Tuombe Mungu sana watoto wetu wasijekuwa kama mwijaku maana huku alipofikia inasikitisha

Tuombe Mungu sana watoto wetu wasijekuwa kama mwijaku maana huku alipofikia inasikitisha

Hapana mkuu sijamfuatilia sana, sema hizi ambazo nimeziona ni anajidharirisha yeye kwa lengo la kupata pesa SASA ni bora anayejidhalilisha yeye kuliko anayewadharirisha wengine kwa manufaa binafsi.
Kudhalilika ni kubaya iwe wewe mwenyewe au kwa kufanyiwa na mtu mwingine.
Na psychology says : ni afadhali kuzalilishwa na mtu au Watu wengine jamii inaweza kukuelewa Pengine umeonewa lakini kujidhalilisha mwenyewe ni kutoitendea haki nafsi yako mwenyewe .
Ni kujikatili nafsi yako mwenyewe ni Sawa na kujiua mwenyewe ambao ni ukatili wa hali ya juu sana.
Inaweza kueleweka kukataliwa na watu wengine lakini sio kujikataa mwenyewe nafsi yako.
 
Na mimi nashangazwa mno na comments za hivyo huku aisee.
Kumbe wapo wengi wenyevakili kama yake jamaa.
Wanasema ukitaka kumjua mtu Mwambie aongee au aandike ndipo utajua yaliyomo moyoni na kichwani nwake.
Ndipo utajua hapa pana mtu au hapana.
Vijana wengi sahv wanataka mafanikio...wako tayari kuuza hata utu wao

Ova
 
Mafanikio kwa kujitoa utu wako ?
Kwani maana ya mafanikio ni nini labda ?!
Kuwa na material things pekee ?
Tafuta kujua zaidi aisee.
Heshima na utu ndio mafanikio ya kwanza kwa binadamu mengine yanafuata.
Tafsiri ya utu haiwezi kulingana kati ya jamii na jamii, mtu na mtu ndio maana Mimi na wewe tonafautiana kwenye huu mtazamo . Kwa maana ndogo tu utu ni kufanya matendo ya kibinadamu.(akili) Mwijaku ana shahada ya sanaa, anachofanya ni sehemu ya kile alichosomea na ubunifu wake unamlipa! Kwa nini uhisi yeye anajiondoa utu wake?

Tukisema Kila kitu tukiangalie kwa undani kwa mitazamo yetu tunapata tafsiri iliyo potofu au kukibeza/ kuona sio sahihi. Mwisho wa siku unapata stress....take it easy bro! Enjoy life
 
Ni ajabu mtu kujaji maisha ya mtu ambaye huwezi ata kumsaidia chochote, kila mtu ana maisha yake na njia yake katika utafutaji, kulikoni ufuatilie maisha ya mtu ambaye hata akikwama huwezi kumsaidia chochote? Ikitokea leo mwijaku akasema aache kufanya hvo halafu umuchangie hela, cha ajabu ata hutatoa chochote mkuu, hvo ishi unavyopenda ww kuishi pia muache na yeye aishi anavyopenda yy kuishi syo uvyopenda ww mkuu, kla mtu na maisha yake na familia yake na kifo chake
 
Kweli vyote anavyo ila pata picha vijana wote au kijana wako anakuwa na mtizamo wa uchawa kama Mwijaku.

Kuna jamii nyingine zimekuwa na maendeleo sababu ya watu walio bora ,sababu marole model walio wazunguka wanafanya vitu vya maana kwa kutumia akili na talent zao na si kujipendekeza mf China. Sometimes China unaweza ukaona wanakosea ila kwa kufilter content za Tiktok na kuondoa vitu vya kipuuzi na kuviacha vya maana,ila ukitizama impact ya social networks ktk kujenga kizazi kilicho bora na chenye mitizamo chanya kwa maendeleo ya jamii China wapo sawa.

Machawa siku hizi wapo mpaka sehemu za kazi,wanawadidimiza wengine kisa yy ni chawa wa boss.Mfano kama huyo Mwijaku kwa tabia yake Kisha chafua Image ya Tanasha akatishia kumpeleka kwa Pilato akaomba Msamaha, juzi kachafua Image ya KP kampeleka mahakamani wameombana msamaha yameisha, hivi huoni huyu jamaa ni mtu wa hovyo,pamoja na hivyo anavyo vimiliki maana yupo tayari kuwaharibia wengine ili yeye atrend.
Ukinisoma vizuri utaona nimeongea kitu neutral sio kwa sababu nafurahia nachokiona Ila ndio uhalisia.

Siku hizi upuuzi ndio unapigiwa promo kwa sababu ni rahisi kuuza kwenye mitandao ya kijamii. Mbaya zaidi hao hao social media influencers wanaokuza majina katika upuuzi ndio wanapewa channels za kupata pesa kama media careers and endorsements

Hata hiyo crown media inaonekana ina unafuu kwa sababu wanachukua sana influencers wa twitter ambao hawana controversies sana Ila sio kwamba wana uwezo mkubwa.

Kwa sasa watu wanajali numbers watazozipata kirahisi kuliko kuumiza kichwa. Mwisho wa siku tuanona tunayoyaona
 
Hizi ni tabia za watu wa pwani, ndiyo huwa ''wanafanya kazi'' kwa kutumia mdomo. Ndiyo maana maeneo hayo hayana maendeleo. Hata Tanzania sasa hivi uongozi umejikita kwenye huu utamaduni wa ''kutenda'' kwa kutumia midomo. Bila shaka hii haiwezi kuwa ndiyo future ya Tanzania sembuse generation. Ni mapitio ya muda tu kwani huwezi kudanganya watu wote kwa muda wote. Nchi haiwezi kuendeshwa kwa maneno na ukweli utadhihirika baada ya muda.

Hao watendaji wenye brains wengi wamekaa kimya ili kulinda positions zao na wengine wakiweka mbele ujasiri. Wanapigwa pesa wananyamaza.

Hii nchi haina nafuu kuanzia juu hadi chini maana watu wenye substance wanawekwa kando kwa sababu wanatoa challenge kuliko hawa ambao wanaweza kujizima data. Unachowaambia ndicho wanachokisema
 
Kudhalilika ni kubaya iwe wewe mwenyewe au kwa kufanyiwa na mtu mwingine.
Na psychology says : ni afadhali kuzalilishwa na mtu au Watu wengine jamii inaweza kukuelewa Pengine umeonewa lakini kujidhalilisha mwenyewe ni kutoitendea haki nafsi yako mwenyewe .
Ni kujikatili nafsi yako mwenyewe ni Sawa na kujiua mwenyewe ambao ni ukatili wa hali ya juu sana.
Inaweza kueleweka kukataliwa na watu wengine lakini sio kujikataa mwenyewe nafsi yako.
Ukweli mkuu tunatofautiana upeo, kwa hoja zako hatutofautiani na misimamo yangu lakini tutambue kuwa hatuwezi kufanana wapo ambao wanajali pesa kuliko utu wao mfano huyo jamaa anayezungumziwa hapa.

Kwangu mimi ni heri nikose pesa lakini sio kuuza utu wangu, maana naamini shida ni sehemu ya maisha ila shida haziwezi kunitesa, sasa hapo ndipo nitatofautiana mimi na huyo jamaa lakini haimaanishi mimi ni bora kuliko yeye, ni uwezo tu wa kutafsiri mafanikio ndo tumepishana.

Hivyo ni lazima tuelewe kuwa hatuwezi kufanana. Kupitia muda atakuja kujifunza kama sio yeye basi kupitia kizazi chake.
 
Ni ajabu mtu kujaji maisha ya mtu ambaye huwezi ata kumsaidia chochote, kila mtu ana maisha yake na njia yake katika utafutaji, kulikoni ufuatilie maisha ya mtu ambaye hata akikwama huwezi kumsaidia chochote? Ikitokea leo mwijaku akasema aache kufanya hvo halafu umuchangie hela, cha ajabu ata hutatoa chochote mkuu, hvo ishi unavyopenda ww kuishi pia muache na yeye aishi anavyopenda yy kuishi syo uvyopenda ww mkuu, kla mtu na maisha yake na familia yake na kifo chake
Da, unasikitisha sana. Mawazo yako yalikuwa yana nafasi kipindi cha Victorian huko UK. Tuache binadamu wafanye chochote kwa sababu tu wakikwama hatuwezi kuwasaidia?
 
Huenda ni miongoni ambao katika Safari yao ya masomo ni Watu wa kudesa mwanzo mwisho.
Ni huzuni kwa kweli .
Ndio maaana wasomi wengi ni waoga kupita kiasi.
Hawajui kujenga hoja, kuuliza maswali, kujibu hoja wala kujielezea.
Wengi ni watu wa kubumba tu.
Mkuu taifa linaongozwa na watu wasiotaka wajenga hoja, wauliza maswali na wala wapiga zumari wanafurahia majibu yasiyojibu maswali wala hoja.
Vijana taifa hili wataendelea kuwa machawa, maslay queen n.k kwa sababu kazi hizo ndizo sasa zenye fedha. Wasomi kwa sasa hawatakiwi na ukipata nafasi ukataka kutumia usomi wako mfumo unakutema. Ili uendelee kusurvive usomi unautupa pembeni unakuwa kama wao.
Never underestimate the power of stupid/evil people in large numbers
 
Njaa ni mbaya sana...... mwachen afanye mm ningepTa nafasi ya uchawa aaah pesa mbele,

Njaa inauma
hii ina maana huwezi kuwa chawa otherwise ungeshakuwa chawa kwa kuanza kujipendekeza tu from nowhere. Anza kwa kujirekodi unakata mauno ukiwa umevaa tshirt ya mama na kofia ya chama ukisifu na kuabudu.... Utatrend watu wakianza kushare video yako wakikundia jinsi gani unajidhalilisha na ambavyo huna akili.
 
Tafsiri ya utu haiwezi kulingana kati ya jamii na jamii, mtu na mtu ndio maana Mimi na wewe tonafautiana kwenye huu mtazamo . Kwa maana ndogo tu utu ni kufanya matendo ya kibinadamu.(akili) Mwijaku ana shahada ya sanaa, anachofanya ni sehemu ya kile alichosomea na ubunifu wake unamlipa! Kwa nini uhisi yeye anajiondoa utu wake?

Tukisema Kila kitu tukiangalie kwa undani kwa mitazamo yetu tunapata tafsiri iliyo potofu au kukibeza/ kuona sio sahihi. Mwisho wa siku unapata stress....take it easy bro! Enjoy life

Kama ukisoma Sanaa unakuwa vile basi hapana aisee.
No mind transformation
Kwa hiyo walosoma Sanaa wote wako na behavior kama yake kwenye jamii ?
Tafsiri ya utu haiwezi kulingana kati ya jamii na jamii, mtu na mtu ndio maana Mimi na wewe tonafautiana kwenye huu mtazamo . Kwa maana ndogo tu utu ni kufanya matendo ya kibinadamu.(akili) Mwijaku ana shahada ya sanaa, anachofanya ni sehemu ya kile alichosomea na ubunifu wake unamlipa! Kwa nini uhisi yeye anajiondoa utu wake?

Tukisema Kila kitu tukiangalie kwa undani kwa mitazamo yetu tunapata tafsiri iliyo potofu au kukibeza/ kuona sio sahihi. Mwisho wa siku unapata stress....take it easy bro! Enjoy life

Education is not a piece of paper (certificate ). Yaani cheti.
Education must be reflected through behavior in the society.
Ndipo tutajua kuna msomi au mfano wa msomi ?!
 
hii ina maana huwezi kuwa chawa otherwise ungeshakuwa chawa kwa kuanza kujipendekeza tu from nowhere. Anza kwa kujirekodi unakata mauno ukiwa umevaa tshirt ya mama na kofia ya chama ukisifu na kuabudu.... Utatrend watu wakianza kushare video yako wakikundia jinsi gani unajidhalilisha na ambavyo huna akili.
Kwani mwijaku na babalevo uchawa wameuanza lini ?

Mimi kukatika siwezi aseeh, nashindwa mno

Kama una kibarua Cha kufagia au kupanda maua hapo home nipe,

siwezi for sure 😂😂
 
Kwani mwijaku na babalevo uchawa wameuanza lini ?

Mimi kukatika siwezi aseeh, nashindwa mno

Kama una kibarua Cha kufagia au kupanda maua hapo home nipe,

siwezi for sure 😂😂

uchawa wa namna ya mwijaku unataka moyo. Sema now kila mtu chawa tu hata AY sikutegemea nikasikia wao wanajiita Samia Kings.
Vijana now ni pesa na nahisi kuna pesa ndiyo maana kila mtu now anajifanya ana mahaba sana na CCM.
Unajua tunawakandia ila watanzania wanawasilikiliza wao kuliko wale tunaosema wana hekima na wasomi. Ukimpa msomi akutangazie jambo watanzania wachache watafuatilia kuliko ukimpa mwijaku.
 
uchawa wa namna ya mwijaku unataka moyo. Sema now kila mtu chawa tu hata AY sikutegemea nikasikia wao wanajiita Samia Kings.
Vijana now ni pesa na nahisi kuna pesa ndiyo maana kila mtu now anajifanya ana mahaba sana na CCM.
Unajua tunawakandia ila watanzania wanawasilikiliza wao kuliko wale tunaosema wana hekima na wasomi. Ukimpa msomi akutangazie jambo watanzania wachache watafuatilia kuliko ukimpa mwijaku.
Upo sahihi kabisa ndugu
 
Huyu jamaa naona uchawa ndio kageuza ajira yake Rasmi.

Inasikitisha namna mtu anavyojidhalilisha kusifia binadamu wengine.

Naamini hata Mungu mwenyewe hapendi.

Napenda kumshauri huyu ndugu atafute shughuli nyingine au anaweza fungua kampuni ya PR awe msemaji wa celebrities na watu wataohitaji huduma kama zake, badala ya kujidhalilisha namna hii.

Yaani hii clip anayosifia bango la harusi ya mobeto limenisikitisha mno, na kunifanya niombee wanangu wasije kuwa machawa. Inasikitisha mno.

Badilika ndugu mwijaku bado una muda wa kufanya hivyo.


View attachment 3236829
When ignorance is bliss to be wise is foolish
 
Back
Top Bottom