Tupe maoni, ushauri, dokezo: Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Makundi Maalum

Tupe maoni, ushauri, dokezo: Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Makundi Maalum

Umefanya jambo jema kuanzisha mjadala huu....

Ila nafasi/cheo ulichonacho hapo wizarani, si nafasi ya kudumu! Maana ni mteuliwa wa Raisi!

Hivyo muda wowote aliekuteua akiamua....Unaweza usiwepo kwenye hiyo nafasi!

Hivyo kama ingependeza ungeanzisha page rasmi ya wizara kama wizara, na si kwa hii account Yako...

Ukianzisha page rasmi ya wizara kama wizara...page hiyo itaendelea kupokea maoni kama wizara hata pale utakapokuwa wewe haupo.

Hizo nafasi za kuteuliwa zinategemea sana maamuzi ya yule aliekuteua, ama wananchi waliokuchagua kama mbunge...then kuteuliwa kama waziri...

Hayo ni maoni yangu tu.
Hakuna shida mheshimiwa kuanzisha ukurasa wake binafsi. Hata Leo hii akiwa sio waziri, bado atabakia kuwa mtanzania mwanamke msomi, ataendelea kuchangia na kuanzisha mijadala hapa ambayo itasaidia ukuaji wa jamii ya watanzamia.
 
Heri ya Pasaka wana JamiiForums,

Mimi ni Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Makundi Maalum.

Ninayo furaha kujiunga nanyi katika mtandao huu. Nimekuwepo hapa tangu 2015 kama msomaji zaidi lakini sasa rasmi nitakuwa active member.

Naamini JF itakuwa sehemu nzuri ya kupokea maswali, maoni na mawazo yenu kuhusu namna tunavyoweza kuboresha maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake, na watu wenye makundi maalum nchini Tanzania.

Hivyo, ninawakaribisha nyote kushiriki kwenye majadiliano haya na mimi niko tayari kujibu maswali yenu na kusikiliza maoni yenu na hata kuyafanyia kazi haraka pale inapobidi.

Unaweza kutoa maoni kwenye mjadala huu au kupitia ujumbe wa faragha (PM).

Karibuni
Karibu jukwaani Mh waziri.
1. Unamaoni gani kuhusu umri wa sasa wa watoto kuanza shule?

2. Una msimamo gani kuhusu umri wa kufunga ndoa kwa mabinti uliopo sasa?

3. Tuna sheria kali kuhusu suala la ushoga na usagaji, unamkakati gani kuona hatua zikichukuliwa kwa watuhumiwa?

4. Je, unaridhika na utendaji wa dawati la jinsia la jeshi la polisi?

5. Wizara yako inafikiria siku moja kuunganisha ofisi ya afisa ustawi wa jamii na dawati la jinsia kuwa eneo moja ili kutoa huduma kwa pamoja?

Nyongeza kwa umuhimu, wewe unatokea Singida, je, unafurahia kuona mabinti wazuri wa Kitanzania wadogo wakiwa wanafanya kazi hatarishi kama kwenye makasino mabar, clubs n.k?

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mheshimiwa karibu sana.

Mimi nina ushauri kwenye mambo makubwa matatu na nitayatenganisha kila moja na post yake.

Jambo la kwanza ni kuhusu jina la wizara.

Wizara inaitwa " Ustawi wa Jamii, Jinsia , wanawake na Makundi Maalum"

Kwa kuwa jinsia ni wanawake na wanaume, neno "wanawake" tayari linawakilishwa na neno jinsia. Hivyo nashauri mabadiliko ya jina.

Aidha, chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, kuna component ya "wenye ulemavu kule " ambapo ni sehemu ya makundi maalum.

Hivyo component hiyo ingehamishiwa kwenye Wizara hii ili kuepuka duplications na contradictions.

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Jina lenyewe la wizara ni absurd! Naamini hata majukumu yake ni absurd. Napendekeza jina la wizara liwe 'wizara ya malezi na faragha'.
 
Jambo la pili ni kuhusu "women empowerment"

Ijapokuwa dhana ya kuinua wanawake na haki sawa ni muhimu : dhana hii kwa kiasi fulani imekuwa ikipokelewa kwa namna tofauti na wanawake wenyewe.

Kuna wanawake wamekuwa wakiitafsiri kuwa wanawake wanatakiwa kuingia kwenye mashindano na wanaume au kujifananisha na wanaume.

Hatimae hii imepelekea mashindano hadi kwenye ngazi ya familia. Miongoni mwa madhara ya hii ni ndoa kuvunjika ovyo, walioko nje ya ndoa kukosa incentives ya kuingia, baadhi ya wanaume wakiona mwanamke anacheza role ya mwanaume wao wanacheza role ya mwanamke n.k

Hii inapelekea kufa kwa taasisi ya ndoa na hatimae kufa kwa taasisi ya familia. In the long run hii inaenda kuleta janga la ajabu ambapo sijui tutafanya nini.

Kwa hiyo pamoja na "empowerment" lakini tukumbuke kuwakumbusha wanawake kuwa bado wao ni wanawake na wana social and family roles kama wanawake ambazo wakiziacha ni hatari.

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Jambo la tatu ni kuhusu watoto wa ntaani na omba omba.

Makundi haya tunatakiwa tuyaondoe mtaani kwa sababu kubwa mbili. Kwanza sababu za kibinadamu na pili kwa sababu za kiusalama.

Hata hivyo hatuwezi kufanikiwa kwenye hilo bila sera na mikakati madhubuti.

Kwenye sera, kuna dhana inaitwa "Distributive Justice". Dhana hii inajibu swali la kwamba 'serikali zinapata wapi uhalali wa kukusanya kodi kutoka kwa wenye kipato na kuwapa wasio na kipato'. Kwa bahati mbaya dhana hii haijawa reflected kwenye Wizara unayosimamia.

Kwenye nchi zilizoendelea, wameenda hatua kubwa. Wanakusanya kodi kwa matajiri na sehemu yake wanasaidia makundi maalum ikiwemo wasio na ajira. Hata hivyo kwa Tanzania hatuwezi kwenda hatua hiyo kwa sababu za kiuchumi lakini pia watu wataamua kutofanya kazi kwa makusudi.

Sisi angalau tukusanye kodi, tutenge fungu la kuwasaidia watoto wa mitaani na omba omba wasiojiweza kabisa . Zijengwe safe houses za serikali wahudumiwe huko, wanaoweza kujitegemea wanaachiwa wasioweza wanatunzwa maisha yao yote.

Hii ni kwa sababu kuna makundi ya watu ambao kwa sababu za kiasili, hawawezi kusimama wenyewe bila kusaidiwa kimkakati. Na watu hao hawafanyi makusudi kuwa kama walivyo. Mfano watoto yatima waliotelekezwa na walemavu wenye ulemavu mkubwa.

Tutapata wapi fedha? Iwekwe kodi ya Tsh 50 kwenye kila chupa ya maji.

Kwa nini maji ya kunywa? Kwa sababu kupitia hapo kila mwenye uwezo kidogo atachangia na asiye na uwezo sio lazima anywe maji ya chupa.

Naomba kuwasilisha.

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Nidokeze tu kwa uchache hili nililokutana nalo mtaani kama litahusu wizara yako itapendeza likifanyiwa kazi ili kuokoa hiki kizazi..

Kuna makampuni yako Mbeya, Masasi pia nasikia kuna mikoa mingine wapo hao (sitotaja majina moja kwa moja ila hili ukilifuatilia majibu yake utayapata).

Hawa huwa wanakusanya vijana na kuwapa elimu ya Biashara na Matibabu kama walivyojitambulisha kwenye serikali kwa mlengo wa kuisaidia jamii ni ktk NGOs.

Na kinachofanyika kila kijana akijiunga kwenye mafunzo yao huambiwa akishawishi wenzake wakaenda kwenye hayo mafunzo basi kila kichwa kimoja yeye hupewa Tshs 36000.

Malengo yaliyopo kwa muonekano wa nje ni mazuri kama yalivyoainishwa kuwa wanafundindwa namna ya kufanya BIASHARA na Elimu tiba ikiambatana na madawa yenyewe na vijana wengi wamechukuliwa wako kwenye hayo mafunzo.

Uhalisia wa hawa jamaa tumeupata kutoka kwa mama wa binti mmoja wa mtaani kwetu ambae kasimuliwa na mtoto wake huyo ambae hadi sasa yapata miezi kama 5 au 6 yuko na hao kimasomo na akanukuu kuwa katika masomo waliyosomeshwa hivi karibuni ni "namna gani ya kumhudumia shoga (gay) na namna ya kuandaa wanawake (lesbian)" na mwisho wa mafunzo kutakuwa na plactical huko bado hawajafikia.

Pia wameambiwa kama wanawajua majumbani kwao wanakoishi watu wenye hizo tabia hususan mitaani mwao wawaendee na kuwashawishi ili wawaunganishe nao ila hapo hakupambanua vizur kivipi watahusishwa na ikumbukwe huyu mama anasimulia haya mambo haoni wa kuhisi ubaya wa hayo bali anaona kama kwa mtoto wake ni sifa na anasimulia kwa ‘kujimwambafai’.

Pia akasema yule mama mwanae kamuona na vilainishi, condom, vipandikizi na vikolokolo viingi ambavyo havijui.

Baada ya kuipata hii taarifa tukajaribu kumbana kijana mmoja ambae ni mwanafunzi wa mafunzo hayo hayo, ila ndio kwanza yuko na mwezi mmoja kimasomo na alikuwa anafanya kazi ya kumshawishi mtoto ambae tunakaa nae maskani muda anampigia simu tukamwambia amwambie afike kijiweni na alipofika tukamhoji mambo yenye kushabihiana na niliyoelezea yeye akakataa kuwa hawafunzwi hayo na vigezo vya kujiunga na hayo mafunzo ni kujua kusoma na kuandika pekee.

Sasa tukahisi labda hawa wapya hawaambiwi mapema hayo mambo au kuna namna ambavyo wanaonywa kufunga siri hatujui.

Niombe tu wewe kama Waziri mjitahidi na timu yako kufatilia hili jambo, maana hawa jamaa wanabeba vijana zaidi ya 1000. Ukilipatia majibu itapendeza ukiyaleta hapa hata kama yakichelewa, maana twafahamu hili jambo ni mtambuka.
 
Mheshimiwa waziri, wizara yako Ina kipengele cha watu maalum. Naomba kujua watu maalum ni wepi haswa?

Pili, nafahamu pia wafanyabihashara wa kati na wamachinga ni mojawapo ya makundi yanayohudumiwa na wizara yako. Je, ni kwanini wananchi hawafahamu hili? Kwanini wasemaji wa wizara hawafanyi jitihada za kutangaza hili ili wananchi na hawa wafanyabihashara wajue hili?

Tatu, je wizara yako ina wanasheria ambao wanaoweza kuwasaidia kisheria wanawake na watoto hata kwa ushauri? Kama wapo, ni kwanini wewe na wasaidizi wako hua mnaelekeza wananchi wawasiliane na maafisa ustawi wa mikoa hata kama jambo linaonekana wazi kabisa linahitaji ushauri wa kisheria?

Nne, kwanini hapo wizarani hamzingatii maswala ya TEHAMA katika mawasiliano? Kwa hali ilivyo mnafikiri ni rahisi kila mwanamke kufika Dodoma kufata msaada hapo wizarani? Mheshimiwa ukiwa kama mwanamke nafahamu unafahamu hali halisia ya mwanamke akiwa na shida, kapigika na anahitaji msaada, mnatakaje wanawake wafike Dodoma na hawana hela ya guest wala nauli?

Tano, kwanini hamna desturi ya kufuatilia hatma ya mwananchi alieleta kero na kuhitaji msaada hapo wizarani kwenu? Mimi shemeji yangu alifikisha suala lake kwa Katibu Mkuu wa Wizara (Mama wa Kizanzibar, very friendly), Katibu akamwelekeza kwa AfIsa aitwae Nandera.

Mwanzoni akafatilia ile issue (ambayo nina uhakika hiyo wizara inapaswa kufuatilia hilo jambo kwa ukaribu maana hapo ndio mahala pake), lakini mwisho wa siku mama yule aliachwa hewani. Yule Nandera wala huwa hapokei simu yake, na mpaka leo yule mama anateseka na watoto wake.

Wewe mwenyewe ulimwambia aende kwa Afisa ustawi anaitwa Denis, yule mama amenyanyaswa kijinsia, analea watoto mwenyewe, ameonewa, ninyi mnadhani wale watoto alionao anajenga taifa gani pale? Hivi Mheshimiwa ninyi hapo wizarani mnafikiri unyanyasaji wa kijinsia ni ubakakaji tu na ulawiti?

Mnafahamu kuna mambo yanazuilika ambayo hupelekea visa hivi vibaya kutokea? Mfano, huyo mama jinsi mmemuignore, akiamua kuwa malaya au mlevi, watoto wake si watageuka majambazi au mashoga? Ni taifa gani litakuwa linajengwa hapo? Unyanyasaji wa kijinsia upo wa aina nyingi, ni lazma muyafahamu hayo.

Sita, tueleze kuhusiana na juvenile court. Mheshimiwa waziri, unaionaje mahakama ya watoto? Je, ni sahihi watoto kuingizwa mahakama ambazo hizo hizo zinatumika na majambazi na majangili?

Mimi nilishuhudia kwa macho mtoto wa miaka saba, mama yake amewekwa lockup kwa amri ya Mheshimiwa Mwakisu, eti ili ampe baba mtoto simply because baba wa mtoto ana hela, hataki kuhudumia mtoto, baba hana mke ni anakesha bar tu na wanawake na shauri limesikilizwa upande mmoja.

Ustawi wa jamii, hawajachunguza sehemu mtoto anayopelekwa, lakini mtoto ametishwa asipoenda kwa baba, mama atafungwa. Na hakimu mwakisu pamoja na ustawi wanamtukana yule mama na kumfedhehesha mbele ya mtoto wake, mama analia kilio kikubwa sana hapo mahakamani.

Nimekupa mfano huo Ili uone jinsi ambavyo mfumo uliopo wa mahakama za watoto hauko sawa, na ustawi wa jamii haswa hapa Arusha una matatizo mno, unahitaji marekebisho ya haraka. Hakimu anaendesha kesi mathalan ya uhujumu uchumi then inafata ya mtoto. Mtoto yupo hapo nje na mama yake au baba, haya ni mazingira Gani tunawajengea watoto?

Saba, mfumo dune katika nchi yetu uko katika haki gani kwa sasa? Serikali imechukua hatua gani kupambana na kuhakikisha inamaliza mfumo dume? Unafahamu hata hawa viongozi wa chini huku kama Watendaji, Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya na Mikoa ni wafuasi wa mfumo dume? Kwenye Taasis za Umma haswa Polisi ndio usiseme.

Mheshimiwa Waziri imefikia hatua kiongozi mwanamke akitoa maamuzi hayafatwi, simply because she is a woman. Hapa kwetu tuliwahi kupata DC mwanamke ambae alikuwa mweledi sana, na hata sasa ni kiongozi mkubwa sana kwenye sekretariet ya chama tawala.

That woman had vision, lakini alipopanda na kuwa RC, DC aliekuja kuchukua nafasi yake alifuta mambo mengi na maamui mengi ya kiongozi yule. Sasa tuambie, wizara yako na serikali imejipangaje kuhakikisha mfumo dume unapungua ama unaisha kabisa? Kwa kuanzia kwa hawa viongozi waandamizi, je, kuna lolote mmewahi kufanya ili kuwaondolea zana ya mfumo dume katika uongozi wao? Mfumo dume ni mbaya na unadumaza taifa.

Nimeyasema hayo nikiwa na uchungu mkubwa sana.

Jumanne njema Mkuu.
 
Karibu sana Mama Dorothy na hongera kua official user wa JF,

Mimi na Mama yangu tunakupenda sana ucheshi wako na uchapakazi wako hasa ulipokua wizara ya Afya uliipatia sana, na sasa wizara hii hujaiangusha pia uchapakazi upo pale pale, umekua karibu sana na jamii na hiyo ni sifa ya kiongozi bora,

Yangu ni hayo tu, Mungu azidi kukubariki.
 
Mama mnatenda vyema ila kuna wenzenu hawataki kwenda naninyi.
Kuna hii inshu ya TASAF.

Story ipo hivi, kipindi cha sensa nilibahatuka kupangiwa maeneo ya Tabora sehemu ya wilaya ya Kaliua jimbo la Ulyankulu sehemu moja itwayo Nhwande, basi kule wananchi walikuwa wakikuona wao walidhani ni msaada wao yaani walikuwa wanaeleza shida zote na ilikuwa ukimkatisha anaweza asikupe ushirikiano kabisa hivyo kuna muda tulikuwa tunawasikiliza tu.

Basi nilifika kwenye mji mmoja nikamkuta mzee hivi na bibi wakanikaribisha, basi nikaanza kudodosa nikipomaliza wakaniambia "Mwanangu nenda kamwambie Rais mimi TASAF walinikata maisha yangu ndiyo kama haya unayoyaona, wanatuacha sisi wazee tusiojiweza wanaowapa wenye nguvu zao halafu pia hao wenye nguvu wanawezeshwa ila wanaenda kunywea pombe. Mwanangu mimi hapa naumwa Madonda ya tumbo lakini viongozi wangu wa hiki kijiji walinikata jina langu sijui halikupelekwa huko TASAF.

Nakuomba mwambie mama kuwa sisi watu tusiojiweza tupo wengi sana ila wanaosajiliwa kwenye hii TASAF ni tofauti, TASAF wenyewe waje huku wajionee wasifikie tu ofisi za kata au vijiji wanadanganywa wakikuta watu wamekusanywa"

Maoni yangu nikuwa waziri wetu fanya jambo katika hili kweli kuna watu wasiojiweza ila wakiwezeshwa watajiweza mfano huyo mzee akiwezeshwa mfano akawa anafuga mbuzi na kuku maisha yanaenda Safi tu kwani pale anatujukuu japo na twenyewe hatusomi kabisa, pia na huu ni mkasa mwingine ila nitauleta siku nyingine.

Nipo tayari kutoa ushirikiano kusaidia huyu mzee kumfikia.
 
Mama kama vile unaweza ukarudishwa kule afya maana mambo yamewakalia wengine ndivyo sivyo
 
Mh kubwa ombi letu sisi tunaomba jina la wizara ibadirishwe na kuwa Wizara ya Ustawi wa Jamii kwasababu unapoongelea makundi maalumu wazee na watoto hawa wote baba yao...
Acha roho mbaya wewe, watu wa maendeleo ya jamii (cDO'S) hawakuzuii wewe kufanya kazi yako jipambanie wewe kama wewe usimkandie mwenzio, huna tofauti na mwanaume ambae hajiamini anaekwenda kutongoza kwa kumkandia mwanaume mwenzie ili mwanamke amkubali.
 
Jina lenyewe la wizara ni absurd! Naamini hata majukumu yake ni absurd. Napendekeza jina la wizara liwe 'wizara ya malezi na faragha'.
Aisee😁😁 sijui maana ya absurd,ila Hilo jina la Wizara la ...Faragha,Ndio absurd zaidi...😄😄😄
 
Acha roho mbaya wewe, watu wa maendeleo ya jamii (cDO'S) hawakuzuii wewe kufanya kazi yako jipambanie wewe kama wewe usimkandie mwenzio, huna tofauti na mwanaume ambae hajiamini anaekwenda kutongoza kwa kumkandia mwanaume mwenzie ili mwanamke amkubali.

Acha roho mbaya wewe, watu wa maendeleo ya jamii (cDO'S) hawakuzuii wewe kufanya kazi yako jipambanie wewe kama wewe usimkandie mwenzio, huna tofauti na mwanaume ambae hajiamini anaekwenda kutongoza kwa kumkandia mwanaume mwenzie ili mwanamke amkubali.

Wana ingilia majukumu ambayoo hawayawezi Mtu wa maendeleo ya jamii how comes anakuja ku solve psychosocial ya mteja ambaye kakutwa na matatizo ya kifamilia na jamii ime mtenga? Hawa watu walitakiwa wakae kwenye wizara ya fedha na mipango kule ndiko wanaweza waka plan mikakato mizuri zaidi ya wao kuwezesha vijana lazima tuseme ukweli maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii ni vitu viwili tofauti ata princpal zetu za ufanyaji kazi unatofautiana wao mara nyingi hawazingatii privacy ya client
 
Heri ya Pasaka wana JamiiForums,

Mimi ni Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Wenye Makundi Maalum.

Ninayo furaha kujiunga nanyi katika mtandao huu. Nimekuwepo hapa tangu 2015 kama msomaji zaidi lakini sasa rasmi nitakuwa active member.

Naamini JF itakuwa sehemu nzuri ya kupokea maswali, maoni na mawazo yenu kuhusu namna tunavyoweza kuboresha maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake, na watu wenye makundi maalum nchini Tanzania.

Hivyo, ninawakaribisha nyote kushiriki kwenye majadiliano haya na mimi niko tayari kujibu maswali yenu na kusikiliza maoni yenu na hata kuyafanyia kazi haraka pale inapobidi.

Unaweza kutoa maoni yako kwenye mjadala huu au kupitia ujumbe wa faragha (PM).

Karibuni
Karibu sana hapa Mh Waziri. Mimi ningeshauri kuwa je katika ngazi ya wizara unayoiongoza hamjaona umuhimu ya kukifanya kitengo cha Ustawi wa Jamii katika halmashauri zatu kuwa Idara kamili inayojitegemea? Hii itawezesha kitengo hiki kuwa na bajeti yake ili kuweza kumudu shughuli zake tofauti na ilivyo sasa ambapo shughuli nyingi za Ustawi wa jamii katika halmashauri zinategemea Mkurugenzi ana fedha au DMO.
 
Dkt. Gwajima D binafsi na kupongeza sana kwa uamuzi huu wa kuwa mwanachama wa jf kwa uwazi. Nadhani ni uamuzi mzuri sana ambao unapaswa kuigwa na wasaidizi wote wa mh Rais kwa lengo na madhumuni ya kuwa hudumia wananchi kwa urahisi .
Upongezwe sana Mheshimiwa.
 
Nadhani wizara yako Mheshimiwa ni wizara nyeti sana kwa muktadha mzima wa maendeleao ya taifa letu, hatutajivunia lolote ikiwa jamii kwa ujumla wake haya akisi kile kilichopo.

Kuna kundi kubwa sana la vijana ambao hawana ujuzi wowote na wenye ujuzi walao kidogo.

Kumekuwepo na mipango ya kuwasaidia vijana hao kupitia mikopo midogo ya vikundi ambayo inatolewa aidha na manispaa, Sido, Jaica, Veta nk.

Kwa bahati mbaya sana hio mipango tokea kuwepo kwake haijawahi kuwa na manufaa yoyote kwa walengwa kwa sababu wahusika hawawafikii walengwa badala yake wanaonufaika sio wahusika.

Sijui wizara yako mh ina mpango wowote wa kuwawezesha vijana wenye ujuzi ambao hawana mitaji, mfano wa vijana hao ni wahitimu wa mafunzo ya ufundi kupitia taasisi za ufundishaji wa ufundi.

Binafsi niko kwenye taasisi ya ufundishaji ufundi kwa vijana wenye mahitaji maalum, wakiisha hitimu mafunzo yao huwa hawana namna yoyote ya kuendelea na kile walicho nacho kichwani kama ujuzi kwa sababu ya ukosefu wa mitaji, lakini kama wangeweza kufikiwa na kusaidiwa ingeweza kupunguza gep la ukosefu wa ajira na kungekuwepo na nguvu kazi ya uzalishaji katika taifa letu.

Niwatakie yote mema naamini mna mpango mizuri na maendeleo ya jamii kwa ujumla wake haswa vijana na wakina mama ambao wanapambana kila leo ili kupunguza mnyororo wa umaskini.
 
Back
Top Bottom