Tusiukubali mradi wa Wachina wa Bandari ya Bagamoyo kwa sababu zozote zile. Utakuwa ni mtego utakaotunasa kama nchi

Tusiukubali mradi wa Wachina wa Bandari ya Bagamoyo kwa sababu zozote zile. Utakuwa ni mtego utakaotunasa kama nchi

Kwani mkataba wake unasemaje? Kwani naona maneno mengi, si uwekwe wazi ndio watu waamue? Huyu anasema vile, huyu anasema hivi hata hatuelewi, utakataaje/utakubalije kitu ambacho hujijui?
Ila unakubali ambacho hukijui?
 
Daaaa!!hivi nyie huwa hamsomi mchango wa mtu hadi mwisho, ?ila ni kurukia tu kujibu!!niliposema kuwa unakubalije/unakataaje kitu ambacho hukijui nilimanisha kukubali??
Hiyo ni Fallacy, kama hukubali means unakataa, na haukatai means unakubali, na sio both at the same time. Hivyo hiyo ya pili ni kama hukuisema, by logical implication.
 
JF inaweka kumbukumbu katika mijadala yetu, hapo chini nimekuta kuna mchangiaji ameweza kuweka mawazo yake na mchango.
C&P.

Moja ya maoni ya wadau👇

Najua topic imepita, lakini ninajua kidogo kuhusu mradi wa Bandari ya Bagamoyo na napenda kumuunga mkono Mhe Spika kwa hoja zifuatazo. Na naamini Serikali yetu itazichukulia kama ushauri wa Mbunge kwa Serikali, ambao ndio wajibu wetu wa msingi kama Wabunge.

Muhimu kujua background ya mradi wa Bandari ya Bagamoyo. Kwanza, mradi huu ulibuniwa na Serikali yetu kama Bagamoyo Special Economic Zone mwaka 2004 chini ya Mpango Kabambe wa Ujenzi wa Sekta Mpya ya Viwanda. Serikali ya Japan ndio ilitusaidia kwenye hili. Mradi huu uliitwa “Tanzania-Mini Tiger 2020” na ulikuwa chini ya Wizara ya Viwanda.

Mamlaka ya Bandari nayo ilibuni Mpango Kabambe wa Miaka 20 wa Uendelezwaji wa Bandari za Tanzania (The Tanzania Port Development Master Plan 2009-2028) ambao ulipendekeza Bandari ya Bagamoyo ijengwe katika miaka ya 2021/2022 ili iwe tayari kujaza nafasi baada ya Bandari ya Dar es Salaam kufikia ukomo wa kuweza kuongezewa uwezo. Kwahiyo mambo mawili ya msingi hapa ni kwamba: (a) Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo tuliubuni sisi wenyewe, ulikuwa sehemu ya mipango yetu ya muda mrefu na haukujengwa kwa msukumo wa Wachina; (b) mradi wa Bandari ya Bagamoyo sio ni mradi wa Bandari, bali ni mradi wa Ukanda wa Kiuchumi ambao unaendana na mji wa viwanda.

Mwaka 2009 Mamlaka ya Bandari, kupitia kampuni ya Hamburg Port Counsulting ya Ujerumani, ilifanya upembuzi yakinifu wa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo na
kuona una manufaa kutekelezwa. Mwaka 2011, Wizara ya Viwanda na Biashara, kupitia CowiConsult, nayo ilifanya upembuzi yakinifu wa Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone (BSEZ), kwa kufungamanishwa na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.

Mipango yote hii ilikuwa ni yetu wenyewe, na tulijiridhisha kama nchi kwamba Bandari ya Bagamoyo tunaihitaji na tukaiweka kwenye Mpango wa Pili wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Taifa kama Mradi wa Taifa wa Kielelezo.

Mwaka 2013 na 2014, Kampuni ya China Merchants Ports Limited, ikiungana na Mamlaka/Mfuko wa Uwekezaji wa Oman (OIA), waliomba kuwekeza katika Mradi wa BSEZ na Bandari ya Bagamoyo. Baadaye kidogo, Korea Kusini nao, kupitia Taasisi yao ya Science and Technology Policy Institute” (“STEPI”) ilikamilisha Upembuzi Yakinifu wa kuwekeza katika kujenga na kuendeleza “Bagamoyo High Technology Park” kwa kushirikiana na EPZA pamoja na COSTECH. Kwahiyo hoja nyingine ya kuzingatia hapa ni kwamba Bagamoyo sio uwekezaji wa Wachina pekee, kama inavyodhaniwa. Yapo mataifa mengine. Oman wanaweka pesa yao nyingi. Na Korea Kusini nao wanaweka pesa na maarifa yao.

Kama nilivyoeleza hapo awali, kwa mujibu wa Mpango wa Pili wa Miaka Mitano wa Maendeleo (“FYDP II), Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone (BSEZ) ni Mradi wa Taifa wa Kielelezo. Mradi huo unatarajiwa kuwa utavutia uwekezaji wa Dola za Kimarekani bilioni 10; utakuwa na Viwanda 760 na hatimaye kutoa ajira 270,000 kwa awamu ya kwanza. Majadiliano ya Utatu wa Serikali ya Tanzania, China Merchants na Mfuko wa Uwekezaji wa Oman yalikuwa yanaendelea kuelekea makubaliano na hatimaye kuingia Mikataba ya Uwekezaji kabla ya kusimamishwa.

Zipo hoja kubwa tatu zinazosemwa kuhusu mradi huu: (1) utatutwika madeni kama vile Kenya na Sri Lanka ambapo Wachina walilazimika kutaifisha Bandari; (2) tutaua bandari ya Dar es Salaam; (3) haturuhusiwi kuendeleza Bandari yoyote na haturuhusiwi kutia mguu pale Bagamoyo kwa miaka 99.

Hoja hizi zote sio za kweli, na kwa kweli wawekezaji wa huu mradi wamekuwa wana-struggle namna ya kuzijibu kwasababu zinatolewa na watu wakubwa, na hao wawekezaji, hasa wa Oman, ni mamlaka za Serikali na wasingependa malumbano na Serikali yetu.

Hoja ya kwanza, kwamba tutakopa na kujitwika deni kubwa sio ya kweli: kwenye mradi huu hakuna hata senti tano ya mkopo tunachukua. Huu ni uwekezaji. Hakuna deni hapa, ni pesa ya kigeni inaingia kuwekezwa.

Hoja ya pili kwamba tutaua bandari ya Dar haina mantiki, kwasababu hata kabla Wachina hawajafika ilikuwa ni ndoto na mipango ya Mamlaka ya Bandari kujenga Bandari ya Bagamoyo. Ukisoma Mpango Kabambe wa Miaka 20 wa Uendelezwaji wa Bandari za Tanzania (The Tanzania Port Development Master Plan 2009-2028), wenyewe Mamlaka ya Bandari walitaka Bandari ya Bagamoyo iwe imejengwa ifikapo mwaka 2023. Bandari za Bagamoyo na Dar sio bandari shindani. Ni bandari zitakazosaidiana kuongeza shehena ya mzigo unaopita nchi mwetu. Full stop! Pia Bandari ya Bagamoyo itajengwa kwa kuzingatia teknolojia ya uundwaji wa meli za kisasa (4th Generation Shipbuilding Technology Port). Meli hizi, ambazo zitakuwa zinaongezeka kadri miaka inavyokwenda, haziwezi kutia nanga kwenye bandari ya Dar. Na kama unaitazama nchi kwa miaka 30, 50 ijayo, Bandari ya Dar ina ukomo wa upanuzi. Lazima kama nchi kujenga Bandari mpya kubwa katika ukanda huu ili kuendelea kunufaika na faida ya kijiografia.

Hoja ya tatu kwamba Wachina wanataka tusijenge wala kuendeleza Bandari yoyote kwa miaka 99 na tuwape wao bandari hiyo bila sisi kutia mguu pale sio ya kweli. Hakuna pahala popote wawekezaji wametoa hayo madai. Ukweli ni kwamba kote duniani mwekezaji anapoweka hela yake mwenyewe kwenye mradi atataka muda wa kutengeneza faida kabla hajakukabidhi mradi. Hapa Wachina na Wa-Oman walitaka miaka 33 ya concession. Je, ni mingi au ni michache? Inategemea pesa iliyowekwa (US$10bn) na standard practice kwingine duniani. Reli ya kuunganisha UK na France, ambayo imejengwa na sekta binafsi ina concession ya miaka 50. Kwa bandari standard practice ni miaka 25-40, kutegemeana na ukubwa wa uwekezaji. Cha msingi kwa timu ya negotiators wetu ni kupata financial models za wawekezaji na kuzichambua na kuona wanaanza kupata faida baada ya muda gani. Na cha kutambua pia ni kwamba concession inahusu tu faida ya Bandari na kwamba katika kipindi hiki cha concession bado TRA itakuwa inakusanya kodi nyingine zote husika za mizito bandarini.

Suala lingine la kutazama katika kufanya maamuzi ni kuangalia dunia inaelekea wapi kwenye biashara ya kimataifa. Tutake tusitake, nchi yetu inategemea biashara ya nje kimapato na China kwasasa ndio kinara wa biashara ya import and exports duniani. Inaongoza kwa kuagiza na kuuza bidhaa nje na itaendelea kuwa kinara kwa miaka 50 inayokuja. Ukifungamana nao, utashinda. Kwa mujibu mpango wa China wa Belt-and-Road-Initiative (BRI), meli kubwa za bidhaa zitakazopita katika 21st Century Maritime Silk Road kusafirisha bidhaa kati ya China na Afrika ya Kati na Kusini, zitafikia katika moja ya Bandari za Mwambao wa Mashariki ya Afrika, kama Mlango na Kituo Kikubwa cha kupokea, kuhifadhi kwa muda na kusafirisha shehena kwa meli au usafiri wa nchi kavu. Kulingana na kudra ya kijiografia ya Tanzania ambayo inaimarishwa na uwepo wa Reli ya Kati (SGR) tunayojenga pamoja na reli ya TAZARA, Bandari ya Bagamoyo ambayo itaunganishwa na Reli ya Kati na TAZARA, itakuwa haina mshindani Nje ya Tanzania katika dhana nzima ya ushirikiano wa maendeleo ya uchumi baina ya China na Afrika, kupitia BRI kwa muktadha wa 21st Century Maritime Silk Road.

Mwisho, ni muhimu kutambua kwamba kuna siasa za ushindani na majirani zetu kwenye hili suala. Jirani zetu Kaskazini yetu wanapigana kufa na kupona mradi huu usitokee. Kwahiyo mtaona disinformation nyingi kuhusu huu mradi huku baadhi ya watu wetu wakitumika bila kujijua.

Wenzetu tayari wameanza tena kuifuata kampuni ya China Merchant kuwashawishi wahamishie ule mradi Kenya kule LAMU. Mwaka 2018 wakati wa mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC), kiongozi wao alikwenda Shenzen kuzungumza na China Merchant kuwashawishi waende kwao. China Merchat walikataa na ndio walikutana na Waziri Mkuu Mhe Majaliwa. Na majuzi, tarehe 25 Machi 2021 wameandika barua tena China Merchant kuomba mradi upelekwe kwao (barua nimeiona).

Mwisho, nitamalizia kwa hadithi ndogo: mwaka 1970, wakati Dubai bado ni kamji kadogo jangwani, wazungu waliona potential ya location ya Dubai kibiashara na wakamwendea mfalme wa wakati huo Rashid bin Saeed Al Maktoum kupendekeza wakajenge bandari na waiendeshe kwa miaka 30. Washauri wake wakamwambia tusiwape Wazungu bandari kwenye nchi yetu. Sheikh akawauliza “sisi tuna pesa ya kujenga?”, wakajibu hapana, akawauliza “tutaipata lini”, wakasema hatujui, akawauliza “Dubai itaendelea kuwepo miaka 30 ijayo?”, wakajibu ndio, akawauliza “baada ya miaka 30 wataing’oa bandari na kuondoka nayo?”, wakajibu hapana, akasema “tuwape”. Wazungu wakajenga Port Rashid mwaka 1972. Miaka 30 ikapita haraka. Watu wa Dubai wakajenga uwezo wa kuendesha bandari na wakaanzisha Dubai Port World (DP World), moja ya makampuni makubwa duniani. Dubai sasa ni kinara wa bandari duniani. Majuzi wamechukua bandari za Senegal na Angola. Na wamejenga bandari hadi Rwanda ambapo hakuna hata bahari, wanawasaidia Rwanda kwenye biashara ya logistics.

Mpendwa wetu hayati Rais Magufuli alipenda maendeleo. Alitaka nchi yetu ipate manufaa kwenye miradi na mikataba. Namna ya kumuenzi na kufanya makubaliano yenye tija kwa taifa kwenye mradi wa Bagamoyo. Na hilo linawezekana kama timu yetu ya negotiators itakuwa makini kuzingatia maslahi ya nchi.
Naamini hakuna mtanzania hata mmoja makini anayepinga ujenzi wa bandari ya Bagamoyo sababu manufaa ya bandari yanajulikana. Tatizo ni mashrti ya huo mkataba kama tulivyoambiwa ni hovyo labda kama viongozi wetu wanatuambia uongo lakini kama kweli ndiyo hivyo hata mimi siwezi kukubali kuuza nchi kijinga namna hiyo.
 
Kwani hatuwezi kwenda nchi za ulaya kwa mabeberu kuomba msaada. Wazungu hawanaga noma tunaweza kuwapa hekari 20000 sehemu walime miaka mia alafu watujengee bandari bure tuindeshe nwenyewe. Mchina masharti yake yakukupiga tu.
Mkuu ni kama TANWAT, nasikia JKN alimpa malkia elizabeti eneo la Njombe wali me miti,chai na wao wAkajenga barabara ya lami Songea Njombe ambayo ipo mpaka leo na mkataba wa miaka 100 unaelekea mwisho.
 
Tuna sababu moja kubwa ya kuukata Mradi wa Wachina wa Bandari ya Bagamoyo nayo ni historia mbaya ya China kona mbalimbali za dunia walipotekeleza miradi ya aina hii au walipozikopesha nchi mikopo mikubwa ya miondombinu. Wamechukua bandari Sri Lanka, Pakistan, Australia na Djibouti kupitia mikataba ambayo haieleweki ni yenye utata sana.

Kama huko wameweza kufanya hivyo sisi hatutaweza kuwadhibiti na kuibakiza bandari ya Bagamoyo kuwa bado mali yetu endapo tukiwakubalia wajenge bandari hapo.
Tusijidanganye, sote tunafahamu jinsi gani mikataba midogo tu ya madini imekuwa changamoto kubwa kwa taifa hili, huu ukizingatia na usiri wa mikataba utakuwa funga kazi, tutauzwa mchana kweupe kama enzi za Mangungo wa Msovero.

Tukubali tu kwamba wao ni wajanja na kutekeleza kwa miradi ya aina hii duniani kumewapa ujanja zaidi. Tusikubali bandari zetu kujengwa na kuendelezwa na wageni kwa sababu yoyote ile. Kama tunafikiri ni muhimu sana na tunatakiwa kuwa na Bandari Bagamoyo tukope pesa tujenge wenyewe, vinginevyo tutaiuza nchi yetu nzuri.
Kuna watu bungeni serikalini walisha kula hela ya mchina ili kupitisha dili zake, na ndio hao wameanzisha mjadala wa kujengwa bandari ya bagamoyo. Mchina ni mkoloni mpya anaeingia kwa mbinu mpya, japo hazipishani sana na zile za enzi za Mangungo. Tofauti ni kuwa Mangungo hakuelewa kilicho andikiwa kwenye mikataba, wa leo kalamu ya ku-sign mikataba inawekwa juu ya box la pesa.
 
Kuna watu bungeni serikalini walisha kula hela ya mchina ili kupitisha dili zake, na ndio hao wameanzisha mjadala wa kujengwa bandari ya bagamoyo. Mchina ni mkoloni mpya anaeingia kwa mbinu mpya, japo hazipishani sana na zile za enzi za Mangungo. Tofauti ni kuwa Mangungo hakuelewa kilicho andikiwa kwenye mikataba, wa leo kalamu ya ku-sign mikataba inawekwa juu ya box la pesa.
Sema kuna MTU anaitwa ndugai anasomeshewa mtoto wake China, Ndugai ni wa kupigwa makofi hazarani haoni tabu wanayoipata wasri Lanka waliwapa wachina Bandari, kama tunavyotaka kuwapa Bagamoyo!? Hili zee linafki sana amekufa JPM limeanza tena wakati Jpm aliwaambia ni kichaa tu anayeweza kukubali ujinga ule.
 
Kongole kwako Mkuu,umegonga penyewe,yes pengine Magu alikuwa anapindisha mambo mengine but kwa hii ni Kama aliamua kuweka wazi kile ambacho kilikuwemo katika mkataba kupitia Kakoko,swali jingine la kujiuliza,Kakoko alisema hawajawazuia kujenga bali wamewaambia hayo masharti ndiyo hapana,kama ni umiliki wa ardhi watapewa wa 33yrs pamoja na masharti mengine kuwa reviewed. Ni nini kiliwafanya Wachina kuingia mitini hata baada ya kuandikiwa barua kukumbushwa warudi kwa meza ya makubaliano waweke terms upya kisha waendelee na ujenzi? Huoni ni kama zile terms walizozitaka wao zilipopigwa chini na wao wakaingia mitini. Hapa ndipo point yako inakuja wale wanaotetea huu mradi mbona wanashindwa kutetea hoja zao kwa kuzipinga za Kakoko? Jibu ni simple tu,kile alichosema Kakoko ndiyo uhalisia wenyewe wa huo mkataba.

Kama unakumbuka, mwezi January 2021 Foreign Minister wa China(Wang Yi) na diplomats wengi from China walikuja TZ na wakaenda mpk Chato kwa mazungumzo ya faragha na JPM.

Huo ugeni sio wa kawaida, mwenye macho na maskio kazi kwenu. It was a matter of time ila Mchina kashawin.
 
Bunge lipi la kujadili mikataba kama Ndugai ameibariki?
Hao wote waliingizwa kibabe na Meko Hawakushinda sasa wataachaje kuunga mkono kitu ambacho Ndugai amekibariki?
System ndio inayoamua tunamtaka huyu ...huyu hatumtaki anapenda kupinga pinga sana ..Nimekuelewa sana Pro Assad 60% ya Viongozi hawana weledi
Na huu ndio ukweli

Sent from my HUAWEI CAM-L21 using JamiiForums mobile app
 

Kwani mkataba wake unasemaje??kwani naona maneno mengi, si uwekwe wazi ndio watu waamue?huyu anasema vile, huyu anasema hivi hata hatuelewi, utakataaje/utakubalije kitu ambacho hujijui?!!
 
Kama unakumbuka, mwezi January 2021 Foreign Minister wa China(Wang Yi) na diplomats wengi from China walikuja TZ na wakaenda mpk Chato kwa mazungumzo ya faragha na JPM.

Huo ugeni sio wa kawaida, mwenye macho na maskio kazi kwenu. It was a matter of time ila Mchina kashawin.
Ugeni ule ulifanikisha mkataba wa ujenzi wa SGR Kahama - Mwanza
 
Hii issue ya Bagamoyo inautata sana...

Na hii yote ni kwa ajili ya yule fulani na mambo yake...
 
Au cyoo tusikubalii kwan wanachukua maoni yetu ndo mkataba usainiwe..!? We pambania life lako liwe njemaa mengne utayakuta uko mbele ya safari
 
Sema kuna MTU anaitwa ndugai anasomeshewa mtoto wake China, Ndugai ni wa kupigwa makofi hazarani haoni tabu wanayoipata wasri Lanka waliwapa wachina Bandari, kama tunavyotaka kuwapa Bagamoyo!? Hili zee linafki sana amekufa JPM limeanza tena wakati Jpm aliwaambia ni kichaa tu anayeweza kukubali ujinga ule.
Kusomeshewa mtoto hiyo sio hongo, ni hela kidogo anaweza ilipa, hata iwe level ya PhD, ni chini ya £10,000 kwa mwaka. Hongo kupitisha mkataba wa kukufilisi mtanzania ni balaa.
 
Ndio ule Mkataba unaowala Djibout, Zambia na Kenya? Ule mkataba nakumbuka Mwendazake aliwahi kuweka baadhi ya masharti pindi tu ilipoibuliwa na Job bungeni. Moja kati ya Masharti alisema ni kutokuendeleza Bandari yoyote ile katika nchi hii na yeye Mchina ndiye angekuwa anasimamia kila kitu kuanzia Ukurugenzi mpaka kibarua hapo ndani kwa miaka 100 arudishe faida yake.
Pamoja na kumchukia Kenge mfu kwa kuua na kutesa watanzania wengi,
Namchukia mchina mara mia
Hii clause ya usijenge wala kuendeleza bandari nyingine kama ukweli ni UMAFIA tosha kuaamini ya hata mchina kutaka kusimamia na kukusanya mapato mwenyewe.
Port of Entry iwe bandari, airport au land border ni mali ya nchi si ya kumpa mchina asisimamie kama alivyochukua airport Zambia
 
TUKUMBUKE!,Sisi Tanzania tunapaswa kuwa na bandari nyingi kuliko nchi ya Afrika Kusini.
Tanzania tunazo bandari muhimu(Tanga,Kilwa,Lindi,Mtwara)! Tena kuna zile bandari za Ziwa victoria,Tanganyika na ziwa Nyasa).
Kuwa na bandari nyingi ni sahihi kabisa ila sio kuua zingine. Bandari ya Bagamoyo moja ya Terms zake ni kuziua bandari zingine za mwambao huu kwa Tanzania mpaka ile ya Mombasa.
 
Back
Top Bottom