Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

Polis wanafanya makosa makubwa sana kisheria, sio kila kosa ni LA kushughulikiwa na polis hata kama linawagusa polis wenyewe.Kwa mfano tukio analodaiwa kutenda lissu limetokea katika mazingira ya kampeni za uchaguzi, polis walipaswa kupeleka malalamiko kamati ya maadili ya tume ya uchaguzi, tukisema kila kinachofanywa na mgombea kipelekwe polis muda huu sio sawa..
Ni kweli hizi Ni kampeni, eidha wapeleke malalamiko time au wamkamate tu Kama Kuna jinai
 
lissu anatafuta sababu ya kushindwa
kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu,maelezo utayakuta polisi,na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote
Ni mazoea au ndio Sheria inasema hivyo?
 
Heheheee.... Ukweli ni kwamba, hiyo ni sawa sawa na barua ya harusi tu!

Wito au barua ya polisi LAZIMA ieleze KOSA ANALOITIWA KWALO ikiambatana na "statement of probable cause" kuhusu kosa hilo!

Huwezi tu kuita mtu kienyeji enyeji! Angalau sio kwenye nchi tunayoiita "Jamuhuri" (sijui hata kama unaelewa maana ya Jamuhuri wewe mataga?)

Vinginevyo hiyo itakuwa ni Jamuhuri ya kihuni tu kama mapolisi watakuwa wanajiendesha kama genge la walevi.

Polisi hawako juu ya sheria. Wafuate hizo procedures waache kujidekeza!
Hivi 'mataga' haina umoja kama ilivyo kwa maneno; mazingira, dini, n.k?
 
Tundu Lissu katika Ukurasa wake wa Twitter, ameweka Barua ya Polisi na kuandika Maneno haya "Wito wa polisi sio barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria. Wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa. Barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama. Huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria. Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho."
View attachment 1587622
View attachment 1587514
Kuigomea polisi kufanya uchunguzi ni kinyume cha sheria; sasa sijui yeye ni mwanasheria gani. Wakati mwingine polisi wanaweza kutaka kukuhoji wewe kama shahidi kuhusu mtumhumiwa mwingine tofauti kabisa ambaye wanaweza kuwa na taarifa zake zaidi. Ni afadhali angejibu tu kuwa sasa hivi ratiba yake iko tight sana anaomba akutane na polisi katika muda mwingine siyo sasa kuliko kuweka jou hilo la kukaidi, kwani tayari ameshaweka ushahidi unaoweza kutumika dhidi yake; ndiyo maana nina mashaka sana na busara za Lissu pamoja na uanasheria wake. Hiyo kisheria ni kuizuia polizi kufanya kazi zake ammbalo ni kosa. Raia kuhojiwa na polisi ni sehemu ya majukukumu ya polisi kabla hawajamchukulia mtu hatua; yeye Lissu anaogopa nini kuhojiwa kama anajua yuko clean?
 
Heheheee.... Ukweli ni kwamba, hiyo ni sawa sawa na barua ya harusi tu!

Wito au barua ya polisi LAZIMA ieleze KOSA ANALOITIWA KWALO ikiambatana na "statement of probable cause" kuhusu kosa hilo!

Huwezi tu kuita mtu kienyeji enyeji! Angalau sio kwenye nchi tunayoiita "Jamuhuri" (sijui hata kama unaelewa maana ya Jamuhuri wewe mataga?)

Vinginevyo hiyo itakuwa ni Jamuhuri ya kihuni tu kama mapolisi watakuwa wanajiendesha kama genge la walevi.

Polisi hawako juu ya sheria. Wafuate hizo procedures waache kujidekeza!

Na inakuwaje barua confidential inapitia kwa mtu mwingine? Confidentiality ipo wapi hapo?
 
Wito wa "kishkaji" siyo wito wa kisheria, polisi ifuate sheria na Lissu atatii sheria!

Lissu hawezi kuacha mambo ya msingi afuate wito ambao haujazingatia sheria, huko ni kupotezeana muda!
Tena ni ujuha kutumia headed paper ya Jeshi la Polisi yenye nembo na kubandika neno confidential wakati barua inapitia kwa mtu mwingine hivyo kuondoa umaana wa confidential na content (maudhui) ya barua hayakidhi haja ya kisheria ya kumuita mtu Polisi.
 
Tundu Lissu katika Ukurasa wake wa Twitter, ameweka Barua ya Polisi na kuandika Maneno haya "Wito wa polisi sio barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria. Wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa. Barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama. Huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria. Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho."
View attachment 1587622
View attachment 1587514
Kubattle na Lissu inahitaji akili mingi, unfortunately so far wote wanaojaribu wanatumia 'nguvu 9 na akili 1', watafeli wote!!
 
lissu anatafuta sababu ya kushindwa
kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu,maelezo utayakuta polisi,na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote
Ambapo huyo mwanasheria utampata muda gani ilhali barua/wito haujakupa hiyo nafasi?
 
Kabudi no waziri wa mambo ya nje ndie bosi wa mabalozi wote aweza ongea nao anytime
Mabwana zako hawa hapa wakijichekesha mbele ya MABEBERU [emoji116][emoji116]
tapatalk_1597997134958.jpeg
 
Back
Top Bottom