Tupia jina la mwalimu aliyekuwa mnoko shuleni/chuoni kwenu

Kuna Mwalimu mmoja anaitwa RUBA alikuwepo Mara Sekondari miaka ya 90, huyu mwalimu ni mnoko hana mfano....halafu huwa hacheki na mtu yeyote, hata walimu wenzake. Siku moja nilidokoa maharage jikoni, kiraja akaniona akanichongea kwa RUBA. Siku ya Jumatatu wakati tukiwa assembly ground akaniita na kuanza kunichana mbele za wanafunzi mbele. Kisha alinipa adhabu ya kupanda majani kwenye korongo lililokuwa karibu na Physics laboratory. Basi akawa anaifuatilia kinoma...aliniambia nimwaguile maji zile nyasi hadi ziote...na kama mnavyojua ukame wa Musoma, nilikomaje! Sitamsahau mshenzy yule kamwe!
 
hii mkuu peleka jukwaa la jokes hapa tunataka tujadili mambo ya kutusaidia kielimu.unapotosha maana ya jukwaa.
 

Nilishauri thread iende jukwaa la utani lakini nimecheka sana.teh teh teh.
 
Kabobe sabasaba sec mtwara ni balaaa bora ukutane na nyati
 
zanaki mwl mwarike jamani mnokoooo na alikua anaongea kiingereza mnacheka hadi bas
 
Kuna mwakaringa a.k.a kibana wa kibasila enzi izo npo pale 2001-2004 usipochomekea shati lazima akubane,siku moja alipigwa getini unoko wote ukaisha

Mwakalinga ni bonge la Ticha. Mtakua marafiki na ukikosea anakubadilikia. Ana mawaidha... Binti hii tabia haikupendezi, haikupendezi kabisa.
Nilikuja kukutana nae wakati fulani alikua AICC Arusha kwenye Mkutano fulani akiwa Mkalimani wa Kifaransa.
 
Bukoba Secondary Mwalimu Nakembetwa 1980s-1990s.
 
Kuna Mwalimu alikuwa anaitwa HAYATI MAREHEMU MAITI SENGOVI! Dah ilikuwa ni noma alikuwa baraaaaa! Alifika shule kwa Mara ya kwanza akajitambulisha kuwa alikufa na akafufuka kijiji kizima kilitikisika hiyo ilikuwa miaka ya 1988/ alikuwa ni tishio jamani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…