Tunduma ni mji wa kipekee. Mapigo yake ni kama Kariakoo

Tunduma ni mji wa kipekee. Mapigo yake ni kama Kariakoo

Ongeeni yooote, mwisho wa siku kwa Tanzania hii hakuna sehemu yenye mzunguko mkubwa wa pesa kama Kariakoo hata ukiweka mahaba yako ila uhalisia utabaki kuwa kama ilivyyo. Ukishangaa uuzwaji wa bidhaa kwa bei nafuu Tunduma, nenda Katoro na Geita kwa ujumla na ni miji ambayo haiko mpakani ila kuna bidhaa zina either bei nafuu kama Kkoo au sawa na Kkoo lakini mwisho wa siku bado wafanyabiashara wanapahitaji Kariakoo.
Walichokiangalia Wadau ni wengi na ukubwa Wa kariakoo unachangiwa na population yote ya Tanzania wanaitwgemea Kariakoo, Ila wanaosifia Tunduma wanaangalia. Udogo wa Mji na Shughuli Zinazofanyika Tunduma utaona napo Panaukubwa kiasi Gani kwenye Shughuli za Kiuchumi. Naifahamu sana Kariakoo na ni mwenyeji mitaa na piya

Nikiangalia Shughuli Zinazofanyika Pale Tunduma kuanzia Mpemba kwenye parking ya Malori, Chapwa, Halafu uangalie kuanzia pale custom halafu upande Juu kusogo kuanzia polisi yale Maduka ya matairi na simu uingie ndani kwenye Maduka ya nguo pale sokoni, uende kwenye Maduka ya electronics , Uende Kwa Wauza Fedha mikonini, Uingie soko la Viatu Nyuma ya Dukani Kwa Manyanya. Halafu usogie Kidogo Black Market uone Elivyoshikwa na Wandali na Wanyakyusa,

Halafu uone Soko la Fedha Mkononi lilivyoshikwa na Wasafwa na Wanyakyusa, Nenda kwenye Maduka ya Nguo ni Wakinga na Wandali, Electronics na Simu ni Wakinga Maduka ya Spare na Hardware ni Wandali na Wakinga, Kwenye Matairi ni Wamalila. Ukiangalia wengi wa watu na biashara Bado Tunduma ipo vizuri Kwa ujumla ukiwacha KKOO hakuna sehemu kama Tunduma Tanzania Hii Kwa mzunguko wa Fedha. Ukienda kwenye mabanki ndio utaona huo mzunguko Kuna wateja watatu tu wanaweza hudumiwa zaidi ya masaa mawili kwenye bulk teller.
 
Hakuna sehemu ambayo hela ni Nje Nje 😁😁

Ndio mnavyodanganya watu si ndio?
Hakika kabisa hakuna sehemu ambayo utakaa tu kizembe zembe alafu utegemee fedha iingie bila kukaza buti .Ule ni mji wa kuchakarika na kama unataka fedha ije kichwa lazima ifanye kazi ,kitu kingine Tunduma licha watu kuwa na hela nyingi lakini watu baadhi pia wanajishughulisha sana na kilimo cha mahindi kitu kinacho ongeza flow of money
Tanzania Kuna nafuu kuliko huko Bush Zambi
 
Sidhani kama Kariakoo Kwa volume ya biashara inaifikia Tunduma,najua mtabisha ila tukija kwenye figures ndio utashangaa.

Mkoa wa Songwe ni WA 6 Kwa mapato makubwa(TRA) Tanzania na 90% ya mapato hutoka forodha ya Tunduma zaidi ya Bil.150

Kariakoo ni bil.40 [emoji23][emoji23]
Mkuu, hivi unaelewa ulichoandika?

Unaijua vizuri Kariakoo?
 
Nenda pale Black Market Kuna Maduka yanauza Tena unawambia unataka upeleke wapi wanampa Boda boda anakuletea Hadi point unayotaka kufikishiwa, Maduka ni ya Wandali na Wanyakyusa ule upande wa Zambia


Ukihitaji ufafanuzi zaidi nita
 
Nilichoka hapo Tunduma baada ya kukuta vijana wamepanga hela mikononi kama milioni kumi kumi hivi wanabadilisha na dollar au kwacha ya Zambia. Hawana wasiwasi na maisha yanaenda tu, nilipowauluza wazawa wakasema hayo ndiyo maisha yao, kwa kweli sijawahi shuhudia sehemu nyingine yeyote ile hali. Inaonyesha mzunguko wa hela ni mkubwa sana hapo mjini Tunduma
Hiyo mbona ni kwaida mipakani mkuu
Ukienda Sirari boda wapo, Tarakea wapo, Namanga nk.
 
Nilikuwa Geita mwaka 2012, nikapita kununua nguo na viatu kwenye boutique za hapo, ebanaeeee! Kuna nguo na viatu pale ambavyo Mwanza havipo
Mpaka sasa ukienda Katoro nguo na mavazi bei ni kitonga, wafanya biashara baadhi kutoka Mwanza na mikoa jirani sikuizi wanafata mzigo kule...
 
Back
Top Bottom