Tunduru: Mama aua mtoto wake kwa sumu ya panya kwa masharti ya kupata kazi za ndani Arusha

Tunduru: Mama aua mtoto wake kwa sumu ya panya kwa masharti ya kupata kazi za ndani Arusha

Kuna hii tabia ya baadhi ya wanaume unampa binti wa watu mimba afu unamtelekeza, inabidi serikali iwachukulie hatua Kali wanaume wa namna hii maana ndio wanasababisha tunakuwa na watoto was mitaani na mauaji kama hayo. Mpaka mama anamuuwa mtoto wake itakuwa akili yake ilikuwa imeathiriwa vibaya na msongo wa mawazo, sonona, na matatizo mengine mengi.
 
Haya ndio matokeo ya kula tunda la masihara!

Binti limezalishwa hovyo..... baba wa mtoto hajulikani...... na mwisho wake toto nalo linakuwa chokoraa!

Aiseee.........
 
Kuna hii tabia ya baadhi ya wanaume unampa binti wa watu mimba afu unamtelekeza, inabidi serikali iwachukulie hatua Kali wanaume wa namna hii maana ndio wanasababisha tunakuwa na watoto was mitaani na mauaji kama hayo. Mpaka mama anamuuwa mtoto wake itakuwa akili yake ilikuwa imeathiriwa vibaya na msongo wa mawazo, sonona, na matatizo mengine mengi.
Ndiyo maana makonda anapaswa kurudishwa ukuu wa mkoa au Waziri wa Ustawi wa Jamii
 
Kuna hii tabia ya baadhi ya wanaume unampa binti wa watu mimba afu unamtelekeza,
Kwani hiyo mimba ni andazi, kwamba unalichukua unalipachika kwa binti?

Kabinti kanaonekana kashangingi haka maana kamezaa kakiwa na miaka 19!

Most likely kalishatoa mimba nyingi hapo kabla!

Baba wa mtoto si ajabu alikimbia kuhofia kubambikizwa mimba!

Hawa watoto wafundishwe kwamba maisha ni zaidi ya kula "tunda la masihara".

Dunia itamfunza vizuri.
 
Kwani hiyo mimba ni andazi, kwamba unalichukua unalipachika kwa binti?

Kabinti kanaonekana kashangingi haka maana kamezaa kakiwa na miaka 19!

Most likely kalishatoa mimba nyingi hapo kabla!

Baba wa mtoto si ajabu alikimbia kuhofia kubambikizwa mimba!

Hawa watoto wafundishwe kwamba maisha ni zaidi ya kula "tunda la masihara".

Dunia itamfunza vizuri.
Taratibu mkuu... Bado tupo njiani na Safari Ni ndefu....
 
Duh, 4yrs kweli??? Si angeenda nako popote kwenye usalama amuache pale malaika huyo......kazi aliyekuwa anaifuata ni gerezani.
 
MKAZI wa Kijiji cha Mwenge, Kata ya Mtina wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma, Neema Athumani (24), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake kwa kumwekea sumu ya panya kwenye soda.

Taarifa za tukio hilo zinadai kuwa mwanamke huyo alitekeleza mauaji hayo Desemba 24, mwaka huu, baada ya kuweka sumu ya panya kwenye soda na kumnywesha mtoto wake Rashfod Tariq, mwenye umri wa miaka minne.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza unyama huo, alichimba shimo na kwenda kumzika na baadaye kutoroka kijijini hapo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo mtuhumiwa alikamatwa akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha alikodai kuwa alikuwa anaenda kwa ajili ya kufanyakazi za dani kutokana na ugumu wa maisha, baada ya mzazi mwenzake kumtelekeza na kukataa kumhudumia mtoto.

Akiwa chini ya ulinzi wa polisi, mtuhumiwa huyo alikiri kufanya tukio hilo baada ya kupewa masharti na mwajiri wake wa mkoani Arusha kuwa kama anahitaji kazi aende bila mtoto.

Nipashe
Daaah hapo kakosa mtoto na kazi kakosa lakini anapata makazi mapya ya jela
 
Sasa huyo ndio angeenda kulea watoto wa mwingine vizuri kweli??kama ameweza kuua wa kwake wa kwako je? Tuwe tunawaombea Sana hawa wasichana wa kazi.
Logic sana. But, kikwazo kikubwa ni maisha magumu. Angefanikiwa huenda angetoboa huko mbeleni. Mauaji yamemgharimu. Angepambana na mwanawe, sema akimchukia baba mtoto likely amchukie na mwanawe. Mungu aepushie mbali
 
Alimwambia Hawa: "Hutakufa, utakuwa sawa na Mungu". Mtu akifa: "Aaa!! Mungu amempenda zaidi, inabidi amchukue, msilie. Mnamchukiza sana Mungu mnapolialia, msipoangalia atamtupa motoni".
Kumpenda hiyo kwhio!??? Kumbe huyu malaika asiye na hatia, wakati ule akingali hai, alikuwa hampendi, siyo!???
 
wanawake tangu siku wameongea na nyoka kisichojulikana sio wa kuwaamini.hata uzao wao wanaua
Ile baada ya kutonywa uongo na nyoka, hichohicho ^kisichojulikana^ akakitransplant kwenye hippocampus ya mumewe. Kwa hiyo usiwe mwepesi saaaaana kuwasingizia mahabiba (ladies) because hata hawa gentlemen (wanaume wapole!?) ni pasuakichwa & vivuruge kwelikweli!!!
 
Back
Top Bottom