaniPolisi watakubali tu yaishe kama tume walivyonyamaza kmya baada ya kuwa wanaropoka ropoka kwenye vyombo vya habari